Showing posts with label Matibabu. Show all posts
Showing posts with label Matibabu. Show all posts

Saturday, April 11, 2020

JIhadhari na Ugonjwa wa Coronavirus



Mgonjwa wa Coronavirus akipata matibabu hospiatlini
Wadau,  tafadhali jikinge dhidi ya ugonjwa wa Coronavirus (COVID-19).  Huo ugonjwa unaua!   Hauchagui rangi, umri, au kama wewe ni maskini au tajiri!

Shemaji yangu, Dennis Whitlow, amefariki kwa coronavirus hapa Boston usiku wa kuamkia jumatatu. Hakuna aliyeruhisiwa kumwona hospitalini hadi amefariki.   Nafahamu wagonjwa wengi, wengine wamepona, wengine wamefariki!  Kuna babu wa miaka 88 aliyefariki niliyekuwa namfahamu na kijana mwenye afya mwenye miaka 28 ambaye amefariki. Coronavirus hauchagui.

Tafadhali mfuate masharti. Ukae mbali na mtu mwingine, kaeni majumbani na ukitoka funika  mdomo na pua!  Nawa mikono kila mara. Usiguse uso wako.

Kifo cha coronavirus ni sawa na kifo cha maji, mapafu yanajaa maji, mwili unashindwa kupata hewa (oxygen).


Mungu Atunusuru!


Kirusi cha Coronavirus
Kaburi la pamoj a ya waliofuka kwa Coronavirus mjini New York

Monday, November 16, 2015

Msaada wa Wasamaria Wema Unahitajika Kwa Ajili ya Matibabu

Ndugu Wasamaria wema
Napenda kutumia fursa hii kukushirikisha habari ya kusikitisha kuhusu dada Joyce Mwambepo (pichani akiwa na mwanaye, na migu yake iliyopooza) mkaazi wa Sinde jijini Mbeya. Dada huyu mwenye umri wa miaka 27 anaishi na bibi yake mwenye umri wa miaka 80 pamoja na mwanaye mwenye umri wa miaka 4.
Kwa bahati mbaya mwezi April mwaka jana dada huyu alipata ajali ya kugongwa na gari ambayo haikusimama kumsaidia. Ila kwa msaada wa wasamaria wema alipelekwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa  Mbeya ambako inasemekana alikaa kwa miezi mitatu bila kupata matibabu.
Katika uchunguzi wa awali ilibainika kuwa Joyce amevunjika miguu yote miwili,  hivyo akahamishiwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili ambako pia baada ya kukaa kwa miezi kadhaa alirejeshwa Mbeya baada ya kukosa shilingi 550,000/- za vipimo na matibabu.
Hadi nakutana naye dada huyu alikuwa amelala nyumbani kwa bibi yake (pichani kushoto) ambaye ni mlezi wake tangu akiwa na miaka minne baada ya wazazi wote wawili kufariki dunia. 
Hawezi kukaa wala kusimama na anajisaidia hapo hapo kitandani kwa msaada wa mwanaye na bibi yake. Inasikitisha.
Hivyo nimejitahidi kufuatialia ili kujua mahitaji halisi lakini sikufanikiwa kumpata daktari bingwa wa mifupa . Ili kumsaidia Joyce inatakiwa aanze process upya za matibabu kuanzia hapa Mbeya referral Hospital  hadi Muhimbili jijini Dar es salaam.
Gharama za matibabu ni kama ifuatavyo:
1. shilingi 300,000/- za kupima CT-SCAN
2. Shilingi 250,000/- za MRI
3. Usafiri wa kutoka Mbeya-Dar kwa gari maalum la kukodi 700,000/-
4. Gharama za msaidizi ambaye ni rafiki yake 300,000/-
5. Chakula 450,000/- (Endapo watakaa hospitali mwezi mzima)
6. Gharama za matibabu (CT-SCAN&MRI ni vipimo tu) 500,000/-
7. Na mahitaji mengineyo wakiendelea kupata tiba 500,000/-

Hivyo kwa kuanzia kiasi cha shilingi 3,000,000/- (milioni tatu) kinahitajika kumpunguzia mateso dada yetu huyu. Asante sana kwa moyo wako wa kujitoa na Mungu atakubariki.

Deo Kakuru Msimu
Msamaria mwema
+255769 512 420

Wakati huo huo kwa niaba ya Michuzi Media Group, Ankal amejitolea kusaidia uratibu wa kufanikisha matibabu ya dada Joyce. Hivyo unaweza kuwasiliana naye kwa email issamichuzi@gmail.com ama whatsapp namba +255 754 271266 kwa jina la Ankal.

Saturday, November 29, 2014

Rais Kikwete Awasili Dar es Salaam, Apata Mapokezi Makubwa!


PICHA NA IKULU



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mmoja wa abiria wakati
ndege aliyopanda ilipotua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye
matibabu leo Novemba 29, 2014
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la
Polisi IGP  Ernest Mangu baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea
Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na
waandishi wa habari na viongozi mbalimbali waliokuja kumlaki baada ya
kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere
jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29,
2014

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mama
Maria Nyerere baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye
matibabu leo Novemba 29, 2014

.Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea mashada ya maua
kutoka kwa wafanyakazi wa Ikulu waliojitokeza kumpokea mara baada ya
kuwasili Ikulu akitokea nchini Marekani kwenye matibabu.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea kadi ya pole toka kwa
mjukuu wake aziza Ridhiwani Kikwete mara baada ya kuwasili Ikulu
akitokea nchini Marekani kwenye matibabu
.

Thursday, March 07, 2013

Tanzanian Journalist Absalom Kibanda Sent to S.A. for Treatment

From THE CITIZEN NEWSPAPER, TANZANIA

By Abela Msikula


The Citizen CorrespondentDar es Salaam.

Tanzanian Vice President Mohamed Gharib Bilal Visits the Injured Mr. Kibanda

As the manhunt for the two individuals who violently assaulted seasoned journalist Absalom Kibanda Tuesday night moves into higher gear, the firebrand chairman of Tanzania Editor’s Forum (TEF) has had to be flown to South Africa for specialised medical care. The journalist, who is also the group managing editor for New Habari Corporation, was grievously wounded following a vicious attack as he came home from work right outside his house at Mbezi Juu in Dar es Salaam. He suffered serious injuries to his left eye. His assailants also knocked several teeth off him and hacked off a finger on his left hand. Just before he was flown out, the TEF chair told local reporters he believes the incident has something to do with his work as a journalist.

After the incident, Mr Kibanda was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH)’s Orthopaedic Institute (Moi), where doctors referred him to a South Africa hospital for further treatment.

The Citizen witnessed him being airlifted at Julius Nyerere International Airport. He left aboard Flight Link around 4pm.

Following these brutal events, the Inspector General of Police, Mr Said Mwema, has assigned four detectives from the Police Force headquarters to beef up investigations into what happened that fateful night, but no arrests had been made when we went to press yesterday.

However, Dar es Salaam Special Police Zone Commander, Mr Suleiman Kova, and Kinondoni Regional Police Commander, Mr Charles Kenyela, said they had formed a joint investigation team to look into the matter.

A statement by minister of Home Affairs Emmanuel Nchimbi said IGP Mwema’s decision is meant “to increase efficiency.” At JNIA, Mr Kibanda shared the harrowing details of Tuesday’s events with the local press.

“I was approaching the gate of my home at midnight. While I was waiting for my gate keeper to open it, two people approached my car and smashed the window screen.”He went on: “As I was trying to escape through the passenger’s door, they grabbed me and began hitting me.” The assailants, he said, attacked him with heavy tools and sharp metals.

“I heard the third person who was off my sight encouraging his colleagues to shoot and finish me…but the two were resisting. An interesting thing is that, they were addressing each other by a title ‘afande’[literally translates ‘Sir’] normally used by police officers,” he noted.

He said when the gatekeeper opened the gate and saw what was happening, he called for help, and the attackers fled.Dr Nchimbi’s statement said Mr Kibanda was found about 30 metres from his car. Nothing was taken from him despite the fact that he had two cellphones and a laptop in his vehicle.

He becomes the fifth journalist to be attacked within the past six months. Two journalists were killed and three others were seriously harmed during this short period.

In September last year TV reporter David Mwangosi was killed by the police in Iringa as he covered a political rally. In January this year Issa Ngumba – a Kakonko-based correspondent with Radio Kwizera –was found dead in the forest with bullet wounds in his body.

Last November, an editor working with Business Times Limited, Mr Mnaku Mbani, was shot and seriously injured by suspected robbers who were attempting to hijack the vehicle he had hired for the day. The following month Shabaan Matutu, a journalist with Free Media Group, was shot in his home by the police in what law enforcement called ‘a case of mistaken identity.’

Mr Kibanda was scheduled to appear in court yesterday as part of an ongoing treason case against him and two others: former group managing editor for Mwananchi Communications Limited (MCL) Theophil Makunga and Tanzania Daima columnist Samson Mwigamba.

They are alleged to have published a “seditious” article in 2011. Following this violent assault on Mr Kibanda, the Kisutu Resident Magistrate’s Court adjourned the case to March 26.

(Additional reporting by Rosina John and Bernard Lugongo)

Local journalists help carry TEF chairperson Absalom Kibanda onto his SA-bound medical flight after he was violently assaulted outside his home in Dar Tuesday night. PHOTO
BY FIDELIS FELIX

Thursday, March 22, 2012

Dr. Mbele Asifia Tiba Aliyopata Dar

Wadau, Prof. Mbele yuko safarini Tanzania.  Ameugua na kwenda hospitalini. Anasema kuwa ameridhika na tiba aliyopata, hakuwa na haja ya kukimbilia nchi za nje kam India kutibiwa.

****************************************

Kutoka  Hapa Kwetu  Blog



Thursday, March 22, 2012

Nimeugua Dar es Salaam; Natibiwa Hapa Hapa, Sio India

Nimeugua Dar kuanzia siku chache zilizopita. Nimejikuta nikiwashwa hasa mikononi, miguuni, na mgongoni. Kwa siku mbili sikuweza kulala usiku. Katika kuulizia watu, nikaambiwa ni "allergy." Na mhudumu mmoja kwenye duka la madawa maeneo ya Sinza aliniambia niende Magomeni, kwenye hospitali ya Dr. Ole.

Nilienda hapo. Wakati wa kuchukuliwa damu ili ipimwe, mpimaji alinipiga mchapo kuwa isije ikawa nimewekewa sumu ya unga. Akazidi kutonya, huku akijifanya ananyunyizia unga mezani, kuwa kaunga kidogo tu kanatosha. Nami nilijibu kuwa mtu huwezi kujua, kwani Bongo haina dogo. Tukawa tunachkea.

Ni kweli daktari alipochunguza ripoti ya upimaji amegundua nina "allergy," na akanielezea sababu zake. Aliniandikia sindano na vidonge vya aina mbali mbali. Alisema kuwa hiyo dozi itafuta kabisa hili tatizo. Nimedundwa sindano jana na vidonge nikaanza. Tayari nimeshaanza kujisikia nafuu. Naendelea vizuri kabisa.

Nimeleta habari hii binafsi kwa sababu maalum. Kwanza, mimi kama m-Tanzania nina imani na madaktari wetu. Ninafundisha Marekani, na ninapougua kule natibiwa kule. Ninapougua Tanzania natibiwa hapa. Tena, miaka yote ya maisha yangu, kabla sijaenda Marekani nilikuwa natibiwa hapa Tanzania, bila matatizo.

Sioni kama kuna tofauti kati ya madaktari wa Marekani na wa kwetu. Kilichopo tu ni kuwa madaktari wa kwetu wapewe mahitaji yanayopasika katika kumshughulikia mgonjwa. Na hilo ni jukumu la serikali, wala isijaribu kukwepa, kwani Tanzania si nchi maskini. Nakerwa ninapowasikia viongozi wa nchi hii wakidai kuwa sisi ni nchi maskini. Juzi hapo nimemsikia waziri kwenye kipindi cha televisheni akitoa huo upupu kwamba Tanzania ni nchi maskini.

Nawashangaa wa-Tanzania waoendelea kuwapigia kura mbumbumbu wa aina hiyo, wasio na upeo kiuongozi, hawana fikra za kuijengea jamii ari ya maendeleo, badala yake wana upeo wa kudumaza na kukatisha tamaa. Nawashauri wajifunze kutoka kwa Rais Obama, ambaye katika mazingira yoyote yale, hawakatishi tamaa raia wake, bali anawahakikishai kuwa Taifa litapambana na litashinda, litafanikiwa. Lakini viongozi wa kwetu, kila kukicha ni vilio kuwa sisi ni nchi maskini!

Uwezo wa kuimarisha hali ya mahospitali yetu tunao, tukizingatia rasilimali nyingi tulizo nazo katika nchi hii. Pia, magonjwa mengi tunayopata hayahitaji daktari bingwa. Yanatibiwa vizuri, iwe ni Marekani au Tanzania. Tena yako magonjwa ambayo ni ya nchi kama zetu, ambayo wataalam wake ni hao madaktari wentu. Mifano ni malaria. Usidhani kuwa ukipata malaria, ukimbilie Marekani. Unaweza ukafia kule, kwa sababu sio madaktari wengi wanaijua malaria na namna ya kupambana nayo kama wanavyojua madaktari wa nchi kama Bongo. Hao madaktari wetu wanasomea magonjwa ya hapa kwetu. Ninavyofahamu, wanapoenda kusomea Ulaya, utakuwa wanasomea "tropical medicine" ambayo ndio uwanja wa mapambano katika nchi kama yetu.

Madaktari wetu wana ujuzi wa hali ya juu, utawakuta wako katika nchi mbali mbali. Ninawafahmu baadhi ambao wako Marekani, katika hospitali mbali mbali, kama vile Mayo Clinic, ambayo ni maarufu sana duniani. Yaani inashangaza kuwa ukienda hizo hospitali, unawakuta madaktari wengi wa kutoka Afrika, yaani madaktari kama hao wanaonyanyasika Tanzania kwa sababu ya viongozi wetu kutokuwa na upeo upasao.

Kwa hiyo, serikali yetu inachopaswa kufanya ni kuwekeza katika huduma za mahospitali yetu hapa hapa nchini. Iweke vifaa na miundombinu, ili madaktari wetu waweze kutumia ujuzi wao ipasavyo. Wakipata vifaa na miundombinu, na wakilipwa ipasavyo, watafanya yale yale ambayo baadhi ya watu nchini wanayatafuta India au ughaibuni. Tunapowapeleka watu nje eti kuchekiwa afya, wakati hizi ni taaluma za madaktari wetu pia, au tunawapeleka watu kutibiwa ugonjwa kama niliopata mimi wiki hii, ambao madaktari wetu wanajua namna ya kuutibu, ni kuwadhalilisha madaktari wetu, na mimi sitalilazia damu suala hilo.

Miezi michache iliyopita, nilipata fursa ya kumsikiliza Dr. Mark Jakobson, ambaye ni mwendeshaji wa hospitali ya Selian, Arusha. Alikuwa akitoa mhadhara Minnesota, kuhusu shughuli za hospitali hiyo. Siku moja nitaelezea katika hii blogu yangu. Jambo mmoja ninalokumbuka ni jinsi alivyowapigia debe madaktari wa ki-Tanzania wanaofanya naye kazi. Anatamani tu angekuwa na uwezo wa kulipa vizuri zaidi, ili wasipate vishawishi vya kwenda sehemu zingine.

Makala hii nimeiandika pia kwa sababu juzi hapo niliandika makala kuhusu mgomo wa madaktari nikaishutumu serikali kwa kudiriki kugombana na madaktari. Kwa hivi, nimejichukulia fursa hii kuelezea zaidi hisia zangu. Kati ya mambo niliyosema ni kuwa kisaikolojia, daktari anapaswa awe kazini akiwa amefurahi na moyo mkunjufu.

Huyu jamaa aliyenipima damu alitoa mchapo na tukacheka. Muuguzi au daktari anapokuwa na moyo mkunjufu na ucheshi, anapokuwa hana msongo wa mawazo, ni baraka kwa wagonjwa. Watafiti wa masuala ya saikolojia ya wagonjwa na matibabu wanathibitisha hilo. Ndio maana niliishutumu serikali kwa kutotambua umuhimu wa kuwaridhisha madaktari.

Saturday, December 03, 2011

Rais wa Guinea Bissau Hoi!

 Ukisikia habari kama hizi ujue hali yake ni mbaya.  Huyo mzee anaumwa kiasi kwamba anashindwa kuongoza nchi yake vizuri kwa vile inabidi aende kwenye matibabu nje ya nchi mara kadhaa. Mungu ambariki na ampe uzima ili aweze kuwaongoza wana Guinea Bissau.


President Malam Bacai Sanha of Guinea Bissau
(AP) - The spokesman for the government of Guinea-Bissau says that President Malam Bacai Sanha has been hospitalized in Paris since Nov. 26.

Aniceto Alves denied rumors on Saturday that Sanha is seriously ill. He said the president left the small West African nation of Guinea-Bissau on Nov. 23 for a medical checkup in Senegal, before continuing three days later to a hospital in Paris.

Alves said that that Sanha went to Paris for a medical checkup that he needs to do every six months in Paris. He said that Sanha did a preliminary exam in Senegal, then continued onto Paris.

Sanha's health has been the subject of intense speculation. Since his election in 2009, he has been hospitalized several times for long stretches in Senegal and Paris with the government always describing the visits as routine checkups.

Sanha is known to be a diabetic.
  

Monday, July 11, 2011

Kisonono sasa haina Tiba!



Wadau, leo kuna habari kuwa kuna aina ya kisonono ambayo haitibiki! Tuombe isiingie Afrika. Huenda umekwishaingia kupitia watalii na malaya! Midume ilizoea ikiambukizwa kisonono basi inaenda kuchoma sindano ya PPF (penicillin), baada ya masaa mnne mambo safi. Haya kama haina dawa mbona kazi ipo! Kwa wanawake wanaweza kuwa na kisonono na wasijue kwa muda mrefu, huko ikiathiri uzazi na wanakuwa na maumivu makali kwenye kiuno. Tumieni kondomu wakati wote! Haya mambo ya kusema, au unatumia kondumu, hunipendi au unficha nini yaishe...la sivyo tutakwisha!

***************************************************************


LONDON (Reuters) - Scientists have found a "superbug" strain of gonorrhea in Japan that is resistant to all recommended antibiotics and say it could transform a once easily treatable infection into a global public health threat.

The new strain of the sexually transmitted disease -- called H041 -- cannot be killed by any currently recommended treatments for gonorrhea, leaving doctors with no other option than to try medicines so far untested against the disease.

Magnus Unemo of the Swedish Reference Laboratory for Pathogenic Neisseria, who discovered the strain with colleagues from Japan in samples from Kyoto, described it as both "alarming" and "predictable."

"Since antibiotics became the standard treatment for gonorrhea in the 1940s, this bacterium has shown a remarkable capacity to develop resistance mechanisms to all drugs introduced to control it," he said.

Mnaweza kusoma habari kamili kwa KUBOFYA HAPA:

Thursday, February 24, 2011

Wanaomba Msaada wa Gharama za Matibabu - Christina Masimba

Christina Alivyo Sasa
Christina Kabla ya Kuugua

Sisi wazazi wa Christina Nasson Masimba, Bw na Bi. Mwinjilist Masimba, tuna ujasiri mbele za MUNGU kukushirikisha/kuwashirikisha hitaji la msaada ili kukidhi gharama za matibabu ya mtoto wetu mpendwa.

Christina ni binti mwenye umri wa miaka 6, akiwa ni mtoto wetu wa mwisho kati ya watatu ambao Bwana ametubarikia. Ni mtoto mchangamfu sana, na anayempenda Mungu wake.

Tangu tarehe 9 Septemba 2009, binti yetu huyo aliugua malaria ambayo inasadikika kupanda kichwani na kumpa shida kubwa katika ubongo wake. Na hiyo imekuwa ndiyo chanzo cha kuugua kwake mpaka sasa. Kufuatia kuumwa huko, Christana alilazwa na kutibiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Kagera (Bukoba Government Hospital) zaidi ya mara tatu. Baadaye Januari 2010, alilazwa pia katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma (Dodoma General Hospital) wakati tukiwa likizo, na kisha akalazwa tena Bukoba Government Hospital, tuliporudi kazini Bukoba baada ya likizo.

Christina katika hali yake ya sasa, akiwa hana furaha tena yakutosha, kutokana na kuugua kwa muda mrefu! Aidha, amelazimika kusimama Shule kwa ajili ya kutibiwa.

Ukweli Christina na sisi wazazi wake tunahitaji sana watu wenye mapenzi mema,(WASAMARIA LUKA 10:25-27) ili aweze kupata huduma ya matibabu ya kumfaa, Pia uone Christina akiwa tayari kwenda shule asubuhi, kabl;a ya kuumwa, alipenda sana kusoma nakufurahia Shule.

Kati ya Aprili na Agosti, 2010 ugonjwa ulizidi kuongezeka na kuonyesha dalili za kupooza baadhi ya viungo vyake upande wa mkono wake wa kuume. Tulijitahidi kwa kila hali kwa maombi na tiba lakini bado hali yake ilizidi kuwa mbaya kadri siku zilivyopita.

Mnamo mwezi Novemba 2010, madaktari wa Bukoba Government Hospital walitutaka twende katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa uchunguzi na matibabu zaidi. Baada ya vipimo na matibabu kwa zaidi ya mwezi mmoja bila mafanikio, madaktari wa Bugando Hospital walitupa rufaa kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili (Muhimbili National Hospital - MNH).

Muhimbili walitupokea tarehe 18 Novemba, 2010 na kumtibu mpaka 21 Desemba, 2010. Walijitahidi kupima kila kipimo walichofikiria na, pale walipohitaji kipimo kilichokuwa hakifanyiki hospitalini hapo, walituelekeza kukipata katika hospitali nyingine nasi tulitekeleza maelekezo yao. Kwa ujumla, vilifanywa vipimo 14 kama vilivyoainishwa hapa chini. Ndipo shida iliyompata alipougua kwa mara ya kwanza ikagundulika.

Vipimo alivyopimwa ni:

CT – Scan (Kichwa).
EEG – (kipimo cha utendaji kazi wa ubongo).
FBP – (kipimo cha damu) Normal.
Sickling test –(Negative).
HB electrophoresis AA.
Echocardiogram (ECG) – normal.
CXR (normal).
Abdominal ultrasound.
LFT (normal).
RFT (normal).
TCD NCA (Middle Cerebral Artery) - both normal.
PT, PTT and INR (all normal).
HIV screening (Negative).
EEG – (consistent with focal seizure disorder).

Hata hivyo, vipimo hivyo na matibabu aliyopatiwa havikuleta ufumbuzi au unafuu katika hali ya Christina, bali hali yake ilizidi kuwa mbaya. Mnamo tarehe 20 Desemba, 2010 MNH walituruhusu (discharge) ili turejee nyumbani kwa kupitia Bugando Referal Hospital kwa kujigharamia, na kututaka turudi hospitalini hapo baada ya muda wa miezi miwili (2) ili waangalie hali yake.

Kwa kuzingatia gharama kubwa za usafiri, na ukweli kuwa hali ya mtoto ilikuwa inazidi kuwa mbaya, hatukuweza kwenda Bugando wala Bukoba. Badala yake, tulipata familia moja hapa Dar es Salaam iliyokubali kutupokea wakati tunaendelea kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya afya ya binti yetu.

Ndipo tulipochukua hatua nyingine ya imani, na kuaza kutafuta jinsi ya kupata matibabu mahali popote. Tuliendelea na huduma za maombezi na matibabu madogo madogo hapa Dar es Salaam na Dodoma. Wakati huo huo, tulianza mawasiliano na hospitali za India ili kuona uwezekano wa kupata uchunguzi wa ziada na matibabu nchini huko.

Hivi sasa nafasi ya matibabu imepatikana katika Hospitali ya Indraprastha Appolo, New Delhi, INDIA.

Mchanganuo wa gharama za safari na matibabu ya Christina katika hospitali hiyo ni kama ifuatavyo:


HITAJI *****BEI**** IDADI ****JUMLA

1 Pasi za Kusafiria ****75,000 ****3 ****225,000
2 Visa**** 150,000 ****3 ****450,000
3 Tiketi ****1,488,000 ****3 ****4,464,000
4 Uchunguzi (siku 7 za mwanzo)**** 8,680,000**** 1 ****8,680,000
5 Makazi nje ya Hospitali (siku ya 8 – 14)***** 1,550,000 ****1**** 1,550,000
6 Matibabu na Makazi (wiki 7 zinazofuata)**** 12,400,000**** 1**** 12,400,000
7 Madeni ya matibabu tangu Disemba, 2010 ****800,000 ****1**** 800,000

JUMLA ZINAZOHITAJIKA

28,569,000/- (T.Shs)

Kiasi hiki ni kikubwa sana kwa uwezo wetu, na tunaomba mchango wako wa kutuwezesha kukidhi gharama hizi. Kwa kadri Mungu atakavyokugusa rohoni, tutashukuru kupokea mchango wako kupitia katika yoyote kati ya akaunti zifuatazo:-

Jina la Akaunti
Benki
Namba ya Akaunti

Nasson Richard Masimba
CRDB
011 205 709 1300

Nasson Richard Masimba
NBC
02 720 108 8567

Nasson Richard Masimba
NMB
318 160 5859

Nasson Richard Masimba
MPESA
076 777 8583

Ahsante sana kwa hatua yako. Tunaamini kuwa, tukinia pamoja, tutapata ushindi na ushuhuda kwa MUNGU wetu.

Bw Nasson R. Masimba na Bi Mariam N. Masimba

Wazazi wa Christina

0784778583, 0715778583, 0767 778583; 0658778583, 0756930810

masimbar2005@yahoo.com
= = = = =

Unaweza pia kuwasiliana nasi au kupata maelezo zaidi kupitia namba zifuatazo, na MUNGU akubariki sana.

Tuesday, March 10, 2009

Inasikitisha

Translation:

Doctor - There is nothing more we can do for the patient. Try to treat him with your love.

Wife - All these hardships and poverty, where will the love come from?

Patient - When you hear talk like that know that you have been buried alive!

**********************************************

Ninakumbuka Bongo miaka ya 80, huko kwenye mahospitali walikuwa wanafukuza wagonjwa ambao wanajua watakufa. Walikuwa wanasema wazi kuwa hawawezi kupoteza dawa kwenye watu ambao watakufa wakati wanaweza kuwapa watakaopona.