Showing posts with label Wazee. Show all posts
Showing posts with label Wazee. Show all posts

Saturday, September 10, 2016

Mkuu wa Mkoa Mwanza Akabidhi Vyakyula Kwa Niaba ya Rais Magufuli Kwenye Kituo cha Bukumbi

To kmwantepele Dotto Mwaibale Mzee Ahmad Michuzi Cathbert Kajuna and 232 more... Message body
Katika kusherehekea Sikukuu ya Idd El Hajj siku ya Jumatatu Septemba 12, 2016, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli, ametoa msaada wa vyakula wenye thamani ya shilingi laki saba na elfu themanini (780,000), kwa ajili ya Kituo cha kulelea Wazee na Walemavu wasiojiweza cha Bukumbi Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.

Akikabidhi msaada huo jana, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, aliuhimiza uongozi wa kituo hicho kusimamia vyema ugawaji wa vyakula hivyo li kuwafikia walengwa, ikizingatiwa kwamba kumekuwa kukiibuka malalamiko kutoka kwa wazee wanaoishi katika kituo hicho kwamba misaada ambayo imekuwa ikitolewa na serikali pamoja na wafadhili mbalimbali imekuwa haiwafikii yote.

Hata hivyo Kaimu Afisa Mfawidhi wa kituo hicho, Georgina Kwesigabo, alitanabaisha kwamba vyakula na misaana ambayo imekuwa ikitolewa na serikali pamoja na wafadhili mbalimbali kituoni hapo, yote imekuwa ikiwafikia walengwa wote isipokuwa kuna changamoto ya baadhi yao kuuza misaada wanayopatiwa ikiwemo vyakula, jambo ambalo linaulazimu uongozi wa kituo hicho kuandaa utaratibu wa kusimamia misaada hiyo hususani kuwapikia chakula wanaoishi kituoni hapo badala ya kuwagawia chakula ili wajipikie wenyewe.

Wazee wanaoishi kituoni hapo waliishukuru serikali kwa msaada huo ambapo walisema wanaendelea kumuombea Rais Magufuli na Serikali yake ili iendelee kuboresha kituo hicho ikiweo kuwekewa uzio ili kuondokana na hofu ya kiusalama waliyonayo kwani wakati mwingine wamekuwa wakiibiwa mali zao ikiwemo kuku ambazo wamekuwa wakizifuga.

Vyakula vilitolewa na Mhe.Rais Magufuli ni, mchele gunia sita (kila gunia kilo 50), mafuta ya kupikia madumu manne (kila dumu lita 20) pamoja na mbuzi wawili.
Baadhi ya wazee wanaoishi kwenye Kituo cha Bukumbi, wakifurahia mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza baada ya Rais Magufuli kuwapatia msaada wa vyakula kwa ajili ya kusherehekea Sikukuu ya Idd El Hajj, itakayofanyika kesho kutwa jumatatu.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella (mwenye kofia), akimsikiliza mmoja wa wazee katika Kituo cha Wazee Bukumbi.
Mmoja wa akina mama kwenye Kituo cha Bukumbi akiishukuru Serikali kwa msaada wa chakula ilioutoa kituoni hapo
Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Mhe.Juma Sweda (kulia), akizungumza wakati wa kukabidhi msaada wa chakula uliotolewa na Mhe.Rais Magufuli katika Kituo cha Wazee Bukumbi wilayani humo. Alisema Serikali inawajali Wazee wanaoishi katika kituo hicho na kwamba ina upendo kwao ndiyo maana inaendelea kuwahudumia.
Kaimu Afisa Mfawidhi wa kituo hicho, Georgina Kwesigabo, alitanabaisha kwamba vyakula na misaana ambayo imekuwa ikitolewa na serikali pamoja na wafadhiri mbalimbali kituoni hapo, yote imekuwa ikiwafikia walengwa wote isipokuwa kuna changamoto ya baadhi yao kuuza misaada wanayopatiwa ikiwemo vyakula, jambo ambalo linaulazimu uongozi wa kituo hicho kuandaa utaratibu wa kusimamia misaada hiyo hususani kuwapikia chakula wanaoishi kituoni hapo badala ya kuwagawia chakula ili wajipikie wenyewe.
Vyakula vilivyotolewa na Mhe.Rais Magufuli kwa ajili ya Makao ya Wazee na walemavu wasiojiweza Bukumbi, Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.
Huyu mbuzi, tehe tehe tehe!!
Makao ya Wazee na walemavu wasiojiweza Bukumbi, Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.
Imeandaliwa na George Binagi-GB Pazzo wa BMG

Wednesday, April 16, 2014

Kumbe Wazee bado Wamo!

Jamani, jamni hebu tuach ule tabia ya kuanika wazee juani na eti kutokurushu hata kucheza ngoma!  Huyo Bi Kizee anafanya vijana waone haya kwa kipaji chake cha kucheza ngoma!

Monday, October 14, 2013

Midume Haitosheki!

Hivi, kwa nini midume haitosheki kwa ngono hata ikizeeka? Babu inaona nyuma lakini inataka kuona mbele pia! Khaa!

Sunday, July 28, 2013

Story ya Wazee Kusubiri Kufa

 Na Nape Nnauye

Nimestushwasana na stori ya gazeti la Mtanzania inayodai kuninukuu kuwa nimesema wazee waliopendekeza serikali tatu wanasubiri kufa!

Kwa kweli nimesikitishwa sana hata na jinsi maneno ndani yalivyopangiliwa kiasi kwamba inanipa tabu kuamini kama mhariri aliipitia hii stori ukiachilia mbali kama aliyetumwa kuja kuandika stori alikua ni "too junior".

Nawaheshimu sana wazee wangu hawa hata kama nikipishana nao kimawazo siwezi kufikia kutamka maneno makali kiasi hicho.

Nilichosema ni kuwa ukilinganisha vijana na wazee, vijana wanawajibu mkubwa wa kuamua kesho yao badala ya kudhani kuna mtu atawaamulia. Hivyo wanawajibu mkubwa kwani takwimu zinaonyesha asilimia 60% ya idadi ya watu nchini ni vijana! Sasa sijui kama kwa mwandishi na mhariri wake tafsiri ndio hiyo?!!!
Imenisikitishasana!

Nape Moses Nnauye
The CCM Secretary for Ideology & Publicity

Mh. Nape Nnauye

Tuesday, April 24, 2012

Thursday, February 23, 2012

Bibi Arusi Ana Miaka 100, Bwana Arusi Ana Miaka 87! Kweli Kabisa!

Duh! Naona Cougar wa miaka 100 kaolewa leo na kijana  mwenye miaka 87 huko Kentucky.  Wanaarusi wanaishi katika nyumba ya wazee na walikutana huko.   Ni kweli mapenzi yakinoga unajisikia kijana.  Bibi Dana Jackson (100) anasema kuwa anajiona kama ana miaka 50 tu! Nawatakia maisha mema ya ndoa! 

Congratulations Mr. & Mrs. Strauss!

***************************************************

(Dana Jackson & Bill Strauss)
Woman Weds on Her 100th Birthday


By Bridal Guide

On February 6th, Dana Jackson celebrated a century of life with about 100 of her nearest and dearest at the Rosewood Health Care Center in Kentucky. An ice cream cake in her honor was frosted with the special message, "Congratulations, you are never too old." But this wasn't your average birthday party, not even for a centenarian: Jackson decided to mark the momentous occasion by marrying boyfriend Bill Stauss, 87.

Stauss never imagined that he would ever wed again, since his previous marriage lasted 55 years. However, Jackson was the exception: "I found one that's just as nice as can be. Treats me good. Like a human being should be treated. It's rare to find a girl like that."

"I feel 50," Jackson told BG Daily News. "I don't feel 100."

This was Jackson's third trip down the aisle, but the first time she wore an engagement ring and traditional gown. Her first wedding took place when she was only 15 years old. She marveled at how much has changed since then: "Gettin' married wasn't a big thing back when I was young. It wasn't no big thing...it was just simple, you know? Just simple...we wore clothes and maybe a bouquet cut out of the yard. It's not what you got, it's what you make out of a marriage," she said.

Jackson's message is timeless, and in the AARP video below, her happiness is infectious, just as with any other bride. But marrying at 100 does have its challenges: The couple sipped grape juice in lieu of cocktails and Stauss had trouble seeing his wife walk down the aisle. The moment didn't disappoint-the husband thought his wife looked "beautiful" when he finally got a closer look.

Kuona Video ya Arusi BOFYA HAPA:

Monday, February 20, 2012

Bi Kizee Amuenzi Whitney Houston Kwa Ngoma!


.
Hebu cheki huyo bibi wa kizungu mwenye miaka 90 anayocheza ngoma. Hii kacheza kuonyesho upendo wake kwa marehemu Whitney Houston. Anasema amefariki dunia mdogo mno. Huyo bibi anasema alikuwa kipenzi cha muziki wa Whitney.

REST IN PEACE WHITNEY HOUSTON.

Lakini jamani hii iwe fundisho kwa sisi waafrika. Tunamwona bibi mwenye umri mkubwa ni wa kuanika juani tu!. Kumbe bado wamo!

Saturday, July 02, 2011

OMBI KWA WAZEE WATARAJIWA WOTE - Tangazo

(Tandika Kilalakala - Wakina mama waliokusanyika sehemu moja kupata misaaada. wengi wao wana ulemavu wa kutembea, hawana kipato na mmoja ana wajukuu wawili walioachwa na wazazi wao)

( pichani - Magomeni Mzee Simba Maduwilo kwa sasa mlemavu wa miguu, na mkewe hali yake ya afya sio nzuri. Wanaishi kwa kumtegemea binti yao anaejishughulisha na mama lishe.)


Kwa mara nyingine tena TUSHIKAMANE PAMOJA FOUNDATION imetembelea wazee wanao ishi katika mazingira magumu na kutoa misaada mbali mbali.

TUSHIKAMANE PAMOJA FOUNDATION tunaomba watu watakaoguswa na watakaopenda kusaidia kikundi hiki kiendelee kutoa misaada kwa wa lengwa, tupigieni simu 0787 558550 au 0787 177077 au 0784 265560 au 0784 950250 Tunapokea nguo mitumba isiochakaa saaana, vifaa vya nyumbani, mashuka, vyakula vikavu, kama, unga, mchele, sukari, Mmaharagwe, majani ya chai n.k...

Bado wapo wazee wengi hatuja wafikia. Lengo letu ni kuwapa angalau vyakula kidogo mwezi mara moja.... TUSHIKAMANE PAMOJA TUFIKISHE MALENGO YETU.

Friday, May 06, 2011

Bwana Arusi ana Miaka 100, Bibi Arusi Miaka 90!

Africa ukifika miaka 40, basi wewe mzee! Ukifikisha 70 basi unstahili kutotelewa nje na kuanikwa juani. Huna thamani tena. Mapenzi, ndo usahau kabisa, unabakia kukumbuka katika ndoto zako ujana wako!

Hapa Marekani, wazee Forrest Lunsway (100) na Bi Rose Pollard (90), wamefunga ndoa. Hebu cheki nyuso zao za furaha, mapenzi motomoto! Inasemekana wamevunja rekodi ya umri wa wafunga ndoa. Doh! Wamejuana karibu miaka 28. wote wanakaa kwenye nyumba ya wazee. Nawatakia maisha mema ya ndoa. Kumbe hata ukiwa na miaka bado wamo! Ila Zaeni matunda mema haifia kusemwa hapa.
***************************************************************************



(pichani wanaarusi Forrest (100) na Rose (93))


Kutoka YAHOO.COM

For some people, it's never too late for love.

That's certainly the case for Forrest Lunsway and Rose Pollard, an Orange County, Calif. couple who were married this March 19, Forrest's 100th birthday. With a combined age of 193--Rose is a spring chicken--they're believed to be the world's oldest newlyweds.

A spokesman for the Guinness Book of World Records said they had been informed of the wedding and are set to verify it as a record. For 27 years, Forrest smoked a pack of cigarettes a day, and he still drinks the odd glass of wine or whiskey and 7-Up, he said in a recent interview with the The Daily. He attributes his longevity to never having had a desk job: He spent his youth trapping animals and selling their fur in Kansas before moving to California, where he worked as a pipe welder.

You can watch a video of them here.

Both Forrest and Rose had been married before, but were single when they met back in 1983 at a senior's dance. Though they soon started dating, wedding bells seemed unlikely.

'I told him up front I had no intention of getting married," Rose said. "But then one day he asked me 'how come we never got married? and I said 'because you never asked me.'"

''So he got down on one knee and said, 'Well I'm asking you now, just set the date.' I told him, 'I'll marry you on your 100th birthday.' And I did."

And being on the older side, the couple also has some wisdom to share on how to make a marriage work. Rose, 93, told The Daily: 'Take your time and get to know one another. Get to know if you like all the things that person stands for. ... Be forgiving and patient and say I love you once in a while."

Rose also told The Daily that their advanced age means that she and Forrest don't have many of the anxieties that can be a challenge for other newlyweds. "That's one of the things we can forget about--time. Because time doesn't mean that much."

And it's time well spent together: They both love ballroom dancing, and they want to kayak in Alaska and walk the coast of California.

"We've got many happy years left as I intend to stick around until I'm at least 110," Forrest said. "You've got to use it or lose it."
(The Daily)

Tuesday, March 15, 2011

Mimi katika Mchezo- 'The Vagina Monologues'

Washiriki wa Boston Community Production of The Vagina Monologues 2011

Wikiendi iliyopita nilishiriki katika Mchezo wa Kuigiza, The Vagina Monologues (Maongezi ya Uke ..nishahishe kama nimekosea kutafsiri).

Kila mwaka vikundi vya wanawake hapa Marekani na nchi nyingi duniani wanasoma na kuigiza huo mchezo mwezi Machi. Hela wanazopata kutoka kwenye viingilio na mauzo ya chakula zinakwenda kusaidia vyama, mashirika yanayosaidia akina mama. Machi ni mwezi ya Wanawake duniani.

The Vagina Monologues ni hadithi fupi mbalimbali zinazotokana na mahojiano aliyofanya Bi Eve Ensler na wanawake kadhaa kuhusu nyeti zao. Kulikuwa na maongezi ya Bi Kizee, Shoga, Mke, Uke uliyokasirika, Mwanamke aliyedhani kapoteza kiharage chake, Kubalehe, Kubakwa, Kutairiwa, na mengine.

Kwa kweli nimetokea kufurahia huo mchezo na hata wanaume niliyowaalika waliyoenda wameipenda sana. Imewafanya wafikirie haki za akina mama na pia jinsi akina mama wanavyoona maswala kama uke zao, ngono, kunyanyyawa kijinisia.

Tanzania kuna hadithi nyingi sana ambazo zinaweza kuingizwa katika huo mchezo.

Mnauliza niliongelea nini? Nililionogelea uzazi, jinsi mwanamke anavyokuwa na uchungu katika uzazi na jinsi uke unavyofunguka ili mtoto atoke.

Tuesday, January 13, 2009

Bikira wa Miaka 107 Anataka kuolewa huko China!!

Leo ni siku ya mabikira!

Huko China, Bi Kizee Wang Guiying (107) anasema anataka kuolewa kwa mara ya kwanza katika maisha yake. Anasema pia bado ni bikira.

Bi Wang, anasema kuwa alikuwa mwoga wa kuolewa kwa vile aliona wanawake walioolewa wakipigwa na waume zao. Alisema hakutaka maisha ya hivyo, hivyo alikuwa na shamba na aliamua maisha yake itakuwa ni ya kulima.

Ila sasa anakaribia kuwa na miaka 108 na amekuwa mpweke. Anasema kuwa sasa anataka mwanaume wa kukaa naye. Yuko tayari kumkubali kijana wa miaka 90 au hata 100! Huko China wasamaria wema wanamtafutia mume huko kwenye nyumba za wazee.

Na kuna watu wamesema itakuwa vigumu kwa Bi Wang kupata mume maana hao wazee wenye miaka 90 wanatafuta maspring chicken wenye miaka 70!

Kwa habari zaidi someni:

http://chattahbox.com/curiosity/2009/01/12/107-year-old-woman-seeks-husband/

http://www.telegraph.co.uk/news/worldnews/asia/china/4222884/Woman-107-seeks-husband.html

http://newsblaze.com/story/20090112100351reye.nb/topstory.html

Monday, January 05, 2009

Mtu Mzee Kuliko Wote duniani sasa ni Mmarekani Mweusi

Mwezi November mwaka jana, mtu mzee kuliko wote, Bibi Edna Parker, alifariki huko Indiana, USA akiwa na miaka 115!

Leo wataalam wametangaza kuwa Bibi Gertude Baines (pichani), mwenye miaka 114 ni mtu mzee kuliko wote duniani. Bibi Baines, ni mtoto wa watumwa. Alizaliwa mwaka 1894 huko Atlanta, Georgia.

Kwa sasa anakaa Los Angeles,California kwenye nyumba ya wazee.

Ni baraka kuweza kuishi muda wote huo tena katika karne tatu! 1800's, 1900's, 2000's. Ila wakati mwingine nafikiria kuna wakati utakuwa mpweke hasa ukifikiria watu wote uliokuwa unawafahamu wamekwisha kufa.

Hivi huko Afrika hakuna watu wenye umri mkubwa hivyo? Maana naona hao wataalam wanachunguza nchi zilizoendelea na hata siku moja sijasikia walienda Afrika kuchunguza.

Namtakia Bibi Baines, maisha marefu zaidi. Mungu amlinde.

Na kitu kingine, hapa Marekani kuna usemi "Black Don't Crack!" yaani ngozi nyeusi haivunjiki. Wana maana kuwa watu weusi hawazeeki kama wazungu ambao ngozi yao inasinyaa vibaya.

Wadau, kama mnafahamu watu wenye umri mkubwa zaidi ya miaka 100 hebu tutoe ripoti kwa hao wanaojiita watalaam wa umri waingie kwenye record books.

Najua watu wanatania, au kuna mzee fulani asubuhi tunamtoa na kumanika juani. Je, ana miaka mingapi?

GOD BLESS YOU MS. BAINES!

************************************************************************

LOS ANGELES, California (CNN) -- Gertrude Baines, ma 114-year-old California resident, will likely be crowned the world's oldest woman, according to the organization that keeps track of such honors.

Gertrude Baines told CNN two years ago that she has taken good care of herself, "the way (God) wanted me to."

The previous oldest woman was Maria de Jesus, who died this week in Portugal at age 115, Guinness World Records said.

Baines -- born to former slaves in a small town south of Atlanta, Georgia, in 1894 -- now lives in a Los Angeles nursing home.

Baines appeared cheerful and talkative when the Los Angeles Times interviewed her in November as she cast her vote for Barack Obama for president, whom she said she supported because "he's for the colored people."

"I'm glad we're getting a colored man in there," she said.

Baines apparently prefers using the older term for her race. She was well into her 70s when "African-American" became the common reference in the United States. Watch Baines speak to CNN
She told the Times she spends most of her time "doing nothing but eating and sleeping."
When CNN interviewed Baines two years ago, she was asked to explain why she thought she has lived so long.

"God. Ask him. I took good care of myself, the way he wanted me to," Baines said.
Her only child, a daughter, died of typhoid fever at age 18.

Much of her long life was lived in Ohio, where she worked as a "house mom" at a state university. She eventually divorced and traveled to Los Angeles, where she retired.
Baines will not officially be given the title until after Guinness World Records completes an investigation, the organization said.

"Maria was crowned the world's Oldest Living Woman by Guinness World Records on 28 December upon the death of Edna Parker," the group said.
Parker -- an American -- was 115 years, 220 days old when she died November 26, 2008, in an Indiana nursing home, it said.

********************************************

KAMA MNA HABARI ZA WAZEE WENYE UMRI MKUBWA TAFADHALI WASILIANA NA GUINESS BOOK OF RECORDS:

http://www.guinnessworldrecords.com/member/how_to_become_a_record_breaker.aspx

Thursday, October 30, 2008

Wazee Wastaafu Wafunga Njia Dar - Wakubwa Hakuna Kupita!


Hii ni aibu kwa serikali! Hebu walipe hao wazee hela yao! Kuwalipa ni sawa na kununua shangingi ngapi?
********************************








Picha hizi ni mazingira yalivyokuwa siku ya mgomo wa staili yake wa wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo ilivunjika mwaka 1977. picha hizi ni kwa hisani ya Jackson Albart wa kampuni ya Ladyband.
**************************************************

Saturday, August 09, 2008

Tendo la Ndoa Uzeeni




Wadau, niliwahi kuposti mada hapa aliyoandika Kaka Lazarus Mbilinyi inatiwa 'Mawaidha Kuhusu Ndoa'

Sasa ameandikia kuhusu tendo la ndoa uzeeni.

Nadhani wengi tunadhani kuwa ukifikisha umri mkubwa ndo basi unaaga ngono/tendo la ndoa. Hiyo wazo inatia watu kiwewe. Kumbe wala, bado wamo! Asante sana kaka Mbilinyi kwa kuelimisha jamii kuhusu ngono tendo la ndoa. Natumaini watu hawatogopa kuzeeka sasa.

*******************************************************************
Na Lazarus Mbilinyi

Je, wazee wenye umri mkubwa bado huwa hamu kubwa ya tendo la ndoa? Utafiti wa sasa unaonesha kwamba jinsi mtu anavyozidi kuwa mzee uwezo wa kuonja, kunusa, kusikia na kuona hupungua. Pia uwezo wa kusisimuliwa kwa kuguswa hupungua pia.

Kiasili uwezo wa kusisimuliwa kimapenzi na uwezo wa kufanya tendo la ndoa pia hupungua (libido)Pia Utafiti unaonesha kwamba uwezo wa kufanya mapenzi huweza kupunguza kutokana na umri kuwa mkubwa ingawa pia umri kuwa mkubwa hauwezi kuzuia kabisa hamu ya tendo la ndoa (terminate).

Kuna ripoti kwamba wanaume na wanawake wenye umri wa miaka 50 hadi 80 bado wana hamu kubwa ya kufanya mapenzi (libido) na si kufanya tu bali kufurahia mno tendo lenyewe.

Kuna imani potofu nyingi kuhusiana na tendo la ndoa katika umri mkubwa zifuatazo ni baadhi tu ya hizo imani; Kushindwa kushiriki tendo la ndoa ni matokeo ya umri kuwa mkubwa.Tendo la ndoa ni hatari kwa wazee wenye umri mkubwa. Uwezo au hamu ya tendo la ndoa (libido) hupungua kwa kadri mtu anavyozeeka.

Yote hapo juu si sahihi kabisa. Hizo imani potofu zipo kwa muda mrefu na zimekuwa zikisababisha watu wenye umri mkubwa (wazee) kushindwa kufurahia tendo la ndoa au uumbaji wa Mungu.

Je, mabadiliko ya mwili kwa wanaume wazee huathiri vipi tendo la ndoa?

Kawaida wanaume wazee huhitaji muda mrefu ili kuweza kusisimka.

Kile kilichokuwa kinahitaji sekunde chache hadi dakika chache katika umri wa miaka 19 huhitaji zaidi ya dakika 15 katika umri mkubwa kwa mwanaume.

Wanaume wengi wenye umri mkubwa hupona ugonjwa wa Kukosa uwezo wa kufanya tendo la ndoa kwa kujifunza matokeo na athari za umri kwenda sana (Uzee) Katika umri ulioenda wanawake wazee wahahitaji kufahamu kwamba wanaume wazee huhitaji muda mwingi na wakutosha kuuandaa jogoo awike.

Mabadiliko mengine ambayo hutokea kwa mwanaume mzee sana ni kupotea kwa uwezo wa kufika kileleni tofauti na wakati akiwa kijana.

Hii ni kutokana na Kukosa hisia (sensation) za tendo la ndoa. Pia kiwango cha sperms anazotoa hupungua hivyo mwanamke mzee asiwe na mtazamo wa kudhani kuwa uwingi wa sperms ndio uzuri wa tendo la ndoa.

Mnaweza kumtembelea kwenye Blogu yake: http://www.mbilinyi.blogspot.com/