Showing posts with label Neema Mushi. Show all posts
Showing posts with label Neema Mushi. Show all posts

Friday, August 08, 2008

Wafukua Kaburi la Neema Mushi!

( Picha Asante Hellen Mlacky -Habari Leo)

Wadau, mnakumbuka majuzi niliposti habari ya binti Neema Mushi kufufuka? Alirudi kijijini na kusema hawajahi kuugua kwa muda mrefu na alikuwa anaishi Tanga na ndugu zake. Sasa ni ktendawili....nani alizikwa kwenye kaburi hilo? Na huyo aliyedai ni Neema Mushi hapo mwanzo ni nani?

**************************************************


MAMIA ya wakazi wa mkoa wa Kilimanjaro leo walifurika katika kijiji cha Nkuu Sinde wilayani Hai mkoani Kilimanjaro kushuhudia ufukaji wa kaburi ambalo miaka mitatu iliyopita lilizikwa binti mmoja ambaye amerejea kijijini kwake akiwa mzima.

Uwepo wa binti huyo akiwa mzima huku jamii ikifahamu kuwa amekufa kulifanya familia kutafuta njia ya kuliondoa kaburi hilo lenye jina la binti yao Neema Mushi ambaye ndiye waliamini wamemzika.

Wafukuaji walitoa jeneza na kukuta mabaki ya mwili wa binadamu ambaye hata hivyo hakuweza kutambulika kwa kuwa alipoletwa kuzikwa hapo na shangazi mtu aliaminika ni yeye Neema Mushi.

Swali linabaki huyu binti aliyezikwa ni nani?Awali ilidaiwa kuwa Neema ambae ni mkazi wa Machame wilayani humo baada ya wazazi wake wote kufariki aliondoka mkoani Kilimanjaro na kwenda kuishi Tanga kwa bibi yake mzaa mama pamoja na mama zake wadogo.

Katika hali ya kushangaza ilidaiwa kuwa mwaka 2004 shangazi yake Neema aliyefahamika kama Mama Peter ambaye ni mfanyabiashara Namanga alipewa taarifa na wenzake kuwa kuna mtoto aliyefika katika eneo lake la kazi na kudai ni ndugu yake na kuahidi atarudi siku nyingine baada ya kumkosa.
Ilielezwa kuwa Neema alirudi tena siku nyingine na kumkuta shangazi yake ambapo alijitambulisha kuwa ni mtoto wa marehemu kaka yake aliyeitwa Eliapenda Mushi na kwa kuwa shangazi yake hakumuona kwa muda mrefu alimpokea na aliamini hivyo na wakaishi nae.
Baada ya kuishi nae mwaka 2005 ilidaiwa binti huyo alianza kusumbuliwa na kifua ambapo shangazi huyo alimuuguza na ilipofika Septemba 5 mwaka 2005 alifariki dunia na kutokana na aneo alilokuwepo kushindwa kuuuhifadhi mwili huo aliwasiliana na ndugu zake waliopo Machame ambapo walifanikiwa kuuzika mwili huo Septemba 7 mwaka 2005.
Katika hali ya kushangaza na hisia za Neema zikiwa zimetoweka katika vichwa vya watu wakiwemo ndugu zake, binti huyo alirejea kijijini kwao Machame kwa bibi mzaa baba Julai 19 mwaka huu majira ya saa 11 jioni.
Kwa upande wake Neema alipohojiwa alidai kuwa hajawahi kufika Namanga na wala hajawahi wadogo. kuugua kwa muda mrefu na siku zote alikuwa akiishi Tanga kwa bibi yake na mama zake.

Habari na mdau wa kaskazini .

Monday, July 28, 2008

Neema Mushi Afufuka!

Wadau, hivi huyo binti ni huyo huyo Neema Mushi au ni mwingine? Shangazi yake anadai kuwa alimfia mikononi mwake. Neema mwenyewe anasema hakufa ila alikuwa anakaa Tanga.

***********************************************************
Kutoka ippmedia.com

Mtu adaiwa kufufuka

2008-07-28

Na Patrick Chambo, PST Hai

Mamia ya wananchi katika Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, wameshikwa na butwaa baada ya kumuona msichana aliyedaiwa kufariki dunia takriban miaka mitatu iliyopita akiranda randa mitaani.

Tukio hilo la aina yake, lilitokea katika kijiji cha Machame Mkuu, mkoani Kilimanjaro na msichana huyo anayedaiwa kufa na baadaye kukutwa akitembea mitaani ametajwa kuwa ni Neema Mushi, mkazi wa kijiji hicho.

Aidha, habari zilizopatikana kijijini hapo zilisema kuwa, binti huyo alisema kuwa alikuwa akiishi Tanga. Mchungaji Elimfoo Mushi wa Usharika wa Machame Mkuu, alisema ndiye aliyeendesha ibada ya kumuombea Neema ambaye mwili wake ulifikishwa kanisani hapo.

Akizungumza na PST, Neema alisema kuwa kweli hilo ni jina lake, lakini alikanusha kuwa alikufa na kuzikwa na badala yake alikuwa akiishi Tanga. Alisema eneo alilokuwa akiishi ni siri yake na kwamba akiwa huko alisikia kuwa alikufa na kuzikwa mwaka 2005. ``Mimi sijui kitu, najua nilikuwa naishi Tanga ?na wala siwaambii nilikokuwa naishi. Nimeshangaa narudi watu wanakimbia hadi nilipopelekwa polisi, wakaja ndugu zangu wakanitambua kuwa eti mimi nilikuwa marehemu,`` alisema.

Shangazi wa Neema, Bi. Liliani Mushi, alisema ndiye aliyemuuguza Neema hadi umauti unamfika na kusafirisha mwili wake hadi kijijini hapo na kuzikwa kwenye makaburi ya kanisa. ``Kweli mimi nimeokoka na sali Kanisa la Ephata, huyo mtoto alinifia mikononi huko Namanga nilikokuwa naishi naye nimeshangaa kuambiwa eti njoo umuone Neema, amekuja Machame kutoka Tanga, nilichoka, hakika huu ni muujiza wa Mungu watu wanasema kuwa eti ni msukule, mimi siamini, ninachojua alinifia tukamzika. Huyu hapa muulizeni wenyewe katoka wapi,`` alisema shangazi huyo.

Naye Mchungaji Mushi alisema, ``nasema nijuacho mimi ni kuwa huyu ndiye Neema ambaye msukule, mimi sijui,`` alisema. Polisi wilayani Hai, wamekiri kuchukua maelezo ya Neema, mwili wake uliletwa hapa kanisani na tukauzika makaburini, kwamba ni muujiza wa Mungu au wazazi, Mchungaji na ndugu wengine walioshiriki katika mazishi.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa mkoa Bw. Lucas Ng'ohoko, hakuweza kupatikana kuzungumzia sakata hilo. Aidha, ndugu na jamaa wa Neema wako kwenye harakati za kupata kibali cha polisi ili waweze kufukua kaburi hilo.

SOURCE: Nipashe