Showing posts with label Torture. Show all posts
Showing posts with label Torture. Show all posts

Friday, November 21, 2014

Amsulubu Aliyemwibia Mume Wake!



Wadau, hii kali! Wanawake wote wangesulubu wanaowaibia wanaume wao hivyo, wizi huo ungepungua sana!

Monday, March 18, 2013

Utekaji watu Tanzania: Baada ya Kibanda Nani Atafuata?


Wadau,  hivi karibuni yametokea matendo ambayo hatjuazaoea kusikia Tanzania. Waandishi wa Habari, Viongozi wa Dini kutekwa, kuteswa na kuuawa!  Gazeti la Mwanachi inachambua.

************************
Kutoka Gazeti la Mwananchi

Posted Jumatatu, Marchi18 2013

Kwa ufupi

Ni matukio ambayo yameacha maswali mengi zaidi ya majibu, huku wengine katika jamii wakisaka mchawi. Polisi na hata vyama vya kijamii, kila mmoja akiibuka na msimamo wake. Hata hivyo, si rahisi kusema ni lini jibu litapatikana!

Padri Auawa Zanzibar kwa Risasi

Tukio lingine ambalo lilishtua wengi ni la kuawa kwa Padri Evarist Mushi, Paroko wa Parokia ya Minara Miwili , Zanzibar. Yeye, aliuawa kwa kupigwa risasi kichwani na kufa papo hapo na watu wasiojulikana asubuhi akielekea kanisani.

Msemaji wa Polisi Zanzibar, Inspekta Mohamed Mhina alithibitisha tukio hilo huku akisisitiza kuwa uchunguzi wa kina zaidi ungefanyika kuhakikisha waliofanya hilo wanachukuliwa hatua.

Mwingine Apigwa Risasi

Awali, Kabla ya kuuawa padri Mushi, padri mwingine, Ambrose Mkenda naye alipigwa risasi na watu wasiofahamika kwenye lango la nyumba yake maeneo ya Kitomondo mjini Zanzibar, ambako ndiko makazi yake yalipo akiwa ndani ya gari aliyokuwa akiendesha pekee yake.

Hali yake siyo nzuri kwani risasi aliyopigwa imemdhuru maeneo ya mdomoni na hadi sasa bado hajaweza kuwa imara. Waliompiga risasi padri huyo inasemekana ni watu waliokuwa kwenye pikipiki, ambao walimvamia akisubiria afunguliwe geti kuingia nyumbani kwake.

Katibu wa Mufti Amwagiwa Tindikali

Pia Zanzibar ilikumbwa na tukio la linalofanana na matukio hayo kwani kiongozi mwingine wa dini aliingia kwenye msukosuko.

Katibu wa Mufti wa Zanzibar, Sheikh Fadhil Suleiman Soraga, alimwagiwa tindikali na watu wasiyojulikana huko Magogoni Msumbiji Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar.

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Yussuf Ilembo, alisema Sheikh Soraga alimwagiwa tindikali majira ya alfajiri alipokuwa akifanya mazoezi ya viungo.

Ni kwamba wakati akifanya mazoezi, alimuona mtu akifanya mazoezi akielekea mbele yake na baada ya kukutana uso kwa uso alimmwagia tindikali na kumjeruhi sehemu za usoni na kifua kabla ya mtu huyo kutoweka.

Dk Stephen Ulimboka

Kiongozi wa jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Stephen Ulimboka, saa sita usiku alitekwa, kupigwa na watu watatu wenye silaha na kisha kutupwa maeneo ya mabwepande ambapo aliokotwa na kupelekwa katika Taasisi ya Mifupa (MOI) jijini Dar es Salaam.

Wengi wanahoji sababu ya kutekwa Dk Ulimboka, hasa kutokana na ukweli kwamba si mfanyabiashara…Nani alimteka kwa lipi? Ni swali lisilo na jibu.

Dk Ulimboka aliwahi kuwaambia waandishi wa habari na baadaye akasisitiza kauli hiyo kupitia wanasheria wake, Oktoba 2012, kuwa aliyehusika na mipango ya kutekwa na kuteswa kwake ni Ofisa wa Ikulu. Kama ni kweli, je, ofisa huyo alitumwa au alijituma ? Na je, aliwahi kuhojiwa polisi ili Ikulu ijisafishe kutoka katika madai haya ya Dk Ulimboka?

Waandishi wa Habari Wauawa

Baadhi ya waandishi wa habari waliouawa katika mazingira ya utata ni pamoja na wa Kituo cha Redio Kwizera wilayani Kakonko mkoani Kigoma, Issa Ngumba (45) ambaye aliuawa kwa kunyongwa na kisha kupigwa risasi mkono wa kushoto.

Mwili wake ulipatikana katika pori la Mlima Kajuluheta Kijiji cha Muhange, wilayani humo asubuhi baada ya wananchi kufanya msako wa siku tatu mfululizo bila mafanikio.


Lakini, pia vitendo kama hivyo vinawakuta wenye ulemavu wa ngozi ambao wengi wameathirika , lakini waliohukumiwa kunyongwa tangu mwaka juzi mpaka sasa hawajanyongwa.

Richard Masatu Auawa

Richard Masatu aliuawa Agosti 2011. Yeye, alikuwa Mkurugenzi wa gazeti la KASI MPYA, alifia Hospitali ya Mkoa ya Sekou Toure mjini Mwanza, akipatiwa matibabu. Taarifa za awali zinaonyesha kuwa marehemu alifariki kutokana na majeraha ya kushambuliwa na watu wasiojulikana.

Thursday, March 07, 2013

Tanzanian Journalist Absalom Kibanda Sent to S.A. for Treatment

From THE CITIZEN NEWSPAPER, TANZANIA

By Abela Msikula


The Citizen CorrespondentDar es Salaam.

Tanzanian Vice President Mohamed Gharib Bilal Visits the Injured Mr. Kibanda

As the manhunt for the two individuals who violently assaulted seasoned journalist Absalom Kibanda Tuesday night moves into higher gear, the firebrand chairman of Tanzania Editor’s Forum (TEF) has had to be flown to South Africa for specialised medical care. The journalist, who is also the group managing editor for New Habari Corporation, was grievously wounded following a vicious attack as he came home from work right outside his house at Mbezi Juu in Dar es Salaam. He suffered serious injuries to his left eye. His assailants also knocked several teeth off him and hacked off a finger on his left hand. Just before he was flown out, the TEF chair told local reporters he believes the incident has something to do with his work as a journalist.

After the incident, Mr Kibanda was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH)’s Orthopaedic Institute (Moi), where doctors referred him to a South Africa hospital for further treatment.

The Citizen witnessed him being airlifted at Julius Nyerere International Airport. He left aboard Flight Link around 4pm.

Following these brutal events, the Inspector General of Police, Mr Said Mwema, has assigned four detectives from the Police Force headquarters to beef up investigations into what happened that fateful night, but no arrests had been made when we went to press yesterday.

However, Dar es Salaam Special Police Zone Commander, Mr Suleiman Kova, and Kinondoni Regional Police Commander, Mr Charles Kenyela, said they had formed a joint investigation team to look into the matter.

A statement by minister of Home Affairs Emmanuel Nchimbi said IGP Mwema’s decision is meant “to increase efficiency.” At JNIA, Mr Kibanda shared the harrowing details of Tuesday’s events with the local press.

“I was approaching the gate of my home at midnight. While I was waiting for my gate keeper to open it, two people approached my car and smashed the window screen.”He went on: “As I was trying to escape through the passenger’s door, they grabbed me and began hitting me.” The assailants, he said, attacked him with heavy tools and sharp metals.

“I heard the third person who was off my sight encouraging his colleagues to shoot and finish me…but the two were resisting. An interesting thing is that, they were addressing each other by a title ‘afande’[literally translates ‘Sir’] normally used by police officers,” he noted.

He said when the gatekeeper opened the gate and saw what was happening, he called for help, and the attackers fled.Dr Nchimbi’s statement said Mr Kibanda was found about 30 metres from his car. Nothing was taken from him despite the fact that he had two cellphones and a laptop in his vehicle.

He becomes the fifth journalist to be attacked within the past six months. Two journalists were killed and three others were seriously harmed during this short period.

In September last year TV reporter David Mwangosi was killed by the police in Iringa as he covered a political rally. In January this year Issa Ngumba – a Kakonko-based correspondent with Radio Kwizera –was found dead in the forest with bullet wounds in his body.

Last November, an editor working with Business Times Limited, Mr Mnaku Mbani, was shot and seriously injured by suspected robbers who were attempting to hijack the vehicle he had hired for the day. The following month Shabaan Matutu, a journalist with Free Media Group, was shot in his home by the police in what law enforcement called ‘a case of mistaken identity.’

Mr Kibanda was scheduled to appear in court yesterday as part of an ongoing treason case against him and two others: former group managing editor for Mwananchi Communications Limited (MCL) Theophil Makunga and Tanzania Daima columnist Samson Mwigamba.

They are alleged to have published a “seditious” article in 2011. Following this violent assault on Mr Kibanda, the Kisutu Resident Magistrate’s Court adjourned the case to March 26.

(Additional reporting by Rosina John and Bernard Lugongo)

Local journalists help carry TEF chairperson Absalom Kibanda onto his SA-bound medical flight after he was violently assaulted outside his home in Dar Tuesday night. PHOTO
BY FIDELIS FELIX

Mhariri Absalom Kibanda Ajeruhiwa Vibaya

Nimepokea kwa E-mail:

Mhariri Absalom Kibanda
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Atekwa na Kujeruhiwa


Kwa ufupi

“Nilifika nyumbani kwangu kama saa sita usiku nikitokea kazini na nilipofika kwenye lango la kuingia ndani nilipiga honi ili mlinzi anifungulie. Lakini ghafla nilivamiwa na kundi la watu

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda ametekwa na watu wasiofahamika na kisha kumjeruhi vibaya kwa nondo, mapanga na kisha kumng’oa meno, kucha na kumharibu jicho la kushoto.

Tukio hilo la kinyama linafanana kwa kiasi fulani na lile la alilofanyiwa Mwenyekiti wa Chama cha Madaktari Tanzania, Stephen Ulimboka.

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea juzi usiku wakati Kibanda akirejea nyumbani kwake Goba Punguni, Kata ya Mbezi Juu, kutoka kazini.

Tayari mwandishi huyo mkongwe wa habari, amesafirishwa jana kwenda Afrika Kusini kwa matibabu zaidi. Aliondoka jana akisindikizwa na daktari kutoka Taasisi ya Mifupa Muhimu (Moi).

Mkasa Wenyewe

Akizungumza kwa tabu alipokuwa katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU), hospitalini Moi, Kibanda ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa New Habari (2006), alisema:

“Nilifika nyumbani kwangu kama saa sita usiku nikitokea kazini na nilipofika kwenye lango la kuingia ndani nilipiga honi ili mlinzi anifungulie. Lakini ghafla nilivamiwa na kundi la watu ambao walivunja kioo cha gari langu upande niliokuwa nimekaa. Nilitokea kupitia mlango wa abiria lakini sikuweza kuwakimbia watu wale kwani walinikamata na kuanza kunishambulia kwa vitu vizito.”

“Baada ya kutoka kwenye gari, nahisi nilikanyaga sehemu mbaya, nikateleza na kuanguka wakanifuata...niliona kama watu watatu hivi wakaanza kunishambulia. Sikuwa nafahamu kilichojiri, lakini nilisikia mwingine akimwambia mwenzake afande ‘mshuti... mshuti’ huyo alipoelekeza mtutu na kujaribu ‘kushuti’ (kupiga risasi) ilikuwa kama vile imegoma.

“Nikiwa bado niko chini, wakanipiga kwa kitu cha ncha kali kwenye jicho la kushoto, wakaning’oa meno na kucha katika vidole vya mkono wa kulia, walinipiga sana na nilipata maumivu makali. Baada ya kunipiga na kunijeruhi waliniburuza hadi bembeni ya nyumba yangu na kunitupa na wakaondoka, baadaye majirani na wasamaria wema walikuja kuniokoa.

Mashuhuda Baada ya Tukio

Akizungumza jana, mzazi mwenzake, Angella Semaya alisema wakati Kibanda alipovamiwa hakusikia lolote: “Niliamshwa na kelele za majirani ndipo nami nikaenda eneo la tukio. Sikuamini kama alikuwa Kibanda kwani alikuwa ametapakaa damu huku akigugumia maumivu makali... kwanza sikumjua kama ni yeye kwa jinsi alivyokuwa.”

“Nina wasiwasi na hawa watu kuwa wametumwa kwa kuwa hawakuchukua chochote zaidi ya kumdhuru mwili,” alisema. Angella aliondoka jana na Kibanda pamoja na Mwandishi wa Habari, Eric Kabendera ili kumsindikiza Afrika Kusini atakapokuwa anapata matibabu.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006), Hussein Bashe alisema: “Tulikuwa na Kibanda hadi usiku kama 5:30 hivi, tukifuatilia matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Kenya na tulipoona hakuna kinachoendelea zaidi, tukaagana kurudi makwetu.”

“Kwa kweli taarifa za kuvamiwa na kushambuliwa kwake zimetushtua, kwani ameumizwa sana hasa jicho. Daktari alishauri jicho liondolewe lakini nilikataa, jopo la madaktari bingwa wa macho wamemtazama na kuthibitisha kweli limeumia sana, tumewasiliana na mwajiri wetu ameamua kumpeleka Afrika Kusini kwa matibabu zaidi.

“Nawashukuru madaktari kwa jinsi walivyompokea na kumshughulikia katika kiwango kinachotia moyo. Pia waandishi kwa umoja waliouonyesha kwa kujitokeza haraka na kumjulia hali.”

Tasnia ya Habari

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), limeelezea kushtushwa na tukio la kutekwa, kupigwa na kujeruhiwa kwa mwenyekiti wake.

Taarifa ya TEF iliyotolewa jana na Katibu wake, Neville Meena, imesema shambulio hilo ni uthibitisho kwamba mazingira ya kikazi ya waandishi wa habari Tanzania siyo salama tena... “Tunapaswa kuchukua hatua za kutathmini upya mazingira ya kazi zetu, ili kuhakikisha kwamba walau tunakuwa salama.”

Alisema mwendelezo wa vitendo vya kuwashambulia waandishi wa habari ambavyo katika siku za karibuni vimeibuka, vinalifanya jukwaa liamini kwamba wanahabari sasa wanatishwa ili wasiweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

“Utesaji huu aliofanyiwa Kibanda unafanana na ule aliofanyiwa Dk Ulimboka. (Rejea vitendo vya kupigwa kichwani, kung’olewa kucha na meno).

Aidha, Meena alisema: “Tunaamini kwamba yaliyomkuta Kibanda hayawezi kutenganishwa na msimamo wake kikazi au kama mtu binafsi. Tunasema hivyo tukizingatia kwamba wahusika hawakuchukua chochote liwe, gari au vitu vilivyokuwamo ndani ya gari hilo vikiwamo laptop, ipad, simu za mkononi na vinginevyo.”

"Tunaamini vyombo vya dola, vitachunguza na kuwatia mbaroni kisha kuwachukulia hatua za kisheria wahusika wa tukio hili na mengine kadhaa ambayo sasa yamegeuka kuwa sehemu ya utamaduni katika nchi yetu.”

Awali, Mjumbe wa Bodi ya TEF, Theophil Makunga alisema wakati huu wanahabari na wanafamilia wakisubiri uchunguzi juu ya tukio hilo, kitendo hicho hakina budi kulaaniwa.

“Hatuwezi kusema nini chanzo cha tukio hilo kwa sasa, lakini tunaamini limetokana na kazi yake. Tunalaani vikali kwani tunaweza kusema kazi yetu sasa si salama tena,” alisema Makunga.

Mhariri Mtendaji wa Nipashe, Jesse Kwayu alisema tukio hilo halina uhusiano na ujambazi kutokana na mazingira ya jinsi lilivyotokea na kutaka hatua za haraka za kisheria zichukuliwe dhidi ya wahusika.

Mhariri wa Habari wa Tanzania Daima, Edson Kamukara alisema: “Matukio ya kutekwa na kushambuliwa kwa waandishi wa habari yamekuwa yakishika kasi... ni jambo la kusikitisha na hatuwezi kukaa kimya kwa hili.”

Baada ya Tukio

Katika taarifa yake jana, Dk Nchimbi alisema Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Said Mwema ameteua timu ya maofisa wa polisi wanne kutoka Makao Makuu ya Upelelezi kuungana na wapelelezi kutoka Kanda Maalumu ya Polisi Mkoa wa Kinondoni ili kuhakikisha waliohusika wanakamatwa.

Baadaye jana Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema ofisi yake imeunda jopo la maofisa wa polisi tisa ambao wameshaanza kazi ya upelelezi wa tukio hilo.

Kova alisema kitendo alichofanyiwa Kibanda si cha kihalifu, bali kukomoana na visasi kwa kuwa upelelezi wa awali umeonyesha kuwa waliomvamia hawakuchukua chochote.

Akizungumzia tukio hilo, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Assah Mwambene alisema Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kupitia idara yake imepokea kwa mshtuko tukio la kupigwa na kutendewa ukatili.

Alisema kitendo kilichofanywa kwa mhariri huyo ni ukatili uliopitiliza na kwamba wanaliachia Jeshi la Polisi lifanye kazi yake.

Wamjulia Hali

Kabla ya Kibanda kupelekwa Afrika Kusini, viongozi mbalimbali wakiongozwa na Makamu wa Rais, Dk Gharib Bilal walifika kumjulia hali. Wengine ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Assah Mwambene na Yussuf Omar Chunda na Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dk Reginald Mengi.

Mengi na Mbowe
Akizungumza tukio hilo, Dk Mengi mbali ya kulaani, aliwataka waandishi wa habari kuandika ukweli na kuhakikisha haki inapatikana kwa kuwa jambo hilo ni zito.

Alisema kuna haja ya polisi kufanya uchunguzi wa kina ili ukweli halisi upatikane na wahusika wafikishwe katika vyombo vya sheria.

Mbowe alisema: “Tuungane katika kutetea uhuru wa vyombo vya habari. Uvamizi wa Kibanda ni doa kubwa katika tasnia ya habari bila kujali yuko chombo gani na yeye ndiye mkuu wa Jukwaa la Wahariri, ni wazi atakuwa amezungukwa na maadui wengi.”

Imeandikwa na Joyce Mmasi, Aidan Mhando, Bakari Kiango, Salhim Shao, Beatrice Moses na Aziza .

Monday, July 02, 2012

Yaliyompata Dr. Ulimboka

Mkanda wa Ulimboka alivyotekwa, mwanzo- mwisho
Kutoka Gazeti la Mwananchi

Na Mwandishi Wetu
"NI saa 12:45 asubuhi, bado kiza kimetanda katika eneo hili la Msitu wa  Mabwepande. Mbele yangu namwona mtu akiwa amekaa chini, pembeni ya barabara akiwa amelowa damu mwili mzima.

"Ninapomkaribia nasikia sauti ya mtu huyo ikisema kwa taabu; naomba msaada jamani… naomba msaada jamani, hivi ndivyo anavyoanza kusimulia Juma Mgaza Abdallah, mtu wa kwanza kumwona Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka baada ya kutekwa, kupigwa na kutupwa katika Msitu wa Mabwepande nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Abdallah, anasema mara baada kumwona daktari huyo akiwa katika hali hiyo, alijaribu kumkokota kumtoa eneo hilo, lakini alishindwa kutokana na hali mbaya aliyokuwa nayo.

Baada ya hapo, aliamua kusubiri mtu mwingine apite eneo hilo ili amwombe wasaidiane kumpeleka Kituo cha Polisi Bunju.

Anasema muda mfupi baadaye aliona gari likija mbele yao, akalinyooshea  mkono kulisimamisha. Liliposimama, akamweleza dereva hali aliyokuwa nayo Dk Ulimboka na kwamba anahitaji msaada wa haraka.

Abdallah ambaye hadi wakati huo alikuwa hamfahamu mtu ambaye alikuwa akimsadia kuwa ni kiongozi wa madaktari kutokana na sura yake kuvimba, anasema walimwingiza katika gari hilo na kumpeleka Kituo Kidogo cha Polisi Bunju.

Anasema, Dk Ulimboka wakati huo alikuwa akiendelea kuvuja damu katika baadhi ya majeraha yake huku akiwa hana suruali na kubaki na bukta tu, huku akizungumza kwa taabu.

Kituo cha Polisi Bunju

Baada ya kumfikisha kituoni hapo, walitoa maelezo namna walivyomwokota na kumsaidia kumfikisha hapo.

Polisi baada kumhoji Dk Ulimboka, aliwatajia namba ya simu ya rafiki yake aitwaye Dk Deo. Walipompigia na kumweleza tatizo hilo, aliamua moja kwa moja kwenda Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, kutoa taarifa hizo na hatimaye kuandamana na watu kadhaa kutoka hapo akiwamo Mkurugenzi wake, Hellen-Kijo Bisimba.

Wawasili kituoni

Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania wa kituo hicho, Onesmo Olengurumwa, anasema waliwafika Polisi Bunju saa 3:36 asubuhi na kumkuta Dk Ulimboka akiwa amekalishwa kwenye benchi huku damu ikiwa imeganda kwenye majeraha mwilini.

Olengurumwa anasema waliwahoji polisi waliokuwa kituoni hapo kwa nini wakae na mtu aliyeumia kiasi hicho muda mrefu bila ya kuita gari la wagonjwa kumchukua ili kuwahi kupatiwa matibabu.

Olengurumwa anasema polisi walisema kwamba, walikuwa wanawasubiri ndugu zake wafike.

Baada ya muda mfupi, akiwa ameingizwa kwenye gari kupelekwa hospitali, Dk Ulimboka aliomba maji ya kunywa akisema ana kiu sana, lakini alipopewa, alikunywa kidogo akashindwa.

Anasema wakiwa njiani, alikuwa akilalamika kuwa anasikika maumivu makali huku akisisitiza kuwa tukio la kutekwa na kupigwa lilikuwa la kumuua.

"Jamani hawa watu walitaka kuniua walikuwa wamepanga kuniua," alisikika mara kwa mara akisema Dk Ulimboka wakati anapelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kupatiwa matibabu.

Maelezo ya Dk Ulimboka

Baada ya Dk Ulimboka kuokotwa aliweza kuzungumza na kurekodiwa muda mfupi baada ya kutolewa msituni na mazungumzo yake yalikuwa hivi;

“Nilikamatwa na watu hao usiku wa Jumanne nikiwa maeneo ya Leaders Club, Kinondoni na daktari mwenzangu baada ya kupigiwa simu na mtu mmoja ambaye alidai kuwa anafanya kazi Ikulu.

“Kuna jamaa mmoja anafanya kazi Ikulu, kama siku tatu mfululizo alikuwa akitaka kukutana na mimi ila nilishindwa kukutana naye kwa kuwa nilikuwa na kazi nyingi na wakati mwingine mpaka usiku,” alisema Dk Ulimboka.

Huku akizungumza kwa taabu kutokana na mdomo wake kuvimba, alisema siku hiyo mtu huyo alimpigia tena simu na kumtaka wakutane.

“ Jana (Jumanne) alinipigia simu na nikamwambia daktari mwenzangu twende tukaonane naye, wakati huo alitueleza kuwa alikuwa maeneo ya Kinondoni Stereo,” alisema Ulimboka na kuongeza:

“Tulipofika maeneo hayo tukampigia simu na akatueleza kuwa alikwisha ondoka, baadaye tukamweleza sehemu tulipo mimi pamoja na mwenzangu.”

Alisema kuwa, wakati anakutana na mtu yule maeneo ya Leaders Club, hakuwa na amani.

“Kwa kweli siku ile nilivyoonana na mtu yule sikuwa na amani kabisa ya kukaa eneo lile,” alisema Dk Ulimboka.

Alisema kuwa wakati wakiendelea na maongezi ya kawaida, bado aliendelea kuwa na mashaka na mtu yule.

“Katikati ya maongezi nikaona ameanza kuzungumza na simu, kila tukitaka kuagana alikuwa akizungumza na simu, sijui nini kilikuwa kinachelewesha sisi kuagana,” alisema Dk Ulimboka na kuongeza:

“ Ghafla walitokea watu kama watano na kusema kuwa hawana tatizo na mtu yeyote katika eneo hilo isipokuwa mimi.
Wakati sijakaa sawa, waliniburuza hadi  barabara ya lami kwa kuwa eneo hilo lilikuwa karibu na barabara.”

Aliongeza, “Nilipowauliza wananipeleka wapi, wakaniambia kuwa mimi nasumbua sana na nitajua hukohuko, waliniingiza katika gari jeusi, lakini halikuwa na namba. Niliwauliza kosa gani nimefanya? Hawakunijibu kitu na kusema, we twende utajua hukohuko.’’

Alisema alipokuwa ndani ya gari hilo watu hao walimpiga na kwamba walipofika maeneo ya Victoria, walichukua sweta nyeusi na kumfunga usoni, jambo lililomfanya ashindwe kuona kinachoendelea ikiwa ni pamoja na alikokuwa akipelekwa.

“Walinipiga mateke ya mbavuni, wakati mwingine walitumia vitako vya bunduki,  kila nilipokuwa najaribu kuangalia ninapokwenda nilishindwa,” alisimulia  Dk Ulimboka.

Alisema kuwa watu hao walimpeleka katika nyumba moja ambayo hakujua iko sehemu gani ambapo walimshusha na kuanza kumshambulia kwa mateke mfululizo kila sehemu ya mwili. Wakati huo, wote walimshinikiza awaambie nani yupo nyuma ya mgomo wa madaktari.

“Tangu saa sita usiku mpaka saa 9:00 alfajiri walikuwa wananipiga tu, kuna wakati nilijaribu kukimbia wakapiga risasi juu nikasimama na sikuweza kukimbia tena,” alisema Dk Ulimboka na kuongeza:

“Nilisimama, wakaendelea kunipiga, niliwasikia wakisema ama wanichome sindano ya sumu nife au kunikanyaga na gari. Baadaye wakaanza kuning’oa  meno na kucha kwa kolea huku wakinilazimisha kusema nani yupo nyuma ya mgomo wa madaktari."

Alisema kuwa, watu hao walikuwa na bunduki kubwa ambayo hakuweza kuitambua ni aina gani.

“Waliniambia kuwa ninajua ninachokifanya hivyo wanaweza kunichoma sindano ya sumu nife au wanikanyage na gari nife,” alisimulia.

Dk Ulimboka alisema kuwa awali hakuwa na shaka na watu hao kwa kuwa alidhani ni polisi, lakini baadaye alishindwa kuwaelewa kwani watu hao walimchanganya.

“Sikuweza kuwatambua ila naweza kusema ni askari, walipokuwa wananipeleka niliwauliza mnanipeleka wapi na wakati huo nilikuwa sioni mbele ila ilikuwa kama maeneo ya Mwenge hivi,” alisema Dk Ulimboka.

Alisema kuwa baadaye alipoteza fahamu na hakuweza kuona chochote zaidi ya kusikia sauti za watu hao kwa mbali.

“Nilikuwa sioni na nilipoteza fahamu nikawa nasikia tu wakinibeba, gari lilitembea muda mrefu, sikujua ni wapi tunakwenda, kumbe ndio huko Mabwepande,” alisema.

Alisema kuwa walifika maeneo ya barabara ya vumbi na baadaye wakamshusha na kumbeba hadi msituni.

“Waliniburuza na kuniacha huko na muda wa  saa kumi alfajiri ndipo nikazinduka na kuanza kujiburuza kuelekea barabarani ambako nilisaidiwa na mtu mmoja ambaye simtambui,” alisema Dk Ulimboka