Showing posts with label Ubakaji. Show all posts
Showing posts with label Ubakaji. Show all posts

Sunday, June 15, 2014

Misukosuko ya Flora Mbasha

Flora Mbasha na Mume Wakewakiwa na furaha kabla ya Skendeli

Kutoka VIJIMAMBO BLOG:

Mpasuko wa ndoa ya wasanii wa nyimbo za Injili, Emmanuel Mbasha na mkewe Florah umewagawa wachungaji wa makanisa mbalimbali nchini baada ya kibao kumgeukia Flora kwamba ndiye anadaiwa kusuka mpango wa kumwangamiza mumewe ili afungwe kwa kosa la ubakaji…..
Wakizungumza na wanahabari wetu kwa nyakati tofauti, wachungaji hao walisema endapo itabainika ni kweli Flora ameshiriki kumsaliti mumewe kwa kutembea na mmoja wa wachungaji maarufu nchini hapatakuwa na haja ya kumwalika kwenye huduma zao kwani hawawezi kuhudumiwa na mwimbaji mzinzi.
Mchungaji Ambonile Mwakipesye na Amani Joseph wa makanisa ya Tanzania Assemblies of God ( TAG) walisema kuwa kama kulikuwa na matatizo kwenye ndoa yao walipaswa kuwaona watumishi wa Mungu na kusuluhisha badala ya kutengenezeana mitego na kuingizana majaribuni kama inavyodaiwa kutokea kwa Mbasha….
Wakati wachungaji hao wakisema hivyo, mchungaji Thomas Methew yeye alisema kuwa ukweli wa jambo hilo wanaujua wanandoa wenyewe kwani mpaka sasa hakuna anayelijua tatizo kubwa mpaka wakafikia hatua ya kutengana.
 
**********************
 Kutoka Jamii Forum
 
SIKU chache baada ya tuhuma za ubakaji na mzozo wa familia ya mwimba Injili mahiri nchini, Flora Mbasha na mumewe, Emanuel Mbasha, mambo mengine yameibuka.



Mwimba Injili mahiri nchini, Flora Mbasha

Yaliyoibuka safari hii ni taarifa kwamba, juzikati, Flora alivamiwa na watu wasiojulikana nyumbani kwake, Tabata Kimanga jijiini Dar dakika chache baada ya yeye kuingia na gari akitokea mafichoni anakoishi kwa sasa.



Kwa mujibu wa chanzo, siku ya tukio ilikuwa saa 9.15 alasiri ambapo Flora aliingia nyumbani kwake na kufunguliwa geti kubwa kisha kuingiza gari ndani na geti kufungwa tena.

Flora aliingia na gari akitokea hotelini anakoishi kwa sasa. Alikuwa ameshaingia na geti likafungwa. Ghafla, watu wakafika na kugonga geti hilo kwa nguvu huku wakisema watalibomoa geti kama wenyeji hao hawatafungua,” kilisema chanzo.



Mwimba Injili mahiri nchini, Flora Mbasha akiwa na mumewe, Emanuel Mbasha,

Chanzo kikazidi kudai kwamba, ilibidi Flora apige simu polisi ili wafike kumuokoa yeye na familia yake.

“Polisi wawili walifika haraka sana wakiwa na bunduki na kukuta wale watu wamekimbia maana walimsikia Flora akiongea na polisi kuomba msaada.


“Lakini polisi wenyewe ilibidi watumie nguvu kubwa kugonga geti na kujitambulisha ndipo akatokea Flora na kuchungulia nje kupitia dirisha dogo. Alipowaona polisi akafungua mlango,” kilisema chanzo hicho.

Akihojiwa na polisi hao, Flora alisema watu hao walikimbia na hakuwajua kwa sura wala hawakujitambulisha ni akina nani.


Alizungumza na gazeti hili baada ya tukio, Flora alisema: “Unajua kwa sasa nina hofu sana na nilihisi wale watu walikuwa wakinifuatilia kwa karibu kila sehemu, sasa naogopa kuendelea kuishi hapa, wanaweza kurudi na sijui lengo lao.”


Hata hivyo, baada ya askari hao kuondoka katika eneo hilo, Flora naye aliingia kwenye gari lake akiwa na mdogo wake na kuondoka.

Mume wa Flora, Mbasha naye yupo mafichoni baada ya kudaiwa kumbaka binti wa miaka 17 ndani ya nyumba yao huku utata ukitawala kuhusu ukweli wa tukio hilo ambalo limeigawa jamii.

Saturday, October 27, 2012

Mwalimu Ajiua Dar Baada ya Hii Picha Kutoka!!!

Mwalimu ni kiungo muhimu sana katika malezi ya wanafunzi hapa nchini.Wao hushinda na watoto wetu kutwa nzima .......
Kwa mantiki hiyo, tabia ya mtoto yeyote aliyewahi kalia madawati ina asilimia zaidi ya 70 ya tabia za walimu wake......
Siku hizi mambo yamebadilika sana.Mwalimu wa miaka ya 90 ni tofauti kabisa na mwalimu wa miaka ya leo.
Walimu wa leo wengi wao ni vijana wadogo ambao wengi wamejawa na tamaa za mapenzi.Wao hawajui kutongoza bali wanajua kulazimisha....
Inashangaza na kusikitisha kuona walimu wetu wakishindana KUTOA BIKRA ZA WATOTO WA KIKE......Mtoto akikataa basi cha motoatakiona ....
Mtandao huu umebahatika kuongea na mwanafunzi mmojaambaye ni mhanga wa tukio hilo la kulazimishwa mapenzi na mwalimu wake..........
HILI NI SIMULIZI LAKE:
--------------------------------------------------------------------
Mwalimu akimbaka mwanafunzi wake darasani. Baada ya picha hii kutoka kwenye gazeti la Udaku Mwalimu huyo mbakaji mshenzi alijiua!

"Mwalimu alianza kunitaka tangu nikuwa form one.Nilipomkataa alianza kunichapa tena bila kosa maalumu na kunipa adhabu kila mara...
Baada ya kufanya hivyo kwa muda, aliamua kuniita ofisini na kuniambia kuwa anatanisaidia kimasomo endapo ntamkubalia.Niliamua kumkubali kwa kwa kuhofia viboko na aliniambia nisimwambie mtu.

Siku ya kwanza kufanya mapenzi alinipeleka gesti na aliniambia kuwa atatumia condom.Kwa kuwa ilikuwa ni mara yangu ya kwanza hatukuweza kutumia kinga na alifanya hivyohivyo.

Baada ya hapo tuliendelea kufanya hicho kitendo hata tukiwa shule.Wakati wa kutawanyika, mwalimu alikuwa akiniita katika ofisi yake na kunilazimisha tufanye.....

Miezi kadhaa baadaye, nilianza kujihisi tofauti na wazazi wangu waliyagundua mabadiliko hayo.Walinipeleka hospitali na vipimo vilionesha kuwa nna mimba.Waliponibana ilinibidi niwaeleze ukweli.....

AFISA ELIMU AINGILIA KATI:
Baada ya kubaini hali hiyo, baba alinipeleka moja kwa moja mpaka kwa afisa elimu wa mkoa.Sikuwa na jinsi zaidi ya kueleza ukweli.Mwalimu aliitwa na kuhojiwa.Mwanzo alikataa kabisa lakini baada ya kubanwa ilibidi akubali.

Mwalimu alisimamishwa kazi kwa muda na kufunguliwa mashitaka.Alikaa polisi kwa siku mbili, siku ya tatu alipata dhamana akatoka.....

Alipotoka, mwalimu aliamua kujiua kwa sumu.Shule niliachishwa.nipo nyumbani na mtoto.

Friday, June 01, 2012

Wito Kutoka Kwa Ndugu wa Queen Butahe

Wadau, nimegundua kuwa Queen alikuwa na kesi mahakamani hapa Boston dhidi ya ndugu yake aliyemleta kutoa Tanzania.  Kesi inahusu mambo ya kuchapwa.  Hapa USA huwezi kumchapa mtoto, ni kosa la jinai. Watoto  kutoka nje wanajanjaruka wakijua hiyo sheria. Utamsikia mtoto, ukinichpa, nitamwambia Mwalimu halafu nitaenda kukaa kwenye nyumba ya DSS (Department of Social Services)! Doh!  huko si ndo kubakwa na kugeuzwa malaya, mlevi, mtumia madawa ya kulevya!

****************************************************
Kindly Post this in your Blog!


From: Rev. G. Kutta

http://www.wavuti.com/4/post/2012/2/the-story-of-queen-b.html

Sorry, was interupted by powers cut! .....

Regards!

Mh! Whoever was and still act behind Queen on this issue had a mission behind! Without your help and mine, they can win! Do not underestimate your opponent! They have great minds! Tell me, what else can you do if you find Queen a threat? Entrench her in her own drain! This is what they wanted to do! Queen is bright and was doing very well in school such that envy and evil sent her opponents to disguise and now they have put her in this mess!

Lets act together to rescue our Girl!

1. Get her to realize that life may have been bad in the past but she was lucky to have a few who cared for her to their best and their simple faults of life activities led them blind of her tragedies, if at all they happened!

2. Get her to realize that Her family still desires to see her grow up good and strong! We are here still here! We want her alive and Blessed!

3. Get her to realize that, long lasting success can only come from a genuine heart!

4. Get her to realize that, the body of good willing Tanzanians, though dismayed by her accusations, yet know that Tanzania is her home! We Love her and she can make it good with us all by simply doing things the right way without defaming the good!

5. That those who play guardianship for her (Queen's) destruction should know that we know their fear! But they need not fear! Queen is born from a Family highly related to the United States! A family that got all its Good Potentials from United States! I myself had my baseline Education, grade One at Jefferson School, Spring field Ohio (1974/5) with Mr. Marckoch Head Master, Mrs. Carry my teacher! i love these guys! I love USA -But lets keep it up that way! Lets get Queen back to life!

Rev.Kutta,G.P.K.

Thursday, May 31, 2012

Site ya Anayedaiwa Kubakwa Ovyo Queen Butahe Haifunguki!

UPDATE June , 1, 2012  -  I have information regarding Queen's missing brother Walter. He is Queen's half brother. Her mother, the late Sgt. Victoria Kutta, of the Tanzania Police Force was married briefly to his father attorney Banda.  At the the time of her death they were separated. Mr. Banda took his son and left Queen with her maternal family. Mr. Banda is also dead now. Walter is said to be living with an uncle now. As soon as I get his whereabouts I will let you know.

Sgt. Victoria never identified Queen's father. The man listed on Queen's documents as her biological father, Robert Butahe, who is said to be deceased, is actually alive and well and lives in Dar es Salaam, Tanzania.


The justice system in Tanzania can prosecute those who abused Queen. They are waiting for her to say the word to bring her abusers to justice, however all I have spoken with say that they are not aware that any such abuses ever took place. They need Queen to talk to them but she has cut off communication with her Tanzanian family.


Sgt. Kutta/Banda alikuwa anafanya kazi pale kituo cha polisi Msimbazi. 
************************************************************ 
Queen Butahe, Franklin, Massachusetts
Wadau, tangu nimeona ile story ya Queen Butahe, kwenye Fox 25 nilifanya juu chini kujua kama kweli mambo hayo aliodai katokea, yalitokea kweli!  Mimi nilimwumbua yule mbakaji wa watoto Mzee Maumba 1990 na story kama yake ilinigusa sana.  Pia mimi ni mmoja wa waanzilishi wa TAMWA na moja ya kazi yetu ilikuwa kusaidia watoto na wakina mama. Lakini baada ya kusoma website yake, nikajiuliza kama yote ni kweli au chumvi, hamira na pilipili yameongezwa?  Site ya Queen ni Hapa. Ajabu Haifunguki sasa: http://www.queenb.antosca.com/  (Hapo kuna details za waliombaka, kutoa mimba etc.)

Haki ya mungu nilipoona tangazo ya hiyo story kuwa binti kateswa Afrika, nilidhani watasema Congo, nikabaki mdomo wazi waliosema Tanzania!


( Story ilitoka Fox 25 tarehe 10/Mei/2011.  Mnaweza kuona Kideo hapa:


http://www.myfoxboston.com/story/18288735/overcoming-the-odds-and-giving-back )

Kilichonishutua ni kuwa alidai kabakwa na watu wengi sana, ndugu, madereva wa school bus (tena kwa kupokezana), walimu.  Katoa mimba akiwa Primary! Duh, nikasema hivi Tanzania wanaume wetu wamekuaje siku hizi.


Baada ya kuposti taarifa kwenye Blog, Niligundua kuwa huyo binti, alililewa katika familia enye uwezo na waliokuwa wanampenda.
Mjomba wake Queen aliniletea ujumbe na niliongea naye kwa simu. Mjomba alililia kwa hasira na kusema hawezi kukubali Queen achafue jina na familia yake na Tanzania kwa ujumla.

Rev. Gilbert Kutta said...

I am her Family Member Senior Guardian, her Mother's Brother and second to the mother in our Family! Her mother passed away, what a tragedy to our family! She calls herself Queen Butahe? ----- Better the media call her again and get the name of her real Father! You may call me +255766551733! I did contact her when this sad news just came to my notice through the Web! She finally ended up blocking my email to her and said "It is bye bye to you"! She has a mission in mind. I will never allow it to take place the way she has planned by putting to shame my Lovely country TANZANIA and my good family! --- and me in effect! I want her to come out again and say the Truth. I don't brush out all what she said! But we have descent ways to deal with all that took place and not the way it seems her new American Caretaker is using! We do not work on half truth/half false and cooked up stories pitched for gain! I am in contact, and continue to contact all who did that interview to get to know what motivated them to shoot it to the mass! To defame? To what gain? How much did they first make due effort to search for truth? Is it just because a simple girl has come up with a story they see interesting they shoot it to the mass? I have plenty more to say! I have entered this debate because I feel this the only way to seek for cure!

god Bless TANZANIA my mother land! I love you and will protect you!

Please Contact me at rnaioth@yahoo.com. If you can help me clear THIS MESS and help Queen come back to her senses not to defame her Mother, please do!

I need that help!
thank you all-
God bless and keep my daughter safe!
regards to you all-
its me:

Rev. Gilbert Phillip Kutta
rnaioth@yahoo.com
+255766551733
Morogoro, Tanzania!

Mimi nilipeleka habari kwa huyo Mwandishi wa Fox 25,  Maria Stephanos na kumwelezea kuhusu mjomba wake. Maria kimya! Nadhani hatasema kitu, si mnajua jinsi hao waandishi wanvyojaribu kutafuta awards. 
*******************************************

Soma Story ya Queen kwa maneno yake mwenyewe hapa:

http://www.wavuti.com/4/post/2012/2/the-story-of-queen-b.html#axzz1wMvqNbjm

Wadau, ninaendelea kujaribu kuwasiliana na Fox 25 ili watoe story au correction, kuwa nchi yetu si ya watu washenzi kama walivyotupakazia.


Posti yangu wa awali mnaweza kusoma hapa:

Niligundua kuwa huyo binti, alililewa katika familia enye uwezo na waliokuwa wanampenda.


http://swahilitime.blogspot.com/search?q=queen+butahe

Friday, May 11, 2012

Binti wa Kibongo Boston Adai Kabakwa Ovyo Tanzania!

Wadau, leo asubuhi kazini niliulizwa kama ni kweli Tanzania haithamini haki za akina mama na kama wnaawake wanabakwa ovyo!  Kisa, ni story iiliyotoka kwenye TV jana jioni kuhusu binti MTanzania, Queen Butahe (19) anayeishi na familia ya kizungu huko Franklin, Massachusetts.

Kwa bahati nzuri jana jioni nilikuwa naangalia taarifa ya habari hapa Boston Fox 25. Wakasema, lazima usikie story ya binti ambaye kateswa na kuishi maisha ya ajabu Afrika.  Basi nikangojea story na kujiuliza ni nchi gani!  Nilidhani Congo. Ajabu, nchi ambayo inadaiwa kateswa kupindukia ni Tanzania!  Story ilivyopangwa utadhani Tanzania ni nchi ambayo mwanamke hana haki, hakuna sheria na wanawake wanabakwa ovyo! Mwisho wakasema kuwa Queen ana mradi wa kukusanya hela kwa ajili ya kujenga maktaba Tanzania! Yaani wadau, utadhani kuwa Tanzania haina maktaba hata moja.  Huyo binti ni yatima, familia yake wamekufa kwa UKIMWI. Natoa pole sana kwake. Lakini jamani, kuponda nchi hivyo!


Queen Butahe

Mnaweza kuona Kideo hapa:

   http://www.myfoxboston.com/story/18288735/overcoming-the-odds-and-giving-back

BOSTON - Maria Stephanos introduces you to Queen Butahe, a senior at Franklin High School, who is originally from Tanzania. Queen lost most of her family in Tanzania by the time she was six to HIV/AIDS. Only she and her brother had survived, and she doesn't know where he is to this day. For years she had been abused, and raped, and four years ago she had the chance to come to America with some relatives. She now lives the life of a normal American teenager, but doesn't forget the life she escaped in Tanzania. She is now raising money to help improve the education for young people in Tanzania, and help to build a library there. ( Ile story haisemi lakini sehemu anyaotaka kujenga ni Kwala, Tanzania.  Sijui ni mkoa gani lakini.)

*********************************

Wadau, nia yangu si kumponda huyo binti Queen.  Na ninapongeza kwa moyo wake wa kutaka kusaidia watoto waliobaki Tanzania.  Lakini kukashifu nchi nzima jamani!  Sehemu yoyote ukienda duniani kuna watu wabaya na wazuri.  Kwa kweli nilishikwa na hasira baada ya kusikia hiyo story, lakini nilisema huyo binti ni mdogo na huenda ni kweli kashindwa kumwambia mtu yaliyompata.   Anasema kuwa kabakwa na hausgeli, madereva wa mabasi, mjomba wake, mwalimu. Anasema kapata mimba ya mjomba wake akiwa darasa la saba lakini aliitoa.  Mwanzo nilidhani ni yatima ambaye alikuwa anaishi mitaani, lakini baada ya kwenda kwenye website yake nikagundua kuwa huyo binti alitoka kwenye familia waliojiweza. Alisomeshwa Olympio Primary na pia alikuwa anapanda School Bus. Ni ndugu yake ambaye alikuwa hapa Marekani ndiye aliyemnunulia tiketi ya kuja Marekani.  Wakati yupo hapa ndo kakutana nahiyo familia Franklin na kwenda kukaa nao.  Alikuwa na nafasi nzuri kuliko wengine. Na nadhani shangazi yake na hata huyo ndugu aliyemwezesha kutoka Tanzania kuja Marekani akisoma alivyoaandika watasikitika mno.  Anasema kuwa hata huyo ndugu yake wa Marekani! 

Na tusisahau kuwa Tanzania ina wanawake wengi wasomi, viongozi, na katika vyombo vya dola na sheria.  Hao anaodai walimbaka wangeweza kufungwa maisha!  Sheria zipo kulinda watoto dhidi ya ubakaji, kumbuka Mzee Maumba. Naona Queen hana habari kuwa gereza za Tanzania zimejaa watu waliopatikana na hatia ya kubaka watoto na kufanya maovu dhidi ya akina mama.

Ningependa kusika maoni yenu. Na pia wenye comments waambie Fox 25 kuwa nchi yetu Tanzani si jungle na tunathamini maisha ya watu wote!

Monday, August 22, 2011

Mashitaka Dhidi ya Strauss-Kahn Yafutwa!

(Pichani aliyekuwa Mkuu wa IMF Dominique Strauss-Kahn akiwa mahakani New York mwezi Mei)
(Pichani Bi Nafissatou Diallo)



Kwa kweli sijui tumhurumie huyo Bi Nafissatou Diallo aliyedai kuwa kabakwa na Dominique Strauss-Kahn. Mambo ya kupambana na matajiri na wenye mamlaka na heshima kama Strauss-Kahn hayawezi kuzaa matunda mema. Maisha yake Bi Diallo yameharibika. Waliomsapoti wanamkimbia sasa.




Kabla ya Bi Diallo kumshitaki Mzee Strauss- Kahn ilikuwa agombee urais wa Ufaransa. Bi Diallo anatoka Guinea nchi ambayo ilikuwa koloni ya Ufaransa. Nina wasiwasi hata ndugu zake wa Guinea watakiona cha mtema kuni shauri ya hii kesi.



Haya kesi imefutwa, sasa IRS wanamchunguza huyo Bibi kwa utapeli, eti alikuwa na akaunti enye $150,000 huko kaandikisha kuwa maskini, ana anakaa kwenye fleti za wasio na uwezo. Wanaokaa Marekani wanaelewa umuhimu wa kusema kweli kweli zile fomu za kodi 4/15.



Wakili wa Bi Diallo kafungua kesi kumdai Strauss-Kahn mamilioni. Anaweza kupata, lakini walivyomchafua huyo mama, duh! Magazeti yameandikia kuwa ni mwongo mkubwa, malaya, anashiriki na wauza unga, Kaomba asylum akidai kuwa kabakwa huko Guinea na wanataka kumkeketa, nk.




Lakini tangu hii kesi itokee nimekuwa nikiuliza, inakuaje jamaa kamlazimisha amnyonye ume wake mpaka ana mwaga? Kama alikuwa hataki si angeling'ata! No huyo Mzee Strauss-Kahn apunguze nyege zake. Nyege ndo zimeponza!




Pole zake Bi Diallo.



*********************************


Former International Monetary Fund chief Dominique Strauss-Kahn will no longer face criminal charges related to allegations that he sexually assaulted a hotel housekeeper, the housekeeper's attorney said Monday after meeting with prosecutors.

A grand jury indicted Strauss-Kahn in May on charges that he sexually assaulted housekeeper Nafissatou Diallo at his luxury New York hotel suite. Strauss-Kahn's attorneys have insisted that any sexual encounter was consensual.

A judge freed Strauss-Kahn on July 1 after prosecutors learned Diallo had lied about the specifics of her whereabouts after the incident and past details of an asylum application and information on tax forms.

******************************







By JOHN ELIGON, WILLIAM K. RASHBAUM and COLIN MOYNIHAN

Updated, 4:01 p.m. Prosecutors in the office of Cyrus R. Vance Jr., the Manhattan district attorney, have filed papers requesting that all charges be dropped against Dominique Strauss-Kahn, the former head of the International Monetary Fund.

The papers, known as a dismissal on recommendation, were filed at 3:20 p.m. Monday afternoon in Manhattan Supreme Court.

At about the same time, the lawyer for Nafissatou Diallo, the hotel housekeeper who accused Mr. Strauss-Kahn of sexual assault, emerged from a brief meeting with prosecutors to offer harsh criticism of Mr. Vance.

The meeting was presumably held to inform Ms. Diallo and her lawyer, Kenneth P. Thompson, of the office’s intention to drop the charges.

“The Manhattan district attorney, Cyrus Vance, has denied the right of a woman to get justice in a rape case,” Mr. Thompson said. “He has not only turned his back on this victim but he has also turned his back on the forensic, medical and other physical evidence in this case. If the Manhattan district attorney, who is elected to protect our mothers, our daughters, our sisters, our wives and our loved ones, is not going to stand up for them when they’re raped or sexually assaulted, who will?”

Ms. Diallo stood by his side, but said nothing.


Mr. Strauss-Kahn’s lawyers, William W. Taylor III and Benjamin Brafman, said in a statement:

“We have maintained from the beginning of this case that our client is innocent. We also maintained that there were many reasons to believe that Mr. Strauss-Kahn’s accuser was not credible. Mr. Strauss-Kahn and his family are grateful that the District Attorney’s office took our concerns seriously and concluded on its own that this case cannot proceed further. We look forward to attending the hearing on Tuesday.”

A chaotic scene unfolded outside the Louis J. Lefkowitz State Office Building, where the meeting between Ms. Diallo’s team and prosecutors took place, with reporters and onlookers lining both sides of Centre Street.

Ms. Diallo had not met with prosecutors in nearly a month, the last time being on July 27 when she went to their office to listen to recordings of telephone conversations she had with a man in an Arizona jail. Prosecutors have said that the recordings showed that Ms. Diallo was talking about exploiting Mr. Strauss-Kahn’s wealth. But Mr. Thompson said that his client never raised the subject of getting money from Mr. Strauss-Kahn during the conversations, in which Ms. Diallo and the man spoke in Fulani, a language of Ms. Diallo’s native Guinea.

The difference in opinion over the substance of the conversation was just one of many points of contention between Mr. Thompson and the district attorney’s office. The relationship between them has deteriorated since prosecutors said in late June that they believed Ms. Diallo had lied to them about several things in her personal life and background.

Mr. Thompson has urged prosecutors to press forward with the criminal case, arguing that physical evidence and other factors outweighed his client’s credibility problems. Ms. Diallo has said that Mr. Strauss-Kahn tried to rape her and then forced her to perform oral sex when she went to clean his suite at the Sofitel New York in mid-May.

But prosecutors have determined that Ms. Diallo had been too untruthful with them to stand up to cross examination if the case were to go to trial. She lied about her past in Guinea on her asylum application and she told prosecutors in an interview a false story about being gang raped in her native country, prosecutors have said.

In their letter to Mr. Thompson, prosecutors said that at Monday’s meeting they would explain how they would proceed at Tuesday’s hearing before Justice Michael J. Obus of State Supreme Court in Manhattan.

Several elected officials and women’s groups planned to hold rallies in front of the courthouse Monday afternoon to urge Mr. Vance to go forward with the case.

Tuesday, August 02, 2011

Marudio - Miaka Baada ya tukio kaniomba Msamaha!

(Pichani Ukaguzi wa Gwaride Mlale JKT Songea - Picha kwa hisani ya Michuzi Blog)

Naona, kuna 'Anonymous' fulani kagusia hii swala ya yalionipata nikiwa jeshini JKT. Watu wengi wamenitumia e-mail kuulizia details. Nimeamua kuibandika tena. Ni posti ya kutoka April 2006. Lakini mjue enzi za JKT, wasichana wengi walinyanyaswa kijinsia, mimi nilikuwa na bahati maana nafahamu wasichana waliokuwa gang raped. Dada fulani, alimkubali afande, alivyomaliza kaita wenzake kwa kusema, "Njooni, Mboga hii hapa!" Yule dada hakuweza kutembea vizuri kama wmezi baada ya hapo!

*****************************************************************************

Nilipokuwa Jeshi ya Kujenga Taifa (JKT) karibu nibakwe na afande Fulani (jina nahifadhi). Lazima niseme kuwa katika kipindi hicho wanaume wengi waliona makambi ya JKT kama ‘buffet’ ya wasichana. Si maafande wa jeshi tu, bali hata viongozi wa serikali walikuwa wanapitia makambi ya JKT kula tani yao!

Mimi nilikuwa Masange JKT, Tabora. Wakati huo huyo jamaa alikuwa ni Kepiteni wa JKT. Nadhani alidhania kwa vile yeye ni kepiteni basi alikuwa na haki ya kutembea na yeyote aliyemtaka. Kwangu aligonga ukuta! Bila shaka alikuwa hajawahi ‘kunyimwa’ mpaka siku hiyo alipokutana na mimi.

Miaka baada ya tukio nikiwa nafanya kazi Daily News mara nyingi nilikuwa napishana naye Posta Mpya. Basi ananisemesha, na mimi namnunia halafu napita zangu kimya bila kumjibu kwa hasira. Siku moja kanisimamisha kaniambia, "Chemi, naomba msamaha, nisemahe tafadhali, kweli nilikukosea!” Aliongeza kuwa miaka mingi imepita hivyo sina sababu ya kuwa na hasira naye! Na mimi nilimjibu, “Mshenzi sana wewe!” nikaenda zangu.

Ikapita kama mwaka mwiingine. Jamaa anaendelea kunisalimia kila nikimpita njiani na mimi kwa uchungu bado nikashindwa kusema kitu. Basi nikafikiria alichoniambia Posta Mpya. Lakini niliona kama jambo hilo linamsumbua. Na nikasema kama Bwana Yesu aliweza kusamehe watu kwa madhambi yao kwa nini mimi nisimsamehe. Basi baada ya hapo ikiwa nikimwona na akinisalimia naitika na naendelea zangu na nikaona kidogo hata yeye alikuwa na raha.

Lakini bado najiuliza kama kitendo chake kilimsumbua miaka na miaka kama ilivyonisumbua mimi.Unauliza ilikuaje mpaka nikajikuta kwenye situation ya kubakwa. Au mnasema nilitaka mwenyewe. Ngoja niwaelezee ilivyokuwa.

Nilikuwa mhudumu Officer’s Mess, mpishi na msafishaji. Huyo jamaa alikuwa ni mgeni kutoka Makao Makuu ya JKT Dar es Salaam. Kwa kweli sikutaka kufanya kazi pale Mess lakini tulichaguliwa special na Matron, mimi kwa vile niijua kupika vyakula mbalimbali hasa za kizungu. Lakini uzuri wa hiyo kazi ni kuwa uanambulia mabaki ya vyakula (leftovers), na mara nyingine kulikuwa hakuna.

Basi huyo Afande alikaa kambini wiki kadhaa. Katika kumhudumia tukawa tunaongea na mimi nikawa namheshimu kama kaka vile. Wala sikusikia mapenzi yoyote kwake. Basi jioni fulani, kanialika chumbani kwake kunywa soda na biskuti na kwa Maongezi zaidi. Sasa kama ulienda jeshi unajua njaa kali unayokuwa nayo. Nikaenda, kanikaribisha vizuri, nilipewa soda na tukawa tunaongea. Basi nikaona mwenzangu anabadilika ghafla! Mara ananikumbatia kwa nguvu, na kunibusu na mengine. Nikajaribu kuaga lakini jamaa hakuniachia. Baada ya ku-plead naye aniachie, kaniachia. Kaomba msamaha na kaniomba niendelee kukaa nimalize hizo soda alizoninulia.

Kama mjinga nikamwamini, nikakaa nakunywa hizo soda. Tukaendelea na Maongezi, kukaa kidogo huyo kanirukia, najaribu kusimama huyo, kanivuta na kuniangusha kitandani! Mimi saa hizo nikawa naogopa kabisa nia yake!Kaniambia eti, “ukipiga makelele najua nitasema nini! Nyamaza! Huna sababu ya kunikatalia!” LOH! Kanizaba kibao! Nikamwuliza kwa nini anaifanyia hivyo, na mimi nilikuwa namwona kama kaka yangu!Hapo sasa ikaniingia. Nabakwa! Loh!

Nilimpiga mangumi na mateke lakini jamaa alikuwa na nguvu huyo kachana chupi yangu! Baada ya hapo, jamaa kashika miguu yangu huko anafoka kwa sauti kama vile anatoa amri “panua miguu! PANUA MIGUU!” Huko katoa ume wake uliyosimama kwenye suruali! Basi kuona sipanui jamaa kaongeza makofi na kafanikiwa kupanua miguu yangu! Kuona kafanikiwa kupanua huyo kajaribu kupenya. Ilipogusa kwangu nilipiga kelele cha kufa! Nikasema, “Nakuufaaaa!”

Heh! Ghafla jamaa kaniachia kaniambia niende. Alisema, “Nimeigusa na ume wangu, unatosha!” Nenda zako! Na ukimwambia mtu najua nitasema nini!”Loh nilikimbia bwenini na giza lile la Masange huko nalia. Wenzangu wananiuliza vipi, nikashindwa niseme nini! Kwanza niliona haya! Fikiria, niliona haya (shame)!Kesho yake nikaenda dispensary na kujiandikisha mgonjwa. Sikwenda kazini Officer's Mess bali nililala bwenini.

Siku iliyofuatia huyo Afande mshenzi kapita bwenini kwetu kaulizia hali yangu, na mimi huko natetemeka kwa woga nikashindwa niseme nini. Alininunulia Orange squash na biskuti na kuzileta bwenini. Sitasahau alivyonitazama! Ilikuwa kama vile anapanga jinsi gani atanipata. Baada ya hapo alimwopoa msichana mwingine na huyo alimkubali kabisa. Akawa analala kabisa huko Officer’s Mess. Hakuna anayemsumbua wakijua ni bibi wa Afisa. Basi, siku za yule jamaa kukaa kambini zikaisha, na yule binti alienda naye Tabora mjini kwa siku kadhaa. Halafu jamaa karudi zake DSM. Yule binti karudi zake kambini! Kumbe alienda bila pass. Alidhania kwa vile yuko na mkubwa hana haja ya pass. Na yule Afande ndo kaondoka kimoja! Maafande waliobakia wacha wamtese huyo binti alivyorudi kambini! Walimtesa kwa Extra drill na mengine mpaka ikabidi Military Police waombe wakuu wamsamehe la sivyo atakufa. Raha yake iliishia kwa suluba! Sijui yule binti alidhania jamaa atamwoa! Kwa nini alimkubali yule mshenzi.

Anyway, kila mtu na vyake. Alivyotoka kwenye suluba tulimwuguza! Siku haizkupita na mimi nilitolewa kazi Officer’s Mess na kupelekwa kwenye kikosi cha Ujenzi na lazima nisema hapo nilifurahi sana. Basi miaka ilipita. Mimi nilikuwa mwandishi wa habari Daily News, tena nilijenga jina. Sasa nikawa napishana na yule jamaa huko kapandishwa cheo na yuko JWTZ. Jamaa anajaribu kunisalimia na mimi napita zangu kimya, namnunia kabisa.

Nilimwona mshenzi, mnyama, na kila kitu kibaya ndo ilikuwa yeye! Angefanikiwa kuingiza na kunimwagia uchafu wake ningejiona mchafu mpaka leo! Miaka kama 20 imepita sasa na bado nina uchungu naye.Jamani nyie wanaume nawaambia kubaka kinaathari zake kwa wanawake. Unataka raha ya dakika na unamwachia mwenzio na uchungu wa maisha! Wengine mpaka wanakuwa wagonjwa wa akili.

Kwa nini nimeamua kuzungumzia kubakwa kwangu hapa, ni kwa sababu naona wasichana wengi wanabakwa, halafu wanaamua kunyamaza kimya. Kisa wakienda polisi na hospitali wanahofia kuambiwa ni Malaya au walitaka wenyewe! Hata mwamanke mwenzako anaweza kukufokea kuwa ulitaka mwenyewe. Tanzania, wanaume walikuwa na usemi wao kuhusu wanawake na ngono. Walisema eti ukimwomba mwanamke halafu akijibu ndiyo, manake ndiyo atafanya. Akisema labda, manake atafanya, akisema hapana, manake hapana. Lakini jamani tendo si inakuwa tamu kama wote mmekubali? Na kama angefanikiwa kuingiza si angeniumiza sana!

Wengine wanasema ningemshitaki. Je, ningemshitaki ingekuaje? Kwanza jeshini mimi ningepewa Extra Drill mpaka niumie au kufungwa jela ya jeshi iliyojaa maji na mbu kusudi niteswe. Kumbuka ilikuwa Tanzania na yule alikuwa ni Kepiteni wakati huo na mimi nilikuwa Private. Hakuna ambaye angekuwa tayari kunisikia zaidi ya wenzangu maPrivate, na yeye alijua hivyo. SHENZI TAIPU!

Friday, May 27, 2011

Wanafunzi Wamwua Mwalimu Wao Iringa!!

Duh! Yaani nimesoma kwa mshangao mkubwa habari za hao akina dada kumwua mwalimu wao! Kisa alitaka kumbaka moja wao. Ubakaji ni mambo mazito, mimi ningempa adhabu ya kukatwa dhakari, lakini kuua hapana! Inaninikubusha ile sinema ya The Women of Brewster Place, yule dada shoga anabakwa na kundi la wahuni halafu anapata kichaa na kumwua kwa kumpiga kichwana mara kadhaa, baba aliyekuja kumsaidia.

Mungu ailaze roho ya Dr. Mafingo, mahala pema mbinguni. Amen. Hao wasichana watafute wakili mzuri la siyo watasota huko jela miaka mingi.

****************************************************************
Kutoka Gazeti la NIPASHE

Wanafunzi wa Kike Wamuua Mwalimu
By Godfrey Mushi
27th May 2011

Wanafunzi wa Chuo cha Uuguzi cha Bulongwa kilichoko Wilaya ya Makete mkoani Iringa, wamemuua kwa kumshambulia kichwani mkufunzi wa chuo hicho, Dk. Jumbe Mafingo, kwa madai ya kupinga jaribio lake la kutaka kumbaka mwanafunzi mwenzao.

Taarifa za awali za makachero wa polisi zilieleza kuwa mkufunzi huyo aliuawa baada ya kutuhumiwa kwamba alitaka kumdhalilisha kijinsia mwanafunzi wa kike, Jean Laison Mwakabuta kwa kutaka kumbaka.

Tukio hilo la kuuawa kinyama kwa mkufunzi huyo ambaye ni mwalimu wa nidhamu chuoni hapo, lilitokea juzi usiku nyumbani kwake mjini hapa.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Evarist Mangalla, Dk. Mafingo alifikwa na umauti baada ya mwanafunzi huyo kuamua kwenda nyumbani kwake usiku ili kumkabidhi maelezo yake ya kimaandishi kuhusu sababu zilizomfanya alale nje ya chuo.

Ilielezwa kuwa muda mfupi baada ya kuingia kwenye nyumba ya mwalimu huyo, mwanafunzi huyo alianza kupiga kelele kuwa anabakwa.

Alisema kufuatia kelele hizo, wanachuo wengine waliamka katika vyumba vyao na kwenda hadi eneo la tukio na kuanza kumshambulia kichwani mkufunzi huyo hadi kumuua.

Kamanda Mangalla alisema Dk. Mafingo aliuawa kwa kushambuliwa na kitu kizito kichwani.

“Huyu Jean Laison Mwakabuta, aliambiwa na Dk. Mafingo ambaye ni mwalimu wa nidhamu chuoni hapo, aandike maelezo ya maandishi kwa sababu gani alilala nje ya chuo,...baada ya kuandika maelezo hayo, aliamua kuyapeleka nyumbani kwa mkufunzi huyo usiku, sasa baada ya kugonga mlango na hatimaye akaruhusiwa kuingia, alianza kupiga kelele kwamba anabakwa…na ndipo wanafunzi wenzake waliposikia kelele wakaamka na kukimbilia eneo hilo na kumshambulia mkufunzi huyo hadi kufa,” alisema Kamanda Mangalla.

Ilidaiwa kuwa siku moja kabla ya tukio hilo, uongozi wa chuo hicho cha Bulongwa ulitoa ridhaa kwa wanachuo wote kwenda kutembea nje ya chuo kwa lengo la kuwapunguzia msongo wa mawazo ya masomo na Jean Laison Mwakabuta hakurejea chuoni hadi siku iliyofuata.

Kamanda Mangalla, alisema wanachuo wanne akiwamo mwanafunzi Jean, wametiwa mbaroni kuhusiana na mauaji hayo.

SOURCE: NIPASHE

Thursday, May 19, 2011

African Maid Causes Downfall of IMF Chief!

(Picha iliyotengenezwa na kompyuta kuiga mambo yaliyotokea kwenye Sofitel Hotel mjini New York kati ya mhudumu wa hoteli na Mkuu wa IMF, Dominique Strauss-Kahn inatoka TOGO FORUM)

Wadau, Mkuu wa IMF ambaye anakabiliwa na mashitaka kadhaa ya ubakaji mjini New York, Bwana Domique Strauss-Kahn amejiuzulu wadhifa wake! Bi Nafissatou Diallo (32) raia wa Guinea, Afrika Magharibi anadai kuwa Mzee huyo alimlazimisha kumnyonya ume wake na baadaye alimwomba nyuma. Ndo Bi Diallo alikimbia kwenda kumshitaki. Bwana Strauss-Kahn amefungwa bila dhamana kwenye gereza la Rykers Island.

Yaani mwanamke maskini kutoka Guinea amemfanya Mkuu wa IMF ajiuzulu! Kwa kweli sipendi kusikia habari za ubakaji na kama ni kweli basi huyo Bwana Strauss-Kahn anastahili kukatwa hiyo dhakari yake asiyojua kuitumia vizuri. Ila nina wasiwasi kweli kuwa maisha ya huyo Mama yatakuwa magumu sasa. Watamnyanyasa yeye na familia yake. Kazi hatapata, na wanaweza hata kumwua! Hao matajiri wanapesa za kunyaynyasa watu waliowakosea acheni tu! Tayari wameanza kumchafua Bi Diallo kwa kusema ni mgonjwa wa UKIMWI kwa vile anakaa kwenye fleti maalum za waathirika mjini New York.

Mnaweza kusoma habari zaidi kwa KUBOFYA HAPA:

Friday, January 28, 2011

Mtoto wa Miaka Mitatu Abakwa Kimara

Kuna mdau kutoka Kimara, Dar es Salaam ambaye ameleta habari hizi za kusikitisha na kutisha!

********************************************************************
MIMI NI MKAZI WA KIMARA STOP OVER GARAGE- KUNA MTOTO WA MIAKA 3 ALIBAKWA HAPA MAENEO YA KIMARA GARAGE MBELE KIDOGO YA KIMARA STOP OVER,,,KWA KWELI MKASA WENYEWE UNASIKITISHA UWEZI AMINI KAMA WATU NA AKILI ZAO WANAWEZA KUFANYA KITENDO CHA KUSIKITISHA HIVI HASA JESHI LA POLISI,,,,STORY YENYEWE ILIANZA HIVI,,,MTOTO MDOGO KWA JINA TUNAMHUIFADHI ALIRUDI KWA MAMA YAKE MCHANA KWEUPE AKILALAMIKA MAUMIVU SEHEMU ZA SIRI.

MAMA YAKE BAADA YA KUMPEKUA AKAMKUTA AKIVUJA DAMU KIBAO ILIYOCHANGANYIKA NA MBEGU ZA KIUME,,HUKU SEHEMU ZAKE ZA SIRI ZIKIWA ZIMECHANIKA KABISAAAAA. MTOTO BAADA YA KUULIZWA NANI KAKUFANYA HIVI AKASEMA FULANI (JINA TUNAMUHIFADHI)KWA KWELI MAMA ALIPIGA UKUNGA MAJIRANI WAKAJAA PALE,,BAADA YA KUAMBIWA KILICHOTOKEA WATU WAKAKIMBILIA KWA MBAKAJI NA MAWE NA MATAIRI WAMCHOME MOTO.

JAMAA TAYARI ALIKUWA KASHATOROKA SAA NYINGI,,IKABIDI WATU WAMSAIDIE MAMA KUMBEBA MTOTO NA KUMKIMBIZA KITUO CHA POLISI CHA MBEZI KWA YUSUF(MBEZI LUIS) WAKAPATA PALE PF3 YA MATIBABU NA RB YA KUMKAMATA MBAKAJI NA KESI IKAFUNGULIWA PALE,. KWA KWELI ILIBIDI UFANYIKE MCHANGO KIDOGO KUMSAIDIA YULE MAMA MAANA ALIKUWA HANA MUME WALA UWEZO KAZI YAKE YEYE NI KUWACHOTEA MAJI MAJIRANI NA KUPATA VIJISENT ANAVYOJIKIMU YEYE NA MWANAWE,.

MTOTO AKAPELEKWA MWANANYAMALA AKALAZWA...JIONI SASA NDO IKAWA KIMBENDE MAANA YULE MVUTA BANGI AU MBAKAJI ALIRUDI NA KUANZA KUWATUKANA WATU KWAMBA HAWAWEZI KUMFANYA LOLOTE,, ALIKUWA ANATUMIA JEURI YA KAKA YAKE ANA PESA NA HATA MKIMUWEKA NDANI ATATOKA TU (KAKA YAKE ANAFANYA KAZI TBL).NA POLISI AKIENDA ATATOKA TU ATA KWA UCHAWI.

WATU WAKAPIGA SIMU POLISI DEFENDER YA POLISI IKAJA IKAMBEBA SAA 5 USIKU AKALALA KITUO CHA POLISI MBEZI KWA YUSUF,,ALILALA LITUONI SIKU MBILI BILA HATA KUPELEKWA MAHAKAMANI. ,KATIKATI YA HIZO SIKU 2 SIJUI NDO MPELELEZI WA KESI AU POLISI HATA HATUJUI (HAWAKUWA WAMEVAA UNIFORM)KUTOKA KITUO CHA POLISI MBEZI WALIENDA HOSPITAL YA MWANANYAMALA NA KUMLAZIMISHA DAKITARI ANAYESIMAMIA VIPIMO VYA UBAKAJI AWAPE FAILI WARUDI NALO KITUONI DAKTARI AKAKATAA KATA KATA KUWAPA,,(KISHERIA HAMNA DHAMANA KWA MBAKAJI NI MAGERZA TU).

CHA AJABU SIKU YA 3 KESI IKACHAKACHULIWA NA POLISI ANAYEIPELELEZA! YULE MBAKAJI AKAPANDISHWA MAHAKAMANI KWA KESI YA UKABAJI BADALA YA UBAKAJI PATAMU HAPO..CHA AJABU HATA MJUMBE WA NYUMBA KUMI KUMI NDO ALITOA KIBALI CHA DHAMANA. HIVI KWELI HII TANZANIA TUTAFIKA KWELI KWA UNYAMA HUU? NASIKIA MAMA WA WATU KAJIFUNGIA NDANI NA MWANAWE KAZI YAKE NI KULIA TU. WATU WALIPOJARIBU KURUDI KITUONI PALE MBEZI ASKARI WAKASEMA ETI WALIKOSEA BADALA YA KUANDIKA MBAKAJI WAKAANDIKA MKABAJI.

WALIPORUDI KUJA KUMKAMATA YULE MBAKAJI TAYARI ALIKUWA AMETOWEKA KUSIKOJULIKANA. KAKA WA MBAKAJI ALITOKA AKAENDA KWA MAMA WA MTOTO NA KUANZA KUMTISHA KAMA AKIFUATILIA ZAIDI HII KESI ATAMHUAMISHA MJINI. INASIKITISHA JAMANI HEBU MTUSAIDIE HATA KUISUKUMA HII MSG TAMWA HATA KWENYE VYOMBO VYA HABARI ILI HAWA POLISI WALIOCHUKUWA PESA WASHITAKIWE....NAOMBA MSINITAJE JINA MIMI NILIERIPOTI VITISHO VIMEKUWA VIKUBWA !

ASANTENI SANA

MLALAMIKAJI

Wednesday, November 17, 2010

Mzee Noma (ONYO- Lugha Chafu)



Haki ya Mungu ningemwona huyo mzee mshenzi ana kwa ana ningempiga! HANA ADABU!!!! Ana mawazo finyo na mdomo mchafu! Haheshimu wanawake hata kidogo!

Wito kwa akina mama mlio karibu naye, mchukue mafimbo mpige, uzuri zaidi, mkate hiyo dhakari yake maana hasthali kuwa nayo!!!

Friday, November 27, 2009

Mzee wa miaka 86 Ambaka Msichana mdogo Dar!

Duniani kuna mambo! Huko Kinyerezi, Dar es Salaam, Mzee mwenye miaka 86 kambaka msichana mwenye miaka mitano! KHAA! Yaani alishindwa kumpata hata malaya wa kumridisha! Na wanasema kuwa alimpenya huyo mtoto! Nadhani huyo mzee atafia jela hivi karibuni! DUH!

Kama miaka mitano iliyopita hapa Boston, kuna Babu mwenye miaka 83 alimtia mimba msichana mwenye miaka 9! Hapa watoto wengine wana vunja ungo mapema. Yule binti alikuwa anakwenda na kikundi fulani cha watoto kwenye nyumba za wazee kuwatembelea na kuwa marafiki na wazee. Si mnajua nyumba za wazee hapa ni nyumba za kusibiri kifo. Tulishangaa kusikia bado vinaongelea na umri huo.

*******************************************************************

Kutoka ippmedia.comhttp://www.ippmedia.com

Elderly man (86) charged with raping kid (5)
By Jacqueline Mosha
27th November 2009

An elderly man, Omari Kitambo (86), was on Thursday arraigned in the Ilala District Court charged with raping a five-year-old girl (name withheld).

The accused, a resident of Kinyerezi on the outskirts of Dar es Salaam, appeared before Resident Magistrate Joyce Minde.

According to Asma Shemweta who read the charge sheet, the accused had carnal knowledge of the girl.

The accused pleaded not guilty to the charges and was remanded in custody after failing to meet bail conditions.

Wednesday, March 18, 2009

Ubakaji na mauji ya watoto wadogo huko Iringa!

Jamani, hivi huko Iringa kuna nini? Kuna habari kuwa watoto wadogo yaani chini ya miaka sita wanabakwa huko! Sasa huo ni mchezo gani? Najua Afrika Kusini watu wanabaka hao watoto wakidhani eti watapona UKIMWI! Na nashangaa baba zima anataka nini na mtoto mdogo hivyo. Kama hao wahalifu watakamatwa napendekeza wakatwe ume/bolo zao mara moja! Tena mbele ya umati!

********************************************************************

Kutoka Lukwangule Blog:

VITENDO vya ubakaji vimeanza kushamiri mkoani hapa, huku matukio ya hivi karibuni yakionesha wanaokumbwa na sakata hilo wakiwa ni watoto wa kike wenye umri chini ya miaka sita.

Katika matukio mawili yaliyotokea ndani ya wiki tatu, mtoto mmoja amekufa baada ya kufanyiwa unyama huo huku mwingine akiendelea kutibiwa katika hospitali ya Mkoa wa Iringa. Tukio lililopelekea mmoja wa watoto hao kufa lilitokea juzi, baada ya mtoto huyo (jina linahifadhiwa) kubakwa na watu wasiojulikana hadi mauti yake yalipomfika na hatimaye kutupwa kwenye bonde dogo la mlima Tagamenda uliopo mita 600 kutoka stendi ndogo ya mabasi ya mikoani ya Ipogolo ya Iringa mjini.

Polisi waliokuwepo kwenye eneo hilo walifanikiwa kuutoa mwili wa mtoto huyo mwenye miaka mitano kutoka katika bonde hilo lenye miti mingi yenye miba akiwa hana nguo na amelowa damu sehemu zake za siri, huku umati mkubwa wa watu waliokuwepo wakiangua kilio kwa uchungu.

Polisi hao wakiongozana na baadhi ya ndugu wa mtoto huyo waliukimbiza mwili huo katika hospitali ya mkoa wa Iringa kwa ajili ya uchunguzi zaidi na wakati tukienda mitamboni ulikuwa umehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali hiyo.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Iringa, Dk Oscar Gabone alisema katika tukio lingine lililohusisha mtoto mwingine wa miaka mitano kubakwa kwamba lilitokea Februari 22 katika milima ya Gangilonga mjini Iringa aliyepokelewa hospitalini hapo Februari 23.

Mama mzazi wa mtoto huyo, Jamila Mashaka alisema kwa uchungu kwamba siku ya tukio, mtoto wake na wenzake walikuwa wakicheza nje ya nyumba yao baada ya kujipatia chakula cha jioni.

“Ilikuwa majira ya saa moja jioni, baada ya kupata chakula cha jioni mwanangu huyu na wenzake wakawa wanacheza nje, hata hivyo dada yake alikuja chumbani kwangu baadaye akiniambia kwamba mdogo wake haonekani,” alisema.

Alisema jitihada za kumtafuta katika maeneo wanayoishi na kwa marafiki zake aliokuwa akicheza nao hazikuzaa matunda na ndipo ilipofika saa 4.30 usiku wa siku ya tukio walipkwenda kutoa taarifa Polisi.

“Kesho yake saa 4.30 asubuhi nililetewa taarifa kwamba kuna mtoto yuko hospitali ya mkoa, na nilipokwenda kumtazama nikabaini kwamba ni wa kwangu. Nawashukuru madaktari wanaomuhudumia kwasababu hivi sasa anaendelea vizuri,” alisema.

habari hii kwa hisani ya Frank wa HabariLeo Iringa