


Blogs in Kiswahili, the main African language of EAST AFRICA.



Maswali na majibu kuhusu sinema ya Bongoland II.
Mwalimu Gibbons na watoto wake

.jpg)
Mungu atunusuru!
********************************************************************************
Watu wawili wametekwa katika ofisi ya mgombea rais wa chama ca Democrats wa Marekani, Senator Hillary Clinton. Ofisi enyewe ni ya kampeni yake na iko Rochester, New Hampshire.
Sakata umeanza saa 7 mchana huu na hivyo navyoandika bado inaendelea. Mama moja aliyekuwa ndani ya hiyo ofisi na mtoto wake wa miezi sita aliachiwa huru pamoja na mtoto.
Jamaa aliyeteka nyara ofisi amejifunga mkanda ambayo anasema ina bomu! Ofisi sasa imezungukwa na polisi, SWAT (FFU) na Secret Service. Kama jamaa hajisalimishi msishangae mkisikia kuwa jamaa katunguliwa kwa kupigwa risasi kichwani na FFU.
Pia polisi wameamuru ofisi za wagombea rais wengine maDeomcrats, Barack Obama na John Edwards zifungwe kwa usalama wa raia na wafanyakazi.
Marekani bwana!
http://www.cnn.com/2007/POLITICS/11/30/clinton.office/index.html
Macho ya waiingereza yamekuwa Sudan tangu jumapili kwa sababu ya mwalimu kutoka Uiingereza anayefundisha katika shule ya International huko. Mwalimu Gillian Gibbons ana miaka 54. Wanafunzi wake wana miaka saba na lazima bado wako kwenye umri wa kupenda toys (vitu vya kuchezea). Walikuwa na mdoli wa darasa. Aliwapa zoezi la darasa kumpa jina. Wengi walichagua jina Mohamed. Kwa kidemokrasia wengi wanashinda. Hao watoto wa miaka 7 ndo waliochagua jina la Mohamed. Majina mengine yaliyopendekezwa ni Hassan na Abdullah.
Huyo mwalimu namhurumiwa sana. Lazima hakuelewa uiislamu vizuri. Hakuna picha ya mtume Mohamed na wala hakuna sanamu yake. Hivyo kumwita huyo mdoli Mohamed ilikuwa tusi kubwa kwa waislamu. Pia kaanza kufundisha Sudani juzi juzi tu. Kwa wazungu kutoa jina kwa midoli ni kawaida. Sasa anashitakiwa kwa kosa la kutukana uislamu.
Sasa nauliza hivi, hao waSudani hawakuweza kumwelezea kuwa kafanya kosa na kumwelimisha. Baadala yake walitishia kumchapa viboko 40 na kufungwa jela.
Leo mahakama huko wameamuru afungwe siku 15 na awe deported akitoka. Tayari waSudani wanaonekana wabaya duniani kwa kuua raia wao wanye asili ya Afrika hasa kabila la Dinka huko Darfur.
Nawauliza wasomaji waislamu, je, walivyofanya waSudani ni sawa au walizidisha kipimo na hii tukio?
Na hao watoto je, waadhibiwe kwa kuchagua hiyo jina au waelimishwe sheria za uisilamu? Lazima wataathirika maishani mwao wakikumbuka mwalimu wao mpendwa alivyonyanyaswa kwa kosa hiyo.
Hii kesi inasisitiza umuhimu wa watu wanaoenda nchi zingine kuelewa mila na desturi na dini za huko!
Kwa habari zaidi someni:
http://www.cnn.com/2007/WORLD/africa/11/29/sudan.bears/index.html
http://www.abcnews.go.com/International/story?id=3931681&page=1
http://www.cfnews13.com/News/International/2007/11/29/briton_convicted_in_sudan_blasphemy_case.html

Mwigizaji maarufu wa Namibia marehemu 'N!xau' katika sinema ya The Gods Must be Crazy!
Mgombea nafasi ya rais wa Marekani kutoka chama cha Democrats, Senator Barack Obama, amekiri kuwa alitumia madawa ya kulevya akiwa kijana.
Hii picha nimeona kwa Michuzi. Ni ya barabara mpya huko Bagamoyo. Sasa nauliza hii ni barabara ya matofali ni ya magari au ya waenda kwa mguu? Naona kuna watu wanatembea kwa mguu na nyuma naona gari inakuja. Sasa hii njia itadumu kweli kama ni ya magari? Hebu nyie wahandisi tuambie.
Hivi Bi Kidude ana miaka mingapi? Sasa anadai kuwa ana mika 113. Lakini anasema hajui alizaliwa lini. Mimi nilimwona Zanzibar mwaka 1993 na wakati huo alisema ana miaka 80. Kwa hiyo nahisi kama ana miaka 94.
Rappers hawana dogo. Wametoa wimbo wa kumtukana Dr. Jan Adams aliyemfanyia mama yake mzazi Kanye West, upasuaji wa urembo na kusababisha kifo chake.
- Dr. Jan Adams alikuwa na TV show kwenye Discovery Channel, Plastic Surgery Before & After
- Alikuwa siyo Board Certified
- Oprah amekaa kimya. Alimwalika kwenye show yake kama mtalaam wa upasuaji wa urembo kumbe jamaa ni feki! Watu wengi waliamini 'utalaamu' wake kwa vile alikuwa kwenye Oprah.
http://www.drjanadams.com/
Cheki website ya jamaa, mambo mengi eti yako "down for maintenance" LOL!
Kinachonisikitisha katika hii kesi ni kuwa huyo jamaa ni mweusi, alikuwa anaonekana kama mtaalamu wa mambo ya plastic surgery. Kumbe jamaa tapeli!

