Showing posts with label Bongoland II. Show all posts
Showing posts with label Bongoland II. Show all posts

Saturday, April 07, 2012

Msanii Lulu Anashikiliwa na Polisi!

Msanii, Elizabeth Michael aka. Lulu (18) anashikiliwa na Polisi Oyster Bay, Dar es Salaam, baada ya ugomvi na mpenzi wake marehemu Steven Kanumba.

Kamanda wa Polisi Wilaya ya Kinondoni Charles Kenyela, amethibitisha kushikiliwa kwa Lulu
Habari zinasema kuwa Kanumba alikuwa anajiandaa kutoka na mpenzi wake usiku wa kuamkia leo, alipokuwa bafuni anaoga akamsikia Lulu akiongea kwenye simu na mwanaume mwingine. Alipotoka bafuni kumwuliza kuhusu simu, Lulu alimsukuma kwenye ukuta, Kanumba kaanguka kufa pao hapo!  Ina maana kuwa kifo cha Kanumba umesabishwa na 'Domestic Violence'!

Mungu ailaze roho ya Steven mahala pema mbinguni.   Ameacha pengo kubwa katika fani ya sinema Tanzania.


pichani - Msanii  Elizaneth Michael aka. Lulu, ambaye alikuwa Mpenzi wa Steven Kanumba

Elizabeth Michael , aka, Lulu,  Julai 1, 2007, alipokuja kwenye audition ya Sinema Bongoland 2, aliigiza katika hiyo sinema kama, Chapati Girl
Lulu akipiga pozi hii karibuni


Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

Kuna picha nyingine ya Lulu HAPA:

Kwa habari za kilio nyumbani kwa KANUMBA MTEMBELEE KAKA MICHUZI KWA KUBOFYA HAPA:

KUSOMA SIMULIZI YA UGOMVI NA MDOGO WAKE KANUMBA ALIYESHUHUDIA BOFYA HAPA:

Wednesday, November 02, 2011

King Kiki Safarini Boston

Saraji, Maneno, King Kiki, mimi na Charles Jackson

King Kiki Cambridge, MA leo jioni

Namkabidhi King Kiki Kanda ya Bongoland 2
Wadau, mwimbaji maarufu wa Tanzania, King Kiki, atafanya  Maonyesho maalum, huko Leominister, MA siku ya jumamosi.  Leo kanitembelea nyumbani kwangu Cambridge. Alikuja na vijana wengine wa Leominister ambao leo ndo nimewajua.  Nilikuwa nasikia majina tu. Nimefurahi mno kuwakaribisha ingawa kwa muda mfupi. Nilimpa  King Kiki zawadi ya DVD ya Bongoland II.

Tuesday, September 20, 2011

Kiswahili Bila Mipaka - Swahili Without Borders

SWAHILI WITHOUT BORDERS



(Kiswahili bila Mipaka)
Aurelia Ferrari

By Josiah Kibira – Fall 2011

How many of you from East Africa would believe me if I told you that there are people in Ghana who are learning to speak Swahili? You would probably say, it could happen. But then what if I said the Swahili teacher is a French woman. You have to admit, that would pique your curiosity.

It’s like in the movies. A French woman teaching Swahili in West Africa. Well, it is not a movie it is real. Her name is Aurelia Ferrari. For her it started as a teenager when she traveled to Senegal on a reforestation camp. As a child, her father traveled a lot and brought gifts and stories from all over the world. This increased her curiosity of the world. After she completed her high school she decided to volunteer in a youth exchange program in her native Paris. Before long she was sent to work as a volunteer in Kenya.

While in Kenya she worked with youth programs and later she would concentrate on working with street children.

She is the first one to admit that clearly Africans do not need guidance from Europeans and that in fact, Africans have tougher survival aptitude than their counterparts in Europe or America considering the hard life they face on a daily basis. Africa was her calling. She had to go there.

It was during her encounter with street children in Kenya that she started to learn Swahili. Her interest grew when she returned to Paris. She enrolled in a Swahili teaching institute and later pursued a PhD in “Sheng”, a slang based Swahili originating in Kenya . And, of course, with a PhD, she could now teach anyone how to speak Swahili. She is fluent in Swahili, English, French and a little bit of Arabic.

She was asked, “Of all languages that you know, why Swahili?”

She said, “ This was to show Africa in a positive light”. She admits that it would have been easy for her to teach French, but feels that the colonial and imperialistic past associated with the French in Africa would not encourage people’s intercultural understanding and commitment to peace and justice. I think she has a good point. She is also very quick to point out the importance of Swahili as a language in the world noting that not only do over 100 million people in the world speak it, but it is taught in over 100 universities in the world. Her mission to teach Swahili to the world has landed her assignments including a two-year stint in Paris and over three years in Ghana.

What is impressive about Aurelia’s immersion in the Swahili culture is her commitment not to use Africa as a place to acquire another entry on her already impressive resume, but to make Africa her home. It was refreshing to find a European who lives in Africa and goes to Europe for a summer vacation.

I was also curious why Ghanaians were interested in Swahili. She said some students take the course as a ploy to get into a second year of the Bachelor’s program, but those who decide to pursue Swahili end up at the University of Dar-Es-Salaam in Tanzania, where they pursue higher levels of Swahili language. Ghana has 70 other native languages and English remains the official language.

In her linguistic studies, she has written a book about the “sheng” Swahili dialect from Kenya and is now working on a book about Swahili in the Democratic Republic of Congo.

But it was her Swahili/French instructional book called “Swahili Bila Mipaka” – or “Swahili Without Borders” that caught our attention.

It is a manual that uses the communicative approach, which is a modern method in language teaching and learning, where the communication and the culture take an important part in the learning process.

The emphasis is on the meaning. The communicative approach gives great importance to the diversity: diversity of types of interaction, diversity of exercises and diversity of subjects.

The data used is authentic data like advertisings, spontaneous conversations and written material. For each lesson, there is a transcription of a conversation.

The manual caught our attention because Aurelia expressed interest in using our film Bongoland 2 as part of conversation transcripts in the manual. After students listen to these conversations, they then go through a series of exercises for comprehension.

Naturally, we were curious why she chose Bongoland 2 to be included in her instructional book. She said, “Other films in Swahili languages concentrated more about the story itself but Bongoland 2gives so many aspects of Swahili culture – the relation between men and women, social organization and the daily life.”

She adds “For instance, we always see on the news that Africans try to run away from Africa, but this film shows us something different and more realistic. There are so many interesting initiatives going on in Africa

We learn so much in this film, to watch this film is like a linguistic and cultural immersion in Tanzania!”

As a French/African woman, Aurelia stands out as a woman on a mission to do good in the world. Her early exposure to the world influenced her not only to see other people as equals, she even took steps to becoming one of them. We can all learn from this great teacher. To see people for who they are, their culture, their feelings and know how they communicate. Isn’t this a simple formula for world peace and understanding? We think so.

Tuesday, September 06, 2011

Mzee Kipara Yu Hoi Anahitaji Msaada!

(Mzee Kipara akijaribu kusimama)
(Mzee Kipara Majuzi akijaribu kutoka kitandani)(Mzee Kipara Mwaka 2007 Akipelekwa nyumbani baada ya kushuti Scenes zake katika Sinema, Bongoland II, katika sinema hiyo aliigiza kama Imam)

Wadau, sielewi nchi yetu Tanzania! Mzee Kipara aka. Mzee Fundi Saidi ni nyota na mkongwe katika sanaa za maigizo Tanzania. Lakini ona anavyoteseka na kuishi maisha ya dhiki! Wasanii wengi wa Tanzania wanaishia kuishi maisha ya dhiki na kusahauliwa kabisa!


Someni Malalamiko ya Mzee Kipara kwa KUBOFYA HAPA:


****************************************************************************
Kutoka Fundi wa Kombo Blog http://fundirkombo.blogspot.com/

Napenda nitoe masikitiko yangu kwa wasanii wa Sanaa ya Maigizo wote Nchini kwa kutoonyesha msimamo wa pamoja ili kuweza kumsaidia Mzee wetu Mzee Kipara (Fundi Said) ambaye kwa sasa ana afya ambayo sio nzuri pamoja na uzee lakini hali ngumu ya kimaisha ndio inayochangia zaidi.

Mzee Kipara ni msanii wa muda mrefu sana katika Tasnia hii ya sanaa ya Uigizaji, ni muigizaji mkongwe sana katika Taifa letu, kwa wale wasiomjua alianza kuigiza sanaa toka mnamo mwa miaka ya 1964 enzi za RTD (Redio Tanzania) kwa sasa TBC hii kwa faida ya vizazi vya sasa msio fahamu hili.

Baadae Mzee kipara walianzisha kikundi cha maigizo ambacho kikawa kinarushwa na TV ya ITV ambacho amedumu nacho kwa muda mrefu sana kikiitwa Kaole. Katika kipindi chote hiki cha Kaole aliwafundisha wasanii wengi sana ambao kwa sasa wengi mnawasikia au mnaziona kazi zao kwenye Luninga zenu.

Cha kunisikitisha wengi wao hawajaonyesha upendo wao hata kidogo kwa mzee huyu, nitakua mnyimi wa Fadhila kama sita mshukuru sana Stephen Kanumba nakumbuka alikua msanii wa kwanza kwanza kwenda kumsaidia huyu Mzee; namshukuru sana, najua wapo wengine ambao pia walikwenda kwa nyakati tofauti tofauti kuweza kumuona huyu mzee au hata kumsaidia kwa chochote kile.

Mimi binafsi kama mwakilishi wa KAPINGAZ Blog napenda kuwashukuru wote waliofanya hivyo, ila ombi langu kwenu ninyi wasanii wa sanaa ya Maigizo ni kwa nini msiandae tamasha lolote ambalo mnaweza mkakusanya kiasi kikubwa cha fedha kikaweza kumsaidia huyu Mzee wenu badala ya kwenda mmoja mmoja kumuona huyu Mzee, kumbukeni na nyie ni vijana kwa leo itafika wakati mtazeeka kama huyu mzee na watatokea wengine mmewafundisha hiyo sanaa naamini na nyie mnaweza mkasikitika kama mzee huyu.

Naomba niwape mfano wa Dada Asha Baraka, Mkurugenzi wa African Star (Twanga Pepeta) nampongeza sana huyu dada aliweza kuandaa tamasha la Dansi kwa ajili ya kukusanya michango ya kumsaidia Mzee Muhidin Ngurumo ili aweze kupata matibabu vizuri, na mpaka leo naandika masikitiko yangu, Mzee Ngurumo leo anapanda kwenye stage kuimba na wenzie katka tamasha la sikukuu ya Idd el Fitr.

Nawaomba wasanii wote katika sanaa ya maigizo muweze kulitazama hili la Mzee Kipara kama ni jambo lenu wote, na hata mnapokua mnakwenda kwenye vikao vyenu na BASATA muweze kuliongelea hili, ili muweze kua na umoja wenye nguvu wa kuweza kusaidiana kwenye matatizo kama haya. Tunawaona mara kwa mara mnaenda kufanya shughuli mbali mbali sehemu tofauti, hasa za kujipongeza katika mafanikio flani ni vema mnapokua huko mkumbushane la mzee huyu msimuache aishi maisha haya ni aibu kwenu wasanii wote hasa zaidi nyie mliopitia Kaole.

Naomba wana Blog wenzangu tushirikiane katika hili. Asante

************************************************************

Kama Unataka kuchangia Mzee Kipara tafadhali tembelea Blogu ya Kaka Michuzi:
au BOFYA HAPA

Thursday, February 18, 2010

Tanzia - Reginald Mhango (Reggie) Bosi wangu Daily News

Reggie na copy yake ya sinema Bongoland II. Sehemu ya hiyo sinema ilipigwa nyumbani kwa Reggie huko Magomeni Mikumi. Nilipomwomba kupiga sehemu ya sinema hapo allikubali bila kusita na pia alifurahi kuona jinsi wanavyotengeneza sinema. Alifurahi uchapa kazi wa crew waliotoka Marekani.
Mimi, Reggie Jr. (katikati) na Mzee Reggie Mhango. Picha hii tulipiga siku ya October 27, 2009 nyumbani kwa Reggie. Nilisikia kutoka kwa kaka Michuzi kuwa alipata stroke lakini hajambo. Nilimpigia Reggie simu kutoka Marekani mwezi wa saba na kumwaidi kuwa nitafika siku hiyo na nilifika. Alifurahi sana.
************************************
Wadau, nimepokea kwa majonzi habari ya kifo cha bosi wangu mpendwa nilipokuwa Daily News, Reginald Mhango (Reggie). Reggie alikuwa na utu, uvumilivu, na upendo kwa kila mtu. Nakumbuka nilikuwa napata shida nikiwa na mimba mwaka 1989. Tumbo ilianza kuwa kubwa na kutembea ilikuwa shida. Reggie aliniambia nikae nyumbani mpaka nijifungue na kumaliza maternity leave. Si hiyo tu lakini kwa kweli sikumbuki kumwona akiwa na hasira au akigombana na mtu. Alitufundisha sisi waandishi chipukizi uandishi wa habari hasa, na kutusaidia katika kuandika habari safi...to the point! Nje ya kazi, ilikuwa hata kama una shida binafsi alikuwa tayari kusikia na kutoa mawaidha.
Mnakumbuka ile kesi ya Mzee Athumani Ali Maumba. Yule babu wa Magomeni aliyekuwa analawiti watoto wa kike wa primary, Reggie alisaidia hizo habari zichapishwe. Hamwezi kuamini lakini mpaka hiyo kesi ya Maumba ilikuwa kama mwiko kuandika habari hizi. Hata waandishi wa habari wengine walikataa kuripoti. Mimi ndo nilikubali kwenda huko kwenye hiyo shule Kisutu na kuchunguza. Baada ya ripoti kukamilika wakuu walitaka kuzuia, Reggie aliongea. Kesho yake walitoa para mbili tena kwa kificho. Baada ya kuona si mwisho wa dunia, habari za Maumba zikawa front page. Msishangae na kusema najiona,lakini mkumbuke kuwa wakati huo kulikuwa na magazeti machache nchini. Daily News (serikali) Uhuru (Chama) na Mfanyakazi, Kiongozi (Wakatoliki). Redio ilikuwa RTD tu. TV ilikuja baadaye.
REST IN ETERNAL PEACE REGGIE. WE WILL MISS YOU DEARLY BUT YOU IMPARTED GREAT KNOWLEDGE AND WISDOM IN US AND WE WILL PASS IT ON!
Mnaweza kusoma habari zaidi kwa Kaka Michuzi.
Na pia someni Daily News:

Wednesday, December 09, 2009

Zawadi za Krimasi kutoka Kibira Films



Looking for a Christmas present idea...try this one from Kibirafilms.com.

Order one to day and have it delivered before Christmas!

HAPPY HOLIDAYS !

Wednesday, May 13, 2009

Josiah Kibira: One Film at a Time

May 11th, 2009 - ANJ Online

From Tanzania to Kansas, comes a man on a mission to change the international film industry, one film at a time.

By: Nneka Onyilofor

Josiah Kibira is that man; the man that came to the U.S. to attend school at Bethany College in Kansas, and ended up founding his own production company, Kibira Films. For more than 20 years in the U.S., Josiah dreamed big, and turned those dreams into reality. By day he’s a software testing engineer, but during the rest of his life, he’s a writer, director, and producer. And it all began with an interest he had in writing scripts as he exercised this interest while he was in college. After college, he moved to Minnesota and began to recruit actors from local Twin Cities colleges and Universities for his first film titled, “Bongoland.”

Many Tanzanian’s may recognize the term “Bongo,” as it is a slang term for the country itself. However, Josiah added a spin to the title of his first featured film by calling it, “Bongoland,” which he describes as a more inclusive term. Bongoland was produced in 2003, which is a film about an immigrant who comes to the U.S. to look for opportunities and runs into a lot of issues that many immigrants can relate to. In this film, the main character makes a decision that brought about the film Bongoland II in 2007. With the support of UCLA, Josiah’s first film proved to be a success in a unique fashion. This uniqueness comes from the fact that both films are spoken in the Swahili language.

Josiah was motivated to do these films in Swahili because there was a lack of movies in this language that is spoken so widely in Africa and in the U.S. Bongoland was performed in about 60 percent Swahili, and in Bongoland II, Swahili was spoken throughout the entire film; 100 percent of the time.

“There are so many things that have to be done that are not known…Africa is full of those people that did great things but it’s only the Edi Amen’s that get the lime light.” There are so many things that are particular to Africa that Hollywood is not interested in,” stated Josiah. Thus, in 2005, Josiah produced a film titled, “Tusamehe,” which means forgiveness, and is about the AIDS epidemic. Swahili is spoken in about 70 percent of this film as well.

So what else can be said about Josiah Kibira? We’ll, his next goal is to continue to break down more barriers. “When you are in Africa, African Americans are looked at as heroes and when I got here, that’s what I was expecting. I was expecting my brothers to embrace me, but it was different,” he stated. This reality is going to open up a dialogue about the relationship between Africans and African Americans in the U.S. in Josiah’s upcoming documentary titled, “Two Africas in America.

” The ultimate goal of this documentary is to dispel the myths that both cultures have about the other and to begin the healing process that is well needed. Currently Josiah is marketing and promoting his films at film festivals in the U.S., UK, and Tanzania. His films have already been featured in various film festivals including the Pan-African film festival in Los Angeles.
“Most of the movies I do are very male centered…you need to find something that is female centered people told me.” Thus, a film that many women can relate to is another project Josiah is working on in addition to his upcoming documentary.
----
For more information you can email info@kibirafilms.com or go to http://www.kibirafilms.com/. Look out for a preview of Josiah Kibira’s new documentary at the African Global Roots Art Festival on July 25th, 2009 from 5pm-midnight at the Grand Rios Ramada Hotel in Brooklyn Park, MN.

Sunday, April 26, 2009

Maonyesho ya Bongoland II - Kansas City

Mwongoza sinema na mtunzi wa sinema, Bongoland II, Josiah Kibira, ameniletea hii barua aliyoandikiwa na watu wa Kansas City Film Festival.

*****************************************************************************
Bongoland II screening in KC a success

Josiah,

Thank you again for working with me, the Sister Cities Association of Kansas City (SCAKC) and The KC Film Jubilee to bring your film Bongoland II to our movie market. Our annual international film festival is being held from April 22nd – 26th. Bongoland II was shown Thursday night at 7:45 PM in our new AMC Main Street theater in downtown KC. It ran with English subtitles, and was well attended by a diverse audience which included Tanzanian immigrants. From 6:00 – 7:30 PM, we also hosted a reception for the Bongoland opening - attended by the mayor, members of our city council and other supporters in the beautiful Marquee Bar & Grill located in the theater.

On a personal note, I had a great experience watching Bongoland II! It was the first movie by an African filmmaker that I have seen. I loved the scenery, the drama and the complexity of modern day issues confronted by people living and working in Tanzania today. For those who can understand Swahili, I’m sure the movie experience would have been even better – not having to read English subtitles. I wish you great success as an up and coming filmmaker.

I hope we can work with you again in the future, and invite you to visit our lovely city one day. In June we are hosting a visit by the Tanzanian ambassador. FilmFest is a film extravaganza that includes a juried film show and is held here every year. For more information about FilmFest and the KC Filmmakers Jubilee got to www.kcfilmfest.org and www.kcjubilee.org.

All the best!

Eslun Tucker

Thursday, April 23, 2009

Bongoland II Itaonyeshwa Kansas City Leo


Wadau, sinema Bongoland II itaonyeshwa katika Kansas City Film Festival leo jioni (7:45pm),

Mnaweza kupata habari zaidi hapa:

http://www.kansascity.com/238/story/1155127.html

Wednesday, February 18, 2009

WaBongo Hatujali!

Msanii, mwandishi na mwanablogu maarufu, Freddy Macha, ameandika feature katika gazeti la The Citizen. Inahusu sinema za Josiah Kibira, Bongoland na Bongoland II na jinsi waBongo wasivyothamini kazi za wenzao. Na anasema kweli. Sisi waBongo tuna tabia mbaya sana ya kupondana. Ukiona mtu anafanya mema unajaribu kumvuta chini ili muwe sawa!

*****************************************

Kutoka gazeti la THE CITIZEN

Saddening indifference to Tanzanian Trailblazers

Freddy Macha

I am watching Bongoland Two, the movie by Kibira Films, for the third time now. I have seen it alone, with a filmmaking colleague and, tonight, with a group of friends of various nationalities. For those who do not know Kibira films, it is a company run by US-based Tanzanian filmmaker Josiah Kibira.

"He is pressing the right buttons," I am saying at the end.

"Ah, this is a load of rubbish," a fellow "Bongolander" chips in.

"Rubbish?" asks Raul, a Brazilian friend.

"I would not waste my money buying this."

"Waste of money?" Zak from Pakistan interjects, incredulously.

Bongo guy: "No one would behave like Juma. Such an ugly girlfriend?"

Juma is the main character of the Bongoland series. In both Bongoland One and Two, Juma is frustrated by his employers and community.

In Bongoland One he finds life in the US tough after he was made redundant. Soon, he is lodging at a friend's flat where he cannot pay the rent. He then breaks up with his white girlfriend whose father is a racist.

The American authorities discover he is an illegal immigrant and finally we see him driving to the airport, hoping for a better life back in Tanzania.

Bongoland Two sees Juma settled in Tanzania with a good job, a place to live and a local girlfriend. Problems, nevertheless, still thrive. His boss favours a lazy colleague, who happens to be his girlfriend.

The place he lives at is noisy and people smoke indoors. When he complains to the landlord or his corrupt boss he is told he is arrogant because he has been living overseas. Top that with a serious family crisis, and life remains a struggle.

At the end of Bongoland Two, we see an introspective Juma walking along a beach, most probably in Dar es Salaam. Josiah Kibira manages to show that Juma's problems may not be resolved by moving from one country to another.

Maybe we shall see Bongoland Three. Maybe the two flicks are enough to make us reflect and create a hypothesis. One of the roles of cinema is to stimulate social thought.

I am interested in two things ? what my fellow viewers are debating about and the implications of the Kibira Films venture.

I notice that all the foreigners in my flat are surprised at the negative reaction of some of my fellow country folks.
Raul, the Brazilian (cameraman and freelance filmmaker), has very captivating views.

"You guys have to thank God that this guy, what is his name again?"

"Kibira."

"He is trying to make a non-Hollywood film. Personally, I did not know there was a language called Swahili. I did not know Tanzania. I had never heard the word 'Bongo'. I have heard there is a Brazilian coach teaching your national team. But there is no information. So making such a film is a good thing. It opens the eyes of people from other countries."

One of the "Bongo" guys is sneering and making faces. He is clearly not amused.

"Won?t you even support by buying the films?"

"No."

It is sad and shows how we see each other.
Here is a man trying to sell us globally. Unlike those films you see from home made in a rush, with inferior sound and acting, Josiah Kibira strives towards quality.

Tanzania has not made a significant film since Fimbo Ya Mnyonge back in the mid-1970s. Some American television stations have even interviewed and spoken about these Swahili films. Kibira has already been invited to major international festivals including the prestigious Edinburgh and Zanzibar events.

Not only is he smart at marketing himself on the Internet, he is giving old and new Tanzanian actors a chance to be seen on the screen. He works with American film crews and technicians, consequently broadening working relationships between the two countries.

This is history in the making. In other words, it is the future of our entertainment industry. Although the $30,000 Kibira invested in the venture might be a small amount in terms of filmmaking, this is an expensive enterprise that demands a lot of time, determination and commitment, and should be applauded by every ?Bongolander?.

We should ask ourselves how various world-famous brands (be it Japanese cars or Bollywood films) came to be established.

We need to support the Buy Bongo, Buy Tanzania brand such as the Kibira Films venture. For more info visit http://www.kibirafilms.com/

http://www.thecitizen.co.tz/newe.php?id=10575

Thursday, February 12, 2009

Bongoland II Inaoyeshwa Los Angeles



Sinema Bongoland II, inayeshwa katika Pan African Film Festival huko Los, Angeles California.

Itaonyeshwa tena kesho Februari 13 saa 2:45 jioni (8:45pm) na Jumatatu 2/16 saa 1:15 jioni (7:15pm).

Bongoland II: There’s No Place Like Home (2008/Tanzania/140min)
Dir: Josiah Kibira -Panorama

Are we poor or short of cash? This is a question Juma wrestles with upon arriving in his native Bongoland. While happy to be re-united with his family, over time he is frustrated by the level of poverty that almost everyone around him faces on a regular basis. He is convinced that most people are not short of cash but poor – which is a state of mind.
Screening Times:

2/6, 1:00pm

2/13, 8:45pm

2/16, 7:15pm

Tuesday, January 27, 2009

Bongoland II Itaonyeshwa Los Angeles


Wadau sinema Bongoland II itaonyeshwa mjini Los Angeles, California kwenye Pan African Film Festival ambayo itafanyika mwezi wa pili.

*************************************************************

Bongoland II: There’s No Place Like Home

(2008/Tanzania/140min) Dir: Josiah Kibira Panorama

Are we poor or short of cash? This is a question Juma wrestles with upon arriving in his native Bongoland. While happy to be re-united with his family, over time he is frustrated by the level of poverty that almost everyone around him faces on a regular basis. He is convinced that most people are not short of cash but poor – which is a state of mind.

Screening Times:

2/6, 1:00pm

2/13, 8:45pm

2/16, 7:15pm
Tembelea:

Wednesday, October 29, 2008

Bongoland II itaonyeshwa Edinburgh Kesho 10/30/08


Bongoland II will be screened in Edinburgh Scotland on this thursday, October 30th at 20:15 The venue is at the FILM HOUSE CINEMA. The address is 88 Lothian road.

For more details.We hope you can attend and see this rare Swahili film which shows the unexposed talents of artists from East Africa and particularly Tanzania. This special screening is part of the Africa-in-motion film festival which started on October 23rd and will end on November 2nd.

This is UK's premiere of Bongoland II.You can get more details about this movie from the movie's OFFICIAL WEBSITE.

In case you cannot make it to the screening, you can buy the DVD from the ONLINE STORE.To watch the movie's trailer CLICK HERE

Tuesday, September 16, 2008

Bongoland II itaonyeshwa Uingereza


Kutoka: Kibira Films Blog:

BONGOLAND II INAKUJA EDINBURGH - UINGEREZA - MWEZI UJAO

Haya wadau wa Uingereza Bongoland II inakuja mwezi ujao wa Oktoba tarehe 30 saa mbili . Pata habari kamili hapa . Bongoland II imechaguliwa katika sinema za Kiafrika (Africa in Motion) ambazo zitaonyeshwa Uingereza kuanzia October 23 Mpaka November 2, 2008

Kama uko Edinburgh au mitaa ya karibu unaombwa ujitahidi kuwakilisha Tanzania na ujionee mwenyewe jinsi wasanii wa ki-Tanzania walivyotuwakilisha katika ngazi za kimataifa. Kuhudhuria kwako kutaonyesha waandalizi wa festival hii kuwa wadau na marafiki zao wana nia ya kutaka sinema za kwao zionyeshwe katika festival kama hizi.

Kama hutaweza kuudhuria siku hiyo, unaombwa kupitisha ujumbe huu kwa marafiki wote walio karibu na mji wa Edinburgh.

Kwa sasa sinema hii inapatikana katika DVD. Unaweza ukaagiza mtandaoni kwa kubofya hapa. Kumbuka kuwa wengi wetu kwa mara nyingi tuna-rent sinema kutoka Hollywood videos au Blockbusters. Tukumbuke kuwa ku-renti kwetu kunachangia katika kuendelea kutengeneza sinema nyingi za Kimarekani. Ni kwa sababu hiyo hiyo na sisi tujitahidi kuwaunga mkono wasanii wa Kibongo ili fani hii iendelee kukua ili utamaduni wetu nao uwakilishwe katika ngazi zaidi nje ya Bongo.

Kwa habari zaidi kuhusu sinema hii au sinema nyingine kutoka Kibira Films tafadhali bofya hapa.

SHUKRANI!!

Tuesday, September 02, 2008

Bongoland II DVD - Zinapatikana Boston


Wadau mliopo Boston, ninazo DVD za Bongoland II.


Wasiliana na mimi chemiche3@yahoo.com

Friday, August 22, 2008

DVD za Bongoland II Zinapatikana sasa!


Kwa wadau wa Boston, nitakuwa nazo wiki ijayo. Unaweza kuwasiliana na mimi kupitia e-mail chemiche3@yahoo.com.

************************************************************************
Taarifa kutoka Kibira Films:

BONGOLAND II - IMETOKA KWENYE DVD - AGIZA LEO

Kusubiri kumekwisha BONGOLAND II imetoka katika DVD. Jipatie nakala yako kwa kubofya hapa.

Kama kawaida ys filamu za Kibira Films , unapojipatia filamu ya Bongoland II unapata zaidi ya filamu yenyewe katika DVD. Utaweza kuona jinsi sinema hiyo ilivyotengenezwa pale mjini Dar, katika vitongoji vya Manzese, Magomeni na Tenki Bovu. Pia utaona milolongo iliyowatesa watengenezaji wa sinema hii walipokuwa pale mjini Dar. Vile vile utaona watu wote walioshiriki katika utengenezaji wa sinema hii kama waliotupatia nyumba, usafiri na kadhalika. Pia katika DVD hiyo utaona scene ambazo ingawaje zilikuwa sehemu ya sinema, lakini hazikutumiwa katika makala ya sinema ya mwisho.

Mwisho unapata sinema iliyotengenezwa na wasanii wa kitanzania waliokubaliwa katika matamasha ya kimataifa kuanzia Zanzibar, Marekani na Uingereza mwezi wa kumi mwaka huu wa 2008.

Kibifa FIlms inakuhakikishia kuwa sinema hii itakuburdisha na kukufurahisha sana maana kusema kweli kama hadithi inavyosema "kuondoka kutoka nyumbani kama Juma ni rahisi kuliko kurudi nyumbani"

Jipatie makala yako hapa.

Kwa wale wote mlioko Bongo, mipango iko mbioni kwa kuwaletea BONGOLAND II!!

Wednesday, August 20, 2008

Bongoland II itaonyeshwa mjini Chicago Leo 8-20-08


Sinema Bongoland II itaonyeshwa tena leo jioni huko Gene Siskel Film Center mjini Chicago. Time 6:15pm (Saa 12 na robo jioni saa za Chicago).
**************************************************************************

Bongoland II: There's No Place Like Home
Gene Siskel Film Center Find Tickets
164 N State St (at Randolph St) Loop/West Loop, Chicago Map
312-846-2600
El: Brown, Green, Orange, Pink, Purple (rush hrs) to State/Lake; Red to Lake; Blue to Clark/Lake. Directions
BONGOLAND II: THERE’S NO PLACE LIKE HOME 2008, Josiah Kibira, Tanzania, 100 min. With Peter Omari, Thecla Mjatta

In his first film BONGOLAND (2003), Josiah Kibira related the misadventures of Juma, a Tanzanian immigrant in Minnesota. In this self-sufficient sequel, Juma returns to Tanzania (aka Bongoland) to manage a company. His American-style ideas about efficiency and motivation meet with a less than enthusiastic response, and, when Mom’s visit produces some jaw-dropping revelations, he discovers that his relationship to his homeland has become even more tenuous. The film’s sharp, angry satire recalls such Ousmane Sembene classics as XALA and GUELWAAR. In Swahili with English subtitles. DV-CAM video. (MR)


Wednesday, August 20, 6:15 pm



Wednesday, August 13, 2008

Walimu wa sinema 'stunts'



Hao ndo walifundisha akina Peter Omari, Shaffi Abdul na Charles Magali stunts zao kwenye sinema Bongoland II. Nilishangaa waigizaji Bongo walivyoniambia kuwa eti watu wanapigana kweli hadi kuumizana wakiwa kwenye shuti. Hizi sinema za Hollywood hakuna kuumizana ingawa utadhani mtu kapigwa kweli kweli.

Tulivyokuwa Bongo niliwashauri watu wajifunze hizo stunts maana walikuwa wanatoa mafunzo bure. Zaidi ya kipigana aliwaonyesha kidogo defensive driving (yaani kuendesha gari kwa stunt). Hapa Marekani watu wanalipa maelfu ya dola kujifunza.

Mwalimu Jason Hilton alitaka kufundisha wabongo wengi lakini hakuna aliyejitokeza zaidi ya waliokuwa kwenye sinema. Nilivyowauliza vijana fulani kama wanataka kujifunza waliuza eti watalipwa shilingi ngapi. Somo inatolewa bure halafu unataka ulipwe? Si ukachukua huo utalaamu uliyopata na uende ukatengeneza pesa? Au, ni wazo baya kwangu?

Bongoland II itaonyeshwa Chicago Ijumaa


Kibira Films inawatangazia kwa mara nyingine kuwa BONGOLAND II inaonyeshwa ijumaa hii mjini Chicago. Unakumbushwa kuja kuiona sinema ambayo kwa kweli imeonyesha ukomaaji wa fani ya usanii wa sinema katika Tanzania.
Watu wengi waliooiona sinema hii wameipenda sana. ANGALIA MAONI HAPABONGOLAND II itaonyeshwa saa kumi na mbili na robo Ijumaa hii tarehe 15.Ukumbi ambapo sinema hii itaonyeshewa ni GENE SISKEL FILM CENTER. Mkurugenzi wa sinema hii atakuwapo katika ukumbi kujibu maswali mwishoni.Anwani ya Ukumbi ni 164 North State Street Chicago Il 60601
SIMU YAO NI - 312-846-2600 KARIBUNI!!

Monday, July 21, 2008

Kwa nini sinema za Tanzania zilifanya vibaya ZIFF

Nimeona watu wanaulizia kwa nini sinema ya Bongoland II haikupata zawadi ZIFF, wala hata mention. Sina jibu. Sikuwepo huko ZIFF.

Ila nimeona hii story kwenye gazeti ya Daily News (TZ) leo iliyoandikwa na kaka Michuzi.

Naona Dr. Martin Mhando anasema kuwa ingawa Bongoland II, ilikuwa sinema pekee ya kiTanzania kwenye mashindano ya 'Feature' ina hadithi mbili, ya familia ya Juma na hadithi ya yeye kurudi Bongo. Alisema ni sinema nzuri kwa ujumla.

Haya, niwaulize wadau walioona sinema ya Bongoland II, mliionaje?

**************************************************************************
ZIFF wants more focus to develop film industry

MUHIDIN ISSA MICHUZI in Zanzibar
Daily News; Tuesday,July 22, 2008

The Zanzibar International Film Festival (ZIFF) believes that developing a funding structure to link up with creative capacity and a local distribution structure is the answer if Tanzania's infant film industry is to grow.

The Chief Executive Officer of ZIFF, Dr Martin Mhando, said this in an exclusive interview with the 'Daily News' here yesterday, adding that one of the key problems with African cinema depended entirely on distribution.

"ZIFF has undertaken research looking into distribution hence the Tanzania Film Chain Study Report that was presented at ZIFF 2008", he said, adding: "We hope we can have time to again discuss it at length with our filmmakers with the view of looking into how to link distribution to production", said Dr Mhando at the climax of the 11th edition of ZIFF on Saturday.

On the poor participation of Tanzanian films at the annual festival, the ZIFF CEO expressed deep concern, saying something should be done to reverse the situation as it makes them feel bad about it.

He said the ZIFF plans to begin serious discussions with local filmmakers so that production efforts on the ground were supported. He, however, pointed out that there a need to encourage local filmmakers to see the use of festivals in marketing or at least promoting their films.

"Festivals generally do not need to chase after filmmakers -- the opposite is the case. However ZIFF needs filmmakers just as filmmakers need ZIFF", he quipped. The ZIFF CEO emphasised that to learn how to distribute films internally was paramount to putting the industry on its feet.

Dr Mhando said until Tanzania reached the point that audiences who clamour for the local product are satisfied one can not say the country has an industry. "Therefore let us deal with what distribution structures exist in the country, know who our audiences are and how to reach them and then start making films for those audiences and their distribution structures" he stressed.

On Bongoland II, which was Tanzania's lone nominated entry in the ZIFF 2008, Dr Mhando said it is a good film but had its setbacks on its story board. He said while the juries did not discuss film by film but one of the things that have been said about Bongoland II is that it went well until it began the story of the family's intrigue.

"The family intrigue needed to be brought in earlier and better fused into the script for the film to work. "Currently it looks like there are two stories - about the young man's problems of resettlement and then the family's", he concluded.