Showing posts with label Academy Awards. Show all posts
Showing posts with label Academy Awards. Show all posts

Sunday, March 02, 2014

MKenya Lupita Nyong'o Ashinda Oscars!!!!




Mwigizaji, Lupita Nyong'o kutoka Kenya ameshinda tuzo za Oscar!!!!!! Anakuwa mwafrika mweusi wa kwa kushinda. Mzungu Charlize Theron kutoka Afrika Kusini amewahi kushinda.  Kweli Hollywood inabadilika maana miaka mingi ilikuwa vigumu mwigizaji mweusi kuteuliwa na hasa kushinda! Katika miaka 86 ya historia ya Oscar Lupita, ni mwanamke wa saba mweusi kupokea Tuzo ya Oscar!

HONGERA LUPITA NYONG'O!!!!


Lupita Nyong'o leo kabla ya Tuzo za Oscars Kuanza

Lupita Nyong'o katika sinema  12 Years a Slave

Lupita akicheza na mwimbaji Pharell


Afrika Inawakilishwa Katika Oscars ya Mwaka Huu!

Wadau, tunangojea kwa hamu kuona kama Lupita Nyong'o kutoka Kenya na Barkhad Abdi mwenye asili ya Somalia watashinda katika tuzo za Oscars leo jioni.

Kwa mara ya kwanza Nchi mbili za Afrika zinawakilishwa katika Tuzo za Juu za Oscars.

Lupita Nyong'o  yuko katika Best Supporting Actress (yaani mwigizaji bora wa kike katika sinema si mwigizaji mkuu).  Na Barkhad Abdi anagombea Best Supporting Actor (yaani mwigizaji bora wa kiume - si mwigizaji mkuu).

Jamani, jamani sijui waafrika tukoje, huyo Barkad kasemwa na waSomali wenzake, eti ana sura mbaya na mengine! Khaa! 

Na nisimsahahau Chiwetel  Ejiofor ambaye ni Mwingereza mwenye asili ya Nigeria.  Yeye anagombea Mwigizaji bora wa kiume. (Best Actor).

Kushoto ni Lupita Nyong'o na Kulia ni Barkhad Abdi

Mara nyingi nchi ya Afrika inayopata sifa katika Osars ni Afrika Kusini.  Waigizaji wao wazungu kama Charlize Theron wanatambulika sana.  Charlize alikuwa Msouth Afrika wa kwanza kupata Oscar.

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

Saturday, January 18, 2014

WaAfrika Wawili Wako Katika Orodha ya Waigizaji Bora Mwaka Huu - OSCARS

Wadau, haijwahi kutokea! Waafrika wawili wako katika mashindano ya Oscars mwaka huu!  Lupita Nyong'o kutoka Kenya ameteuliwa katika kundi la Waigizaji Bora wa Kike (Supporting), na pia Kijana Barkhad Abdi kutoka Somalia amaeteuliwa katika kundi la Waigizaji Boara wa Kiume (Supporting). Je, watashinda?

Bi Lupita aliigiza kama Mtumwa katika sinema 12 Years a Slave.  Alikuwa anaigiza katika television ya Kenya. Pia alisoma Uigizaji hapa Marekani katika Chuo Kikuu cha Yale. Alichaguliwa kuigiza katika sinema 12 Years a Slave mara baada ya kumaliza Yale.

Lupita Nyong'o katika sinema 12 Years a Slave



Barkhad Abdi aligiza katika sinema Captain Phillips. Kabla ya kupata nafasi ya kuigiza katika sinema hiyo, alikuwa anaendesha limo huko Minneanapolis, Minnesota.  Barkhad alienda Open Casting Call na kuchaguliwa.  Wadau nikiwaambia muende Open Call, Nenda!

Barkhad Abdi Katika Sinema Captain Phillips



Kuona Orodha ya wote walioteuliwa kaitka Oscars 2014 BOFYA HAPA:


Wednesday, July 31, 2013

Afisa Uhamiaji Asimamishwa Kazi Kwa Kukaa Vibaya Kazini!

  http://www.arabnews.com/news/458770

JEDDAH: Saudi authorities arrested a local airport officer after social networks published a picture of the man showing him in a “rude sitting position” while checking the passports of passengers, a newspaper reported on Sunday.


The picture, which was captured by a Saudi passenger at the airport in Jeddah, showed the uniformed officer giving his back to the passengers as he sat on the desk and his legs rested on a chair.

Newspapers had earlier said the unnamed officer was suspended this week after the photograph triggered online criticism by hundreds of viewers.

“The passport officer was ordered arrested after his suspension this week ... the director of the passports department ordered his arrest for questioning about his behavior and uncivilized way of sitting,” the Arabic language daily Arar said.

.

The Saudi Immigration Sitting in a Rude Position


Saturday, January 15, 2011

Clip From Maangamizi the Ancient One



Hii ni clip ktuoka sinema Maangamizi the Ancient One. Ni sinema ya kwanza ambayo Tanzania ilietua katika Academy Awards (Foreign language category). Ingawa haikuchaguliwa kuwa katika sinema tano bora za mwaka huo 2000 ilikuwa hatua kubwa sana kwa Tanzania kujulikana katika dunia ya sinema.

Je, sinema gani kutoka Tanzania itakuwa ya pili kutueliwa? Kwa wasiojua mimi niliigiza kama Nesi Malika katika Maangamizi, ilikuwa sinema yangu ya kwanza. Ilipigwa Bagamoyo mwaka 1994 kabla mji haujajengwa kama ilivyo sasa.

Monday, January 28, 2008

Academy Awards wanaijua Tanzania







Mwaka 2001, Tanzania ilipeleka sinema, Maangamizi The Ancient One, kushindana katika, 74th Academy Awards. Ilishindana katika kipengo cha 'Foreign Language' (Lugha za kigeni). Sinema hiyo ilikuwa ya kwanza kutoka Tanzania kupelekwa. Ilikuwa kati ya sinema 51, zilizopelekwa na nchi kadhaa huko mwaka huo.

Hatimaye haikufika katika sinema tano bora zilioingia katika raundi ya mwisho kupewa tuzo ya Oscar. Mwaka huo sinema ya 'No Man's Land' kutoka Bosnia Herzegovina, ilishinda.

Ili sinema ifike Academy Awards ni lazima iwe na sifa kadhaa. Sinema ya Maangamizi ilikuwa na sifa zote.

Je, sinema ya Bongoland II, itakuwa sinema ya pili kutoka Tanzania kupelekwa Academy Awards?

Mnaweza kusoma Press Release ya Academy Awards 2001, hapa:

Tutaona mambo yatakavyokuwa.