Showing posts with label Assassination. Show all posts
Showing posts with label Assassination. Show all posts

Saturday, January 18, 2014

Tunamkumbuka Mh. Patrice Lumumba

 Mh. Patrice Lumumba alikuwa Waziri Mkuu wa Congo baada ya nchi hiyo kupata Uhuru kutoka Ubelgiji. Aliuawa na CIA, na maiti yake iliyeyshhwa kwenye pipa la tindikali.  Wadau, wazungu waliuumiza sana maendeleo ya Afrika miaka ya 1960's-1970's wakati nchi nyingi za Afrika zilikuwa changa. 

******************

Kutoka THE GUARDIAN

Patrice Lumumba: the most important assassination of the 20th century

The US-sponsored plot to kill Patrice Lumumba, the hero of Congolese independence, took place 50 years ago today
patrice lumumba
Patrice Lumumba became the first prime minister of the Democratic Republic of the Congo in 1960, and was killed in 1961. Photograph: EPA
Patrice Lumumba, the first legally elected prime minister of the Democratic Republic of the Congo (DRC), was assassinated 50 years ago today, on 17 January, 1961. This heinous crime was a culmination of two inter-related assassination plots by American and Belgian governments, which used Congolese accomplices and a Belgian execution squad to carry out the deed.
Ludo De Witte, the Belgian author of the best book on this crime, qualifies it as "the most important assassination of the 20th century". The assassination's historical importance lies in a multitude of factors, the most pertinent being the global context in which it took place, its impact on Congolese politics since then and Lumumba's overall legacy as a nationalist leader.
For 126 years, the US and Belgium have played key roles in shaping Congo's destiny. In April 1884, seven months before the Berlin Congress, the US became the first country in the world to recognise the claims of King Leopold II of the Belgians to the territories of the Congo Basin.
When the atrocities related to brutal economic exploitation in Leopold's Congo Free State resulted in millions of fatalities, the US joined other world powers to force Belgium to take over the country as a regular colony. And it was during the colonial period that the US acquired a strategic stake in the enormous natural wealth of the Congo, following its use of the uranium from Congolese mines to manufacture the first atomic weapons, the Hiroshima and Nagasaki bombs.
With the outbreak of the cold war, it was inevitable that the US and its western allies would not be prepared to let Africans have effective control over strategic raw materials, lest these fall in the hands of their enemies in the Soviet camp. It is in this regard that Patrice Lumumba's determination to achieve genuine independence and to have full control over Congo's resources in order to utilise them to improve the living conditions of our people was perceived as a threat to western interests. To fight him, the US and Belgium used all the tools and resources at their disposal, including the United Nations secretariat, under Dag Hammarskjöld and Ralph Bunche, to buy the support of Lumumba's Congolese rivals , and hired killers.
In Congo, Lumumba's assassination is rightly viewed as the country's original sin. Coming less than seven months after independence (on 30 June, 1960), it was a stumbling block to the ideals of national unity, economic independence and pan-African solidarity that Lumumba had championed, as well as a shattering blow to the hopes of millions of Congolese for freedom and material prosperity.
The assassination took place at a time when the country had fallen under four separate governments: the central government in Kinshasa (then Léopoldville); a rival central government by Lumumba's followers in Kisangani (then Stanleyville); and the secessionist regimes in the mineral-rich provinces of Katanga and South Kasai. Since Lumumba's physical elimination had removed what the west saw as the major threat to their interests in the Congo, internationally-led efforts were undertaken to restore the authority of the moderate and pro-western regime in Kinshasa over the entire country. These resulted in ending the Lumumbist regime in Kisangani in August 1961, the secession of South Kasai in September 1962, and the Katanga secession in January 1963.
No sooner did this unification process end than a radical social movement for a "second independence" arose to challenge the neocolonial state and its pro-western leadership. This mass movement of peasants, workers, the urban unemployed, students and lower civil servants found an eager leadership among Lumumba's lieutenants, most of whom had regrouped to establish a National Liberation Council (CNL) in October 1963 in Brazzaville, across the Congo river from Kinshasa. The strengths and weaknesses of this movement may serve as a way of gauging the overall legacy of Patrice Lumumba for Congo and Africa as a whole.
The most positive aspect of this legacy was manifest in the selfless devotion of Pierre Mulele to radical change for purposes of meeting the deepest aspirations of the Congolese people for democracy and social progress. On the other hand, the CNL leadership, which included Christophe Gbenye and Laurent-Désiré Kabila, was more interested in power and its attendant privileges than in the people's welfare. This is Lumumbism in words rather than in deeds. As president three decades later, Laurent Kabila did little to move from words to deeds.
More importantly, the greatest legacy that Lumumba left for Congo is the ideal of national unity. Recently, a Congolese radio station asked me whether the independence of South Sudan should be a matter of concern with respect to national unity in the Congo. I responded that since Patrice Lumumba has died for Congo's unity, our people will remain utterly steadfast in their defence of our national unity.

Tuesday, February 19, 2013

Taarfif ya Jumuiya ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA) - Kuwawa kwa Father Mushi

TAARIFA YA JUMUIYA YA MAIMAMU ZANZIBAR (JUMAZA) TAREHE 18/2/2013 KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSIANA NA TUKIO LA KUUWAWA KWA KUPIGWA RISASI PADRI EVARIST MUSHI WA PAROKIA YA KANISA KATOLIKI MJINI UNGUJA

Shukurani njema zote anastahiki Allah Ambaye ametuwezesha kuwa hai tukiwa na afya njema. Tunamuomba Allah atuwafikishe kufanya mema na aujaalie uhai wetu wote uwe kwa ajili ya kumtumikia Yeye katika Dini hii ya Kiislamu. Rehema na amani ya Allah zimwendee kipenzi chetu, mtukufu wa viumbe Mtume Muhammad (Sallallaahu ‘alayhi wasallam), masahaba zake, jamaa zake na wale wote waliomfuata kwa wema mpaka Siku ya Malipo.

Ama baada ya hayo,Jumuiya ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA) inachukua fursa hii kutoa taarifa rasmi kwa vyombo vya habari kufuatia tukio la kupigwa risasi na kuuwawa kwa Padri Mushi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mjini jana tarehe 17/2/2012 Beit – El – Ras.

JUMAZA kwa mshtuko mkubwa imepokea kwa masikitiko taarifa ya kuuwawa kwa Padre Mushin na inalaani kwa nguvu zote kitendo hicho cha kiharamia ambacho kinaashiria kuitia doa Zanzibar kisiwa cha amani na ukarimu tokea enzi na enzi. Kufuatia kadhia hii JUMAZA inawataka Wanzanzibari wote wa dini na madhehebu zote kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu na kuendelea kutunza amani na mshikamano tulionao chini ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa na kutotoa mwanya kwa watu au vikundi ambavyo vina nia mbaya ya kutaka kuleta kutokuelewana kwa wananchi kwa malengo yao binafsi.

Aidha JUMAZA inaungana na kauli iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuliagiza Jeshi la Polisi nchini kufanya uchunguzi wa kina na waharaka ili kubaini nani waliohusika na tukio hili na hatimaye sheria ichukue mkondo wake.

Aidha JUMAZA inaliomba Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kiuadilifu na usioambatana na shindikizo la mtu au kikundi chochote ili hatimae ukweli halisi ujulikane na bila ya kuwadhuru wasiohusika.

JUMAZA inakemea vikali kauli za baadhi ya vyombo vya habari vinavyonasibisha waislamu na tukio hili na kuvitahadharisha vyombo vya habari ikwemo magazeti na redio hizo kutoanza kutoa taarifa ambazo kwa makusudi zinaweza kupandikiza chuki na uhasama katika jamii na hatimae kuotesha mizizi ya fitna na kupelekea Taifa kuingia kwenye machafuko bali viachiwe vyombo vinavyohusika kufanya uchunguzi wake na kutoa taarifa sahihi. Aidha JUMAZA inaziomba Serikali zote mbili kuwa waamgalifu sana katika kipindi hiki kwa kujizuia kutoa maneno yanayoashiria kuhusisha tukio hili na upande fulani wakati bado uchunguzi unaendelea.

Imesaniwa na:
KATIBU WA JUMAZA
MUHIDDIN ZUBEIR MUHIDDIN.

Sunday, February 17, 2013

Priest Shot Dead in Zanzibar Another Beheaded on Mainland

 Kutoka : http://atlasshrugs2000.typepad.com/atlas_shrugs/2013/02/priest-shot-dead-in-zanzibar-pastor-beheaded-on-mainland.html

 Sunday, February 17, 2013

Padri Auwawa Zanzibar Akielekea Kanisani Leo!

TAARIFA  KUTOKA JAMII FORUM:

Default Update: Watatu wahojiwa Zanzibar kuhusiana na mauaji ya Padre na Taarifa ya Polisi


17/02/201




Padre Evaristus Mushi


UPDATE/TARIFA MPYA (saa nane u nusu mchana) Taarifa ya Polisi:

Watu watatu wanashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za mauaji ya Padre Mushi. Tafadhali bofya vipande vya picha zilizopachikwa hapo ili kuvikuza na kusoma taarifa ya Polisi inayoonekana hapo (shukurani kwa Francis Dande).









UPDATE/TAARIFA MPYA (saa saba mchana) Taarifa ya habari Radio One Stereo:

Taarifa ya habari ya Radio One Stereo iliyosomwa saa 7 mchana imeripoti kuwa Padre Mushi aliuawa na watu walipolisimamisha gari la Padre huyo alipokuwa akielekea katika kanisa la Mtakatifu Theresia lililoko eneo la Mtoni, na alipopunguza mwendo ili awasikilize, ndipo alipopigwa risasi kichwani na kusababisha gari alilokuwamo kukosa uelekeo na kuigonga nyumba iliyokuwa jirani. Watu walioshuhudia tukio hilo walimchukua Padre Mushi ili kumwahisha hospitalini katika jitihada za kuokoa uhai wake, lakini alifariki dunia. Waliomwua Padre Mushi bado hawajakamatwa.
-----------------------


Akina mama wakilia kwa uchungu kuomboleza kifo cha ghafla cha kupigwa risasi Padre Evaristus Mushi kilichotokea leo asubuhi muda mfupi kabla ya kuanza Misa ya Jumapili kwenye kanisa la Kigango cha Mtoni, Zanzibar. (Picha na Martin Kabemba via Lukwangule blog)
Taarifa kutoka Zanzibar zikiripotiwa na mwanahabari Donisia Thomas wakati kipindi cha Patapata cha WAPO radio FM kinaendelea, zinasema kuwa Padre Evaristus Mushi wa Kanisa la Parokia ya Minara Miwili huko Zanzibar amepigwa risasi majira ya saa moja asubuhi -na watu wasiofahamika- na kufariki dunia.

Taarifa za kufariki kwake zimethibitishwa na madaktari kutoka hospitalini alikopelekewa katika harakati za kuuokoa uhai wake.


Padre Mushi aliuawa akiwa anashuka kwenye gari lake tayari kuingia Kanisani kwa ajili ya kuendesha misa ya kawaida ya Jumapili katika kanida la Mtoni, mjini St. Joseph. Inaelezwa kuwa gari lisilofahamika lilifika na kufyatua risasi zilizomlenga Padre Mushi sehemu ya kichwani na hivyo kumsababisha majeraha yaliyokuwa yakivuja damu nyingi.


Mwanahabari anasema tukio hilo limezua taharuki kubwa miongoni mwa waumini ambao wamekataa kuahirisha ibada iliyokuwa iendeshwe na Padre huyo na kusema ikiwa kusudio ni kuwaangamiza Wakristo wote, basi na waangamizi wafike Kanisani wawaangamize wakiwa pamoja.


Jeshi la Polisi limeshafika katika eneo la tukio na kuanza uchunguzi.


Wakizungumza kuhusu hilo, raia wamesema hawana imani na Polisi wala Madaktari na hawatarajii jipya zaidi ya ripoti kuwa suala hili ni la uhalifu kwa kuwa tukio kama hili liliwahi kutokea mwishoni mwa mwaka jana kwa Padre Ambrose kupigwa risasi na taarifa zilisema lilikuwa ni tukio la kihalifu na kwamba risasi hazikutumika jambo ambalo halikuwa kweli kwani Padre Ambrose alikutikana na risasi alipohamishiwa katika hospitali ya Taifa, Muhimbili.

Kwa taarifa zaidi, tafadhali fuatilia vyombo mbalimbali vya habari.


Father Mushi Alipokuta mauti yake