Showing posts with label magaidi. Show all posts
Showing posts with label magaidi. Show all posts

Wednesday, September 25, 2013

Al Shaabab ni Nani?



Al Shaabab Ni Nani? ( Makala Raia Mwema)

Na Maggid Mjengwa,

ULIMWENGU umepatwa na mshtuko mkubwa kwa kuona picha za tukio kubwa la kigaidi kwenye moja ya maduka makubwa jijini Nairobi. Hili ni shambulio kubwa la kigaidi kupata kutokea Afrika Mashariki tangu lile la mwaka 1998. Na ajabu ya kihitoria ni kuwa matukio mengi ya kigaidi yametokea katika mwezi wa Septemba.

La Nairobi ni shambulizi la kigaidi la kulaaniwa vikali na wapenda amani wote ulimwenguni. Hata hivyo, moja ya tafsiri ya vitendo vya kigaidi tunavyovishuhudia Nairobi ni kuwepo kwa hali ya vita vya kigaidi vyenye kuendeshwa kwenye maeneo ya mijini (Urban terrorism).

Ni shambulizi lenye athari mbaya kiuchumi si tu kwa nchi ya Kenya, bali hata majirani zake ikiwemo Tanzania. Ni shambulizi lililowaogopesha wageni wengi wakiwamo wawekezaji pia. Kwamba Al Shabaab inalenga pia nchi za Magharibi. Hivyo basi, hata raia wake. Kunahitajika jitihada za pamoja kuwaondoa hofu watu wa mataifa ya nje, kuwa kilichotokea Nairobi kitadhibitiwa kwa njia zote, kisitokee tena.
Na hakika, aina hii ya ugaidi ni ngumu sana kudhibitika hatakama nchi ina jeshi kubwa na lenye vifaa vya kisasa. Inahitaji ushiriki wa raia wema katika kutoa taarifa za wahalifu hata kabla hawajafanya matendo yao maovu. Inahitaji pia maandalizi makini, ya kuwa na vikosi vilivyo tayari wakati wote kukabiliana na matukio kama haya.

Ni dhahiri, kuwa mbinu inazotumika kikundi cha kigaidi cha Al Shaabab ambacho maana hasa ya jina hilo ni ' Vijana', ni moja ya changamoto kubwa katika mapambano dhidi ya ugaidi.

Al Shabaab iliundwa mwaka 2006. Kinasemekana kuwa na wapiganaji wenye silaha wapatao 10,000. Al Shabaab katika miaka ya karibuni wamepoteza maeneo mengi ya mijini waliyokuwa wakiyadhibiti, ikiwamo mji wa Kismayu ambao majeshi ya Kenya yaliudhibiti baada ya kuwasambaratisha Al Shabaab. Kwa sasa Al Shabaab bado wana nguvu maeneo ya vijijini katika Somalia.

Kufuatia Kenya kujiingisha kijeshi kupanbana na Al Shaabab, kikundi hicho kimeifanya Kenya kuwa adui na kutangaza wazi azma yake ya kuishambulia Kenya. Mwezi Aprili mwaka huu watu watano walipoteza maisha nchini Kenya baada ya wapiganaji wa Al Shabaab kuingia kwa nguvu wakiwa na silaha kwenye mgahawa mmoja kwenye mji wa Garissa nchini Kenya.

Mwaka 2012 ndipo Al Shabaab walipojiunga rasmi na mtandao wa kigaidi wa Al qaida chini ya kiongozi wa Al qiada, Ayman al- Zawahiri.
Hakika, hapa duniani matukio ya kigaidi yameongezeka.
Kwa faida ya wasomaji, nitaanza kwa kuangalia chimbuko la ugaidi kihistoria. Ni rahisi kusema kwamba ulimwengu umebadilika baada ya ugaidi wa Septemba 11 mwaka 2001 kule Marekani. Kwamba ugaidi umesogea karibu zaidi katika fikra zetu. Watanzania bado tunakumbuka tukio la shambulizi la kigaidi dhidi ya jengo la Ubalozi wa Marekani jijini Dar Es Salaam Agosti 7, 1998.

Sura ya ugaidi imeonekana vema zaidi miongoni mwa walimwengu. Bila shaka, picha ya filamu ya televisheni yenye kuonesha majengo mawili ya World Trade Centre kule Marekani yakitunguliwa na kuanguka, zimeonwa na takribani asilimia 75 ya watu wa ulimwengu huu. Katika hili la kuchambua ugaidi, hebu
basi tuanze na kujiuliza; Ugaidi ni nini?

Itakumbukwa wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano walipokutana Dodoma mwaka 2002 walipitisha Muswaada wa Ugaidi. Wabunge wetu walitumia muda mwingi sana kujadili tafsiri ya neno "ugaidi".
Kwa kifupi, ugaidi ukitafsiri kutoka neno la Kiingereza "Terrorism" tunapata maana ya "hofu". Neno la Kiingereza "Terror" lina maana ya hali ya "kutisha".

Vitendo vya kigaidi hutumiwa na mtu au makundi ya watu ili kuwaingizia watu hofu ndani ya mioyo yao na pengine hata kuchukua madaraka ya kisiasa. Ugaidi ni njia ya mnyonge na hata mwenye nguvu kutimiza malengo yake. Hili litafafanulika zaidi kadri utakapofuatilia maandiko haya.

Kihistoria tunaona kuwa, vitendo vingi vya kigaidi humu duniani vimefanywa pia na dola zilizo madarakani kwa minajili ya kuendelea kushika hatamu za dola. Mathalan, msemo wa " Utawala dhalimu" kwa tafsiri ya Kiingereza "Terror regime" hutumika tunapoielezea dola yenye kutumia mabavu na nguvu nyingi kupita kiasi. Dola au mtawala asiyezingatia sheria wala haki za kibinadamu.

Msamiati huu wa utawala dhalimu unatokana na lugha ya Kifaransa na una chimbuko la Mapinduzi ya Wananchi kule Ufaransa kati ya mwaka 1789 hadi 1799. Utawala dhalimu wenye kutisha" la terreur" ulikuwepo kule Ufaransa kunako miaka ya kati ya 1792 hadi 1794. Katika kipindi hicho watu takribani 40,000, wengi wao wakiwa wakulima na wahunzi waliuawa.

Mifano ya tawala dhalimu na za kutisha katika sehemu nyingine za dunia ni kama Urusi ya zamani chini ya dikteta Stalin, utawala wa Kinazi wa Ujerumani kati ya 1933-1945 chini ya Fashisti Hittler.
Katika Afrika, tuna pia mifano kadhaa ya tawala dhalimu na za kutisha ambazo kimsingi ni tawala za kigaidi. Uganda ya Idd Amin, Afrika ya Kati ya Bokassa, Zaire ya Mobutu, na nchi nyingine nyingi. Hizi zilikuwa tawala dhalimu.

Ugaidi kimsingi ni ile hali ya mtu, kikundi au dola, kwa maana ya taifa,kutumia nguvu nje ya wigo wa sheria ili kufikia malengo yao. Mwenye kuendesha vitendo vya kigaidi huchagua watu wake watakaoathirika na vitendo hivyo. Si lazima mtu au watu hao watakaoathirika wawe ni wahusika wa moja kwa moja wa mgogoro husika, isipokuwa, waathirika mara nyingi huchaguliwa na huonekana kama wawakilishi wa malengo ambayo magaidi wanataka kuyafikia.

Malengo au sababu za ugaidi zaweza kuwa ni za kidini, kijamii na kisiasa.
Ugaidi huwa wa kimataifa pale tukio la kigaidi linapofanywa nje ya mipakaya yule anayatenda tendo la kigaidi, au raia wa nchi moja wanapokuwawalengwa na kauthirika na tendo la kigaidi katika nchi ya tatu, mathalan,magaidi kutoka Colombia wanapofanya tendo la kigaidi dhidi ya raia waUingereza katika nchi ya Zambia.

0754 678 252, http://mjengwablog.com

Saturday, September 21, 2013

Magaidi Waua Watu Zaidi ya 20 Kwenye Mall Nairobi Kenya

Eti hao magaidi walisema waIslamu wote watoke, tunataka kuua waKristo! Jamani!  Hizi chuki za kidini zimezidi Afrika Mashariki!

***********************************************
A body lay outside the Westgate Mall in Nairobi on Saturday . Picha kutoka New York Times

Mwanamke aliyejerhuiwa leo huko Westgate Mall, Nairobi. Picha kitoka New York Times

Customers run following a shootout between unidentified armed men and the police at the Westgate shopping mall in Nairobi September 21, 2013. (Reuters / Thomas Mukoya)


From the Associated Press

   NAIROBI, Kenya (AP) - Gunmen threw grenades and opened fire Saturday killing at least 10 people in an attack targeting non-Muslims at an upscale mall in Kenya's capital that was hosting a children's day event, witnesses said.

   A local hospital was overwhelmed with the number of wounded being brought in hours after the attack, so they had to divert them to a second facility.

   Elijah Kamau, who was at the mall at the time of the midday attack, said that the gunmen made a declaration that non-Muslims would be targeted.

   "The gunmen told Muslims to stand up and leave. They were safe, and non-Muslims would be targeted," he said.

   Manish Turohit, 18, said he saw gunmen with AK-47s and vests with hand grenades on them inside the mall before he escaped to hide in a parking garage for two hours.

   "They just came in and threw a grenade. We were running and they opened fire. They were shouting and firing," he said after being marched out of the mall in line with about 15 people who held their hands in the air.

   Rob Vandijk, who works at the Dutch embassy, said he was eating at a restaurant inside the mall when attackers lobbed hand grenades inside the building. He said gunfire then burst out and people screamed as they dropped to the ground.

   It appears the attack began at the outdoor seating area of Artcaffe at the front of the mall, witnesses said.

   Patrick Kuria, an employee at Artcaffe, said:  "We started by hearing gunshots downstairs and outside. Later we heard them come inside. We took cover. Then we saw two gunmen wearing black turbans. I saw them shoot."

   Some people were shot at the entrance to the mall after volleys of gunfire moved outside and a standoff with police began. Ambulances continued to stream in and out of the mall area, ferrying the wounded who were gradually emerging from hiding inside the mall.

   Many of those running from the mall clutched small children. Others were crying. Mall guards used shopping carts to wheel out wounded children.

   Associated Press journalists at the mall said they saw at least 10 dead bodies and dozens wounded hours after the attack began. Officials did not yet give an official death toll.

   "We are treating this as a terrorist attack," said police chief Benson Kibue, adding that there are likely no more than 10 attackers involved. Gunfire continued to be exchanged outside the mall, as a group of people remained in hiding inside the building.

   Police did not say what group was responsible for the attack.

   Somali's rebel group al-Shabab vowed in late 2011 to carry out a large-scale attack in Nairobi in retaliation for Kenya's sending of troops into Somalia to fight the Islamic insurgents.

   The Westgate Mall is situated in Nairobi's affluent Westlands area and is frequented by expatriates and rich Kenyans.

Kwa habari zaidi  na Video BOFYA HAPA: 

Thursday, August 08, 2013

Mabinti waKizungu Wamwagiwa Tindikali Mjini Zanzibar



 Jamani, kisa cha kuwaumiza watoto wa watu? Hao mabinti walikuwa Zanzibar kama walimu wa Kiingereza, kisa cha kuwaumiza?  Je, hao wahuni waliwamwagia tindikali watakamatwa?

************************************
Two British women injured in Zanzibar Acid Attack



Still image taken from video of one of the two British teenage victims of an acid attack being comforted by an unidentified man in a vehicle at the airport in Zanzibar

.


One of the two British teenage victims of an acid attack is comforted by an unidentified man in a vehicle …

Kutoka Yahoo News

By Fumbuka Ng'wanakilala

DAR ES SALAAM (Reuters) - Men riding a motorbike threw acid at two British teenage girls in Tanzania's semi-autonomous Zanzibar region, leaving them with facial, chest and back injuries, a senior police official said on Thursday.

The pair, both 18 and from England's northern city of Manchester according to police in the Indian Ocean archipelago, were flown to Tanzania's commercial capital Dar es Salaam.
They had been volunteering at a local school in Zanzibar, an island that is popular with international tourists but has suffered a wave of deadly protests last year as supporters of an Islamist group repeatedly clashed with the police.

Britain is concerned about Wednesday's attack and is "in contact with the Tanzanian authorities", the Foreign Office said in a statement.

The police described the attack as "an isolated incident", refusing to link it to rising religious tension on the island between majority Muslims and its Christian population.

"The attackers approached the girls as they were walking on a street at around 7:15 p.m. and threw acid at them," Zanzibar Urban West regional police commander Mkadam Khamis Mkadam told Reuters. "The incident occurred when the streets were deserted as most people were breaking their Ramadan fast."
Television images showed one girl obviously in pain in the back of a car at the Zanzibar airport.
"The victims sustained facial, chest and back injuries from the acid attack," Mkadam said.
The Britons were expected to fly home on Thursday.

The attack comes during the tourist season in the historic town and after a Zanzibar Muslim leader, Sheikh Fadhil Suleiman Soraga, was hospitalized with acid burns in a November attack.
Two Christian leaders were killed early this year in separate attacks.

A separatist group in Zanzibar, Uamsho (Awakening), is pushing for the archipelago to exit from its 1964 union with mainland Tanzania, which is ruled as a secular country. Uamsho wants to introduce Islamic Sharia law in Zanzibar.

Supporters of the group have engaged in running street battles with the police in the past, but authorities have not linked the group with the attacks on Christian clerics.

Kwa Habari Zaidi Tembelea BBC.Com

Tuesday, May 07, 2013

Rais Kikwete Atembelea Kanisa Lililopigwa Bomu Arusha

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea wakati alipotembelea Mei 7, 2013 katika kanisa la Mtakatifu Joseph kitongoji cha Olasiti jijini Arusha lililoshabuliwa na magaidi Jumapili iliyopta Video kwa hisani ya Kaka Michuzi

Sunday, February 17, 2013

Padri Auwawa Zanzibar Akielekea Kanisani Leo!

TAARIFA  KUTOKA JAMII FORUM:

Default Update: Watatu wahojiwa Zanzibar kuhusiana na mauaji ya Padre na Taarifa ya Polisi


17/02/201




Padre Evaristus Mushi


UPDATE/TARIFA MPYA (saa nane u nusu mchana) Taarifa ya Polisi:

Watu watatu wanashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za mauaji ya Padre Mushi. Tafadhali bofya vipande vya picha zilizopachikwa hapo ili kuvikuza na kusoma taarifa ya Polisi inayoonekana hapo (shukurani kwa Francis Dande).









UPDATE/TAARIFA MPYA (saa saba mchana) Taarifa ya habari Radio One Stereo:

Taarifa ya habari ya Radio One Stereo iliyosomwa saa 7 mchana imeripoti kuwa Padre Mushi aliuawa na watu walipolisimamisha gari la Padre huyo alipokuwa akielekea katika kanisa la Mtakatifu Theresia lililoko eneo la Mtoni, na alipopunguza mwendo ili awasikilize, ndipo alipopigwa risasi kichwani na kusababisha gari alilokuwamo kukosa uelekeo na kuigonga nyumba iliyokuwa jirani. Watu walioshuhudia tukio hilo walimchukua Padre Mushi ili kumwahisha hospitalini katika jitihada za kuokoa uhai wake, lakini alifariki dunia. Waliomwua Padre Mushi bado hawajakamatwa.
-----------------------


Akina mama wakilia kwa uchungu kuomboleza kifo cha ghafla cha kupigwa risasi Padre Evaristus Mushi kilichotokea leo asubuhi muda mfupi kabla ya kuanza Misa ya Jumapili kwenye kanisa la Kigango cha Mtoni, Zanzibar. (Picha na Martin Kabemba via Lukwangule blog)
Taarifa kutoka Zanzibar zikiripotiwa na mwanahabari Donisia Thomas wakati kipindi cha Patapata cha WAPO radio FM kinaendelea, zinasema kuwa Padre Evaristus Mushi wa Kanisa la Parokia ya Minara Miwili huko Zanzibar amepigwa risasi majira ya saa moja asubuhi -na watu wasiofahamika- na kufariki dunia.

Taarifa za kufariki kwake zimethibitishwa na madaktari kutoka hospitalini alikopelekewa katika harakati za kuuokoa uhai wake.


Padre Mushi aliuawa akiwa anashuka kwenye gari lake tayari kuingia Kanisani kwa ajili ya kuendesha misa ya kawaida ya Jumapili katika kanida la Mtoni, mjini St. Joseph. Inaelezwa kuwa gari lisilofahamika lilifika na kufyatua risasi zilizomlenga Padre Mushi sehemu ya kichwani na hivyo kumsababisha majeraha yaliyokuwa yakivuja damu nyingi.


Mwanahabari anasema tukio hilo limezua taharuki kubwa miongoni mwa waumini ambao wamekataa kuahirisha ibada iliyokuwa iendeshwe na Padre huyo na kusema ikiwa kusudio ni kuwaangamiza Wakristo wote, basi na waangamizi wafike Kanisani wawaangamize wakiwa pamoja.


Jeshi la Polisi limeshafika katika eneo la tukio na kuanza uchunguzi.


Wakizungumza kuhusu hilo, raia wamesema hawana imani na Polisi wala Madaktari na hawatarajii jipya zaidi ya ripoti kuwa suala hili ni la uhalifu kwa kuwa tukio kama hili liliwahi kutokea mwishoni mwa mwaka jana kwa Padre Ambrose kupigwa risasi na taarifa zilisema lilikuwa ni tukio la kihalifu na kwamba risasi hazikutumika jambo ambalo halikuwa kweli kwani Padre Ambrose alikutikana na risasi alipohamishiwa katika hospitali ya Taifa, Muhimbili.

Kwa taarifa zaidi, tafadhali fuatilia vyombo mbalimbali vya habari.


Father Mushi Alipokuta mauti yake