Ni mara chache sisi waandishi wa habari, tunakuwa habari!
********************************
Habari na picha kutoka
FACEBOOK:
 |
| Askari wa Trafiki Akimkamata Ephraim Kibonde |
 |
| Ephraim Kibonde ndani ya Lock Up |
Mtangazaji Mahiri wa Redio 88.5 Clouds FM kupitia kipindi cha Jahazi,
Ephrahim Kibonde akipingana na Askari wa Usalama barabarani wakati
alipotakiwa kutii sheria bila shurti,mapema asubuhi hii jijini Dar es
salaam.
Kibonde anadaiwa kusababisha ajali asubuhi hii eneo la Makumbusho, ikiwa
gari aliyokuwa akiendesha kuigonga gari ya dereva mwingine kwa nyuma.
Trafiki walifika eneo la tukio na kupima ajali, Kibonde alipoona hivyo
akarudi nyuma na kuendesha gari lake kuondoka eneo la tukio bila kufuata
taratibu za usalama barabarani,hali iliyomlazimu yule Trafiki katumia
gari lililogongwa kumfukuzia.
Walifanikiwa kumkamata eneo la Mwenge na Trafiki aliingia katika gari
lake na kumwomba arudi eneo la ajali ili wakapime na kuchora mchoro wa
ajali. Kibonde aligoma na kumtaka trafiki ashuke katika gari
lake,Trafiki naye hakutana kufanyi kwa maana ya kuwa aligoma kushuka na
kumuamuru Kibonde arudi eneo la tukio.
Kibonde aliondoa gari na kuendelea na safari yake huku yule Trafiki
akiwa ndani ya gari hiyo, Trafiki aliwasiliana na wenzake ambao walianza
kuifuatilia gari hiyo ya Kibonde kama walivyopewa maelekezo na mwenzao
aliopo ndani ya Gari hiyo.
Mara Kibonde akatokea maeneo ya mataa ya Ubungo, hapo kulikuwa na
Trafiki mwingine aliyekua eneo hilo akaipiga mkono gari ya Kibonde na
ambapo inasemekekana hakusimama na badala yake ikaja gari nyingine na
kuichomekea kwa mbele na hapo ndipo alipotiwa mbaroni! Aligoma kuendesha
gari ikabidi livutwe hadi polisi Urafiki na yeye kuwekwa chini ya
ulinzi na baadae akahamishiwa Kituo cha Oystabay ambako yupo mpaka sasa.
Inadaiwa kuwa Kibonde alikuwa amelewa sana,hali iliyopelekea kufanya hayo yote ikiwa ni pamoja na kuwajibu vibaya Askari hao.