Showing posts with label Arrested. Show all posts
Showing posts with label Arrested. Show all posts

Saturday, June 17, 2017

MBongo Afungwa Jela Miezi Mitatu Uiigereza kwa Kuposti Picha za Maiti FaceBook!

Aibu! Aibu!   Mwanaume mwenye asili ya Tanzania, Omega Mwaikambo  (43), alifungua begi iliyokuwa na maiti ya mtu aliyekufa kwenye ile ajali ya moto London, na kupiga picha za marehemu na kuziposti Facebook. Inaelekea marehemu alijitupa kutoka ghorofani ilikukwepa moto. Polisi walimkamata na kahukumiwiwa kifungo cha miezi mitatu jela.

Mwaikambo anasema kuwa aliposti picha ya maiti ili watu waweze kumtambua.  Kosa lake hasa ni kufungua ile begi ya maiti (body bag). Anadai maiti ilikuwa pale nje ya fleti yake zaidi ya masaa mawili.

***************************************************


Man jailed for opening body bag and taking picture of Grenfell Tower victim

Read more: http://metro.co.uk/2017/06/16/man-jailed-for-opening-body-bag-and-taking-picture-of-grenfell-tower-victim-6714707/#ixzz4kGTdgMGU



A man has been jailed after admitting posting photos of a Grenfell Tower fire victim on Facebook after opening body bags.

Omega Mwaikambo, 43, pleaded guilty to two offences contrary to section 127 of the Communications Act, Scotland Yard said.


He was sentenced to three months at Westminster Magistrates’ Court on Friday.
Mwaikambo, of Testerton Walk, west London, was arrested after images were posted online of what appeared to be a partially-covered body following the fatal blaze in north Kensington, west London.
'
In one of his posts, Mwaikambo claims the body of a victim was left outside his flat for two hours before police or ambulances arrived.

Omega Mwaikambo (43)

Mwaikambo akihijiwa na polisi

Omega Mwaikambo akifungwa pingu na polisi London

Saturday, August 09, 2014

Kibonde wa Clouds FM Akamatwa na Polisi Leo

Ni mara chache sisi waandishi wa habari, tunakuwa habari!

********************************
 Habari na picha kutoka FACEBOOK:

Askari wa Trafiki Akimkamata Ephraim Kibonde

Ephraim Kibonde ndani ya Lock Up


Mtangazaji Mahiri wa Redio 88.5 Clouds FM kupitia kipindi cha Jahazi, Ephrahim Kibonde akipingana na Askari wa Usalama barabarani wakati alipotakiwa kutii sheria bila shurti,mapema asubuhi hii jijini Dar es salaam.

Kibonde anadaiwa kusababisha ajali asubuhi hii eneo la Makumbusho, ikiwa gari aliyokuwa akiendesha kuigonga gari ya dereva mwingine kwa nyuma. Trafiki walifika eneo la tukio na kupima ajali, Kibonde alipoona hivyo akarudi nyuma na kuendesha gari lake kuondoka eneo la tukio bila kufuata taratibu za usalama barabarani,hali iliyomlazimu yule Trafiki katumia gari lililogongwa kumfukuzia.

Walifanikiwa kumkamata eneo la Mwenge na Trafiki aliingia katika gari lake na kumwomba arudi eneo la ajali ili wakapime na kuchora mchoro wa ajali. Kibonde aligoma na kumtaka trafiki ashuke katika gari lake,Trafiki naye hakutana kufanyi kwa maana ya kuwa aligoma kushuka na kumuamuru Kibonde arudi eneo la tukio.

Kibonde aliondoa gari na kuendelea na safari yake huku yule Trafiki akiwa ndani ya gari hiyo, Trafiki aliwasiliana na wenzake ambao walianza kuifuatilia gari hiyo ya Kibonde kama walivyopewa maelekezo na mwenzao aliopo ndani ya Gari hiyo.

Mara Kibonde akatokea maeneo ya mataa ya Ubungo, hapo kulikuwa na Trafiki mwingine aliyekua eneo hilo akaipiga mkono gari ya Kibonde na ambapo inasemekekana hakusimama na badala yake ikaja gari nyingine na kuichomekea kwa mbele na hapo ndipo alipotiwa mbaroni! Aligoma kuendesha gari ikabidi livutwe hadi polisi Urafiki na yeye kuwekwa chini ya ulinzi na baadae akahamishiwa Kituo cha Oystabay ambako yupo mpaka sasa.

Inadaiwa kuwa Kibonde alikuwa amelewa sana,hali iliyopelekea kufanya hayo yote ikiwa ni pamoja na kuwajibu vibaya Askari hao.

Friday, March 29, 2013

Mtuhumiwa wa Mauaji ya Father Evaristus Mushi Akamatwa Zanzibar!

BREAKING NEWS: MTUHUMIWA WA MAUAJI YA PADRI EVALIST MUSHI AKAMATWA ZANZIBAR

Jeshi la polisi linamshikilia Omari Musa Mkame Mkazi wa Mwanakwerekwe Zanziba anaye sadikiwa kuwa ni muuaji wa padre Evalist Mushi. Amekamatwa alasiri hii maeneo ya Kariakoo, Zanzibar.

Ni kwa msaada wa mchoro wa mfano wa muhusika ulioachorwa na FBI.

Suspect in Father Mushi Killing




Saturday, June 09, 2012

Mchungaji Creflo Dollar Akamatwa na Polisi

Kuna habari kuwa Mchungaji maarufu Creflo Dollar, amekamatwa na polisi huko Atlanta kwa kumpiga binti yake. Habari zinasema kuwa ugomvi uliaanza binti yake alipotaka kutoka kwenda kwenye party!

Bahati mbaya kamwumiza, lakini watoto wengine ha Marekani hawasikii. Pia wengine wanajua hiyo sheria na wanatishia wazazi wao kuwa watawaripoti kama hawapati wanachotaka.


Hapa Marekani ni kosa la jinai kumpiga mtoto.

*********************************************************************

Megachurch Pastor Creflo Dollar Arrested.


Creflo Dollar Police Mugshot

ATLANTA—Megachurch pastor and televangelist Creflo Dollar -- who has drawn scrutiny for his flashy lifestyle and preaching that prosperity is good -- was arrested early Friday after authorities say he slightly hurt his 15-year-old daughter in a fight at his metro Atlanta home.
Fayette County Sheriff's deputies responded to a call of domestic violence at the home in unincorporated Fayette County around 1 a.m., said investigator Brent Rowan. The pastor and his daughter were arguing over whether she could go to a party when Dollar "got physical" with her, leaving her with "superficial injuries," Rowan said.
The 15-year-old was the one who called authorities, and her 19-year-old sister corroborated the story, Rowan said.
Dollar faces misdemeanor charges of simple battery and cruelty to children. He bonded out of Fayette County jail Friday morning.
"As a father I love my children and I always have their best interest at heart at all times, and I would never use my hand to ever cause bodily harm to my children," Dollar said in a statement released by his lawyer Nikki Bonner. "The facts in this case will be handled privately to further protect my children. My family thanks you for your prayers and continued support."
Dollar will make no further comments since he's involved in the ongoing criminal matter, but he is expected to preach Sunday, Bonner said.
The 50-year-old leads the Creflo Dollar Ministries and is the pastor for World Changers Church International in the Atlanta suburb of College Park, which serves nearly 30,000 members, according to the church's website. World Changers Church-New York hosts over 6,000 worshippers each week, the website says. Four satellite churches are located in Georgia along with others in Los Angeles, Indianapolis, Washington, Cleveland, Dallas and Houston.
He and his wife Taffi, a co-pastor at the church, have five children, according to the website.

SOMA HABARI KAMILI KWA KUBOFYA HAPA:

Thursday, February 09, 2012

Mkurugenzi wa TAMWA Ananilea Nkya Akamatwa na Polisi

UPDATE:  Dada Nkya ametoka kwa Dhamana jioni hii!

Dada Nkya akishika bango jana, Picha kwa hisani ya Global Publishers

Kutoka The Guardian:

Senior Tanzanian journalist arrested

The director of the Tanzania Media Women's Association (Tamwa), Ananilea Nkya, was arrested early today in Dar es Salaam.

She was detained along with several activists and journalists during a public demonstration calling for the government to resolve an ongoing doctors' strike.

Several hospitals have been closed during the strike by junior doctors and medical interns, which began on 30 January. They are protesting about pay and working conditions.

Some specialists have also joined the strike, and the Tanzanian government has come under mounting pressure to resolve the dispute.

The reason for Nkya's arrest remains obscure. She did make a statement yesterday about the need "to make the public disabuse themselves of the commonly held belief that prominent people care little about what is going on because they can access medical attention outside Tanzania."

But concerned supporters do not believe that to have been the reason for her detention.
Sources: Daraja/AllAfrica.com/IPPmedia/The Citizen

Tuesday, April 12, 2011

Rais Gbagbo wa Ivory Coast Akamatwa!



Wadau, Rais Laurent Gbagbo wa Ivory Coast na mke wake wamekamatwa na askari wa Upinzani huko Abidjan. Mdau Mobhare Matinyi amekusanya picha za kukamatwa kwao. Zinatia huruma hasa huyo mke wa Gbagbo. Mara nyingi watu wanasherekea kukamatwa kwa viongozi wao, lakini wanajuta wakigundua anayemfuta ni mbaya zaidi. Rais Gbagbo na Mke wake Simone mara baada ya kukamatwa na askari wa Upinzani huko Abidjan. Walikuwa wamekimbilia kwenye hoteli.
Mama Simone Gbagbo, mke wa Rais Gbagbo mara baada ya kukamtwa kwao
Askari wa Kiongzoi wa upinzani Ivory Coast Allasane Ouattara wamemzunguzka Raia Gbagbo akiwa anavaa
Rais Gbagbo akijifuta na taulo huko kwenye hoteli alikokamatwa Abidjan.
Wakazi wa Abidjan wakisherekea kukamatwa kwa Rais Gbagbo
Rais Laurent Gbagbo wa Ivory Coast na mke wake Simone wakiwa kwenye mkutano wa kampeni ya kugombea urais mwaka jana


*************************************


Kwa habari zaidi za Utawala wa Rais Gbagbo na Kukamatwa kwake someni:




Monday, July 20, 2009

Prof. Henry Louis Gates Akamatwa na Polisi hapa Cambridge!

Prof. Gates Mugshot (Cambridge Police)

Wadau, bila shaka mmesikia habari za Prof. Henry Louis Gates, Jr. wa Chuo Kikuu cha Harvard kukamatwa na polisi akijaribu kuingia nyumbani kwake. Polisi walivyomkamata alikuwa amekwishaingia nyumbani kwake na liwaonyesha vitambulisho! Anasema kuwa kitendo hicho cha kukamatwa kwake ni cha kibaguzi (racial profiling). Nakubaliana naye!

Sisi weusi wachache tuliobaki kwenye nyumba za kawaida hapa Cambridge, Massachusetts tunakaa roho juu juu! Jirani zetu wazungu wanatazama kila tunachofanya na hawasiti kuita polisi wakidhani unafanya kosa lolote. Mfano kuna mitaa fulani ukitembea mweusi wanaweza kuita polisi, "THERE'S A BLACK MAN WALKING DOWN MY STREET!" Na polisi watakuja na uwe na kitambulisho cha kuonyesha la sivyo uende ukalale jela! Unaogopa kwenda duka la jirani bila kitambulisho! Wiki mbili zilizopita nilikuwa naedesha gari langu, nilikuwa na rafiki yangu ndani ya gari. Nilisimama kwenye mtaa fulani ila nicheki GPS kujua tuelekea wapi. Wazungu walitoka ndani ya nyumba ya na kuandika pleti ya gari!

Hizi nyumba za kawaida zimekuwa gentrified na wanaishi wazungu na yuppies na mbwa wao! Mbwa na paka ni watoto wao. Weusi wamefukuzwa kiujanja. Walipandishiwa kodi, au kuna kundi ilikuwa inapita kwenye nyumba ziliokuwa zinamilikiwa na weusi na kununua nyumba zao kwa bei nzuri. Lakini nia yao ilikuwa kusafisha eneo kusudi kusiwe na weusi. Eneo nayo kaa Cambridgeport kati vyuo vikuu ya Harvard na MIT, zamani ilikuwa ya weusi lakini sasa ni la wazungu. Ukiona ilivyo sasa huwezi kujua!

Mwaka juzi nikiwa napita kwenye sidewalk nyumba ya jirani nikaulizwa nakwenda wapi kwa hasira na mzungu fulani. Nilikuwa nimevaa koti la winter, hivyo hakuniona vizuri. Alipogundua ni mimia aliona haya na kudai eti hakusema hivyo! Shenzi Taipu! Zee lingine la kizungu kaniuliza nafanya nini nikiwa naosha gari langu mbele ya nyumba nayo kaa. Nikamwambia yaani miaka yote nakaa hapa leo ndo unaongea na mimi! Hebu nenda zako!

Na hao vijana wetu ndo usiombe. Ukisikia kuna wizi nini umetokea tunawaambia watoto waingie ndani haraka, maana hao polisi wa Cambridge hawasiti kuwakamata hata kama hawana hatia. Unasikia Polisi wanatafuta, black male, 5'8 wearing a sweatshirt! Jamani si anaweza kuwa mtu yeyote! Na maskini, mnakumbuka kesi ya kijana wetu Justin Cosby alivyouwawa huko Harvard. Yaani mara tu, walikuwa wanauliza alikuwa anafanya nini Harvard!


Kuna siku mwanangu na rafiki zake walikuwa wanatembea kutoka kwenye shule yao ya msingi karibu na Harvard. Wakawa wanakatisha Harvard Yard. Walikuwa vijana weusi kama saba wote chini ya miaka 13. Walikuwa wanacheka cheka na kuongea kwa sauti kama kawaida ya vijana. Mvulana wa kizungu alishikwa na hofu na kusema eti kuna kundi la weusi linataka kumwibia na polisi waliitwa! Baada ya siku hiyo hao vijana hawajakatisha Harvard Yard tena kwa hofu wataitwa wezi. Na wesui wengi wanaokaa Cambridge hawana hamu ya kusoma Harvard shauri ya ubaguzi walioshuhudia.

Siku nyingine tukiwa kwenye basi, msichana wa kizungu ghalfa aliaanza kumshambulia binti mweusi aliyokuwa amekaa naye kwenye kiti. Polisi walimkamtaa yule mweusi aliyeshambuliwa kwanza mpaka tulivyowaeleza ni mzungu alimyemshambulia mweusi! KHAA! Hata hivyo mzungu aliachiwa. We mweusi umshmabulie mzungu bila sababu au ukiwa na sababu na utakiona cha mtema kuni!


Ubaguzi upo mpaka mashuleni ya msingi na hiyo Cambridge Rindge & Latin School ambayo ni shule pekee ya sekondari serikali hapa Cambridge. Loh, nina story za kuwasimulia lakini moja ya kusikitisha ni kuwa KKK walikuwepo hapa Cambridge, na walimfanya Mwalimu Mkuu wa Agassiz School (sasa Baldwin), Peggy Avarette kukimbia na kuacha kila kitu, baada kutishia kumwua na kuchoma gari lake mbele ya nyumba aliyokuwa anakaa karibu na Harvard! Mwanangu alikuwa anasoma hapo wakati huo na nilipambana vikali na hao wabaguzi. Lakini itabidi niwasimulie siku nyingine!

Prof Gates ana heshima kubwa hapa Cambridge na dunia nzima kwa utafiti aliyofanya kuhusu historia ya watu weusi. Sasa kama yeye anaweza kukamatwa, sisi makamchape tulie tu!

Kwa sasa mjue, RACISM IS STILL ALIVE AND WELL IN CAMBRIDGE, MASSACHUSSETTS! Ndiyo wadau, tuna Rais mweusi lakini ubaguzi bado upo Marekani!


***********************************************************************

A black Harvard professor, who has been named by Time magazine as one of the top 25 most influential Americans, accused police of racism after he was arrested trying to get into his own home.

Henry Louis Gates was arrested for disorderly conduct after police said he "exhibited loud and tumultuous behaviour". He was later released.

The head of Harvard's WEB DuBois Institute for African and American Studies, shouted to a police officer "this is what happens to a black men in America" according to a police report.

The incident happen last Thursday after a call to police that "two black males" were breaking into Gates's home near the university campus in Cambridge, Massachusetts.

Later Gates refused to discuss the incident. But his lawyer said he was arrested after he forced his way through his front door because it was jammed. The professor's colleagues blamed the arrest on racial profiling.

Gates initially refused to show the officer his identification, but later showed his university pass. "Gates continued to yell at me, accusing me of racial bias and continued to tell me that I had not heard the last of him," the police officer wrote.

His friend and fellow Harvard scholar Charles Ogletree, said: "He was shocked to find himself being questioned and shocked that the conversation continued after he showed his identification."

Allen Counter, who has taught neuroscience at Harvard for 25 years, said he was stopped on campus by two police officers in 2004 after being mistaken for a robber. They threatened to arrest him when he could not produce identification.

"We do not believe that this arrest would have happened if Professor Gates was white," Counter said. "It really has been very unsettling for African-Americans throughout Harvard and throughout Cambridge that this happened."

Lawrence D Bobo, professor of Social Sciences at Harvard, said he met Gates at the police station and described his colleague as feeling humiliated and "emotionally devastated."

"It's just deeply disappointing but also a pointed reminder that there are serious problems that we have to wrestle with," he said.

Bobo said he hoped Cambridge police would drop the charges.
***************************************************************

Kwa habari zaidi someni:
http://www.nytimes.com/2009/07/21/us/21gates.html

http://www.bloomberg.com/apps/news?pid=20601103&sid=anupUHzw.F0Y

http://www.pbs.org/kcet/tavissmiley/voices/725.html