Showing posts with label Tiba. Show all posts
Showing posts with label Tiba. Show all posts

Saturday, November 19, 2016

Makamu wa Rais Kuzindua Kampeni ya Uchunguzi wa Bure wa Saratani ya Matiti

Rais wa Chama cha Madaktari Wanawake Tanzania (MEWATA), Dkt.Serafina Mkuwa (kulia), akitoa taarifa kwa wanahabari kuhusu uzinduzi wa kampeni ya uchunguzi na matibabu ya Saratani ya Matiti na mlango wa kizazi mkoani Mwanza.

Kampeni hiyo itazinduliwa kesho katika Uwanja wa Furahisha Jijini Mwanza na Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan na baadaye kufanyika kwa siku mbili bure.
Na BMG
Kutoka kushoto ni Dkt.Mary Charles ambaye ni Makamu wa Rais MEWATA, Mganga Mkuu mkoa wa Mwanza, Dkt.Leonald Subi, Rais wa MEWATI, Dkt.Serafina Mkuwa, Mwenyekiti Kamati ya Kampeni na Mjumbe kamati tendaji MEWATA, Dkt.Magdalena Lyimo pamoja na Mratibu wa huduma za afya ya uzazi na mtoto mkoa wa Mwanza, Secilia Mrema.
Pia watumishi wa afya mkoani Mwanza wamepatiwa mafunzo kwa ajili ya kusaidia utoaji wa huduma za uchunguzi wa saratani ya matiti na mlango wa kizazi
Na George Binagi-GB Pazzo
Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Hassan Suluhu, kesho anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa kampeni ya uchunguzi na matibabu ya saratani ya matiti na mlango wa kizazi bila malipo mkaoni Mwanza.

Rais wa Chama cha Madaktari Wanawake nchini MEWATA, Dkt.Serafina Mkuwa, ameyasema hayo hii leo Jijini Mwanza wakati akitoa taarifa ya kampeni hiyo kwa wanahabari.

Amesema baada ya ufunguzi wa kampeni hiyo, akinamama na wasichana mkoani Mwanza, watapata fursa ya kufanya uchunguzi na matibabu ya Saratani ya matiti na mlango wa kizazi kwa muda wa siku mbili ambazo ni kesho na kesho kutwa katika vituo vinne ambavyo ni Uwanja wa Furahisha, Vituo vya Afya Makongoro, Karume pamoja na Igoma Jijini Mwanza ambapo huduma zitakuwa zikitolewa kuanzia majira ya saa moja asubuhi.

Tatizo la saratani ya matiti na mlango wa kizazi bado ni changamoto kubwa mkoani Mwanza ambapo Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dkt.Leonald Subi, anabainisha kwamba takwimu zilizopatikana katika halmashauri za Ukerewe, Buchosa pamoja na Kwimba, zinaonesha kwamba kati ya wanawake 1,294 waliochunguzwa, 58 wanamabadiliko ya awali ya saratani na 18 wanamabadiliko makubwa ya saratani na wamepewa rufaa kwenda hospitali ya rufaa Bugando kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Hata hivyo Dkt.Subi amewahimiza wananchi kuepuka matumizi ya tumbaku, sigara pamoja na pombe kali ambayo huchangia ongezeko la magonjwa ya saratani ya matiti na mlango wa uzazi kwa akinamama huku akiwahimiza kufanya uchunguzi angalau mara moja kwa mwaka ili kubaini tatizo mapema kwani tiba ya mapema husaidia kupambana na magonjwa hayo.

Chama cha Madaktari Wanawake nchini kimeshirikiana na Wizara ya Afya, Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza pamoja na wadau wengine wakiwemo Gender Health, PSI pamoja na Tayoa katika kufanikisha huduma hiyo ya uchunguzi na matibabu ya saratani ya matiti na mlango wa kizazi bila malipo mkoani Mwanza.

Saturday, February 13, 2016

Fahamu Jinsi Radiotherapy Inavyoweza kuokoa Maisha

Dk. Mahadev, mshauri mwandamizi wa radiotherapia kutoka Hospitali za Apollo.


Na Mwandishi wetu,
Matibabu ya kawaida ya saratani huwa yanahusisha upasuaji, radiotherapia na kemotherapia. Hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa kwenye tiba kwa njia hizo mbili. Katika hatua za mwanzo, saratani huwa ni ugonjwa unaotibika kwa dozi moja mahususi lakini saratani iliyosambaa au kukomaa inahitaji dozi zaidi ya moja katika kuitibu. Radiotherapia, ni tiba iliyopo katika mfumo maalumu unaoleta matokeo katika mwili mzima.
Dk. Mahadev , mshauri mwandamizi wa tiba ya uvimbe kwa mionzi kutoka hospitali za Apollo anaeleza kwamba radiotherapia inahusisha chembe chembe ndogo za mionzi ya gamma au X-rays katika kutibu saratani na hata matatizo ambayo sio ya saratani pia. Mionzi hii imegawanyika katika ile mionzi ya mbali (external radiotherapy) ambayo chanzo cha mionzi kinakuwa mbali na mwili na ile mionzi ya karibu ambayo mionzi inawekwa karibu ili kuchoma sehemu yenye uvimbe peke yake.

Mionzi ya karibu ni aina nzuri ya kutibu saratani ila kwa uvimbe unaoonekana kirahisi na unaofikika. Hivyo saratani iliyopo mdomoni, saratani ya tezi dume, saratani ya kizazi zote zinaweza kutibiwa kwa mionzi ya karibu peke yake. Faida kubwa ya mionzi ya karibu ukilinganisha na mionzi ya mbali ni kwamba mionzi ya karibu inahusisha uponyaji ndani ya muda mfupi (siku 3-5) wakati mionzi ya mbali inachukua hadi wiki 7 hadi 8. Uvimbe wowote uliokomaa unahitaji mionzi ya mbali.

Lengo kubwa la matumizi ya radiotherapia ni kuchoma sehemu pekee yenye uvimbe na kuepuka kuchoma sehemu nyingine za pembeni katika mwili. Mionzi ya mbali inahistoria ndefu kutoka enzi za cobalt kwenda kwenye hali ya teknolojia ya juu ya kutoa tiba ya mionzi kwa moduli ya hali ya juu (IMRT), mionzi kwa kuongozwa na picha (IGRT), upasuaji kwa njia ya sterio (SRS) na njia ya sterio kwa mionzi mwilini (SBRT). Mashine yenye program maalumu kwa ajili ya upasuaji (Cyberknife robotic radiosurgery ) ni njia bora zaidi katika kufanya SRS na SBRT, aliongeza Dk. Mahadev  kuwa teknolojia hizi zinapatikana katika hospitali za Apollo.

Umuhimu pekee wa kutumia mashine yenye program maalumu kwa ajili ya upasuaji ni kukata milimeta sahihi na uponyaji katika siku chache. Ni tiba ya mgonjwa bila kulazwa na hahihitaji nusu kaputi katika kufanyika. Hivyo saratani ya mapafu na tezi dume inaweza kutibika ndani ya siku 3 hadi 5, wakati muda wake kawaida huchukua wiki 7-8 kwa uangalizi wa karibu. Mashine yenye program maalumu kwa ajili ya upasuaji ni muhimu katika kutibu uvimbe, ambao hauwezekani kufanyiwa operesheni kwa sababu ya eneo ilipo aidha katika ubongo au uti wa mgongo. Inatumika kutibu magonjwa kama meningiomas, uvimbe katika pituitary, mishipa ya ateri iliyodhofika (AVM) na madhara kutokana na saratani katika ubongo, mapafu na ini.

Dk. Mahadev  anaelezea njia bora ya kutumia radiotherapia ni kwa protoni. Faida kubwa ya protoni ukilinganisha na njia ya kawaida ni katika kutoa mionzi kwa umakini zaidi hasa kuchoma sehemu yenye uvimbe peke yake. Hiyo inapelekea matokeo mazuri na madhaifu machache. Kutokana na kutokuwa na dozi zaidi katika kutibu uvimbe, ni vyema kudhibiti uvimbe ukiwa katika hatua za mwanzo ambapo huwa tunaogopaga madhara ya kutumia mionzi. Matumizi ya protoni ni mapinduzi katika tiba ya saratani. Saratani ya kichwa na shingo, mapafu na tezi dume huwa zinatibika kirahisi kabisa kwa mionzi hii ya protoni.

Baadhi ya saratani zinazotibika kwa upasuaji, inaweza kutibika kirahisi kwa radiotherapia tu. Ikiwa hatua ya mwanzo, saratani ya mdomoni, mfumo wa chakula, tezi dume, zaweza tibiwa kwa mionzi peke yake. Faida katika kutibu aina hizi za saratani ni kuwa zipo sehemu zinazofikika. Mgonjwa anaweza kuwa na ogani inayofanya kazi vizuri hivyo kuona ubora wa maisha. Saratani nyingi zilizokomaa huwa zinahitaji kwa pamoja upasuaji, radiotherapia na kemotherapia katika kuitibu ambazo zote zinapatikana katika teknolojia ya juu kutoka hospitali za Apollo.

Tumetoka kwenye enzi za kufanya operesheni kubwa na kuingia kwenye utunzaji wa ogani zetu kwa msaada wa teknolojia ya mionzi bora na dawa mpya na bora za tiba kwa kemotherapia. Kwa mfano saratani ya matiti ndio saratani inayoongoza kwa wanawake duniani. Hapo kabla, titi lote lilikuwa linakatwa. Ila kwa sasa wagonjwa wengi wanabaki na matiti yao salama kwa upasuaji mdogo tu unaofanywa.

Tiba hiyo ndogo katika tiba inawasaidia wanawake kuwa na saikolojia chanya inayowafanya wapone haraka pia. Kichwa na shingo, mfumo wa chakula, saratani ya tezi dume na sehemu nyingine ambazo huwa kutokuondoa ogani ni kitu cha muhimu katika tiba.
Radiotherapia ni mbadaka zuri kuepuka upasuaji au kemotherapia katika kupambana na saratani. Mabadiliko makubwa katika teknolojia na matumizi ya kompyuta yamewezesha utoaji bora wa huduma ya tiba ya mionzi kwa madhara kidogo sana.



Kuhusu Hospitali ya Apollo

Hospitali za Apollo ni za kwanza katika eneo Asia Pacific kutoa huduma za upasuaji kwa kutumia mfumo huu wa Robot, ambayo ni aina ya upasuaji isiyokuwa na madhara. Taasisi ya upasuaji kutumia Robot iliyopo hospitalini hapo wamejitoa kipekee katika kutoa huduma bora kwa wagonjwa.

Taasisi ina wataalamu waliobobea kwenye mafunzo ya upasuaji, upendo katika utoaji wa huduma vifaa vya matibabu vya kisasa vinavyolenga kutoa uzoefu bora kwa mgonjwa. Vifaa hivyo ni pamoja na vifaa Robot ya Da Vinci inayotumika katika upasuaji.

Mfumo huu wa upasuaji hutumika katika teknolojia ya upasuaji wa magonjwa yanayohusiana na mfumo wa mkojo (Urology), magonjwa ya wanawake (Gynaecology), moyo, utumbo, na magonjwa ya watoto na matatizo ya uti wa mgongo.
--

Saturday, September 19, 2015

MKenya Agundua Tiba ya COPD - Ugonjwa wa Kupumua Kwa Shida

AJABU AFRICA wametoa taarifa kuwa Mkenya amegundua Tiba ya Uginjwa wa Kupumua kwa Shida (COPD).  Dr. George Kiongera ni Mkenya kwa kwanza kuwa na shahada la Ph.d katika uuguzi (Nursing).  Alifanya utafiti kuhusu ugonjwa wa COPD na athari zake kwa wazee.  Tiba aliyogundua umekuwa na mafanikio kwa wengi.
 
 
****************************************************

BREAKING NEWS...Kenyan Man in Boston Discovers COPD treatment, Featured in Nursing's Leading Journal

BOSTON__Dr. George Kiongera, the Kenyan man who several years ago became the first Kenyan known to hold a Doctorate Degree in Nursing Practice has achieved another rare feat; a research study he conducted recently on the first ever known treatment of older patients with Chronic Obstructive Pulmonary disease (COPD) was accepted and published in the Journal of Gerontological Nursing--the world's leading resource for nursing care of older adults.

The piece, titled "inpatient pulmonary rehabilitation program in a long-term care facility" was featured from page 44 to 52 of the most recent issue (August 2015) of the nursing care journal that is published only once a month.

Currently, there is no any other Kenyan known to have been published in the world renowned journal.

Following the success of Dr. Kiongera's study findings and recommendations in treating patients stuck in long term care facilities due to COPD, a debilitating breathing problem with no previously known cure, and as a result accepted and featured nursing care journal, Dr. Kiongera's research now officially becomes a resource for healthcare providers and medical students all over the world dealing with COPD patients. KWA HABARI KAMILI BOFYA HAPA  FULL STORY >>>>>


Thursday, March 22, 2012

Dr. Mbele Asifia Tiba Aliyopata Dar

Wadau, Prof. Mbele yuko safarini Tanzania.  Ameugua na kwenda hospitalini. Anasema kuwa ameridhika na tiba aliyopata, hakuwa na haja ya kukimbilia nchi za nje kam India kutibiwa.

****************************************

Kutoka  Hapa Kwetu  Blog



Thursday, March 22, 2012

Nimeugua Dar es Salaam; Natibiwa Hapa Hapa, Sio India

Nimeugua Dar kuanzia siku chache zilizopita. Nimejikuta nikiwashwa hasa mikononi, miguuni, na mgongoni. Kwa siku mbili sikuweza kulala usiku. Katika kuulizia watu, nikaambiwa ni "allergy." Na mhudumu mmoja kwenye duka la madawa maeneo ya Sinza aliniambia niende Magomeni, kwenye hospitali ya Dr. Ole.

Nilienda hapo. Wakati wa kuchukuliwa damu ili ipimwe, mpimaji alinipiga mchapo kuwa isije ikawa nimewekewa sumu ya unga. Akazidi kutonya, huku akijifanya ananyunyizia unga mezani, kuwa kaunga kidogo tu kanatosha. Nami nilijibu kuwa mtu huwezi kujua, kwani Bongo haina dogo. Tukawa tunachkea.

Ni kweli daktari alipochunguza ripoti ya upimaji amegundua nina "allergy," na akanielezea sababu zake. Aliniandikia sindano na vidonge vya aina mbali mbali. Alisema kuwa hiyo dozi itafuta kabisa hili tatizo. Nimedundwa sindano jana na vidonge nikaanza. Tayari nimeshaanza kujisikia nafuu. Naendelea vizuri kabisa.

Nimeleta habari hii binafsi kwa sababu maalum. Kwanza, mimi kama m-Tanzania nina imani na madaktari wetu. Ninafundisha Marekani, na ninapougua kule natibiwa kule. Ninapougua Tanzania natibiwa hapa. Tena, miaka yote ya maisha yangu, kabla sijaenda Marekani nilikuwa natibiwa hapa Tanzania, bila matatizo.

Sioni kama kuna tofauti kati ya madaktari wa Marekani na wa kwetu. Kilichopo tu ni kuwa madaktari wa kwetu wapewe mahitaji yanayopasika katika kumshughulikia mgonjwa. Na hilo ni jukumu la serikali, wala isijaribu kukwepa, kwani Tanzania si nchi maskini. Nakerwa ninapowasikia viongozi wa nchi hii wakidai kuwa sisi ni nchi maskini. Juzi hapo nimemsikia waziri kwenye kipindi cha televisheni akitoa huo upupu kwamba Tanzania ni nchi maskini.

Nawashangaa wa-Tanzania waoendelea kuwapigia kura mbumbumbu wa aina hiyo, wasio na upeo kiuongozi, hawana fikra za kuijengea jamii ari ya maendeleo, badala yake wana upeo wa kudumaza na kukatisha tamaa. Nawashauri wajifunze kutoka kwa Rais Obama, ambaye katika mazingira yoyote yale, hawakatishi tamaa raia wake, bali anawahakikishai kuwa Taifa litapambana na litashinda, litafanikiwa. Lakini viongozi wa kwetu, kila kukicha ni vilio kuwa sisi ni nchi maskini!

Uwezo wa kuimarisha hali ya mahospitali yetu tunao, tukizingatia rasilimali nyingi tulizo nazo katika nchi hii. Pia, magonjwa mengi tunayopata hayahitaji daktari bingwa. Yanatibiwa vizuri, iwe ni Marekani au Tanzania. Tena yako magonjwa ambayo ni ya nchi kama zetu, ambayo wataalam wake ni hao madaktari wentu. Mifano ni malaria. Usidhani kuwa ukipata malaria, ukimbilie Marekani. Unaweza ukafia kule, kwa sababu sio madaktari wengi wanaijua malaria na namna ya kupambana nayo kama wanavyojua madaktari wa nchi kama Bongo. Hao madaktari wetu wanasomea magonjwa ya hapa kwetu. Ninavyofahamu, wanapoenda kusomea Ulaya, utakuwa wanasomea "tropical medicine" ambayo ndio uwanja wa mapambano katika nchi kama yetu.

Madaktari wetu wana ujuzi wa hali ya juu, utawakuta wako katika nchi mbali mbali. Ninawafahmu baadhi ambao wako Marekani, katika hospitali mbali mbali, kama vile Mayo Clinic, ambayo ni maarufu sana duniani. Yaani inashangaza kuwa ukienda hizo hospitali, unawakuta madaktari wengi wa kutoka Afrika, yaani madaktari kama hao wanaonyanyasika Tanzania kwa sababu ya viongozi wetu kutokuwa na upeo upasao.

Kwa hiyo, serikali yetu inachopaswa kufanya ni kuwekeza katika huduma za mahospitali yetu hapa hapa nchini. Iweke vifaa na miundombinu, ili madaktari wetu waweze kutumia ujuzi wao ipasavyo. Wakipata vifaa na miundombinu, na wakilipwa ipasavyo, watafanya yale yale ambayo baadhi ya watu nchini wanayatafuta India au ughaibuni. Tunapowapeleka watu nje eti kuchekiwa afya, wakati hizi ni taaluma za madaktari wetu pia, au tunawapeleka watu kutibiwa ugonjwa kama niliopata mimi wiki hii, ambao madaktari wetu wanajua namna ya kuutibu, ni kuwadhalilisha madaktari wetu, na mimi sitalilazia damu suala hilo.

Miezi michache iliyopita, nilipata fursa ya kumsikiliza Dr. Mark Jakobson, ambaye ni mwendeshaji wa hospitali ya Selian, Arusha. Alikuwa akitoa mhadhara Minnesota, kuhusu shughuli za hospitali hiyo. Siku moja nitaelezea katika hii blogu yangu. Jambo mmoja ninalokumbuka ni jinsi alivyowapigia debe madaktari wa ki-Tanzania wanaofanya naye kazi. Anatamani tu angekuwa na uwezo wa kulipa vizuri zaidi, ili wasipate vishawishi vya kwenda sehemu zingine.

Makala hii nimeiandika pia kwa sababu juzi hapo niliandika makala kuhusu mgomo wa madaktari nikaishutumu serikali kwa kudiriki kugombana na madaktari. Kwa hivi, nimejichukulia fursa hii kuelezea zaidi hisia zangu. Kati ya mambo niliyosema ni kuwa kisaikolojia, daktari anapaswa awe kazini akiwa amefurahi na moyo mkunjufu.

Huyu jamaa aliyenipima damu alitoa mchapo na tukacheka. Muuguzi au daktari anapokuwa na moyo mkunjufu na ucheshi, anapokuwa hana msongo wa mawazo, ni baraka kwa wagonjwa. Watafiti wa masuala ya saikolojia ya wagonjwa na matibabu wanathibitisha hilo. Ndio maana niliishutumu serikali kwa kutotambua umuhimu wa kuwaridhisha madaktari.

Tuesday, January 03, 2012

Babu Wa Loliondo Janga La Kitaifa 2011 - Maggid Mjengwa


Mh. Lukuvi na Binti yake Mwalimu Nyerere wakipata 'kikombe' kutoka kwa Babu
Imeandikwa na Maggid Mjengwa

Babu Wa Loliondo Janga La Kitaifa 2011

 “Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote”,ni wimbo unaovutia ni wimbo; unaelezea wasifu wetu wasifu wa nchi yetu Tanzania kweli jina lako ni tamu tulalapo tunakuota wewe, Ndoto wakati mwingine uashiria kitu kijacho !

Naam ndugu zangu Watanzania, tukiwa tunakaribia kumaliza mwaka nchi yetu imekumbwa na majanga kadhaa likiwepo hili la mafuriko napenda kuchukua nafasi hii kuwapa pole wote  waliofikwa na mafuriko najua Mungu atasimama upande wao, janga hili ni  muendelezo wa majanga mengi yaliyoikuta Tanzania yetu tunayoiota utalalapo, Ambikile Mwaisapile maarufu kama babu wa loliondo ni moja ya majanga hayo .

Inayodaiwa kuwa tiba ya Babu wa Loliondo, badala ya kuwa msaada kwa taifa, imeonyesha madhara zaidi ya kiafya, kijamii na kiuchumi. Tuliandika kutahadharisha na kushauri. Tumepuuzwa; maana, kwa wengine, tiba ya Babu ilikuwa ni mradi, na kwa kweli kugeuzwa kuwa mradi wa kitaifa.

Na kilichojikita katika kuwaacha watu wetu wakitaabika ni unafiki wetu. Tuna maradhi mabaya, na ni sugu. Ndio, miongoni mwetu kuna wenye kusumbuliwa na maradhi ya unafiki. Nitatoa mfano nilipata kukaa na wasomi wawili, tena wana digrii zao. Tukazungumzia ya Babu wa Loliondo.

Mimi na wasomi wale tulikuwa na misimamo ya kufanana, tulipinga upotoshaji unaoendelea katika jamii kuwa Babu wa Loliondo, Ambilikile Mwasapile, anatibu ukimwi, kansa, kisukari na mengineyo. Na kwa vile wote tumekwenda shule, hoja kuu ilikuwa hii; kuwa hadi sasa hakuna hata wagonjwa watatu wa ukimwi waliothibitishwa kitaalamu kuwa wamepona ukimwi kwa dawa ya Babu.

Badala yake, kuna wengi wamekufa baada ya kuacha kutumia madawa waliyoelekezwa na madaktari watalaamu waliosomea tiba.

Wakati tukiendelea kuzungumza, mara akatokea mheshimiwa fulani, naye akaingia moja kwa moja kwenye mjadala. Alimtetea Babu na kusisitiza kuwa. Babu ni lulu ya taifa, lazima aenziwe. Wasomi wale afadhali wangekaa kimya, hapana, walianza kumuunga mkono mheshimiwa kwa hoja nyepesi.

Hawakuwa wapumbavu, walijifanya tu wapumbavu wakiniacha mimi nikipambana peke yangu kuziponda hoja za mheshimiwa yule. Kwa kiasi fulani, niliogopa kuona hulka hii ya wasomi wetu. Wasomi ambao, kwa unafiki, wanashindwa kutetea na kusimamia katika hoja zao za msingi. Na hii, bila shaka, ni moja ya majibu ya swali la kwa nini Tanzania ni masikini?

Hakika, ya Babu wa Loliondo ni aibu yetu kitaifa. Katika karne hii ya 21 nchi yetu inatumia raslimali zake kufanya promosheni ya ndoto ya Mtanzania mmoja kati ya Watanzania milioni 42! Ndio, tunafanya promosheni ya jambo lisilo na uthibitisho wa kisayansi. Si tuliona, haikupita siku bila kusikia  habari za Babu wa Loliondo?

Kwa sasa, tunaweza kabisa kusema, kuwa habari za huduma za Babu wa Loliondo zilitangazwa na kuufikia umma kuliko habari za Wizara yeyote ile katika  Serikali ya Awamu ya Nne. Babu wa Loliondo si mchezo bwana, alikuwa na ‘maafisa habari wake’ wanaowafunika hata maafisa habari wa Wizara za Serikali.

Na katika mzaha huu wa mambo ya msingi kitaifa, tuna maelfu kwa maelfu ya Watanzania wanaotaabika na hata baadhi kufa kwa kuamini kuwa Loliondo kuna tiba, na iko Loliondo tu! , kuna Watanzania walioweka rehani mavuno yao ya  mwaka mzima ili wapate nauli ya kwenda kwa Babu. Si wameambiwa, kuwa hata mawaziri wanapanga foleni ya kwenda kupata kikombe cha Babu!

Na wakishapata kikombe wanapiga picha ya ukumbusho, au labda ya kisiasa.  Asubuhi yake ’maafisa habari’ wa Babu wameshatundika picha ya waziri ukurasa wa kwanza gazetini! Jimboni kwa mheshimiwa wapiga kura wake watamwona au  kusikia kuwa Mheshimiwa naye anaumwa kama sisi, na amepata kikombe cha Babu!

Kikombe cha Babu ni abrakadabra, nilipata kuandika hilo. Na Watanzania, baadhi, kwa hiyari yetu, tumekubali kujifanya, wajinga na hivyo kuwapumbaza wengi wengine. Kwanini? Tulitafute jibu kwa kufikiri kwa bidii.

Hebu jiulize; wakati Shirika la Afya Duniani (WHO), Juni mwaka huu, liliadhimisha miaka 30 ya mapambano dhidi ya ukimwi, je, Tanzania, kama nchi, tulikuwa na banda la maonyesho likielezea ugunduzi wa tiba ya ukimwi  iliyotokana na ndoto ya Babu?!

Labda ndio maana, magazeti yetu ya lugha ya Kiingereza hayakufanya sana promosheni ya tiba ya Babu. Maana, kama habari za Babu zingepewa uzito kama  ilivyo kwenye magazeti yetu ya lugha ya Kiswahili, basi, wana jumuiya ya  Kimataifa, wakiwamo wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, huenda  wangeshindwa kuamini wanachokisoma.

Maana, wawakilishi wa mashirika kama PSI na FHI yenye miradi ya kupambana na ukimwi nchini na mengineyo wangejiuliza; nini hasa wanachokifanya katika  nchi yetu. Na pengine wameshatafsiriwa tunachooandika juu ya Babu kwa Kiswahili chetu!

Si ajabu basi, Ubalozi wa Marekani ulikuja na tamko lake Mei 5 mwaka huu.  Wamarekani hawa, kwa kuwaonea huruma Watanzania, wameshauri watu wanaotumia  tiba mbadala wasiache kutumia dawa walizopewa na madakatri na vile vile  waendelee kujikinga na maambukizi.

Na wakaweka msisitizo kuwa, kuacha kutumia dawa hizo za madaktari watalaamu kunafanya dawa hizo zinapotumiwa tena kushindwa kufanya kazi ipasavyo (drug resistance). Na ajabu ya habari ya tamko lile la Wamarekani ilichapishwa katika gazeti moja tu kwa lugha ya Kiingereza - The Citizen, jina la gazeti  hilo lina maana ya Mwananchi; ingawa wananchi wengi hawakupata habari hiyo kwa lugha yao!

Kwa hakika, hatuhitaji kuambiwa na Wamarekani juu ya ukweli huu na wajibu wetu. Huu ni wakati kwa wizara inayohusika kufanya jitihada za dhati kutoa tamko litakaloweka bayana kuwa tiba inayodaiwa kutolewa na Babu bado haijathibitika kitalaamu kama inaponya maradhi sugu kama vile ukimwi, kansa; na kisukari.

Wakati utafiti huo ukiendelea, umma ukumbushwe kuwa, dawa zinazotambulika kitalaamu kwa sasa ni zile zinazotolewa na madaktari wetu watalaamu. Kwamba  wanaokwenda kwa Babu wana ruhusa ya kufanya hivyo, lakini, kikombe cha Babu  kinaweza kunywewa pamoja na dawa za hospitalini.

Tufanye hivyo sasa, na ujumbe huo usambazwe kwa nguvu zote na maafisa wa  habari wa wizara husika. Ndio, maofisa habari wa Wizara ya Afya nao  washindane na ‘maafisa habari’ wa kujitolea wa Babu wa Loliondo!

Watanzania tunapita kwenye kipindi kigumu sana. Na huu ni wakati wa  kutafakari kwa kina. Na nimepata kumwuliza jamaa yangu swali hili; mwanadamu ; unafanyaje unapoamka na kukuta dunia unayoishi ardhi yake imeanza kumegeka na kuchotwa na bahari? Naye akanijibu; ” Huo ndio utakuwa mwisho wa dunia!”

 Aliyenijibu alikuwa amechoka kufikiri. Nilidhani angetamka kuwa, angeanza kujifunza kuogelea. Maana, kwa kuogelea majini angeweza kukutana na kisiwa, au nchi kavu.

Wanadamu tumejaliwa akili ili tuweze kufikiri. Na kufikiri ndio njia  mojawapo ya kuiteka kweli. Kufikiri kunahamisha milima na hata kuiweka kando  kuruhusu mwanga upite. Inakuwaje basi mwanadamu anapoacha kufikiri?

Haya ya kwa ‘Babu wa Loliondo’ ni kielelezo cha Watanzania kuamua kuacha kufikiri. Kuna umma uliojifunika vilemba vya ujinga. Umma uko gizani, ; unahitaji mwanga.

Yumkini wakatokea Watanzania wenzetu wakaoteshwa na Mungu juu ya  dawa za tiba kwa mwanadamu. Na hapo wakaingiza suala la imani. Lakini, jambo hilo halituzuii wanadamu kuhoji na kudadisi. Ndio, kuuliza maswali. Na kwa Serikali, jambo hilo haliizuii kufuata taratibu zake za kawaida ikiwamo kufanyia utafiti jambo hilo na kutoa msimamo wa kiserikali.

Hata kama Watanzania watakuwa na uhuru wa kwenda kwenye tiba za imani, lakini msimamo wa Serikali uwepo. Na kwa wengi utabaki kuwa ndio mwongozo;  maana, watakuwa wameufanyia utafiti. Nahitimisha.

Niwatakieni Heri ya Mwaka Mpya.

Maggid Mjengwa.

http://mjengwablog.com/

*************************

 SOMA HABARI ZAIDI ZA VIFO LOLIONDO GLOBAL PUBLISHERS:

http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/loliondo-1

Monday, July 11, 2011

Kisonono sasa haina Tiba!



Wadau, leo kuna habari kuwa kuna aina ya kisonono ambayo haitibiki! Tuombe isiingie Afrika. Huenda umekwishaingia kupitia watalii na malaya! Midume ilizoea ikiambukizwa kisonono basi inaenda kuchoma sindano ya PPF (penicillin), baada ya masaa mnne mambo safi. Haya kama haina dawa mbona kazi ipo! Kwa wanawake wanaweza kuwa na kisonono na wasijue kwa muda mrefu, huko ikiathiri uzazi na wanakuwa na maumivu makali kwenye kiuno. Tumieni kondomu wakati wote! Haya mambo ya kusema, au unatumia kondumu, hunipendi au unficha nini yaishe...la sivyo tutakwisha!

***************************************************************


LONDON (Reuters) - Scientists have found a "superbug" strain of gonorrhea in Japan that is resistant to all recommended antibiotics and say it could transform a once easily treatable infection into a global public health threat.

The new strain of the sexually transmitted disease -- called H041 -- cannot be killed by any currently recommended treatments for gonorrhea, leaving doctors with no other option than to try medicines so far untested against the disease.

Magnus Unemo of the Swedish Reference Laboratory for Pathogenic Neisseria, who discovered the strain with colleagues from Japan in samples from Kyoto, described it as both "alarming" and "predictable."

"Since antibiotics became the standard treatment for gonorrhea in the 1940s, this bacterium has shown a remarkable capacity to develop resistance mechanisms to all drugs introduced to control it," he said.

Mnaweza kusoma habari kamili kwa KUBOFYA HAPA:

Thursday, September 02, 2010

Hatimaye Dawa ya UKIMWI?

Wadau, ingawa siku hizi kuna dawa za kurefusha maisha ya walioathirika na HIV/AIDS bado hakuna tiba. Mwakani kutakuwa na majaribio ya kuona kama wanaweza kusafisha virusi hivyo kutoka kwenye miili ya walioathrika. Tuombe Mungu kuwa watafanikiwa.

************************************************************
Kutoka Bloomberg.com

AIDS Quest to Kill `Sleeping' Virus Enlists Merck Cancer Drug

By Simeon Bennett - Sep 2, 2010

The 30-year-long search for a cure for AIDS, the world’s deadliest viral infection, may get a renewed boost from an unlikely source: a little-used Merck & Co. cancer drug.

Researchers at the University of North Carolina in Chapel Hill plan to test Merck’s drug, Zolinza, next year in about 20 people infected with HIV, the AIDS virus. The goal is to determine if Zolinza, or a medicine like it, can force HIV out of cells where it can reside, concealed from attack by potent antiviral treatments, said David Margolis, a professor of medicine who’s leading the research.

While AIDS drug cocktails can eliminate more than 99 percent of virus from an infected person, the treatment isn’t a cure because a remnant of the virus remains hidden in certain cells. For years, scientists have sought a simple way to drive the remaining virus into the bloodstream where the drugs can clear them from the body. Zolinza, approved in 2006 for use against a rare type of blood cancer, may work by blocking an enzyme that helps the virus avoid detection.

“It’s really all about trying to move the field ahead,” Margolis said in a telephone interview. “We don’t expect to cure anybody, but we expect to really show whether it can work the way we think it does in people -- or not.”

Zolinza earned Whitehouse Station, New Jersey-based Merck $15 million in 2008, the last year it disclosed sales of the drug, for treating a malignancy of white blood cells that affects the skin. In a laboratory test published last year, Margolis used the medicine to coax HIV out of hiding in cells taken from infected patients. Now he wants to replicate the result inside the body. Success would show he’s on the right track to finding a cure.

Mysterious Illness

“There is a good chance that it will cause some activation of latently infected cells,” said Robert Siliciano, a professor of medicine at Johns Hopkins University in Baltimore who first identified the cells in which HIV hides out, and isn’t involved in the Zolinza trial. “Nobody knows if it will work, but it’s important to try.”

AIDS was first observed as a mysterious illness among gay men in the U.S. in 1981, the same year Margolis started medical school at Harvard University in Boston. Since then it’s killed more than 25 million people, mostly in Africa.

Kusoma taarifa kamili Bofya HAPA:

Thursday, November 13, 2008

Tiba ya UKIMWI!!!


Wadau, hivi kweli inawezekana tiba imepatika ya UKIMWI? Ila navyoona kama ni tiba itakuwa ghali sana. Hizo tiba za kansa zina bei kweli.

Tuombe kuwa hii tiba ni tiba ambayo dunia umeusubiri kwa muda mrefu mno na utaponyesha watu wengi walioathirika na UKIMWI na virusi vya UKIMWI.


*******************************************************************

Kutoka: http://www.dw-world.de/dw/article/0,2144,3787690,00.html

Cancer Treatment Might Offer Clue To AIDS Cure

Doctors at a Berlin hospital were surprised to discover that, while treating a man for cancer, they also rid his blood of the HIV virus. This could yield a new direction in the fight against AIDS.

The patient in question was a 42-year-old American living in Berlin who was undergoing a bone marrow transplant at that city's Charite hospital.

The bone-marrow donors were selected because they possessed a rare HIV-resistant genetic mutation since the man had to stop taking AIDS-inhibiting medication for the cancer treatment to work.

On Wednesday, Nov. 12, doctors announced that after two years of treatment, not only had the patient not contracted AIDS -- his blood now appeared to be clear of HIV infection.

"There is no longer demonstrable evidence that the patient is infected," Eckhard Thiel, Director of Charite's Clinic for Hematology and Oncology, told reporters. "We're very happy and proud to have achieved this breakthrough."

Thiel added that the result was the first of its kind ever recorded in the world.

The question is now: What could it mean in the search for a cure for HIV-AIDS?

No immediate remedy
Some 2 million people died of AIDS in 2005

Scientists cautioned that the fact that the HIV virus can no longer be detected in the patient's blood stream does not necessarily mean it is absent from his entire body.

"The HIV virus could be in the spleen, the lymph nodes, the nerve cells -- anywhere really," Norbert Brockmeyer, a clinic director at the university hospital of Bochum, told the online edition of the news magazine Der Spiegel.

And even if effective against HIV, several factors argue against the idea that similar treatments could be carried out on a wide-spread basis.

Bone marrow transplants and the accompanying chemotherapy are themselves dangerous procedures, and the patient in question was fortunate in having a genetic make-up that allowed for an unusually high number of potential donors.

Charite doctors say they are monitoring the patient's health and are prepared to put him back on anti-retroviral drugs if the HIV infection reappears.

"We cannot say with certainty that the virus won't begin replicating itself in the future," Thomas Schneider, Charite's Director of Infectology, told a press conference. "But the mere fact that it hasn't yet done so, is a minor sensation."

More research will be needed to determine what exact significance, if any, the breakthrough at the Charite has for the overall fight against AIDS.

Today, more than 38 million people, mostly in Africa and Asia, are estimated to be infected with HIV, the virus which causes AIDS.