Showing posts with label dawa. Show all posts
Showing posts with label dawa. Show all posts

Thursday, June 26, 2014

GARANI MW1 - Eti ni Dawa ya Kutibu UKIMWI Kutoka Malawi

Eti, kuna dawa ya kutibu UKIMWI huko Malawi.  Hii dawa ni unga ambao unaweza kuchanganya na chakula chako.  Waliotengeneza wanadai kuwa pamoja na kutibu, muathirika atakuwa na hamu ya kula chakula kingi na atakuwa na kiu mara kwa mara.

 Lakini watu wamejitokeza na kusema hiyo dawa ni feki na haitibu ugonjwa wowote!

Wadau, watu wanaotaka kupona watakuwa na hamu ya kutumia kitu chochote ambacho kinaweza kuwatibu! Mnakumbuka Kikombe cha Babu?  Mnakumbuka waliozuka na vilombe baada ya hapo?  Nakumbuka miaka ya 90 kuna mtau alidai ana dawa Nairobi! Wagonjwa walimiminika kule! Watu wanachezea tumaini ya wagonjwa!  Ni dhambi!

Mnaweza kusoma habari ya  wanaodai GARANI MW1 ni feki kwa KUBOFYA HAPA:


******************************************************

GARANI MW1 - Herbal AIDS MEDICINE



GARANI MW1 is a herbal preparation that is being used to treat people that have HIV and AIDS. It has strong antiviral properties and therefore also positively affects immune system. The medicine improves the immune system by increasing ones CD4 cell count because viral replication is reduced/halted. The body is then able to fight opportunistic infections that come due to the compromised immunity.  The viral load is reduced to undetectable levels and people have tested non reactive to the HIV tests using both anti body and HIV DNA/ PCR tests. 
 As Garanimw1 is available in powder form, it is taken through porridge made from maize flour with no sugar or salt, one tea teaspoon per day, once a day for three consecutive days, repeated after a period of two weeks from the same pack. Some have become totally cured after taking only one pack while others may need to repeat the dose at 1 month intervals.  
DISEASES

Frequent and nonstop headaches, chest pains and breathlessness, chronic undefined coughs, skin rashes, other skin conditions, cancer, hair loss, swollen lymph nodes, painful legs, asthma, unexplained weight loss, numbness in the legs and other body parts, hormonal imbalances, general body weaknesses and pains, chronic wounds, diabetes, high blood pressure, loss of memory, cancerous growths, anaemia, skin discolorations and many others. 
 
 There are many people that have taken the medicine but did not have the HIV virus and have reported success stories on diseases and conditions such as diabetes, high blood pressure, asthma, stomach ulcers, sickle cell, and other abdominal swellings in the body, amenorrhea and others. Some people who had lost their shape due to the effects of ARVs (lipodystrophy) have regained it even while taking the drugs.  
INSTRUCTIONS

1.The full course of the medicine is three teaspoons of the powder taken over a period of three days, one teaspoon per day for three days – put in porridge with no sugar or salt. The remaining powder should be taken after two weeks in the same manner until it is finished. One should choose time when to take the medcine
 2. The porridge should be put in a bowl or cup before adding the medicine and not in a pot.
3.For couples, both should take the medicine and abstain from sex or use condoms correctly and consistently until they go for the HIV test when time is due  
4.One can go for test after 12 months. This is the HIV antibody test in which a small amount of blood from a finger prick is tested since antibodies may persist in the blood for several months even after when the disease causing organism has disappeared from the blood stream.  
5.HIV DNA PCR test can be done after 10 months which looks into the presence of the actual virus.  
6.If one is on ARVs or any other medication they should continue taking the medicine and one will be advised to stop taking the ARVs by a qualified physician when all the above tests are done and are negative 
 7.The known effects of the medicine is that others may develop increased appetite and thirst therefore food and water should be taken as required.
 NOTE: For better and faster results, the dosage should be repeated at 1 month interval for two or more times with condom use at all times although one dose

Sunday, April 06, 2014

Kumbe Paka ni Dawa!

Kumbe paka anatibu magonjwa! Acheni kuwatibua na mawe na kuwamwagia maji ya moto. Umekumbatie kama rafiki yako mepndwa! Utaishi maisha marefu!

****************************




Thursday, May 02, 2013

Dawa ya Mbu - Ndimu na Karafuu!






Wadau, kumbe ndimu na karafuu ni dawa ya mbu!  Hebu mjaribu muone kama mbu wanapungua!

Monday, July 16, 2012

Dawa ya Kuzuia Maambukizi ya UKIMWI Yapatikana!

Hatimaye kuna dawa ya kuzuia maambukizi ya UKIMWI.  Hii dawa itafiaidi wasiowathirika tayari.  Ina maana kuwa kama mtu anataka kufanya mapenzi na muathirika akimeza hiyo dawa haatambukizwa ugonjwa!  Vita dhidi ya UKIMWI unaendelea lakini, tiba bado haijapatikana. Ila kwa sasa kuna dawa za kurefusha maisha na wenye virusi vya UKIMWI wanaweza kuishi maisha ya kawaida.

**************************************************************
KUTOKA CNN.COM

FDA approves Truvada for prevention of HIV/AIDS


Adults who do not have HIV but are at risk of getting the disease will now be able to take a drug to reduce their chance of getting infected. For the first time, the U.S. Food and Drug Administration approved a drug for this use on Monday.

The drug is Truvada, an antiretroviral medication made by Gilead Sciences, Inc., which was already approved by the FDA in 2004 to help control HIV infection.

Truvada is a combination of two HIV medications - emtricitabine (Emtriva) and tenofovir (Viread) - into one pill that is taken once a day. As a treatment for HIV, it is always used in combination with other HIV drugs.

Recent studies showed pre-exposure prophylaxis or PrEP can reduce transmission of the virus significantly–up to 96% - when uninfected partners of people infected with HIV took Truvada.

Dr. Debra Birnkrant, M.D., director of the Division of Antiviral Products, Center for Drug Evaluation and Research at the FDA stressed Truvada alone should not be used to prevent HIV infection. It should be used in combination with other safe sex practices.

“Practicing safer sex and good health practices must be part of the treatment," Birnkrant said. “We will be putting a box warning to let those using Truvada know that it is part of the therapy with combination of safer sex practices, and that doing this, will reduce the risk of the development of AIDS/HIV.”

Dr. Anthony Fauci, director of the National Institute for Allergy and Infectious Diseases at the National Insitutes of Health, agrees.

“The approval of Truvada to prevent HIV infection in uninfected individuals who are at high risk of sexually acquired HIV infection is a signficant development, providing an important addition to our toolkit of HIV prevention interventions,” Fauci says. “However, it is critical to stress that Truvada as ‘pre-exposure prophylaxis’ should not be considered a stand-alone method, but should be used in conjunction with other proven HIV prevention stratgies such as condom use, risk-reduction counseling, and frequent HIV testing.”


Birnkrant says she hopes the right messages will get out, and that Truvada is used properly. "We have the box warning that a negative HIV test must be reported before Truvada is prescribed," she said.

According to Gilead, Truvada the most-prescribed antiretroviral in the United States. “Today’s decision is the culmination of almost 20 years of research involving investigators, academic and medical institutions, funding agencies and nearly 20,000 trial participants around the world, and Gilead is proud to have been a partner in this effort,” said Norbert Bischofberger, Executive Vice President, Research and Development and Chief Scientific Officer, Gilead Sciences.

Dr. Robert Grant, the lead investigator of the iPrEx trial at the University of California San Francisco who looked at Truvada as a prevention treatment among high-risk men who have sex with men (MSM), says the approval is a major milestone in the 30-year fight against AIDS. “The use of PrEP alongside routine HIV testing gives us a tremendous opportunity to reduce the rate of new HIV infections in this country and around the world.”

At the University of Washington another PrEP study proved very successful in reducing infection rates in couples where one partner is infected and the other is not (called serodiscordant).

“The data clearly demonstrate that Truvada as pre-exposure prophylaxis is effective at reducing the risk of HIV infection acquired through sexual exposure,” said Dr. Connie Celum, Professor of Global Health and Medicine at the University of Washington and lead investigator of the Partners PrEP trial. “It is exciting to consider the potential impact of this new HIV prevention tool, which could contribute to significantly reducing new HIV infections as part of a combination HIV prevention strategy. Although the implementation of PrEP will bring challenges, they can be anticipated and systems developed to address these challenges."

But the AIDS Healthcare Foundation, the nation's largest HIV/AIDS group, blasted the FDA's decision. "The FDA’s approval of Gilead’s Truvada as a form of HIV prevention today, without any requirement for HIV testing is completely reckless and a move that will ultimately set back years of HIV prevention efforts,” said Michael Weinstein, AHF’s President.

“From the beginning, we believe there was a rush to judgment by government officials and others in favor of such approval despite decidedly mixed studies offered in support. And while the FDA recommends a negative HIV test prior to use of Truvada as PrEP and states that use by people with an ‘…unknown or HIV positive status…’ is ‘contraindicated,’ it in no way actually requires HIV-testing in any manner-just strengthening of the ‘Boxed Warning’ on Gilead’s packaging. The FDA’s move today is negligence bordering the equivalence of malpractice which will sadly result in new infections, drug resistance and serious side effects among many, many people."

Wednesday, June 06, 2012

Wiki ya Famasi ya Taifa/ National Pharmacy Week


TAMKO

CHAMA CHA WAFAMASIA TANZANIA (PST)

KINAZINDUA WIKI YA FAMASI YA TAIFA 2012, 11-15 Juni

Okoa Maisha: Ujulishe Umma Matumizi Sahihi na Utunzaji Bora wa Dawa Nyumbani

Dar es Salaam, 06 Juni 2012 – PST inapenda kuujulisha umma wa watanzania kuwa inazindua Wiki ya Famasi ya Taifa "National Pharmacy Week (NPW)" ambayo itaadhimishwa nchi nzima. Kauli mbiu ya mwaka huu ni: “ Okoa Maisha: Ujulishe Umma Matumizi Sahihi na Utunzaji Bora wa Dawa Nyumbani"

Lengo la kuchagua Kauli Mbiu hii ni katakana na kuongezeka kwa dawa nyingi zisizohitaji cheti kulinganisha na zile ambazo zinatumika kwa kutibu magonjwa ya muda mrefu. Aisha, katokana na utandawazi na kukua kwa teknolojia, mahitaji ya dawa yameongezeka katika jamii.

Kilele cha Wiki ya Famasi kitafanyika tarehe 16 Juni ambapo pia tutasherehekea Siku ya Famasi kwa Nchi za Jumuiya ya Madola "Commonwealth Pharmacy Day (CPD)". Katika Mwaka 2012, Kilele cha Wiki ya Famasi kitafanyika katika viwanja vya Karimjee kuanzia saa 2.00 asubuhi.

Kutokana na ongezeko la mahitaji ya dawa, PST iliona kuwa ni vema kuhamasisha na kuelimisha umma kuhusu matumizi sahihi na utunzaji bora wa dawa nyumbani ili kuokoa maisha. Katika wiki inayoanza 11 - 15 Juni, PST imepanga kufanya shughuli mbalimbali katika jamii inayotuzunguka, kikubwa ni kutoa elimu kwa jamii. Kutakuwepo na mahojiano ya papo kwa papo kwa wagonjwa na wananchi katika maeneo mbalimbali ambapo vipeperushi vilivyobeba ujumbe wa wiki vitagawiwa. Vilevile ujumbe kwa wananchi utatolewa kwa kutumia vyombo vya habari ili elimu ya matumizi sahihi na utunzaji bora wa dawa majumbani uweze kuwafikia walio wengi.

Siku ya tarehe 16 Juni 2012, katika viwanja vya Karimjee, PST itasherehekea kilele cha Wiki ya Famasi na kuadhimisha Siku ya Famasi kwa Nchi za Jumuiya ya Madola. Katika siku hiyo, shughuli mbalimbali zinazohusu jamii zitafanyika zikiwemo uchangiaji wa damu, ushauri nasaha na virusi vya ukimwi. Ushauri mbalimbali utakaotolewa na wataalamu wa afya. Shughuli hizi zitakuwa na mchango katika kuhakikisha matumizi sahihi ya dawa na kuepuka upotevu wa rasilmali fedha kwa kununua dawa kiholela. Aidha, tunatarajia kuwapatia wananchi elimu ambayo endapo wataizingatia wataokoa maisha na hatimaye nchi yetu kuwa na jamii iliyo na afya katika kuleta maendeleo ya nchi.

PST inatoa wito kwa jamii ya watanzania kutumia fursa hii na kushiriki kikamilifu shughuli zote zitakazoendeshwa katika wiki itakayoanza tarehe 11 Juni hadi siku ya kilele tarehe 16 Juni 2012. Tunatarajia ushirikiano wakati tutakapopita majumbani na sehemu mbalimbali. Matarajio yetu ni kuleta mabadiliko katika kuhakikisha maisha bora kwa jamii inayotuzunguka. PST pia inategemea mwitikio na uwepo wako siku ya tarehe 16 Juni 2012.

TUUNGANE PAMOJA ILI TUOKOE MAISHA.

**********************************
PHARMACEUTICAL SOCIETY OF TANZANIA (PST)


INAUGURATES NATIONAL PHARMACY WEEK 2012 -11th-15th June.

Inform the Community on Rational Use and Storage of Medicines in Households: Save Lives.

Dar es Salaam, 06 June 2012 – PST today is announcing the inauguration of National Pharmacy Week (NPW) to be celebrated countrywide. The theme for this year is “Inform the Community on Rational Use and Storage of Medicines in Households: Save lives”. The reason for choosing this theme is based on the high demand of over the counter medicines let alone prescription medicines needing long term compliance. The effects of globalization and the power of technology compound on the behavior of demand for over the counter medications. The culmination of NPW shall be on the 16th June which is also a Commonwealth Pharmacy Day (CPD). This year, 2012, the culmination of National Pharmacy Week celebrations will take place at the Karimjee grounds.

Based on self medication behavior among others, the Society felt a need to intervene through raising awareness on Rational Use and Storage of Medicines aiming at Saving Lives. The focus is at households and community at large. PST is planning to conduct several activities that will be implemented during this year's National Pharmacy Week 11th to 15th June. There are shall be face to face interactions with the patients, the use of Information, Education and Communication (IEC) materials as well as media to deliver knowledge on rational use and proper storage of medicines to the public.

On the 16th June 2012, at Karimjee grounds, PST will culminate the National Pharmacy Week and mark the Commonwealth Pharmacy Day. During that day, several health and humanitarian activities will take place. These will include blood donation, HIV Testing, free healthcare checking and consultations by clinicians.

PST is aiming to use various supporting materials to propagate the theme. These materials with messages will include posters, stickers, banners, SMS messages, brochures, and articles in the newspapers, magazines, cards and advocacy letters to various authorities, institutions, association and consumers.

These activities will contribute to rational use of medicines and discourage waste. The aim is to equip households with this knowledge, which if properly followed will help to save lives and hence, complement the government in empowering the community, the national task force.

PST urge the community to uptake this opportunity and participate in the activities at their capacity as citizens of Tanzania. We look forward to their cooperation and support when visited at their households and communities. The activities envisaged are geared to bring a positive change and eventually save lives. PST expects their response and presence at the Karimjee grounds on 16th of June 2012.

Let's all join hands to save lives.

General information about PST

The Pharmaceutical Society of Tanzania (PST) is the national professional body of pharmacists engaged in various facets of the profession of pharmacy. The PST is committed to promote the highest professional ethical standards of pharmacy, focus the image of pharmacists as competent healthcare professionals, sensitize the community, government and others on vital professional issues and support pharmaceutical education and sciences in all aspects.

PST was established in 1967 and has a network of more than 1000 members. Two branches in Lake zone (Mwanza) and Northern branch (Moshi, Kilimanjaro) serving pharmacists, pharmaceutical Assistants and dispensers in the pharmacy profession working in various facets of health and development.

PST’s values embrace professional relationship with the patient and acts with honesty, integrity and compassion. The professionals honour the individual needs, values and dignity of the patient. The members support the right of the patient to make personal choices about pharmacy care with consciousness of guiding them through education and care when need arise.

Hence, we urge the community to seek pharmaceutical care at designated areas where they will be guided appropriately on rational use and storage of medicines.

For further information, please contact:

Pharmaceutical Society of Tanzania
Tel: +255 767-276255
+255 713-290780
E-mail: pst@aol.com

Pease visit http://www.pst.co.tz/

Wednesday, April 04, 2012

Waliopata 'Kikombe cha Babu' Wafariki Dunia - Habari Leo

Mgonjwa wa  UKIMWI
Waliopata ‘Kikombe cha Babu’ Wafariki Dunia
Imeandikwa na Waandishi Wetu; Tarehe: 4th April 2012
 
Idada kubwa ya wagonjwa waliokwenda kutafuta tiba kwa Mchungaji mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwaisapile, Loliondo wamepoteza maisha.

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambayo sasa itatangaza matokeo ya utafiti wa tiba hiyo ya ‘Kikombe cha Babu’ imesema wengi ni wale wenye Ukimwi walioacha matumizi ya dawa za kurefusha maisha (ARVs).

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Regina Kikuli, aliiambia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) jana Dar es Salaam, kwamba hadi sasa Serikali inafanyia utafiti watu 206 ambao walipata kikombe hicho.

Utafiti unaofanywa na Wizara hiyo inataka kubaini kama kweli dawa hiyo ina uwezo wa kuponya Ukimwi, kisukari, saratani na magonjwa mengine sugu. Wanaofanyiwa utafiti huo walipata ‘kikombe’ hicho baada ya kuugua kisukari na Ukimwi.

“Kwa sasa ni vigumu kusema dawa hiyo inaponya au haiponyi, tusubiri utafiti wa kitaalamu. “Baada ya miezi miwili tutatangaza matokeo kwa umma,” alisema Kikuli na kuongeza kuwa utafiti huo unafanywa katika hospitali mbalimbali nchini chini ya usimamizi wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR).

Utafiti huo unafanywa katika hospitali za Bugando, Mwanza; Mbeya; Mount Meru, Arusha; Hydom, Manyara na KCMC, Kilimanjaro. Hospitali hizo ziko maeneo ambayo wananchi wengi walijitokeza kupata ‘kikombe’ Loliondo. Kikuli pia alisema kwa sasa idadi ya Watanzania wanaokwenda Loliondo kupata tiba hiyo imepungua; lakini bado wananchi wa kutoka Kenya na nchi zingine wanaendelea kwenda kupata ‘kikombe’ hicho.

Hata hivyo, Kaimu Mganga Mkuu wa Serikali, Donan Mmbando, alikiri kuwa wagonjwa wengi wa Ukimwi waliokwenda kupata tiba hiyo na kuachana na ARVs wamepoteza maisha. Mbunge wa Nkasi, Ali Kessy Mohamed (CCM), aliishauri Wizara hiyo kuacha siasa badala yake iwaambie wananchi kwamba dawa ya Babu wa Loliondo haina madhara kwa binadamu, lakini pia haina uwezo wa kuponya magonjwa.

“Msiogope kusema kama wanasiasa, ninyi ni wataalamu, ni kweli kuwa ile dawa haina madhara kama yalivyo maji, lakini tusidanganyane, haitibu, kwa nini mnaendelea kudanganya wananchi?” Alihoji Mbunge huyo. Makamu Mwenyekiti wa PAC, Zainab Vullu, ndiye aliyetaka Wizara itoe taarifa ya utafiti wa tiba ya ‘kikombe cha Babu’.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, John Cheyo, alitaka kujua kama bado kuna idadi kubwa ya Watanzania wanaokwenda kupata tiba hiyo Loliondo. Mbunge wa Mufindi Kusini, Mendrad Kigola, alitaka kujua kama Wizara hiyo imewasiliana na nchi zingine za Ulaya ambazo raia wake walikwenda kupata tiba ya ‘kikombe’ kama walipona magonjwa waliyokuwanayo.

“Wenzetu wale Wazungu ni wepesi katika masuala haya ya utafiti, nataka kujua kama mmefanya juhudi za kuwasiliana nao?” Alihoji mbunge huyo na kujibiwa na Kaimu Mganga Mkuu kuwa kila nchi ina utaratibu wake wa utafiti.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA!

***********************************************

Hii imetoka kwenye gazeti la Habari Leo.   Mwaka jana saa hizi kila mtu alitaka kwenda kwa Babu. Inasikitikisha kuwa idadi kubwa ya wagonjwa wamekufa.  Babu yuko wapi leo hii, je, watu bado wanajazana kule Loliondo kutafuta 'Dawa ya Babu'?

Friday, February 24, 2012

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Uwepo wa Dawa Bandia Kutiba Malaria

TAARIFA KUHUSU UWEPO WA DAWA BANDIA YA KUTIBU UGONJWA WA MALARIA IITWAYO ELOQUINE
 
TAARIFA KWA UMMA
TAARIFA KUHUSU UWEPO WA DAWA BANDIA YA KUTIBU UGONJWA WA MALARIA IITWAYO ELOQUINE (Quinine Sulphate 300mg USP)

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) ni wakala wa Serikali iliyo chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii yenye jukumu la kudhibiti ubora, ufanisi na usalama wa vyakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba ili kulinda afya ya jamii.

TFDA inapenda kuutaarifu umma kuwa imebaini kuwepo kwa dawa bandia ya kutibu ugonjwa wa Malaria katika soko. Dawa hiyo inaitwa Eloquine (Quinine Sulphate 300mg U.S.P) na ipo katika makopo ya vidonge 1000 (elfu moja) kila moja. Maelezo yaliyopo katika lebo yanaonesha kuwa dawa hiyo imetengenezwa na kiwanda cha Elys Chemical Industries Ltd cha nchini Kenya.

Hata hivyo, TFDA imebaini kuwa kiwanda cha Elys Chemical Industries Ltd hakitengenezi dawa yenye jina la biashara la ‘ELOQUINE’. Kiwanda hicho kimesajili Tanzania Quinine Sulphate 300mg B.P isiyo na jina la kibiashara. Aidha, kiwanda cha Elys Chemical Industries Ltd kimebainisha tofauti mbalimbali zilizopo katika lebo ya dawa bandia ikilinganishwa na dawa halisi inayotengenezwa na kiwanda hicho iliyosajiliwa na TFDA na hivyo kuthibitisha kuwa kiwanda hicho hakitengenezi dawa hiyo.

Katika kudhibiti usambazaji wa dawa hiyo hapa nchini, hadi sasa TFDA imekamata jumla ya makopo 155 ya dawa hiyo bandia ya Eloquine jijini Dar Es Salaam yaliyokuwa yakisubiri kusambazwa. Aidha, kopo moja lenye vidonge 115 limekamatwa Moshi, Kilimanjaro. Tayari mtuhumiwa mmoja amekwishafikishwa mahakamani na upelelezi wa chanzo na wasambazaji wa dawa hii unaendelea kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi.

Uchunguzi wa dawa bandia katika maabara umebaini kuwa vidonge hivyo havina kiambato hai (active ingredient) cha Quinine Sulphate kwa ajili ya kutibu ugonjwa wa Malaria na hivyo matumizi yake ni hatari kwa afya ya binadamu.

Maelezo ya kina yanayotofautisha dawa halisi iliyosajiliwa na dawa bandia ni kama yalivyoainishwa katika jedwali hapa chini.

Dawa halisi iliyosajiliwa
Maelezo ya dawa bandia

· Jina la dawa: Quinine Sulphate 300mg B.P

· Jina la biashara: Haina jina la biashara

· Mtengenezaji: Elys Chemical Industries Ltd, Road B, Off Enterprise Road, P.O Box 40411, 00100 Nairobi, Kenya

· Rangi ya Lebo: Nyeupe na kahawia (Brown)

· Namba ya toleo: Huanzia na namba na siyo herufi. Kwa mfano: 2167E

· Muda wa matumizi (Shelf life): Miaka 4

· Jina la dawa: Quinine Sulphate 300mg U.S.P

· Jina la biashara: ELOQUINE

· Mtengenezaji: Elys Chemical Industries Ltd, Road B, Off Enterpises Road, P.O Box 4011 00100 Nairobi, Kenya

· Rangi la Lebo: Njano na Nyekundu

· Namba ya toleo: GE410

· Tarehe ya kutengenezwa: 04/2009

· Tarehe ya mwisho wa matumizi: 4/2014 (Miaka 5)

Wafanyabiashara wote wa dawa na wananchi wanatahadharishwa kutozitumia dawa hizi na wale wote waliouziwa dawa hizi wanaelekezwa kuzirudisha dawa hizo katika ofisi za TFDA, vituo vya afya vya Serikali au vituo vya polisi vilivyo jirani nao.

TFDA inapenda pia kuwakumbusha wafanyabiashara wa dawa, wasafirishaji wa vifurushi na wananchi kutoa taarifa haraka iwezekanavyo pale wanapohisi kuuziwa dawa duni, bandia au zilizoisha muda wa matumizi. Taarifa zitolewe ofisi za TFDA makao makuu zilizopo Barabara ya Mandela, EPI Mabibo External, Dar es Salaam na Ofisi za Kanda zilizopo mtaa wa Nkurumah, Mwanza, Mtaa wa Sakina – Arusha, Hosptali ya mkoa ya Dodoma na Jengo la Ofisi ya Mifugo Mkoa wa Mbeya.

Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana na:-

MKURUGENZI MKUU
MAMLAKA YA CHAKULA NA DAWA
EPI MABIBO EXTERNAL,
S.L.P 77150, DAR ES SALAAM
Simu: + 255 222 450512/450751/452108
Nukushi: + 255 222 450793
Barua pepe: info@tfda.or.tz
Tovuti: www.tfda.or.tz

Tuesday, January 03, 2012

Babu Wa Loliondo Janga La Kitaifa 2011 - Maggid Mjengwa


Mh. Lukuvi na Binti yake Mwalimu Nyerere wakipata 'kikombe' kutoka kwa Babu
Imeandikwa na Maggid Mjengwa

Babu Wa Loliondo Janga La Kitaifa 2011

 “Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote”,ni wimbo unaovutia ni wimbo; unaelezea wasifu wetu wasifu wa nchi yetu Tanzania kweli jina lako ni tamu tulalapo tunakuota wewe, Ndoto wakati mwingine uashiria kitu kijacho !

Naam ndugu zangu Watanzania, tukiwa tunakaribia kumaliza mwaka nchi yetu imekumbwa na majanga kadhaa likiwepo hili la mafuriko napenda kuchukua nafasi hii kuwapa pole wote  waliofikwa na mafuriko najua Mungu atasimama upande wao, janga hili ni  muendelezo wa majanga mengi yaliyoikuta Tanzania yetu tunayoiota utalalapo, Ambikile Mwaisapile maarufu kama babu wa loliondo ni moja ya majanga hayo .

Inayodaiwa kuwa tiba ya Babu wa Loliondo, badala ya kuwa msaada kwa taifa, imeonyesha madhara zaidi ya kiafya, kijamii na kiuchumi. Tuliandika kutahadharisha na kushauri. Tumepuuzwa; maana, kwa wengine, tiba ya Babu ilikuwa ni mradi, na kwa kweli kugeuzwa kuwa mradi wa kitaifa.

Na kilichojikita katika kuwaacha watu wetu wakitaabika ni unafiki wetu. Tuna maradhi mabaya, na ni sugu. Ndio, miongoni mwetu kuna wenye kusumbuliwa na maradhi ya unafiki. Nitatoa mfano nilipata kukaa na wasomi wawili, tena wana digrii zao. Tukazungumzia ya Babu wa Loliondo.

Mimi na wasomi wale tulikuwa na misimamo ya kufanana, tulipinga upotoshaji unaoendelea katika jamii kuwa Babu wa Loliondo, Ambilikile Mwasapile, anatibu ukimwi, kansa, kisukari na mengineyo. Na kwa vile wote tumekwenda shule, hoja kuu ilikuwa hii; kuwa hadi sasa hakuna hata wagonjwa watatu wa ukimwi waliothibitishwa kitaalamu kuwa wamepona ukimwi kwa dawa ya Babu.

Badala yake, kuna wengi wamekufa baada ya kuacha kutumia madawa waliyoelekezwa na madaktari watalaamu waliosomea tiba.

Wakati tukiendelea kuzungumza, mara akatokea mheshimiwa fulani, naye akaingia moja kwa moja kwenye mjadala. Alimtetea Babu na kusisitiza kuwa. Babu ni lulu ya taifa, lazima aenziwe. Wasomi wale afadhali wangekaa kimya, hapana, walianza kumuunga mkono mheshimiwa kwa hoja nyepesi.

Hawakuwa wapumbavu, walijifanya tu wapumbavu wakiniacha mimi nikipambana peke yangu kuziponda hoja za mheshimiwa yule. Kwa kiasi fulani, niliogopa kuona hulka hii ya wasomi wetu. Wasomi ambao, kwa unafiki, wanashindwa kutetea na kusimamia katika hoja zao za msingi. Na hii, bila shaka, ni moja ya majibu ya swali la kwa nini Tanzania ni masikini?

Hakika, ya Babu wa Loliondo ni aibu yetu kitaifa. Katika karne hii ya 21 nchi yetu inatumia raslimali zake kufanya promosheni ya ndoto ya Mtanzania mmoja kati ya Watanzania milioni 42! Ndio, tunafanya promosheni ya jambo lisilo na uthibitisho wa kisayansi. Si tuliona, haikupita siku bila kusikia  habari za Babu wa Loliondo?

Kwa sasa, tunaweza kabisa kusema, kuwa habari za huduma za Babu wa Loliondo zilitangazwa na kuufikia umma kuliko habari za Wizara yeyote ile katika  Serikali ya Awamu ya Nne. Babu wa Loliondo si mchezo bwana, alikuwa na ‘maafisa habari wake’ wanaowafunika hata maafisa habari wa Wizara za Serikali.

Na katika mzaha huu wa mambo ya msingi kitaifa, tuna maelfu kwa maelfu ya Watanzania wanaotaabika na hata baadhi kufa kwa kuamini kuwa Loliondo kuna tiba, na iko Loliondo tu! , kuna Watanzania walioweka rehani mavuno yao ya  mwaka mzima ili wapate nauli ya kwenda kwa Babu. Si wameambiwa, kuwa hata mawaziri wanapanga foleni ya kwenda kupata kikombe cha Babu!

Na wakishapata kikombe wanapiga picha ya ukumbusho, au labda ya kisiasa.  Asubuhi yake ’maafisa habari’ wa Babu wameshatundika picha ya waziri ukurasa wa kwanza gazetini! Jimboni kwa mheshimiwa wapiga kura wake watamwona au  kusikia kuwa Mheshimiwa naye anaumwa kama sisi, na amepata kikombe cha Babu!

Kikombe cha Babu ni abrakadabra, nilipata kuandika hilo. Na Watanzania, baadhi, kwa hiyari yetu, tumekubali kujifanya, wajinga na hivyo kuwapumbaza wengi wengine. Kwanini? Tulitafute jibu kwa kufikiri kwa bidii.

Hebu jiulize; wakati Shirika la Afya Duniani (WHO), Juni mwaka huu, liliadhimisha miaka 30 ya mapambano dhidi ya ukimwi, je, Tanzania, kama nchi, tulikuwa na banda la maonyesho likielezea ugunduzi wa tiba ya ukimwi  iliyotokana na ndoto ya Babu?!

Labda ndio maana, magazeti yetu ya lugha ya Kiingereza hayakufanya sana promosheni ya tiba ya Babu. Maana, kama habari za Babu zingepewa uzito kama  ilivyo kwenye magazeti yetu ya lugha ya Kiswahili, basi, wana jumuiya ya  Kimataifa, wakiwamo wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, huenda  wangeshindwa kuamini wanachokisoma.

Maana, wawakilishi wa mashirika kama PSI na FHI yenye miradi ya kupambana na ukimwi nchini na mengineyo wangejiuliza; nini hasa wanachokifanya katika  nchi yetu. Na pengine wameshatafsiriwa tunachooandika juu ya Babu kwa Kiswahili chetu!

Si ajabu basi, Ubalozi wa Marekani ulikuja na tamko lake Mei 5 mwaka huu.  Wamarekani hawa, kwa kuwaonea huruma Watanzania, wameshauri watu wanaotumia  tiba mbadala wasiache kutumia dawa walizopewa na madakatri na vile vile  waendelee kujikinga na maambukizi.

Na wakaweka msisitizo kuwa, kuacha kutumia dawa hizo za madaktari watalaamu kunafanya dawa hizo zinapotumiwa tena kushindwa kufanya kazi ipasavyo (drug resistance). Na ajabu ya habari ya tamko lile la Wamarekani ilichapishwa katika gazeti moja tu kwa lugha ya Kiingereza - The Citizen, jina la gazeti  hilo lina maana ya Mwananchi; ingawa wananchi wengi hawakupata habari hiyo kwa lugha yao!

Kwa hakika, hatuhitaji kuambiwa na Wamarekani juu ya ukweli huu na wajibu wetu. Huu ni wakati kwa wizara inayohusika kufanya jitihada za dhati kutoa tamko litakaloweka bayana kuwa tiba inayodaiwa kutolewa na Babu bado haijathibitika kitalaamu kama inaponya maradhi sugu kama vile ukimwi, kansa; na kisukari.

Wakati utafiti huo ukiendelea, umma ukumbushwe kuwa, dawa zinazotambulika kitalaamu kwa sasa ni zile zinazotolewa na madaktari wetu watalaamu. Kwamba  wanaokwenda kwa Babu wana ruhusa ya kufanya hivyo, lakini, kikombe cha Babu  kinaweza kunywewa pamoja na dawa za hospitalini.

Tufanye hivyo sasa, na ujumbe huo usambazwe kwa nguvu zote na maafisa wa  habari wa wizara husika. Ndio, maofisa habari wa Wizara ya Afya nao  washindane na ‘maafisa habari’ wa kujitolea wa Babu wa Loliondo!

Watanzania tunapita kwenye kipindi kigumu sana. Na huu ni wakati wa  kutafakari kwa kina. Na nimepata kumwuliza jamaa yangu swali hili; mwanadamu ; unafanyaje unapoamka na kukuta dunia unayoishi ardhi yake imeanza kumegeka na kuchotwa na bahari? Naye akanijibu; ” Huo ndio utakuwa mwisho wa dunia!”

 Aliyenijibu alikuwa amechoka kufikiri. Nilidhani angetamka kuwa, angeanza kujifunza kuogelea. Maana, kwa kuogelea majini angeweza kukutana na kisiwa, au nchi kavu.

Wanadamu tumejaliwa akili ili tuweze kufikiri. Na kufikiri ndio njia  mojawapo ya kuiteka kweli. Kufikiri kunahamisha milima na hata kuiweka kando  kuruhusu mwanga upite. Inakuwaje basi mwanadamu anapoacha kufikiri?

Haya ya kwa ‘Babu wa Loliondo’ ni kielelezo cha Watanzania kuamua kuacha kufikiri. Kuna umma uliojifunika vilemba vya ujinga. Umma uko gizani, ; unahitaji mwanga.

Yumkini wakatokea Watanzania wenzetu wakaoteshwa na Mungu juu ya  dawa za tiba kwa mwanadamu. Na hapo wakaingiza suala la imani. Lakini, jambo hilo halituzuii wanadamu kuhoji na kudadisi. Ndio, kuuliza maswali. Na kwa Serikali, jambo hilo haliizuii kufuata taratibu zake za kawaida ikiwamo kufanyia utafiti jambo hilo na kutoa msimamo wa kiserikali.

Hata kama Watanzania watakuwa na uhuru wa kwenda kwenye tiba za imani, lakini msimamo wa Serikali uwepo. Na kwa wengi utabaki kuwa ndio mwongozo;  maana, watakuwa wameufanyia utafiti. Nahitimisha.

Niwatakieni Heri ya Mwaka Mpya.

Maggid Mjengwa.

http://mjengwablog.com/

*************************

 SOMA HABARI ZAIDI ZA VIFO LOLIONDO GLOBAL PUBLISHERS:

http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/loliondo-1

Tuesday, June 14, 2011

Madaktari wa Kenya Hawampendi Babu wa Loliondo!

Madaktari Kenya wanalamika kuwa idadi ya wagonjwa wanaokuja kuwaona katika kliniki/hospitali imepungua. Wanasema kuwa wagonjwa wengi wamekwenda Loliondo, Tanzania kwa Babu na kudhani kuwa wamepona baada ya kupata 'kikombe'.

Madaktari hao wanawaonya kuwa wasiache kutumia dawa zao maana dawa ya babu si tiba ya kudumu bali ya kifikra.

Huko Kenya, waKenya wengi wameamua kwenda kwa babu baada ya kuona maajabu. Watu ambao walikuwa wagonjwa mahututi na hata vipofu wamepona maradhi yao baada ya kwenda Loliondo kwa Babu.

************************************************************************

Doctors alarmed as patients seek Loliondo 'wonder drug'
Medical practitioners in Trans Mara District have raised alarm over a worrying trend of patients withdrawing from treatment after travelling to Loliondo, Tanzania for the "wonder drug cure".

Led by the area District Medical Officer of Health, Aggrey Ouko, the medical professionals said patients undergoing treatment for HIV, tuberculosis, diabetes, hypertension, among other life threatening ailments, were stopping treatment after visiting the ‘healer’.

He said records at various health facilities have shown a sharp decline in the number of patients attending the facilities after visiting Loliondo.

The officer reported that some HIV patients had abandoned taking anti-retroviral drugs under the belief they had been cured.

Lives at stake

Addressing an HIV advocacy forum in Kilgoris, which brought together local leaders and the Provincial Administration, Ouko said several lives of patients were at stake if no immediate action was taken to address the issue. He said some of the patients who had withdrawn from hospital treatment have developed Multi-Drugs Resistance (MDR), a condition that makes it possible for a disease-causing organism to resist distinct drugs.

Separately, doctors in Nakuru say that 30 years since the first HIV/Aids case was reported, self-stigmatisation remains a major barrier in provision of medical services to those living with the disease.

Lawrence Otemba, an advisor with the International Planned Parenthood Federation, says most of those infected still avoid seeking medical services for fear of discrimination. Dr Otemba said it’s important to increase care and support for those infected and also intensify the fight against stigmatisation of those living with the virus.

"People fear that if they come out and seek medical services they will be discriminated and as a result a lot of people do not even know their status," he added. He was speaking in Nakuru during a visit by a Japanese delegation to a project run by Family Health Options Kenya (FHOK).

Infected and Affected

The delegation was on a tour to evaluate the activities carried out by FHOK aimed at improving quality of lives of people infected and affected with HIV/Aids in Nakuru.

FHOK project Coordinator Jane Adero said that the formation of support groups in the town has assisted those infected to cope and live longer.
*****************************************************************

USHUHUDA ******* WAKENYA WAPONA MAGONJWA YAO BAADA YA KUPATA 'KIKOMBE'

Trans Nzoia Residents Healed in Loliondo

Business came to a standstill in Kitale town following the return of a busload of Trans Nzoia residents, who had travelled to Loliondo to seek intervention from the famous traditional doctor Mzee Ambilikile Mwasapile. Curious residents jammed the main bus terminus to talk to the passengers about the doctor.

Most passengers looked tired from the long journey that had taken several days. Peter Kiarie, who said he has been diabetic for the last 20 years, could not hide his joy as he narrated to the Star how he is cured and is now back to his normal diet. "Immediately I took the magic drug from Mzee Mwasapile and followed his instructions strictly, I felt a strange feeling in my body, and then a sigh of relief for my 20 years of fighting with diabetes," he said.

He said the condition had almost broken his marriage and used up all his money buying expensive drugs to control his condition. Kiarie said after years of visiting several hospitals in vain in search of treatment, he is happy that God used Mzee Mwasapile to heal him. "The man is God sent and I believe very many will be healed through the process," he said.

He believes only those with a strong faith will be healed saying that not all who travelled to Loliondo village were cured. Kiarie said the drug was not allowed out of the "holy shrine" saying Mzee Mwasapile insisted that the concoction became poisonous once it left the place.

He believes that Mzee Mwasapile's shrine is a holy place that despite thousands of people jamming the small dusty village there were no scenes of immorality, theft or robbery. Kiarie also had boils on his legs and head but they disappeared after he drank the concoction.

An elderly woman who was on the trip said she had lost her sight seven years ago but could now see after drinking the concoction. "Before I went to Loliondo I could not read my Bible and was depending on my grandchildren. But I can now read my Bible. God is great," she said.

Bus conductor Stanely Mwangi said most of those who boarded two weeks ago could not walk and were literally carried into the vehicle, but he is surprised to see them walking without help and showing faces of good health. "I am equally surprised with the turn of events of the wonder drug, because when we left this place to Loliondo, I thought most of these people were going die on the way, but here they are," he said .

The patients interviewed also told the star that people close Mzee Mwasapile had hinted that the magical powers were to last till June of this year and thats why people were jamming the dusty village.

The bus company is making booming business as it makes a trip to Loliondo every Thursday. Each passenger pays Sh6,000 .The bus carries 41 passengers while the bus booking office in town has a conspicous sign post written " Loliondo hospital bus Direct". According to the director of the bus company James Wanyoike the demand for the services is growing fast and they are contemplating increasing the number of buses.

http://allafrica.com/stories/201105190143.html

Thursday, May 26, 2011

Habari Njema Kuhusu Matumizi ya Dawa ya UKIMWI

Wadau, leo kuna habari kuwa mtu mwenye virusi vya HIV akianza kutumia dawa mapema, hawezi kumwambukiza mtu mwingine virusi! Inaelekea serikali ya Marekani watafanya kampeni ya kusambaza dawa kwa waathrika hivi karibuni katika nchi zilizoathrika vibaya na UKIMWI.
************************************************************************

U.S. Mulls Implications Of Early Use Of HIV Drugs To Stop AIDS Spreadby Richard Knox

May 26, 2011

The Obama administration is beginning to think through the ramifications of what may be the most far-reaching AIDS study ever done.

Earlier this month federal officials announced the results of a big clinical test that showed if HIV-infected individuals get antiviral drugs early — while they still feel fine and their immune systems are intact — their chances of passing the virus on to someone else go down to almost zero.

The implication: If all the HIV-infected people in the world got the drugs, the 30-year-old pandemic could be brought to an end. Nobody expects that to happen overnight, maybe not ever. But the administration's chief AIDS strategist is leading a what-if discussion within the government.

Mnaweza kusoma habari kamili kwa KUBOFYA HAPA:

Friday, May 06, 2011

Wataalam Wasema Dawa ya Babu Inafanya Kazi Kiasi

Scientists at work on 'Babu' cure

Kutoka: The Guardian Tanzania



A technical report on retired pastor Ambilikile Masapila’s “miracle cure” has indicated that scientific data supports his claims to its positive effects on a number of ailments.

A report by experts from the National Institute for Medical Research (NIMR) Department of Traditional Medicine Research and Institute of Traditional Medicine, Muhimbili University of Health and Allied Sciences seen by The Guardian, says study findings have revealed that ‘Babu’s miracle cure’ prepared by boiling the roots of Carissa edulis plant is safe and has positive effects on cancer, epilepsy, herpes simplex virus, liver ailments, diabetes, blood pressure and anti-viral activity.

However, the scientists said since the remedy is being widely used by an exceedingly large number of patients, the government should advance the work of focused pre-clinical studies to establish pre-clinical efficacy and safety of the remedy.

“The dose provided by Pastor Masapila which is one cup (about 200 mls) prepared through boiling an estimated 3.0 kg of whole root material in 60 litres of water “falls within safety window and no any overdose or acute poisoning event is expected.”

The results suggested that the plant has anticonvulsant activity which supports the claim of the use of the plant in the management of epilepsy as claimed by Pastor Ambilikile Masapila.

It further indicated that the herb has antidiabetic activity which supports the claim of the use of the plant in the management of diabetes.

The herbal has blood pressure lowering activity which supports the ethnomedicinal claim of the use of the plant in the management of high blood pressure.

Research results show that the pastor’s concoction has hepatoprotective and antioxidant activity which are beneficial in the prevention of liver disorders and cancer.

“This result also reveals that Carissa edulis has potent anti-viral activity against herpes simplex viruses. Taking into consideration that, herpes simplex virus (HSV) infection is a major opportunistic infection in immunosuppressed persons, these findings supports the ethnomedicinal claim of the use of the plant in the management of HIV/Aids as claimed by Pastor Masapila,” said the report.

Drawing general conclusion, scientists said that the plant is safe and the dosage prescribed by Rev. Mwasapila is below the toxic level.

They, however, recommended that since the remedy is being widely used by an exceedingly large number of patients, focused pre-clinical studies need to be conducted to establish pre-clinical efficacy and safety of the remedy.

Scientists also recommended standardisation and formulation of “Babu’s cupful” for human use.

“MoHSW should conduct clinical trial on the prescribed remedy to establish in vivo efficacy and safety in humans and answer questions on optimum dosage, dosing schedule and duration of treatment per ailment,” stated part of the report.

It added “MoHSW should conduct clinical follow up on all patients recorded to have used the remedy for their prognosis.”

Recently, many people have been flocking Samunge village in Loliondo, Arusha, seeking the cure for chronic diseases such as diabetes, asthma, epilepsy, cancer and HIV/Aids.

According to Rev. Masapila, God instructed him through dreams since 1991 about the medication and that, it will heal people with chronic illnesses namely: diabetes, asthma, epilepsy, cancer and HIV/AIDS. The dream kept recurring to him several times since then and on August 26, 2010 he decided to obey on the instructions and started the healing work.

Earlier this month, HIV/Aids stakeholders blamed the government over its silence on HIV/Aids patients who abandon antiretroviral drugs after taking the herbal concoction being dispensed by Pastor Masapila in Loliondo.

HIV/Aids stakeholders said there was need to give correct messages to the people to avoid negative impacts in future.

SOURCE: THE GUARDIAN

Thursday, May 05, 2011

Wagonjwa wa UKIMWI Wafa Baada ya Kunywa 'Kikombe'



Habari za kusikitisha kutoka mkoa wa Manyara zinasema kuwa wagonjwa wa UKIMWI watano kutoka kijiji cha Sunya wilaya ya Kiteto, mkoa wa Manyara wamefariki dunia baada ya kunywa kikombe cha Babu wa Loliondo. Habari zinasema kuwa wagonjwa hao walienda Loliondo, walikunywa 'kikombe' na walisema kuwa wanajisikia. Wagonjwa hao watano waliacha kabisa kunywa dawa zao za ARV walizoandikiwa na madakatari. Mungu alaze roho zao mahala pema mbinguni. Amen.

*****************************************************************

Kutoka The Citizen:

5 Kiteto villagers die of Aids after abandoning ARVs

Monday, 02 May 2011 22:17

By Joseph Lyimo

Kibaya. Five residents of Sunya village in Kiteto District, Manyara Region who had tested HIV positive are reported to have died after abandoning anti retroviral drugs (ARVs) in favour of a herbal concoction from a 'miracle healer' in Loliondo.

Their deaths occurred shortly after arriving back from Samunge village where the retired pastor Ambilikile Mwasapila has been dispensing liquid drink from a local herb he claims cures a range of chronic diseases, including Aids. A councillor for Sunya Ward, Mr Mussa Brighton, confirmed the deaths of the villagers, saying they had just returned back home from Loliondo where they went to seek treatment from Rev. Mwasapila.

Mr Brighton, who is the vice chairman of the Kiteto District Council, said the five had reportedly abandoned using the life-prolonging ARVs as recommended by medical doctors as one of the arsenals against killer Aids.Unconfirmed reports said the deceased had been telling people after returning from Loliondo that they had stopped using ARVs because they were feeling better after taking a cupful herbal drink from "Babu.”

The councillor warned that the trend was not good because, people who had tested positive should not abandon the ARVs dose from medical facilities. He could not disclose the names of the deceased.He argued that the sudden rush to Loliondo for herbal cure offered by the spiritual healer should not make people discard the recommended medicines.

Wednesday, April 13, 2011

Ushuhuda wa Kupona Kansa Baada ya Kunywa Dawa ya Babu

Wadau, Hebu mtembelee Da Subi kusoma shuhuda za watu waliopona saratani (Kansa) baada ya kunywa dawa ya babu wa Loliondo. http://www.wavuti.com/4/post/2011/04/ushuhuda-kupona-saratani-dawa-masapile.html#axzz1JK62Bn7R

Thursday, March 31, 2011

Breaking News - Babu wa Loliondo Atatibu Wagonjwa Dar!

Wadau, Nimepigiwa simu na rafiki yangu Tanzania kuwa Babu wa Loliondo amekubali kufika Dar na kutibu wagonjwa. Huduma itakuwa kwenye viwanja wa Jangwani. Tarehe bado haijatangazwa lakini utaratibu wa kugawa vikombe itakuwepo. (Natumaini siyo utani wa April Fools)

Sunday, March 27, 2011

Maoni ya Mdau Kuhusu Mjengwa Blog na Dawa za Babu

ndugu mjengwa...

habari za kazi.

kwanza nakupongeza kwa kutumia muda wako mwingi kuelimisha umma wa watanzania ambao kwa bahati mbaya wengi wamo katika giza nene.

nimeshawishika kukuandikia mail hii baada ya kusoma makala zako kadhaa kuhusu dawa ya babu wa loliondo. niliona matusi, kubezwa na kudharauliwa unakokupata kufuatia kuwaambia watanzania ukweli, jamii ambayo kwa miaka kadhaa imezoea kuambiwa uongo, blah blah na kupumbazwa.

kimsingi nakubaliana nawe kuwa dawa ya babu ni abra kadabra. ni pumbazo ambalo limeingia katika jamii yetu kwa wakati huu na kwa bahati mbaya wasomi, wanasiasa na watu mashuhuri wamekuwa ni baadhi ya watu wanaofurika huko loliondo kupata kitu kinachoitwa kikombe.

hivi karibuni televisheni ya kenya ya ntv imetoa documentary kwa lugha ya kiswahili na lugha ya kiingereza kuelezea kile kinachoitwa maajabu ya loliondo. watu wamehojiwa wakiwemo wagonjwa, madaktari na baadhi ya wananchi wa kawaida hasa wa arusha. kuna maoni mchanganyiko kuhusu suala hili lakini ni wazi kuwa watu wamepumbazwa na maelezo kuwa mtaalamu wa dawa hiyo ni mchungaji mstaafu. kwa kuwa ni mchungaji mstaafu basi bila shaka dawa yake ni ya kweli!!!!

suala hili linaendeshwa kidini zaidi badala ya kijamii. wengi wa watu wanaodai kuponywa hisia zao wameziegemeza zaidi katika cheo au hadhi ya uchungaji wa babu. hii ni psychological treatment ambayo kwa vyovyote itaonekana kwa siku kadhaa kama sio miezi lakini baadae itaondoka na ndipo watu watakapojiona kuwa ni wapumbavu na hawakupata nafuu yoyote kutokana na kikombe cha babu.

ingekuwa mtaalamu huyu wa loliondo hakuwa mchungaji mstaafu hwenda hali ingekuwa tofauti kwa wanasiasa wetu na viongozi wa kijamii lkn hili la uchungaji ndilo linalowapumbaza watu na kujiona kuwa kumpinga babu na dawa yake ni sawa na kupinga imani jambo ambalo kwa mtazamo wangu si sahihi na ni kujipotosha wenyewe. dawa ya babu na imani ya dini hapa ni vitu viwili tofauti ambavyo vimewekwa pamoja.

kuna wengi duniani wanaotumia kivuli cha dini kwa maslahi yao na watu kupumbazika kwa kuona kuwa kinachosemwa na mtu husika hakipaswi kupingwa maana ukipinga utakuwa umepinga dini na dini inaogopwa. mtu huogopa kuwa akipinga ataonekana ameasi au atalaaniwa na dini au mungu.

maslahi ya dawa hiyo tunaambiwa yanagaiwa kwa kanisa husika, wasaidizi wake na kiasi kidogo huchukuwa yeye babu. katika hali kama hiyo iwapo kanisa linapata share fulani jee unategemea kuna kiongozi wa kanisa lake atakaemkataza? hilo haliwezekani maana kanisa litakosa mapato ambayo halikutegemea kuwa yangetokea.

mnakumbuka kufukuzwa kwa father NKWERA na waumini wake na kutengwa na kanisa lake? sababu kuu ilikuwa ni kufanya maombi na kuponyesha wagonjwa jambo ambalo lilisemwa kuwa si katika mafundisho ya kanisa. inawezekana kanisa la babu na la father NKWERA ni tofauti lakini hoja ipo pale pale. father NKWERA hakuwa ananufaisha kanisa kwa wakati ule lakini babu analiingizia kanisa fedha za kutosha hivyo watu wanafumba macho.

kwa bahati mbaya wanasiasa nao wamekumbwa na uozo huu. wakati waziri wa afya alitoa tamko awali kabisa la kupiga marufuku dawa hiyo hadi uchunguzi ufanyike, waliibuka wanasiasa uchwara ambao kwa kutaka sifa waliona tamko lile la waziri halina maana. kina SHIRIMA NA LUKUVI wakalivalia njuga jambo hilo na kudai kuwa serikali ipo pamoja na babu. waziri wa afya kwa kuepusha shari ya udini aliamua kukaa pembeni na kujinyamazia kimya.

hawa kina SHIRIMA na LUKUVI wanadai kuwa ni suala la kiimani hivyo serikali isiingilie imani za watu. wamesahau siku chache tu kabla ya uchaguzi mkuu mwaka jana mtu mmoja aliyejipa cheo cha mtabiri maafuru afrika mashariki na kati alitangaza kuwa mgombea mmoja wa uchaguzi angefariki dunia kabla ya uchaguzi mkuu na kupelekea uchaguzi kuahirishwa.

serikali hiyo hiyo wanayoisema kina LUKUVI na SHIRIMA ilitoa tamko kali la kupinga kauli hiyo na kumtaka mtabiri huyo anyamaze kimya au atachukuliwa hatua. serikali haikusema kuwa mambo yake ya utabiri ni maswala ya kiimani anayetaka aamini na asietaka aachane nae. lakini sasa tunaambiwa kuwa masuala ya imani serikali haiwezi kuingilia. hatua ile ya serikali kwa mtabiri yule ilikuwa sahihi kabisa lakini kwa sasa tunaona serikali ikiwa na kigugumizi kuhusu babu huyu.

hivi sasa kina babu wanaongezeka, wengine wakitokea mbeya. si hasha baada ya siku chache tukasikia mwengine ameibuka dar es salaam au mtwara au mwanza au hata pemba akidai nae ameoteshwa kuwa awahudumie watanzania kwa dawa ambayo formula yake haijulikani.

kwa ufupi dawa ya babu ni kanyaboya kwa hoja zifuatazo:

1. maradhi anayosema inatibu ni maradhi yanayosababishwa na vitu tofauti. baadhi husababishwa na virusi, mengine bakteria na mengine ni matatizo ya kutokuwa na uwezo wa homoni fulani mwilini. kwa vyovyote vile dawa ya matatizo haya haiwezi kuwa ni moja kwa sababu hata chanzo chake si kimoja. kwa mfano huwezi kupeleka gari gereji kwa matatizo tofauti kisha ufumbuzi wake kuwa ni huo huo mmoja. tatizo la gear box, chasis au tyre haviwezi kuondoshwa kwa aina moja ya ufumbuzi.

2. kauli za babu anapohojiwa na vyombo mbali mbali vya habari zinatofautiana. kuna sehemu anasema kuwa dawa yake inatibu maradhi matano kama alivyoambiwa na mungu. kuna sehemu anasema kinachotibu sio huo mti bali ni maombi yake na kuna sehemu anadai kuwa kinachotibu ni kikombe hivyo dawa husika isipotekwa kwa kikombe chake (kikitumika cha mtu mwengine) haitamsaidia mgonjwa. hizi ni kauli zenye mgongano. kwa mtu mwenye kutumia akili, hapa babu anajaribu kutumia ujanja wa kuzuia watu wengine wasiweze nao kujitengenezea dawa hiyo na kugawa kwa watu. anajaribu kutengeneza dominancy au monopoly katika jamii. kutakapokuwa na babu wawili au watatu bila shaka idadi ya wagonjwa wanaokuja kwake itapungua na hatimae maslahi kupungua pia.

3. kuna wakati babu hueleza kuwa dawa husika haiwezi kufanya kazi kwa mtu aliyefanya ujanja kwenye foleni kwa kuwapiku wenzake aliowakuta. hii ni njia nyengine ya ajabu kwa kuwa hakuna uhusiano wowote wa kitiba na suala la mtu kupanga foleni au kutokaa foleni.

4. kuhusu malipo ndo ujanja wa wazi kabisa. babu anadai ameambiwa na mungu kuwa atoze shs 500 tu kwa watz na dola 1 kwa wageni. hata hivyo hakusema iwapo kutakuwa na mabadiliko ya kupanda au kushuka thamani ya pesa itakuwaje? jee shs 500 au dola 1 itabakia hivyo milele? na jee binaadamu wanaotoka nchi ambazo hazitumii dola wala shs? au mungu hatambui fedha za nchi nyengine katika dunia yake zaidi ya dola na shilingi?

5. dawa husika anadai ni lazima itolewe loliondo tu. hii pia ni ujanja wa kuhakikisha kuwa hakuna babu wengine wanaoweza kufanya kazi hiyo katika mikoa mengine. ukitaka usitake ni lazima uende loliondo tu. ni kucheza na akili za watu na kwa bahati mbaya watu wamepumbazika.

6. kuhusu kulipia hapa napo pana jambo. kazi ya mungu huwa ya kujitolea lakini hakuna pahala babu anaweka utaratibu kwa watu wasio na uwezo wa hiyo shs500. jee anataka kutwambia kuwa mungu hajali watu mafukara ambao hata hiyo shs500 kwao ni kiwango kikubwa? vitabu vyote vya dini vinataja haja ya kuwahurumia mafukara na wasio na uwezo. lkn kwa hili babu yupo kimya sana. labda baada ya mfuko kujaa ndipo atakapotoa ofa kwa wasio na uwezo.

7. mwisho dawa ya babu haina dozi. hiki ni kituko chengine. kwa aliye mahututi aliye na nafuu nk wote ni kikombe kimoja tu. hili ni la kuchekesha kama sio kusikitisha. hata hao waganga wengine wa kienyeji hutoa dawa kwa mujibu wa hali ya mgonjwa. lakini pia kabla ya mgonjwa kupewa dawa huchunguzwa kama ana aleji au tatizo lolote kama vidonda vya tumbo nk. lkn hilo halipo kwa babu. kikombe hicho hakijali uzito wa ugonjwa wala afya yake. hakijali presha ya mgonjwa wala lishe yake. iwe ameshakula au ananjaa kikombe ni kimoja tu. hii ni hatari kwa jamii. hata katika mambo ya kawaida ya binaadamu hali haipo hivyo. gari la tani 3 litabeba mzigo wa tani 3 na la tani 10 litabeba mzigo wa tani 10. huwezi kusemwa magari yote yabebe tani 10 wakati yana uwezo tofauti.

sikutaka kutumia hoja za kisayansi kuwa dawa hii haijathibitishwa kwa kuwa watu wengi wanajidanganya kuwa dini ni zaidi ya sayansi. kwa maoni yangu dini na sayansi havipingani hata siku moja. ukiona hivyo kuna tatizo pahala.

mbali na hali niliyotaja hapo juu, kuna madaktari na wataalamu wa afya huko arusha ambao walishuhudia wagonjwa wakitolewa hospitali na kupelekwa kwa babu wamethibitisha kuwa baadhi yao pamoja na kupata kikombe hicho na kujidanganya kwa siku chache kuwa wamepona wamejikuta wapo hoi na kurudi tena hospitali. huu ndio ukweli ambao utajulikana siku si nyingi kwa kuwa maji hayo yaliyochemshwa hayana dawa yoyote na hayasaidii kuondoa ugonjwa.

kwa bahati mbaya pamoja na ukweli huu baadhi ya watu hudai kuwa wagonjwa hao waliojiona kuwa hawajapona eti walikwepa foleni au kutofuata utaratibu wa babu!!! huu sasa ni ujinga mwengine. wengine wanadai kuwa madaktari hao wanamuonea wivu babu eti kwa sababu kawanyanganya wateja wao!!! wakati watu wanawatahadharisha wao kuepuka kanyaboya wao bado wamo katika usingizi mzito wa kulewa kikombe cha babu...

kwa ufupi wafuasi wa babu wanataka kusema kuwa ni lazima watu wote waliopata kikombe hicho kumsifu babu na anayekwenda kinyume kwa kudai kuwa hajapona huonekana ndio mkorofi. kuna haja ya watanzania kutafakari na kuchukua hatua. tukumbuke kauli ya mhe rais KIKWETE kuwa AKILI YA KUAMBIWA CHANGANYA NA YA KWAKO....

Wakatabahuuu,

mdau
ughaibuni...

Saturday, March 26, 2011

Tiba ya Loliondo - Msimamo wa Mjengwa Blog

(Pichani) Baadhi ya waliofanikiwa kupata kikombe cha 'Dawa ya Babu' huko Sumange Village Loliondo

Nimesikia habari za watu kupona magonjwa yao baada ya kunywa dawa, pia nimesikia habari za watu amabo walizidiwa baada ya kunywa hiyo dawa na kuacha kutumia madawa waliopewa mahospitalini. Pia nimesikia habari za watu kufariki wakiwa wanasubiri kupata dawa ya ya babu.
Ningependa kusikia kutoka kwa watu waliokunywa daw ya babu kabla ya kuaamua kama inafanya kazi au la. Mungu yu Mwema na kweli kama ametupa dawa ya kuponyesha magonjwa yasiyo na dawa basi ingekuwa vizuri dunia nzima wajue habari hiyo.

******************************************************************************
Hii ni tamko rasmi kutoka Mjengwa Blog:

Ndugu Zangu,

Hii ni nchi yetu. Tunayaandika haya kwa mapenzi ya nchi yetu. Yanayotokea Loliondo yanaanza kubeba sura ya kashfa. Taratibu, Loliondo inaonekana kuwa ni aibu ya kitaifa kwenye masuala ya kimsingi ya afya ya watu wake.

Si kawaida, na yawezekana ni mara ya kwanza kutokea, kwa blogu ya jamii kutoa msimamo juu ya jambo la kitaifa. Tunauona umuhimu huo, tunafanya hivyo. Ndio, Hali ni mbaya Loliondo. Kuna Watanzania wenzetu wanakufa kila siku. Wanakufa wakiwa kwenye foleni ya kupata kikombe cha Babu au baada ya kunywa kikombe hicho na kuacha kutumia dawa zao walizokuwa wakitumia kabla.

Asubuhi hii nimepokea simu kutoka Dodoma. Kuna mganga aliyenielezea hali mbaya zinazowapata wagonjwa wake wa kisukari mara baada ya kupata tiba ya Babu na kuacha kutumia dawa zao. Anasema ni mbaya zaidi kwa wagonjwa wa kisukari, maana, kisukari kinapanda haraka. Anasema kuna wagonjwa waliokufa baada ya kuacha kutumia dawa zao.

Baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa mstari wa mbele katika kupigia debe tiba ya Babu bila kufanya uchunguzi yakinifu. Ndio, duniani kuna fikra dhanifu na fikra yakinifu. Ya ‘ Babu’ wa Loliondo ni dhania iliyopaswa kuhojiwa kabla ya kupigiwa debe.

Hivi, wanahabari wetu wanashindwaje mpaka hii leo, kuwahoji madaktari bingwa kwenye maradhi kama UKIMWI, kisukari, na mengineyo. Madaktari hawa wako Agha Khan, wako Bugando, Mount Meru na kwengineko. Hivi, Watanzania wenzetu hawa, katika kazi zao, mpaka hii leo hawana cha kusema, cha kitaalam juu ya Tiba ya Babu? Au media imechagua kuficha ukweli?

Tunajua, kuwa habari za ‘ Babu wa Loliondo’ zinauza magazeti kwa sasa. Lakini, ni dhambi na kutoitendea haki nchi yetu kama tutaamua kufanya biashara na afya za watu wetu. Ni laana kubwa.

Ona sasa, Watanzania kwa maelfu wanakwenda gizani bila kuhoji, au kusaidiwa kuhoji. Katika dunia ya sasa ya Sayansi na Teknolojia hatuwezi kwenda mbele kwa kuendekeza ‘ Abrakadabra’ kama hizi za Loliondo.

Huu ni wakati, kwa Wizara na waziri mwenye dhamana, kutoa tamko rasmi juu ya ukweli kuhusu tiba hiyo ya Babu. Na kama ‘ Babu’ ataruhusiwa aendelee na tiba yake kwa wenye imani, basi, Babu huyu asaidiwe kuhamishia shughuli zake Arusha mjini. Lifanyike hilo ili tunusuru maisha ya Watanzania wenzetu walio katika hatari ya kupata maradhi mapya katika mazingira ya sasa ya Loliondo.

Tunayasema haya kwa mapenzi ya nchi yetu, basi.

Maggid,
Iringa,
Ijumaa, Machi, 25,2011
http://mjengwa.blogspot.com

Thursday, March 24, 2011

Mh. Lukuvi na Rosemary Nyerere Nao Wapata Kikombe cha Babu

Wadau, naona vigogo wanakimbilia Loliondo kupata 'kikombe cha dawa'. Je, walipanga foleni na wengine au walipata 'bump'? Pia, eti kuna uvumi (au huenda ni kweli) kuwa Mzee Mandela wa Afrika Kusini naye alienda huko kisirisiri kupata kikombe. Kama hiyo dawa kweli inafanya kazi basi huyo babu apatiwe ulinzi mkali hata wa FFU 24/7. Maana wazungu wakipata fununu watamwua. Kisa makampuni ya madawa (Pharmacueticals) watafilisika kwa kukosa wateja.

Dawa ya babu OYEEEEE!


Waziri wa Nchi Ofisi ya Wazri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), William Lukuvi (wa pili kulia) na Rosemary Nyerere (kulia) wakipata 'kikombe cha babu' kutoka kwa mchungaji mstaafu wa KKKT , Ambilikile Mwasapila (kushoto) waliopkwenda Loliondo. (Picha kwa Hisani ya Michuzi Blog)

Friday, March 18, 2011

Lowassa Naye Apata Dawa ya Babu Loliondo

Bila shaka mmesikia habari za dawa ya Loliondo. Kuna mchungaji mstaafu ambaye amegundua dawa ya mitishamba inayotibu magonjwa karibu yote. Watu wanahaha kwenda Loliondo, wengine wamekodi hata helikopta! Na serikali ya Tanzania imebariki dawa ya babu! Sasa wagonjwa wanatoroka Muhimbili kwenda kufuata dawa Loliondo!

*****************************************************************************


Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwasapile aka. BABU akipima dozi

Msongamano wa wangonjwa na wananchi wakienda kupata dosi. Dozi ilikuwa shs 500/- tu. Sijui kwa sasa ni bei gani.

Picha na Habari kutoka Michuzi blog:

Lowassa apata kikombe Loliondo, huduma zaimarishwa, bei ya mabasi Ubungo zapanda
Source: Gazeti la Mwananchi

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa juzi alipata tiba ya magonjwa sugu inayotolewa na Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwasapile katika Kijiji cha Samunge, Tarafa ya Sale, Loliondo, mkoani Arusha.

Lowassa alifika katika eneo hilo mchana akiwa na viongozi kadhaa wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro na Serikali kisha kupata kikombe kimoja chenye dawa kinachotolewa na mchungaji huyo kwa ajili ya tiba.

Tofauti na viongozi wengine, Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli (CCM), Jimbo linalopakana na Kijiji cha Samunge, alikwenda huko akiwa na viongozi mbalimbali wakiwamo viongozi wa dini na baadhi ya wapigakura wake.

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Lowassa alithibitisha kwenda Loliondo na kuwataja viongozi wa dini alioambatana nao katika msafara wake kuwa ni Askofu Msaidizi wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini, Dk Frederick Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Dayosisi ya Kaskazini Kati (Arusha), Mchungaji John Nangole.
Katika ramani ya utendaji kazi ya KKKT, Jimbo la Masai Kaskazini ndipo kilipo Kijiji cha Samunge ambako ni makazi ya Mchungaji Mwasapile.

“Ni kweli, nimekwenda pale na wapigakura wangu pamoja na viongozi wa dini, Msaidizi wa Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini, Dk Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Mchungaji Nangole,” alisema Lowassa na kuuliza: “Kwani hiyo nayo ni habari jamani?”

Baada ya Lowassa kufika katika kijiji hicho akiwa na ujumbe wake, aliongoza moja kwa moja hadi kwa Mchungaji Mwasapile na kuzungumza naye kisha akapata kikombe cha tiba na kuondoka.

Kabla ya Lowassa kwenda kupata tiba, amekuwa akitoa msaada wa nauli kwa wagonjwa mbalimbali wa jimbo lake kwenda kwa mchungaji huyo ambaye dawa yake inadaiwa kutibu magonjwa ya saratani, kisukari, pumu, shinikizo la damu na Ukimwi.

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

Thursday, August 26, 2010

Tani 9 za Madawa Bandia Yakamatwa Afrika Mashariki


Kila siku tunasikia habari ya madawa bandia Bongo. Tunasikia watu wameugua zaidi na hata kufa shauri ya kununua au kupewa madawa bandia. Mwisho wake utakuwa lini? Serikali ifanye nini kukomesha hayo madawa bandia yasiingizwe nchini?

****************************************************

Kutoka CNN.Com

9 tons of fake medicine seized in East Africa

August 26, 2010 10:54 a.m. EDT

(CNN) -- Authorities have seized 9,072 kilograms (20,000 pounds) of counterfeit medicine and arrested 80 people suspected of illegal trafficking in six East African nations, Interpol said Thursday.

More than 300 premises were checked or raided in the two-month operation across Uganda, Burundi, Kenya, Rwanda, Tanzania and Zanzibar, according to a news release from the international police agency.

The confiscated loot included anti-malaria drugs, vaccines and antibiotics. There was also a significant quantity of government medicines diverted to illegal resale markets.

It was the third such seizure operation in as many years in East Africa, intended to curb the manufacture and distribution of counterfeit medical products.

Representatives of the six nations are scheduled to meet in Zanzibar next week to discuss the seizure and the extent of the counterfeiting problem, Interpol said.

The World Health Organization defines counterfeit drugs as "medicine, which is deliberately and fraudulently mislabelled with respect to identity and/or source."

Counterfeiting can apply to both brand-name and generic products, and forged products may include those with the correct ingredients or with the wrong ingredients, without active ingredients, with insufficient active ingredients, or with fake packaging, WHO says.

The United Nations agency created a global task force in 2006 to deal with the problem, which has been growing as international markets expand and become globalized and internet commerce has taken off.

The fake products can prove detrimental to public health efforts in disease-ridden countries and in worst-case scenarios can cause death, according to the WHO task force.