Showing posts with label Chadema. Show all posts
Showing posts with label Chadema. Show all posts

Friday, September 08, 2017

Opposition Leader Tundu Lissu Airlifted for Treatment in Kenya

DODOMA, Tanzania (AP) - An official says a Tanzanian opposition figure who was seriously wounded in a shooting has been transferred to a hospital in neighboring Kenya. Lawmaker Joseph Selasin of the opposition Chadema party says Tundu Lissu was airlifted to Nairobi early Friday. Health officials in Tanzania's capital, Dodoma, say Lissu was shot in the stomach, leg and arm on Thursday. Police are looking for multiple gunmen. The attack has been condemned by both the opposition and the government. Lissu, who heads the lawyers' association in Tanzania, is one of the most vocal critics of President John Magufuli. He recently was charged with using abusive language after he called Magufuli a dictator over alleged attacks on the opposition and the media.

Saturday, January 10, 2015

Mr Sugu Apata Ajalia ya Gari Iringa

 Kutoka Facebook:


Picha zikionesha Mbunge wa Mbeya mjini Mr Sugu na rafiki yake wakiwa kando ya gari lao baada ya kupinduka katika mteremko wa Kitongo leo.

MBUNGE wa jimbo la Mbeya mjini Joseph Mbilinyi a.k.a Mr Sugu (Chadema) amenusurika kifo baada ya gari lake kupinduka katika mlima wa Kitonga wilaya ya Kilolo kwenye barabara kuu ya Iringa - Dar es Salaam.

Ajali hiyo imetokea mchana wa leo wakati gari la mbunge huyo likiwa na watu wengine wanne likitokea Mbeya kuelekea jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo vyanzo vya habari hizi viliueleza mtandao huu wa www.matukiodaima.co.tz kuwa mbunge huyo amepatwa na michubuko kiasi na hakuna aliyepoteza maisha katika ajali hiyo .
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi akimethibitisha kutokea kwa ajali hiyo japo amesema taarifa kamili zitapatikana mara baada ya askari waliokwenda eneo la tukio kurejea.




Friday, February 07, 2014

Muungano

Mungu Ibariki Jamhuri ya Muungano ya Tanzania!  Hii picha inasema mengi, Nimeitoa Facebook.


Saturday, December 21, 2013

Hotuba ya Mh. Zitto Kabwe Leo Huko Kigoma

 
Mh. Zitto Kabwe - File Photo


HOTUBA YA MH ZITTO Z. KABWE - KIGOMA – 21 DESEMBA 2013

Leo nina furaha kubwa sana kwani baada ya safari ndefu na yenye changamoto nimerudi nyumbani kuwasalimu wananchi wenzangu! Na hii si salamu za kawaida bali nawasalimu kwa salaam za demokrasia, uadilifu, uzalendo na uwajibikaji. Nawasalimu si kama mbunge bali kama mwana wenu wa Kigoma! Na popote niendapo najivunia kujitambulisha kama Mtanzania; kama mwenyeji wa mkoa wa Kigoma na zao la Ujiji.
 
Tuna mengi ya kujivunia kama taifa lakini Ujiji na watu wake mna nafasi ya pekee katika historia. Watu wa Ujiji mlipokea harakati za kudai uhuru wa nchi yetu mapema kabisa mapambano ya uhuru yalipoanza. Watu wa Ujiji mlikuwa wa kwanza kabisa kupokea mfumo wa vyama vingi mwaka 1992. Na Jimbo la Kigoma Mjini ilikuwa miongoni mwa majimbo ya mwanzo kabisa kutoa mbunge wa CHADEMA mwaka 1995. Kabla ya hapo mlitoa madiwani wengi mwaka 1994. Wakati Watanzania wengine wakiwa wanajiuliza mara mbili mbili kuhusu kujiunga na vyama vipya vilivyoanzishwa, watu wa Ujiji, watu wa Kigoma hamkusita kupokea mabadiliko. Wengi wamepoteza maisha yao, wengine kazi zao na wengine hata ndoa zao katika kupata mbegu ya mabadiliko katika nchi yetu. Nawataka msichoke. Wekeni nguvu mpya katika kusimika mabadiliko kwani bado kazi ya kuimarisha demokrasia katika nchi yetu haijaisha na inahitaji uvumilivu, kusameheana na kuaminiana.
 
Na nchi yetu Tanzania ni nchi inayoonyesha uwezo mkubwa katika kupendana, kuaminiana, kuvumiliana na hata kusameheana. Na haya si maneno tu ambayo ninayazungumza kama mwanasiasa. Hii ni hali halisi na maisha niliyoyaishi kwa mifano nilipokuwa ninakua na kusoma katika shule ya Msingi Kigoma na baadaye Shule ya Sekondari Kigoma. Malezi yangu yalikuwa yanaongozwa na jamii nzima ya Kigoma. Nimekuwa nikiwaeleza rafiki zangu niliokutana nao kwenye masomo na kwenye siasa kwamba nimeanza kuvaa viatu kwa mara ya kwanza nikiwa darasa la tatu. Viatu hivyo viliitwa 'asante Salim' vilivyokuwa vinatengenezwa na Kampuni ya Bora Shoes. Vililinunuliwa na mama Coretha Furugunya ambaye tulikuwa tunakaa mtaa mmoja wa Kisangani Mwanga. Mama Coretha hakuninunulia viatu kwa sababu alikuwa ana uwezo mkubwa, la hasha! Alifurahishwa na matokeo yangu ya mitihani ya darasa la pili kwenda la tatu. Ninaamini kitendo cha mama huyu ni ushahidi wa uungwana, upendo na hata uwajibikaji ambao tunao sisi watanzania. Uwajibikaji kwani alichukua jukumu kunilea ingawa hakuwa mzazi wangu, lakini aliona kuwa kama mwanajamii ana nafasi kubwa katika kuwaendeleza watoto wote. Jamii hii ya watu wa Kigoma ilinifunza kuwa nikijitahidi na kukazana kwa bidii kwenye masomo na majukumu, nitafanikiwa. Siwezi kusahau somo hili katika maisha yangu na ni somo hili ndilo limenifanya nijitahidi kwa kadiri ya uwezo wangu kuwatumikia kwa uadilifu na mafanikio ya hali ya juu sana.
 
Nikiwa nimejaa matumaini haya kuhusu wananchi wenzangu, leo nataka niwakumbushe kwa nini kama jamii tulichagua kufuata njia ya demokrasia. Demokrasia ina maana pale ambapo inatumika kuleta mabadiliko chanya kwenye maisha ya wananchi. Maisha yanayotakiwa ni yale yanayomwezesha mwananchi kupata huduma zake stahili kama Elimu, Afya, Maji na miundombinu. Demokrasia haina maana pale wananchi wanakufa njaa kwa kukosa ajira na kukuza umasikini. Demokrasia inahusu maendeleo. Tumejitahidi kwa upande wetu kuondoa mkoa wa Kigoma kutoka mikoa isiyo na miundombinu kabisa ya maendeleo mpaka kuwa mkoa unaotumika kama mfano kwa miradi mingi ya Maendeleo ikiwemo Daraja la Malagarasi, Uwanja wa ndege wa Gombe-Mahale, barabara za lami na upanuzi wa Bandari, ujenzi wa bandari ndogo mpya na ujenzi wa kituo cha Usafirishaji Mwandiga. Asije mtu akasema yeye ndio kafanya haya. Haya ni matunda ya nyinyi watu wa Kigoma kupokea demokrasia na bila woga kuchagua viongozi wenu bila kujali vyama bali kwa kuangalia uwezo. Haya ni matunda ya viongozi wenu kupaza sauti yenu kwenye baraza la Taifa, Bunge. Haya ni matunda ya uvumilivu wenu na uamuzi wenu wa kutaka maendeleo. Juhudi hizi lazima ziendelezwe kwa nguvu zote ili kuhakikisha kuwa nafasi ya mkoa wa Kigoma katika uchumi wa Tanzania inaonekana dhahiri na hivyo kuchochea maendeleo ya nchi yetu kwa kuwa kituo cha biashara katika nchi za maziwa makuu.
 
Lakini tukumbuke pia kuwa Demokrasia ni Uwajibikaji. Katika kipindi cha utumishi wangu kwenu,kutokana na malezi niliyoyapata kutoka kwenu,nimekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa Serikali inawajibika kwa Wananchi. Nakumbuka wakati napambana kuhusu sheria mbovu ya madini kuna watu hapa nyumbani walisema 'sasa huyu kawa mbunge wa Taifa' lakini watu wengi zaidi wakasema tumemtuma Dodoma kusemea Watanzania wote na sio Kigoma tu. Tuliweza ndani ya miaka mitano kufanya mabadiliko makubwa sana kwenye sera ya Madini na sheria ya madini ambapo baadhi ya mambo ambayo yalikuwa hayafikiriki sasa yametungiwa sheria ikiwemo Serikali kuwa na hisa kwenye migodi, Tanzanite kumilikiwa na Watanzania sio chini ya asilimia 50 na kuzuia kabisa wageni kuchimba vito vya thamani. Uwajibikaji ulipelekea kumshinikiza Rais kufanya mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri kwa kuwafukuza mawaziri wanane mwaka jana. Hii ilitokana sio tu na hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu bali pia ushiriki mkubwa wa wananchi kupitia simu na mitandao ya kijamii ambapo wabunge walishinikizwa kuweka saini kwenye karatasi za kumtoa Waziri Mkuu. Toka wakati huo kumekuwa na utaratibu sasa ambapo wabunge hawaoni taabu kutaka uwajibikaji waziwazi ili kuzuia ubadhirifu wa fedha za Umma. Ni hivi jana tumeshuhudia mawaziri wanne wamejiuzulu na kufukuzwa kazi kutokana na kashfa ya operesheni Tokomeza ujangili iliyoibuliwa na ripoti ya kamati ya bunge. Mabadiliko haya ni hatua muhimu katika kuimarisha demokrasia yetu.
Pamoja na matunda haya mengi mazuri lakini bado kuna changamoto katika juhudi zetu.
 
Changamoto kubwa tuliyonayo wananchi ni kukosekana kwa imani katika demokrasia yetu.
Kutoaminiana. Ni dhahiri kuwa kutoaminiana katika nchi yetu kumekuwa kwa kiasi kikubwa. Taarifa za kitafiti zinaonyesha kuwa katika kila Watanzania kumi, wanane hawaaminiani. Ni changamoto kubwa sana. Wananchi wameacha kutuamini wanasiasa na wanasiasa wameacha kuaminiana wenyewe kwa wenyewe. Hivi sasa uongo umegeuzwa kuwa ukweli na ukweli umekuwa ni uongo. Hivi sasa ukitaka kuwa mwanasiasa maarufu inabidi ujue kudanganya na ukitaka kuitwa mwanasiasa msaliti inabidi uwe msema kweli. Kukosekana kwa uaminifu na kuaminiana imekuwa ni kansa katika siasa zetu. Itachukua muda mrefu sana kujenga demokrasia imara katika nchi yetu kama hatutapata jibu la changamoto hii ya kutoaminiana na kugeuza uongo kuwa ukweli na ukweli kuwa uongo. Hivi sasa ukweli umekuwa unatengenezwa badala ya kutafutwa. Ni majanga! Juzi bungeni Mwanasheria Mkuu wa Serikali alielekeza shutuma kwangu kwamba sikushirikiana na kamati maalum iliyoundwa na Bunge kufuatilia mabilioni ya uswisi na kwamba chini ya kiapo nilisema sina majina ya watu wenye akaunti huko Uswisi. Huu ulikuwa ni uongo. Ni uongo kwa sababu niliitika wito wa kamati hata nilipokuwa katika mafunzo ya mgambo huko Tanga na nilikutana nao mara nne. Ni uongo kwa sababu niliwapa wajumbe wa Kamati Maalaum maelezo na taarifa nyingi sana kuhusu utoroshwaji wa fedha nje ya nchi na umiliki wa mali nje ya nchi kinyumecha sheria. Ni uongo kwa sababu mimi kutotaja majina haya haina maana sina majina, bali ni kwamba ninaheshimu utaratibu na nimeachia vyombo husika vikamilishe uchunguzi. Kwani mimi kama mtu binafsi nikianza kuchukua majukumu ya taasisi ninaweza kutia dosari harakati hizi muhimu na hata kupelekea mchakato mzima kuvurugika. Sitaingia mtego huu! Lakini hatua hii ya Mwanasheria Mkuu imenipelekea kujiuliza maswali mengi kwa mfano uongo kama huu ulifanywa kwa malengo gani? Na ninajikuta hata mimi ninaingia katika hali ninayoilalamikia ya KUTOAMINIANA. 
 
Lakini mtambue pia kuwa kutoaminiana kunaleta kutovumiliana. Hivi sasa kuwa na mawazo tofauti katika vyama vya siasa au hata asasi za kijamii ni uhaini. Lakini bila kuenzi tofauti za mawazo hatuwezi kujenga vyama imara wala Taifa imara. Demokrasia imara ni zao la tofauti za mawazo na uhuru wa mawazo. Kama hatuwezi kujenga vyama vinavyorutubisha uhuru wa mawazo na tofauti za mawazo, tutajenga Taifa lenye watu wenye kuogopa na waliojaa woga. Wanachama wanapoogopa uongozi ni udikteta, lakini uongozi unapoogopa wanachama ni demokrasia. Bila demokrasia ya uwazi na kuvumiliana tutakuwa Taifa la kidikteta. Lazima vyama vya siasa, viongozwe kwa namna ile ile ambayo Taifa litaongozwa.
 
Demokrasia bila kuaminiana, demokrasia bila kuvumiliana sio demokrasia ya kweli.
Juzi nilipoingia Bungeni kwa mara ya kwanza baada ya matukio kadhaa yanayoendelea ndani ya chama chetu nilikaa pamoja na mbunge Tundu Lissu. Wabunge wengine walidhani tutarushiana ngumi na badala yake ikawa ni vicheko na mazungumzo. Hii ni kwa sababu sina chuki na mtu yeyote yule. Mmenifunza kutojenga chuki na watu na badala yake kuchukua kila tukio kama changamoto ya maisha. Siasa ni kupambanisha mawazo tofauti na hatimaye kutafuta suluhu ya pamoja. Na siasa ina misingi yake ambayo sisi wanasiasa huwa tunasahau kwa maksudi. Msingi wa siasa ni kuwa inapaswa kuleta unafuu wa maisha ya wananchi na sio malumbano tu ya kurushiana maneno na kuzushiana ili kujijengea umaarufu wa kisiasa. Siasa si kuwekeana chuki na kuonyeshana ubabe.
Na hapo ni muhimu muelewa wanaKigoma mnapoambiwa kuwa eti ninapofuatilia mabilioni ya Uswisi ninatafuta umaarufu, ni uongo! Mnaposikia eti kukataa kwangu kuchukua posho ni unafiki na kujitafutia umaarufu, ni uongo! Kinachonisukuma kufanya vyote hivi ni ninyi. Ninasukuwa kila ninapowaona watoto bado wanatembea bila viatu;kila ninapoona akina mama wanapoteza maisha yao katika uzazi;kila ninapoona vijana ambao hawana uhakika wa kupata hata mlo moja kwa siku kwa kukosa kazi; ninapoona wazee wa Kigoma kukosa hata shilingi mia moja kununua chai asubuhi. Ninawaona si wanaKigoma bali mamilioni ya watanzania wakiishi katika hali hii. Alafu nalinganisha na taarifa tunazozipata kuhusu ufujaji na utoroshwaji wa pesa zetu. Hebu sasa linganisheni na ukweli kuwa ripoti ya kimataifa iliyotolewa hivi karibuni imeonyesha kuwa mwaka 2010 pekee, jumla ya dola za kimarekani milioni 1315 (bilioni 1.3), yaani shilingi trilioni  2,113,930,000,000 (sh trilioni 2.1) zilitoroshwa kutoka nchini Tanzania. Mwaka 2011 kiasi cha dola za kimarekani milioni 817 yani shilingi za kitanzania zipatazo trilioni 1,315,370,000,000 (trilioni 1.3) zilitoroshwa. Ripoti hiyo inaeleza kuwa jumla ya fedha za Watanzania zilizotoroshwa nje ya nchi katika miaka kumi iliyopita zilifikia dola za kimarekani milioni 4526 (bilioni 4.5) sawa na shilingi za kitanzania trilioni 7,286,860,000,000 (trilioni 7.3).  Nimewatajia hapa namba chungu nzima na matrilioni na mabilioni hayaleti maana. Lakini hii ina maana kwamba kiasi cha pesa zilizotoroshwa katika miaka 10 pesa - robo yake tuingeweza kujenga barabara ya lami ya kiwango cha juu kabisa kutoka Kigoma mpaka Dar-es-salaam! Pesa hizi zingeweza kuajiri na kuwalipa vizuri walimu, madaktari na wafanyakazi wengine ili kuhakikisha tunapata huduma bora na kutengeneza ajira bora kwa vijana wetu. Pesa hizi zingeweza kununua madawa muhimu na kuokoa maisha ya maelfu ya akina mama tunaowapoteza kila mwaka wakati wa uzazi. Pesa hizi zingeweza kuwanunulia watanzania wote si watoto tu angalau pea 10 ya viatu. Sasa nikitafakari haya siwezi kuchapa usingizi mnono na kufumbia macho utoroshwaji wa fedha au matumizi mabaya ya fedha za umma kwa njia ya sisi wabunge kujilipia posho! Hapana! Nafsi yangu hainiruhusu kukaa kimya kwa kuogopa kuitwa mbinafsi au msaliti!
 
Lakini naomba niwasihi kuwa katika nyakati kama hizi za changamoto za kisiasa jambo la msingi kuliko yote ni kutulia maana hakuna linalotokea bila sababu. Licha ya kwamba kuna watu wengi wanapaza sauti zao katika mambo haya lakini pia kuna wengi zaidi ambao wapo kimya lakini wana mawazo yao, ndani na nje ya chama chetu;ndani na nje ya Serikali na ndani nanje ya nchi yetu. Ndio maana lazima kuibadili nchi yetu ili kuweza kuhakikisha kila raia anakuwa na fursa ya kutoa mawazo na fikra zake zinakuwa huru.
 
Maisha ni mabadiliko; mabadiliko hayana ukomo; mabadiliko hayazuiliki kwa sababu bila mabadiliko hakuna ukuaji, bila mabadiliko hakuna maendeleo. Mabadiliko ni kiu kikubwa cha Tanzania kwa sababu mabadiliko huleta matumaini. Na kiu hii ni kubwa zaidi kwetu sisi vijana wa kizazi hiki kipya. Siasa za kizazi kipya cha viongozi ni siasa za majawabu ya kero za wananchi. Siasa za mabadiliko ni siasa za kujenga na kuimarisha; ni siasa za kuaminiana na kuheshimiana hata pale mnapopingana kimawazo. Ninataka tujenge siasa mpya Tanzania;siasa za mabadiliko; siasa zinazojenga matumaini ya kweli;siasa zinazowajali na kuwajengea uwezo wananchi wa Tanzania. Mungu ibariki Tanzania.

Wednesday, November 20, 2013

Tamko kutoka kwa Mh.Zitto Kabwe kuhusiana na kinachoitwa “Taarifa ya Siri ya Chadema”

 
Mh. Zitto Kabwe


NILIPOKUWA katika ziara ya bara la Ulaya kati ya Oktoba 21 mpaka Novemba 2 mwaka huu (2013), nilipokea kwa njia ya barua pepe ripoti inayoitwa “Taarifa ya Siri ya Chadema” ambayo pia ilikuwa imesambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.
“Taarifa ya Chadema inasema kwamba chama hicho (chama changu) kilikuwa kimechunguza mwenendo wangu tangu mwaka 2008 hadi 2010 na kubaini kuwa mimi napokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuivuruga Chadema.
Ripoti hiyo ilinihusisha pia na mwananchi raia wa Ujerumani, Andrea Cordes ambaye, kwa mujibu wa ripoti hiyo, alinisaidia kupokea na kuhifadhi kiasi cha dola 250,000 za Marekani kupitia kwenye akaunti yake binafsi.
Taarifa hii ya kutunga na iliyojaa uongo wa kiwango cha kutisha, imenifadhaisha, kunisikitisha na kunikasirisha.
Taarifa hii iliibuliwa katika kipindi ambacho nilikuwa safarini kutetea haki za Watanzania na Waafrika ambao utajiri wao wa rasilimali unafaidiwa na watu wachache waliohifadhi mali katika nje za nje na pia kupigania makampuni ya mataifa tajiri yalipe kodi stahiki katika nchi zetu.
Pengine lengo la ripoti hiyo lilikuwa ni kutaka kunipoteza kutoka katika nia na dhamira yangu ya dhati ya kutaka Watanzania wafaidike na utajiri wao. Muda ambao watunzi wa ripoti hiyo waliamua kutoa taarifa yao unazua maswali mengi kuliko majibu.
Nafahamu kwamba mimi ni mwanasiasa ambaye nimekuwa mlengwa (target) wa mashambulizi kutoka kwa makundi mbalimbali ya wanasiasa na vikundi vyao. Kama mwanasiasa, niko tayari kupokea changamoto zozote zinazokuja na uanasiasa wangu.
Hata hivyo, ambacho sitakubali ni kwa watu kutumia jina langu na uanasiasa wangu kunichafua mimi binafsi na watu wengine wasiohusika kwa sababu ya kutaka kutimiza malengo yao ya kidhalimu.
Raia huyo wa Kijerumani tayari amekana kuhifadhi fedha zangu. Kwa maelezo yake kwa baadhi ya viongozi wa Chadema amekana kuwa na akaunti inayotajwa na amekana pia kuwepo nchini Ujerumani katika siku na wakati uliotajwa kwenye ripoti hiyo.
Ripoti hiyo imemtaja pia mtu kama Dk. Charles Kimei, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB ikidai kwamba nilikutana naye na alishiriki kwenye igizo hilo la kunipa fedha.
Niseme mapema kwamba tangu kuzaliwa kwangu sijawahi hata mara moja kukutana na Dk. Kimei popote pale ndani au nje ya nchi. Kumuingiza mtu ambaye amejenga jina lake kwenye taaluma ya kibenki kwa sababu tu ya lengo ovu la kumchafua Zitto Zuberi Kabwe si uungwana bali ni unyama.
Kutokana na uchafuzi huu wa wazi dhidi ya taswira yangu binafsi na watu wengine walioingizwa kwenye mkumbo huu, nimeandika rasmi kwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk.Wilbrod Slaa kumwomba athibitishe kwamba kinachoitwa Taarifa ya Siri ya Chadema ni kweli ni taarifa ya chama au kiikanushe ili niweze kuchukua hatua za kisheria dhidi ya waandishi wa hekaya hiyo.
Cha ajabu, nimepokea ujumbe wa kutishiwa maisha kutoka kwa mtu anayejiita Theo Mutahaba na kuahidiwa KUPOTEZWA endapo nitaendelea na jitihada zangu za kupambana na ufisadi na kutafuta haki kwa Watanzania wote pasipo kujali tofauti zao za kiitikadi, kikanda, kikabila na kidini.
Natarajia kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wote ambao wamehusika na utungaji na uenezi wa taarifa hii. Nitahakikisha kwamba wahusika wanatafutwa na kufunguliwa mashitaka stahiki ya upotoshaji na kuchafuana.
Ni matarajio yangu kwamba wale wenye mapenzi mema na Tanzania, mimi binafsi na utawala wa sheria, wataelewa nia yangu ya kutafuta haki katika suala hili.
Nimeamua kujitolea maisha yangu kwa ajili ya Watanzania na kama alivyopata kusema Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela; “Struggle Is My Life.”
Forward Ever, Backward Never- Kwame Nkrumah

Andrea Cortes Makes Demand to Chadema - Reipoti ya Siri Juu Juu ya Zitto Kabwe

Dear Hon. Dr. Slaa,

Dear Hon. Mbowe,

Dear Hon. Mnyika,


With great disappointment I got to learn that members of your party are spreading lies about my person.
A report with the title "RIPOTI YA SIRI JUU YA ZITTO KABWE" of November 4th, which indicates that it is by CHADEMA headquarters *Nyaraka hii imechomolewa kwa siri toka Chadema makao makuu*, was first published in parts in the Internet platform "Jamii Forum" on the weekend of the 26th of October 2013.
 After bringing my complaint towards the owner of Jamii Forum the threads got deleted.

On the morning of the 6th of November 2013 the address of a created blog with the report was publically circulated by Mr. Yericko Nyerere via Twitter. The blog address http://halihalisi255.wordpress.com/2...a-zitto-kabwe/ only contained the above mentioned report.

 The report mentions me as a person to be involved in corrupt activities with your Deputy Secretary General Hon. Zitto Kabwe. It has indicated my private telephone number and the place where I am working.
 This defamation of my person is not acceptable.

I have reacted on the 6th of November by mentioning several facts to refute the report. Please find these tweets in the attachment. The tweets were mentioned towards Mr. Yericko Nyerere, who pretends to be a member of your party, to Hon. Kabwe and to Hon. Mnyika.

After my reaction the report was deleted in the evening of the 6th of November from the blog.
The deletion thus does not resolve the problem that a report which indicates to be from your party has tried to slander my name in the public. Moreover bringing my workplace into the game and therefore putting my organization in a wrong light and even bringing my appointment with this organization in danger.

I therefore request you to take necessary actions to recover my name in the Tanzanian public.
CHADEMA has to dismiss this report as not being written by the party but by an individual who intends to defaming one of your party leaders.
 If CHADEMA will not dismiss the parts of the report which mention my person then I kindly ask you to bring forward the proofs against me that I can accordingly refute them with the necessary actions.

I am awaiting a statement and clear position by your party to recover my name and to take necessary actions to take the authors of this report to court.

My organization and lawyer are informed about the slander campaign in regard to my person. Accordingly legal actions will be taken if CHADEMA will not refute the report officially and bring justice to the people affected from it.

 With warm regards
 Andrea Cordes

Tuesday, September 04, 2012

CHADEMA Yamtaka Rais Kikwete Kuwawajibisha Polisi!

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi Chadema, John Mnyika akionesha picha ya polisi wakizingira Ofisi ya Tawi la chama hicho katika Kijiji cha Nyololo, Mufindi iliyochapishwa na gazeti la Tanzania Daima

DAR ES SALAAM, Tanzania


CHAMA cha Demokrasi na Maendelea (Chadema), kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kuwasimamisha kazi vigogo wote wa Jeshi la Polisi, ambao wamekuwa wakitoa taarifa mbalimbali za uongo kuhusu mauaji ya mwandishi Daudi Mwangosi, ama awatake wajiuzuru nyadhifa zao, kupisha uchunguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho, John Mnyika, aliwataja vigogo hao wa polisi kuwa ni Kamanda wa Operesheni wa Polisi, Paul Chagonja na RPC wa Iringa, Michael Kamuhanda

Wawili hao kwa mujibu wa Mnyika, kwa nyakati tofauti walidai kuwa marehemu alifikwa na mauti baada ya kuchoropoka kutoka kwa kundi la wafuasi wa Chadema na kukimbilia mikononi mwa Polisi na ghafla kulitokea mlipuko wa bomu la machozi uliosababisha kifo chake, jambo ambalo sio la kweli.

Mnyika alisema maneno hayo yanayotafuatiana na kuyaita kuwa ni ya uongo ukizingatia kwamba picha mbalimbali zimeonesha ikiwemo waandishi waliokuwemo eneo la tukio kutoa ushuhuda wao.

Kutokana na hali hiyo, Mkurugenzi huyo alisema ipo haja ya vigogo hao kung’oka kupisha uchunguzi, ili uweze kufanyika kwa haki na kuongeza kwamba Rais atumie madaraka yake kuhakikisha askari saba wanaoonekana katika picha 'wakimsghulikia' marehemu kukamatwa haraka na kuhojiwa ni nani alifyatua bunduki, kwa namna gani na vigogo gani walitoa amri hiyo.

Kwa mujibu wa Mnyika, Polisi imekuwa na tabia ya kukamata raia wanaokuwa eneo la tukio pindi kunapotokea mauaji kama hayo, hivyo ni wakati sasa wa Polisi wanaoonekana katika picha wakimshambulia marehemu Mwangosi nao kukamatwa.

Aidha alilitaka Jeshi la Polisi nchini lisitumie vibaya fedha za walipa kodi kwa kuchunguza nani alihusika na mauaji hayo wakati wauaji wanaonekana.

Mwandishi wa Habari Auwawa na Polisi Bongo!

The Late Daudi Mwangosi
Tanzanian Journalist Killed Reporting Police-Opposition Clash

               SEE HOW HE WA MURDERED AND HIS BODY MUTILATED HERE:
By Fumbuka Ng'wanakilala

DAR ES SALAAM
Tue Sep 4, 2012
DAR ES SALAAM (Reuters) - A leading Tanzanian editor accused police on Tuesday of beating up and killing television journalist Daudi Mwangosi, who died on Sunday during clashes between anti-riot police and supporters of the opposition CHADEMA party.

A police commissioner denied police responsibility but said he had ordered a joint military-police inquiry into the killing. Photos of the victim were uploaded onto the Internet and published by local newspapers.

Opposition leaders and activists linked the incident to a wider trend of rapidly growing violence against dissent in Tanzania and called for an independent inquiry.

Mwangosi was killed in a village in the Iringa region, about 500 km (315 miles) west of the capital Dar es Salaam, while reporting the clashes between police and CHADEMA supporters.

It was the first time in modern Tanzanian history that a journalist had been killed while doing his job, the Tanzania Editors' Forum (TEF) said.

"It was a deliberate move by the police, who clearly targeted this journalist. Eyewitnesses said the journalist was surrounded by police, beaten up and brutally killed," TEF secretary-general Neville Meena told Reuters.

Police fired a tear gas shell into Daudi's stomach at close range, Meena said. "Photos of fragments of Daudi's blown-up body hit the Internet less than one hour after the incident. We believe that the police are deliberately targeting journalists in a violent crackdown."

The police denied responsibility and said they had moved in to disperse an illegal gathering of opposition supporters.

"Police deny any deliberate involvement in the death of the journalist," police commissioner of operations Paul Chagonja said in a statement. "A commission of inquiry comprising officials from the police and military has been formed to investigate the death of the journalist."

Journalists at the scene uploaded images onto the Internet that they said showed Mwangosi's mutilated body lying on the ground, his abdomen ripped open and intestines spilling out.

Local newspapers published photos that showed a man lying on the ground, surrounded by anti-riot police officers who were beating him. The newspapers identified the man as Mwangosi, though the face was not recognizable.

"We condemn the killing ..." the Guardian newspaper of Tanzania said in an editorial. "It is unacceptable for the government and the public to rely on police investigations, knowing only too well that they are in this case one of the parties being blamed for the death of our colleague," it added.

Mwangosi's death came a week after one person was killed and several were wounded when police fired tear gas to break up an opposition protest in Morogoro town, a stronghold of the ruling CCM party.

(Editing by Yara Bayoumy and Tim Pearce)

MNAWEZA KUONA PICHA ZA MAUJI NA MAZISHI YA MAREHEMU DAUDI KWA KUBOFYA HAPA:

Monday, August 27, 2012

Polisi Waua Morogoro Leo!

Marehemu Ally Zona,  alikuwa ni muuza magazeti. Alipigwa risasi kichwani akiwa ameshika magaztei yake!  Hiyo jieraha inaonyesha kuwa marehemu alikuwa anakimbia kutoka kwa polisi. Alipigwa kwa nyuma.


Hapo awali ilielezwa kuwa wakati Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kikisitiza kufanya maandamano leo kisha mkutano mkubwa wa hadhara, kuliibuka mvutano baina yake na Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro, kufuatia Kamanda wake, Faustine Shilogile kupiga marufuku mandamano hayo.

Kamanda Shilogile alieleza sababu za kuzuia maandamano hayo kuwa ni udogo wa barabara za Morogoro na kwamba leo ni siku ya kazi hivyo yanawezesha kusababisha usumbufu kwa wakazi wa mji huo.

Wakati Shilogile akieleza kuzuia maandamano yanayotarajiwa kuanza saa 5 asubuhi, Mkuu wa Operesheni Sangara, Benson Kigaila, alisisitiza kuwa watafanya maandamano kwa kuwa waliskubaliana na Kamanda Shilogile kabla ya kuwageuka.

Kwa mujibu wa Gazeti la Nipashe la 27 August 2012, ilielezwa kuwa Kamanda Shilogile alidai kuruhusu baiskeli na watu kutumia barabara kwa sababu ya mikutano ya Chadema itakuwa ni kuwanyima haki wananchi wengine, na hivyo wataruhusu watu wasiozidi 50 kupita kwa wakati mmoja pasipo kuwa na ishara ya kuonyesha kama wanaelekea katika maandamano.

Pichani ni kijana aliyeelezwa kupigwa risasi kichwani katika tafrani hizo na baadae kupoteza maisha Ametambulishwa kwa jina la Ally Zona, ambae alikuwa ansoma magazeti katika stendi ya Msamvu. Tukio hili lilitokea mapema leo asubuhi kuelekea saa sita mchana wakati Polisi walipokuwa wakiwatawanya wafuasi hao wa chadema. Mtoa taarifa anasema Polisi wanadaiwa kutumia risasi za moto pamoja na mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamani hao.

Watu wengine waliojeruhiwa katika tafrani hiyo wameelezwa kuwa ni mwenesha baiskeli Hashim Seif ambae amejeruhiwa kwa risasi mguuni akiwa napita na baiskeli yake na kijana mwingine aliielezwa kuwa ni muuza matunda Frank Valimba ambae amejeruhiwa na risasi tumboni.


KWA HABARI NA PICHA ZAIDI TEMBELEA KIBONGO BONGO BLOG:

********************************
TAMKO KUTOKA TANZANIA JOURNALIST ALLIANCE (TAJOA)


Jumuia ya Waandishi wa Habari Tanzania (Tajoa) inalaani kwa nguvu zote mauaji ya makusudi yaliyofanywa na Jeshi la Polisi leo mjini Morogro. Inashangaza Tanzania sasa inataka kugeuka taifa la polisi wauaji. NI vyema busara, ujuzi na mbinu stahiki zikatumika badala ya kuendelea kuua raia hata wasiokuwa na hatia.

Hebu ona huyu masikini alivyouawa kwa kupigwa risasi kwenye paji lake la uso na kumsab
abishia kifo cha papo hapo. Inaelezwa alikuwa muuza magazeti aliyekuwa kibandani kwake. Sasa tusubiri taaria ya Polisi ambayo huenda ikasema alikuwa amebeba silaha.

Tanzania, tusikubali kuwa taifa la polisi wauaji.

Marafiki wa Tajoa, nini sasa kifanyike kukomesha hali hii ambayo inaonekana kuota mizizi? Toa maoni yako hapa ili nasi tuyapeleke kwa Jeshi la Polisi

— 
Wafuasi wa Chadema wakiwa na maandamao hayo mjini Morogoro


Moshi wa mabomu yaliolipuliwa kutawanya maandamano ya Chadema leo mjini Morogoro

Akina Mama wakikimbia mabomu ya machozi

Monday, February 20, 2012

Taarifa ya CHADEMA Kuhusu Ombi la CCM kw Dr. Slaa

  TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KURUGENZI ya Habari na Uenezi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA) inapenda kutoa taarifa kuhusu habari zilizoripotiwa kupitia
njia mbalimbali za upashanaji habari, juu ya maombi ambayo Chama Cha
Mapinduzi (CCM) kimesema kinafanya usiku na mchana ili eti Katibu Mkuu
wa CHADEMA, Dkt. Willibrod Slaa, agombee ubunge, kwenye uchaguzi mdogo
unaotarajiwa kufanyika Jimbo la Arumeru Mashariki, Aprili 1, 2012.

Ingawa haijajulikana maombi hayo yanafanyika msikiti upi au kanisa
lipi au sehemu ipi yoyote ile nyingine ya kufanyia maombi, Kurugenzi
imeshangazwa sana na mantiki ya kuwepo kwa maombi hayo ya CCM
yakionesha upendo wa kutiliwa mashaka kuwa chama hicho kimefikia
mahali kinaweza kufanyia maombi vyama vingine ili vipate wagombea
makini wa kukibwaga vibaya sana katika uchaguzi.

Kurugenzi inapenda kusema yafuatayo juu ya maombi hayo ya CCM, ambayo
kwa mujibu wa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye,
kama ilivyoripotiwa katika njia mbalimbali za upashanaji habari,
imedhihirika dhahiri kuwa ni maombi yanayoongozwa zaidi na hila,
husuda kwa CHADEMA na Katibu Mkuu wake, Dkt. Slaa;

Tunapenda CCM wajue kuwa CHADEMA na viongozi wake makini, akiwemo
Katibu Mkuu, Dkt. Slaa, si watu wa kurudi nyuma. Chama hiki daima muda
wote kinapanga mikakati na mipango ya kusonga mbele, kikionesha
utawala mbadala, kikijiandaa kushika dola na kutekeleza malengo ya
Watanzania!

Kwa mantiki hiyo, chama hiki hakiwezi kurudi nyuma, hakiwezi
kumrudisha nyuma Katibu Mkuu wake, Dkt. Slaa kuwania ubunge. Kiongozi
huyu makini, ambaye umma wa Watanzania una imani kubwa naye,
ameshavuka viwango vya ubunge, si mtu wa kuwania nafasi ya ubunge
tena, (is not parliamentary material).

Kwa nafasi yake ndani ya CHADEMA, anao wajibu mkubwa kujenga chama.
Kwa kutimiza wajibu huo, Dkt. Slaa anafanya kazi ya kutengeneza na
kuivisha watu wengine makini zaidi, kuweza kuwa viongozi ndani ya
chama, nafasi za udiwani na ubunge, ili kuendeleza umakini na uimara
wa chama hiki ambacho dhahiri ni tumaini jipya la Watanzania katika
kutoa uongozi mbadala wa nchi.

Kwa umakini wa CHADEMA, uwezo wa Dkt. Slaa na matumaini makubwa ya
Watanzania, ambayo wameendelea kuyaonesha kwa chama hiki tangu mwaka
2007, kilipoanzisha rasmi mapambano dhidi ya ufisadi na mafisadi,
kisha kudhihirika wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, nafasi pekee
inayomstahili Dkt. Slaa ni urais kwa maana ya kuwa ni ‘presidential
material’, si ubunge.

Lakini pia, tunatambua kuwa CCM, wameweza kutoa kauli hiyo ya
kukurupuka baada ya Dkt. Slaa kuwa tayari ametamka wazi tangu awali na
kurudia kauli yake thabiti mara kadhaa kuwa hana nia wala mpango wa
kuwania ubunge mahali popote pale nchini. Hawezi kufanya hivyo kwani
hata ubunge wa Karatu hakushindwa bali aliacha mwenyewe kwa hiari
yake, ili kutekeleza mahitaji ya umma wa Watanzania.

Kurugenzi ya Habari na Uenezi inatumia nafasi hii kuwaambia CCM kuwa
watambue CHADEMA ni chama makini. Kimedhihirisha hivyo mara kadhaa
katika masuala makubwa kwa maslahi ya Watanzania. Kitaendelea
kudhihirisha hivyo pia katika uchaguzi wa Arumeru kwani kina utaratibu
wa kuwapata wagombea wake, kutokana na maamuzi ya wanachama wake.

Tunatambua kuwa kauli hiyo ya CCM pia ni sehemu ya mkakati wa makusudi
kuwakatisha tamaa baadhi ya watu wanaotaka kugombea jimbo hilo kupitia
CHADEMA. Kurugenzi ya Habari na Uenezi inapenda kusisitiza taarifa ya
awali, kuwataka wanachama wetu wajitokeze kwa wingi kuwania uteuzi wa
kugombea ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki.

Tunataka CCM wajue kuwa suala la kuteua mgombea wa CHADEMA ni la
CHADEMA yenyewe, kwa kutumia utaratibu wake, ikiongozwa na katiba,
kanuni na mahitaji ya umma, wala hatuhitaji ushauri wa chama ambacho
kadri siku zinavyokwenda, kinadhihirisha kila dalili ya kuchoka
kujisimamia chenyewe, kusimamia wanachama wake, kusimamia serikali na
maendeleo ya watu, hivyo kupoteza kabisa ushawishi kwa wananchi. Wala
hatujawahi kuomba ushauri kutoka kwao hata siku moja.

Lakini maombi hayo ya CCM, kama ambavyo Nape amenukuliwa katika vyombo
vya habari akisema, yamedhihirisha namna ambavyo chama hicho bado
kinaandamwa na mzimu wa CHADEMA na Dkt. Slaa tangu baada ya uchaguzi
mkuu, kwa kuiba kura na kuvuruga matokeo ya uchaguzi huo.

Kauli ya Nape kuwa iwapo maombi yao yatafanikiwa na Dkt. Slaa akawania
ubunge, CCM watakuwa wamemaliza kazi katika uchaguzi mkuu wa mwaka
2015, inathibitisha tuhuma hizo na namna ambavyo CCM hakikushinda kwa
haki uchaguzi huo.

Kurugenzi ya Habari na Uenezi ya pia inataka CCM waelewe kuwa umaarufu
wa CHADEMA hautokani na umaarufu wa mtu mmoja mmoja wala hausubiri
matukio pekee, bali unatokana na uongozi makini, kuanzia ngazi ya
taifa hadi ya msingi, kikijikita katika kusimamia masuala yenye
maslahi kwa Watanzania na nchi yao muda wote!

Imetolewa leo Februari 18, 2012, Dar es Salaam na

Tumaini Makene
Afisa Habari wa CHADEMA

Sunday, January 15, 2012

Utaratibu wa Mazishi wa Marehemu Mh. Regia Mtema

 Sekretarieti ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) imefanya kikao cha dharura leo, Januari 15, 2012, chini ya uenyekiti wa Katibu Mkuu, Dkt. Wilbrod Slaa, pamoja na mambo mengine, kupanga utaratibu wa chama na viongozi wake wakuu, wakiongozwa na Mwenyekiti wa CHADEMA taifa, Mheshimiwa Freeman Mbowe kuendelea kushiriki kikamilifu kwenye maombolezo, heshima za mwisho na hatimaye maziko yaliyopangwa kufanyika Ifakara.

Wakati huo huo, Kamati ya Uogozi ya Wabunge wa CHADEMA, imefanya kikao cha dharura, kufuatia kifo cha Mbunge wa Viti Maalum, Regia Estelatus Mtema, Pamoja na mambo mengine kamati imezingatia, uzito msiba uliotokea na kupitisha azimio kwamba wabunge wote wa CHADEMA watashiriki katika kutoa heshima ya mwisho kwa marehemu Januari 17, 2012.
Aidha, wabunge wote watasindikiza mwili wa marehemu wa marehemu hadi Ifakara na kushiriki mazito yaliyopangwa kufanyika Januari 18, 2012. Viongozi wakuu wa chama, wabunge wa CHADEMA, hivi sasa wanaendelea kujumuika nyumbani kwa Baba wa Marehemu Regia Mtema, eneo la Tabata Chang'ombe, pamoja na familia, viongozi wakuu wa serikali na bunge katika kuwafariji wafiwa.

Pia pamoja na heshima za mwisho kibunge na kichama kutolewa Jumanne, Januari 17, 2012, familia imeandaa ibada Januari 16, 2012, katika Kanisa la Parokia ya Segerea, kuanzia saa 9, alasiri, ambapo mwili utaagwa na ndugu, jamaa na marafiki.

Taarifa zaidi zitaendelea kutolewa, kutokana na mashauriano kati ya familia, chama na Ofisi ya Bunge.


Imetolewa, Januari 15, 2012
John Mnyika
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi

Saturday, September 17, 2011

Kuna Nini Igunga? Chadema Wakamata Mkuu wa Wilaya Igunga!

Mkuu wa Wilaya ya Igunga Fatma Kimario Akishikiliwa na WanaCHADEMA

 9/15/11

Kutoka  Gazeti la Mwananchi

Na Boniface Meena na Daniel Mjema, Igunga

VURUGU zimezuka jana katika Kata ya Isakamaliwa, wilayani Igunga zikiwahusisha viongozi wa Chadema na Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Fatma Kimario.Katika sakata hilo, wanachama wa Chadema walimkamata Mkuu huyo wa Wilaya kwa tuhuma za kuendesha mkutano wa ndani na watendaji wa serikali za vijiji, wakati akijua kuwa kulikuwa na mkutano wa kampeni za chama hicho karibu na eneo hilo.

Msafara wa Chadema ulifika katika eneo la kampeni saa 8.00 mchana na kabla mkutano haujaanza, Meneja Kampeni wa chama hicho, Sylivester Kasulumbai, aliwaambia waandishi wa habari kuwa mkuu wa wilaya ya igunga alikuwa akifanya kikao cha ndani katika eneo hilo kinyume na taratibu, hivyo wanakwenda kumshughulikia.

Kasulumbai ambaye ni Mbunge wa Maswa Mashariki akiwa na Mbunge wa Viti Maalum, Susan Kiwanga, baadhi ya wananchi na vijana wao, walifika katika ofisi ya Mtendaji wa Kata kulikokuwa kunafanyika mkutano huo na kuanza kuhoji aliko Mkuu huyo wa Wilaya.

Mmoja wa wananchi alimnyooshea kidole mama ambaye alikuwa amekaa mbele na kusema; “..yule ndiye Mkuu wa Wilaya”.Kundi hilo la vijana na viongozi wa Chadema, waliingia katika ukumbi huo na kumtoa nje mama huyo huku wakimtaka aeleze kwa nini anafanya vikao vya ndani katika Kata hiyo wakati anajua kuwa chama hicho kilikuwa na mkutano katika eneo hilo.

Kitendo hicho kilizua purukushani na kutokuelewana kati ya waliokuwa kwenye mkutano wa ndani na viongozi wa Chadema, jambo lililovuta umati mkubwa wa watu.

Maelezo ya DC
Baadhi ya vijana wa Chadema walikuwa wamewashikilia watu waliokuwa wakishiriki mkutano huo huku mama huyo akitolewa nje na kuketishwa kwenye kiti alitakiwa atoe maelezo kuhusu mkutano wake.

Baada ya kukaa kwenye kiti huku akionekana kuchanganyikiwa, alisema yeye ni Mkuu wa Wilaya ya Igunga, jina lake ni Fatma Kimario na kwamba, hakuwa na taarifa za mkutano wa kampeni za Chadema.

“Sina ratiba, iko katika ofisi za halmashauri, hivyo sikujua kama kuna mkutano hapa, hata hivyo watu walikuwepo niliwaruhusu waende mkutanoni na mimi nilikuwa naondoka sasa hivi,” alisema na kuongeza:

“Nilichokuwa nafanya ni mkutano wa viongozi wa serikali kwa ajili ya kuangalia hali ya mifugo inayoibwa sana, elimu kwa wote hasa watoto na ujenzi wa nyumba bora na masuala ya amani”.

Kimario aliwasihi wafuasi wa Chadema kusoma karatasi ya ajenda ili wafahamu kilichokuwa kikijadiliwa kwenye kikao hicho.

Karatasi aliyokuwa akiizungumzia Mkuu huyo wa Wilaya ilikuwa na ajenda tano za kikao hicho ambazo ni; Uhamishaji wa mifugo; Kuwa na choo chenye ubora na nyumba bora; Elimu;  Mipaka ya shule na ajenda ya mwisho ilikuwa Uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Igunga.

Hata hivyo mbunge Kiwanga alimtaka mkuu huyo wa wilaya aeleze tangu lini kikao cha viongozi wa serikali kikahudhuriwa na wazee maarufu na mabalozi wa nyumba kumi, swali ambalo lilionekana kumchanganya mkuu huyo wa wilaya kwa kutoa majibu tata.

Mkutano wa Chadema

Wakati hayo yakiendelea, mkutano wa kampeni ulikuwa nao ukiendelea, hivyo viongozi hao wa Chadema walimtaka DC huyo afike kwenye mkutano huo ili aweze kuonana na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa.

Kimario alikubali, lakini akataka dereva wake atangulize gari na kwamba yeye angefuata. “Nitakwenda kwani napaswa kuwepo pale kama msimamizi wa usalama, sijahudhuria mkutano wowote hivyo nitakwenda,” alisema.

Akizungumzia tukio hilo kwenye mkutano wa kampeni, Dk Slaa alisema wakuu wa wilaya na mikoa kufanya mikutano wakati wa kampeni ni kinyume cha sheria, hivyo Kimario alienda kuanzisha vurugu.

“Hapaswi kufanya mkutano wowote hapa hasa akijua kuwa sisi tuna mkutano wa kampeni na yeye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama wa Wilaya,” alisema Dk Slaa na kuongeza:

“DC anafanya nini huku wakati hiki ni kipindi cha uchaguzi au ndiyo wanapanga mikakati ya uchakachuaji halafu wanadai sisi ndiyo tunaofanya vurugu?”

Mkutano wa kwanza na wa pili wa Chadema, hakukuwa na ulinzi wa polisi kama ilivyokuwa kwenye mikutano mingine.

Askari wamwagwa
Wakati gari la waandishi wa habari likirejea mjini Igunga, lilipisha na magari mawili ya polisi yakiwa yamejaa askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), ambayo yalikuwa katika mwendo kasi yakielekea eneo la tukio.

Magari hayo yalifuatiwa kwa nyuma na gari aina ya Toyota Landcruiser ambalo lilikuwa na vioo vyeusi yote yakiwa yamewasha taa kuashiria hali ya hatari.

Hata hivyo polisi wilayani Igunga kupitia kwa Mkuu wake (OCD), Issa Maguha, waliliambia Mwananchi kuwa hawakuwa na taarifa ya tukio hilo na kwamba magari hayo yalikuwa katika doria za kawaida.


CCM yawaangukia wananchi

Katika hatua nyingine CCM kimewaangukia wananchi wa Igunga kikiwataka kuacha jazba na hasira kwani madhara ya kuchagua mbunge kwa chuki yataligharimu jimbo hilo kwa miaka minne ijayo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu wa NEC ya CCM Uchumi na Fedha, Mwigulu Nchemba wakati akihutubia mkutano wa kampeni katika kijiji cha Usongo kata ya Nyandekwa kinachoaminika kuwa ngome ya Chadema.

Habari zilizopatikana kijijini hapo kabla ya kuanza kwa mkutano huo zilidokeza kuwa Chadema walitangulia kufanya mkutano wa kampeni kijijini hapo na kumwaga ‘sumu’ ili wananchi waichukie na wasiichague CCM.

Akihutubia mkutano huo, Nchemba alirudia mara kadhaa kusema, “shusheni jazba” na “punguzeni hasira” ambayo ilitafsiriwa na wengi kuwa ni kujaribu kung’oa mizizi ya Chadema.

Katibu huyo alisema Chadema kimekuwa kikipandikiza chuki kwa wananchi kwamba Serikali ya CCM haijafanya lolote katika kipindi cha miaka 50 ya Uhuru. Alisisitiza kuwa huo ni uongo wa karne unaopaswa kupuuzwa.

“Kuwa na vuguvugu la kifikra inaruhusiwa na pia kuwa na mtizamo tofauti inaruhusiwa lakini si katika kipindi hiki ambacho wananchi wa Igunga wanahitaji mgombea wa CCM kuliko kipindi kingine chochote,” alisema.

Nchemba aliendelea kusema: ”kwenye uchaguzi mdogo nawaombeni mshushe jazba.…hata kama ulikuwa tayari na mlengo fulani, basi badilika kwa manufaa ya wana Igunga…, tusishabikie vyama bali tujadili hoja”.

Katibu huyo ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Mashariki, aliwasihi wananchi wa kijiji hicho na Jimbo la Igunga kuacha kushabikia mambo ya maendeleo kama wanavyoshabikia timu za soka hata ambazo hawazijui.

Kwa upande wake, mgombea Ubunge wa CCM, Dk Dalaly Kafumu aliahidi kusimamia mradi wa kuvuta maji kutoka Ziwa Victoria hadi Igunga kupitia majimbo ya Kahama na Nzega.

Dk Kafumu aliahidi kutumia utaalamu wake wa madini kuhakikisha kuwa wachimbaji wadogo wanatengewa maeneo yenye madini katika jimbo hilo na kutatua tatizo na kero ya muda mrefu ya daraja la Mbutu.

Sunday, September 11, 2011

Taifa Msibani, Umoja Wetu na Utu Wetu Shakani

Mh. Zitto Kabwe
Ndugu zangu wanawavuti salam kwenu, naomba mnifikishie ujumbe huu kwa watanzania. Shukrani zangu za dhati.

*******************************************
(Nimeandika makala haya nikiwa katika Benchi la Hospitali ya Mnazi Mmoja hapa Zanzibar. Mniwie radhi kama kuna spelling mistakes kwani nilitaka hisia zangu ziwe as raw as possible -Zitto Zitto and not Zitto a politician).

Jana asubuhi tarehe 10 Septemba 2011 Taifa liligubikwa na habari za kushtusha za maafa. Mwanzoni taarifa zilisambaa kwamba zaidi ya watu 2000 walikuwa kwenye Boti MV Spice Islander lililopinduka na kuzama mbele kidogo ya Nungwi likielekea kisiwani Pemba.

Habari hazikuwa za uhakika sana kwani vyombo vyetu vya habari na hasa Televeshini ya Taifa havikuwa vikitoa habari juu ya ajali hii. Habari zilisambaa kupitia mitandao ya intaneti na kufuatia uchu wa habari nilianzisha #ZanzibarBoatAccident katika mtandao wa twitter ili tuweze kufuatilia kwa karibu habari zote za ajali hii.

Habari zilisambaa kuwa Televisheni ya Taifa ilikuwa inaonyesha muziki wa Taarab na Baadaye vipindi vingine vya kawaida bila kutoa habari kwa Umma kuhusu msiba huu.

Watanzania waliokoa wakiwasiliana kupitia twitter na facebook walikuwa na hasira sana na kituo cha TBC1 kutoonyesha au kupasha habari juu ya ajali hii. Mpaka saa moja jioni kituo hiki cha Televisheni ya Taifa kilikuwa kinaonyesha watu wakicheza muziki wa Kongo, wanawake wakikatika viuno na hata ngoma za asili. 'Hallo, washa TBC1 uone Televisheni yenu inachoonyesha' yalikuwa ni maneno ya Mwakilishi Ismael Jussa Ladhu aliponipigia kuonyesha kusikitishwa kwake na kituo hiki.

Mpaka jioni tulikuwa tumepata taarifa kuwa Watanzania wenzetu 198 walikuwa wamepoteza maisha. 570 hivi walikuwa wameokolewa. Binafsi nilipotembelea Hospitali ya Mnazi Mmoja niliweza kumwona Binti aliyeitwa Leyla, akisoma darasa la Nne huko kisiwani Pemba. Leyla alipona, aliokolewa. Nilimwambia leyla atapona na kurudi Shuleni. Mpaka ninapoandika tumeambiwa kuwa Watanzania 240 wamegundulika kupoteza maisha na zaidi ya 600 wameokolewa. Napenda kuwapongeza sana waokoaji wetu, wavuvi wa kijiji cha Nungwi na vijiji jirani, wamiliki wa mahoteli waliojitolea vifaa vyao kwenda kuokoa watu na wanajeshi wetu wa majeshi ya ulinzi na usalama kwa kazi hii kubwa ya kuokoa. Kwa kweli tumeokoa watu wengi kuliko ilivyotarajiwa. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imejitahidi sana, ilitulia na kuonyesha uongozi dhabiti katika juhudi za uokoaji.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akafuta ziara yake huko Canada, ziara iliyokuwa imeandaliwa muda mrefu na kwa gharama. Lakini Rais aliona ni vema kupata hasara kuliko kuwa nje ya Nchi kipindi hiki. Hakutaka hata kumtuma Makamu wa Rais au Waziri Mkuu. Alifuta. Akatangaza siku 3 za kuomboleza. Hata hivyo waandaaji wa Miss Tanzania waliona hasara kubwa kuahirisha shindano la Urembo usiku huo. Wangepata hasara! Hata wafadhili wao Kampuni ya simu za mkononi ya vodacom ambao miongoni mwa waliofariki wamo wateja wa vodacom, waliendelea na shindano hili. Jumatatu, tarehe 12 Septemba 2011 ni siku ya khitma ya kuwaombea marehemu wetu. Nimeamua kutotumia simu ya ngu ya Voda kwa siku nzima, sina njia ya kuiadhibu Kampuni hii isipokuwa kugoma kutumia simu yao japo kwa siku moja kuonyesha kutoridhishwa kwangu na uamuzi wao wa kutojali msiba huu kwa Taifa.

Misiba huweka jamii pamoja. Msiba huu uliotokea Zanzibar ni jaribio kubwa kwa Umoja wa Taifa letu. Shirika la Utangazaji la Taifa limeshindwa jaribio hili la kudhihirisha Umoja wetu katika kipindi hiki. Nataraji wakubwa wa Shirika hili linaloendeshwa kwa kodi watawajibika au kuwajibishwa!

Jumla ya Majeruhi na marehemu sasa inafikia zaidi ya Abiria 800! Asubuhi ya jana 10 Septemba 2011 tuliambiwa na Serikali kwamba uwezo wa Boti la MV Spice Islander ilikuwa ni abiria 500 na wafanyakazi 12. Pia tumejulishwa kuwa boti hili lilikuwa la Mizigo na sio la Abiria. Natumai mara baada ya kumaliza maombolezo haya ya siku tatu Wakuu wa Mamlaka zinazohusika na usafiri wa Majini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar watawajibika au kuwajibishwa. Mkuu wa Bandari ya Zanzibar Mustafa Aboud Jumbe na Waziri wa Miundombinu Hamad Masoud wanapaswa kufukuzwa kazi mara moja kama hawatawajibika wenyewe kwa kujiuzulu.

Kufukuzwa kwao kazi hakutarudisha ndugu zetu duniani bali itakuwa ni somo kuwa hatutarudia tena kufanya makosa yaliyoleteleza ajali kama hii.

Mwenyezimungu atupe subira wakati huu wa msiba mkubwa katika Taifa letu. Alaze roho za marehemu wetu mahala pema peponi na awape unafuu wa haraka majeruhi wetu.

Zitto Kabwe

--

Kabwe Z. Zitto,MP- Kigoma North, Tanzania.
Chairman Parliamentary Public Investments Accounts Committee (POAC),
Deputy Secretary General CHADEMA and Deputy Leader of the Opposition,
Shadow Minister of Finance
Mobile: +255756809535
Blog: http://www.zittokabwe.com/

Saturday, January 15, 2011

Statement by the Tanganyika Law Society on the Arusha Incident of 5th January

9th January, 2011

DAR ES SALAAM

The Tanganyika Law Society (“TLS”) is the National Bar Association for mainland Tanzania, which was established under The Tanganyika Law Society Act, Chapter (CAP) 307 R.E. of 2002. Under the said Act, the TLS has the mandate to, among other things, assist the Government in matters affecting legislation, the administration and practice of law, as well as to protect and assist the public in all matters touching, ancillary or incidental to the law – in short, the observance of rule of law and good governance.

Following media and individual reports on the clashes in Arusha between the Police Force of the United Republic of Tanzania (“Police Force”) and Chama Cha Demokrasia (Chadema) supporters in Arusha Municipality, the TLS communicated with several sources in Arusha, including its members, members of the media and victims of the violence to confirm the veracity of the reports. Our attempts to communicate with or contact the police officers in charge of Arusha Municipality were not successful.

It was brought to our knowledge that on 5 th January, unarmed Chadema leaders and supporters staged a peaceful procession in Arusha Municipality, pursuant to a notification of the same delivered to the Arusha Municipality Officer Commanding District (OCD) on 31 st December, 2010 and in furtherance of a 4th of January letter from, and consultative meeting with, the OCD confirming the security detail for the procession and assembly. We know that the Inspector-General of Police (IGP) on national news at 8PM (that is, less than twenty four hours before the intended procession) on 4th January issued a verbal warning stopping the procession but allowing the public assembly. We also know that despite the warning, the procession took place as planned.

We are informed that subsequent to this, the Police Force used force to stop the procession and to disperse the assembly, which resulted in at least two (2) deaths and injuries to several unarmed civilians. We are further informed that during the fracas, journalists conspicuously identified as such were targeted by the Police Force for simply covering the unfolding events, and that after the fracas the Police Force did not initially allow advocates to gain access to the people who were in police custody.

Article 20 of the Constitution of the United Republic of Tanzania, 1977 (“the Constitution) guarantees every citizen the right to freedom of association and assembly.

Section 43 (1) of The Police Force Auxiliary Services Act, CAP 322 R.E. 2009 prescribes a procedure for anyone desirous of convening, collecting, forming or organizing any assembly or procession in any public place pursuant to their constitutional right to assembly, which only requires notifying the Police Force in the area of the place and time at which the meeting will take place and the purpose of the meeting. It is our understanding that the requirement of notification is prescribed by 2 law to ensure that the Article 20 constitutional right is preserved and protected - and not infringed upon - by the Police Force. It is our view that the verbal warning issued by the IGP, in effect, banned the procession by Chadema because it did not provide for a clear alternative to when Chadema could hold its procession. But where there is a right, there is a remedy and Chadema should have sought recourse within the confines of the law. However, we are not certain that the IGP’s verbal warning afforded Chadema with adequate opportunity to pursue any means prescribed in law to either overrule the IGP’s warning or to stop the procession from physically taking place. That notwithstanding, the Police Force should neither be the cause of nor cause violations of constitutionally protected rights.

Article 18 of the Constitution guarantees every person the right to freedom of expression, which includes the right to freely express ideas and opinions as well as the right to communicate and be informed. This right serves to protect expressions, information and communications, including that of media personnel. From the reports we received, it seems that this right was abridged by the Police Force.

Section 54 of The Criminal Procedure Act, CAP 20 R.E. 2009 obligates a police officer to cause reasonable facilities to be provided to enable a restrained person to communicate with a lawyer, a relative or friend of his choice. From the reports we received, it seems that this right was – at least initially - infringed upon by the Police
Force.

Firmly committed to upholding and strengthening the rule of law and good governance by the State, knowing that when properly upheld, rule of law and good governance protect people from the arbitrary powers of the State; ascribing to the notion that impunity always leads to greater crimes; and believing strongly that justice must not only be done but must be seen to be done:

I. The TLS calls upon civilians and the State and its organs to observe and abide by the laws, the rule of law and good governance; and

2. The TLS strongly condemns the actions taken by the Police Force in denying the constitutional rights of association and assembly and of expression; and

3. The TLS strongly condemns the use of excessive force by the Police Force in dispersing the crowd of unarmed, peaceably processing and assembled civilians; and

4. The TLS calls on the Government of Tanzania to probe into the cause of and to investigate this unfortunate incident, to bring those accountable to task in accordance with the laws, and to continue using peaceful means of upholding rule of law and securing democracy for the national good.

Submitted by and on behalf of the Tanganyika Law Society


PRESIDENT

Tuesday, September 07, 2010

Dr. Slaa Afunguliwa Mashitaka Mahakama Kuu!

(Pichani Dr. Wilbrod Slaa - CHADEMA)

Jamani, sasa badala ya kuwa kampeni ya siasa, ugombea rais wa Dr. Wilbrod Slaa wa chama cha CHADEMA, unageuka kuwa Soap Opera (Tamthiliya)! Majuzi huko Babati walimwuliza Dr. Slaa ana wake wangapi(BOFYA HAPA kupata maelezo zaidi), leo eti mume halali wa mke wa Dr. Slaa, kaenda mahakamani na kusema kuwa Dk. Slaa kamwibia mke wake! Kusoma habari zaidi za kesi BOFYA HAPA.
Huo mchezo wa kukuchunguza mpaka umevaa chupi gani kama ni mwanasiasa ni mchezo mkuu hapa Marekani. Ukiwa mwanasiasa lazima uwe msafi. Kwa maana hiyo usitembee nje ya ndoa, usiwe na kimada, usizae nje, usifanye ngono na malaya... listi ni ndefu. Bado wanafanya na wakigundulika wengi wanalazimishwa kujiuzulu.

Enzi za Mwalimu ulikuwa husikii kwenye vyombo vya habari kiongozi fulani anatembea na fulani! Sasa ni jambo la kawaida, sijui ndo uhuru wa vyombo vya habari au nchi kukua kisiasa. Wangekuwa wanasema mambo ya watu enzi za Mwalimu mbona yangesemwa mengi. Ungesikia fulani kazaa katika kila mkoa wa Tanzania, fulani ana familia nyingine sehemu fulani, binti fulani katoa mimba ya kiongozi fulani n.k. Sidhani kama kuna kiongozi 'msafi', hata kwa upande wa wanawake! Kiongozi fulani kazaa sehemu fulani, kiongozi huo kapata ugonjwa fulani mahala fulani.....Doh! Tunaelekea wapi?

Mwisho nauliza kwa nini wanamsakama Dk. Slaa sasa? Naona kampeni yake imepamba moto kweli halafu ndo jamaa anataka alipe eti mabilioni!

Wednesday, January 21, 2009

Ajali ya Lifti Dar

Wadau, hivi lifti zinakaguliwa kweli Bongo?

********************************************************************
Kutoka Gazeti la Majira:

Ofisa CHADEMA Aporomoka na Lifti Ghorofani

*Ni kutoka ghorofa ya kumi, ashtuka ubongo

Na Joyce Magoti

OFISA Habari na Uenezi wa CHADEMA, Bw. Devid Kafulila, amenusurika kifo baada ya kuporomoka akiwa ndani ya lifti iliyokuwa mbovu kutoka ghorofa ya kumi hadi ya pili, katika Hotel ya Concord iliyopo mtaa wa Agrey, Dar es Salaam.

Mkurugrenzi wa vijana wa chama hicho, Bw. John Mnyika, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa moja usiku wakati Bw. Kafulila alipokuwa akitoka katika semina iliyokuwa ikifanyika hotelini hapo na kwamba amelazwa katika Tasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI).

"Bw. Kafulila alikuwa mtoa mada katika semina iliyokuwa ikifanyika katika hoteli hiyo iliyohusisha vijana na wanawake ambapo aliwahi kuondoka. Wakati akitoka, aliingia katika chumba cha lifti ambacho mlango wake ulikuwa wazi.

"Baada ya kuingia lifti hiyo, alimshusha hadi ghorofa ya pili wakati yeye akitokea gholofa ya kumi, tulimkuta ghorofa ya pili akiwa amepoteza fahamu tukamwahisha hospitalini kwa ajili ya matibabu," alisema Bw. Mnyika.

Alisema kabla ya tukio hilo, uongozi wa hoteli hiyo ulipewa taarifa za ubovu wa lifti hiyo na baadhi ya washiriki waliokuwa katika semina hiyo lakini kutokana na kutojali hawakuchukua tahadhari yoyote.

"Baada ya kutokea ajali hiyo tuliangalia eneo la tukio ambalo halikuwa na maandishi yoyote wala kitu chochote kilichoashiria kuwa lifti hiyo ni mbovu, tunaomba uchunguzi ufanyike, inaonesha lifti hiyo ni mbovu kwa muda mrefu lakini hakuna tahadhari yoyote iliyochukuliwa na uongozi wa hoteli hiyo," alisema.

Afisa muuguzi wa MOI, Bi. Mercy Temu, alisema vipimo vya X-Ray alivyofanyiwa ngonjwa huyo vinaonesha kuwa ameumia sehemu ya nyonga katika mguu wa kushoto ambapo amewekewa jiwe lenye uzito wa kilo nne kwa ajili ya kumpunguzia maumivu na kurudisha nyonga hiyo katika sehemu yake.

"Mbali na kuumia sehemu hiyo pia ubongo wake ulishtuka hali aliyosababisha kupoteza fahamu lakini hali hiyo itatulia na anaweza kurudia katika hali yake ya kawaida baadaye.

"Ni jambo la kumshukuru Mungu kwa sababu mgongo wake haujaumia anaweza hata kuinua miguu yake na kugeuka peke yake," alisema Bi. Temu.

Waandishi wa habari walifika katika hoteli hiyo kwa lengo la kupata ufafanuzi kuhusiana na tukio hilo ambapo msichana mmoja aliyekuwa mapokezi alimwita Meneja wa hoteli hiyo ambaye hakutaka kutaja jina lake.

"Mnataka niwasaidie nini, mimi sina shida na waandishi wa habari wala sitaki kuzungumza chochote na nyie, mnaweza kwenda sina habari ya kuwapa," alisema Meneja huyo.