Showing posts with label Daktari. Show all posts
Showing posts with label Daktari. Show all posts

Saturday, January 24, 2015

Punguza Hasira!

Daktari aliingia hospitalini kwa haraka sana baada ya kuitwa kwa shughuli ya Upasuaji wa haraka, alipokea simu haraka, na kuvaa nguoza kazi na kuelekea moja kwa moja kwenye chumba cha upasuaji.
Wakati akielekea kwenye chumba cha upasuaji alimkuta Baba wa mtoto anazunguka huku na huku karibu na chumba hicho akimsubiria Daktari.
Baada ya kumuona tu, Baba mtoto akapayuka: “ Kwanini umechelewa kuja? Hufahamu kama maisha ya Mtoto wangu yapo hatarini? Hivi unayajua majukumu yako?”
Yule Daktari alitabasamu na kumwambia: “ Samahani sana, Sikuwa Karibu na Hospitali na nimejitahidi kuja kwa haraka sana baada ya kupokea simu kutoka hapa hospitalini….. Na kwakuwa nimeshafika ningekuomba upunguze jazba na hasira ili nifanye shughuli yangu” “Punguza hasira?!
Hivi ingekuwaje kama Mwanao ndiye angekuwa chumba cha upasuaji sasa hivi, ungeweza kupunguza hasira? Kama mwanao ndiye angekuwa anakufa sasa hivi ungefanyaje?” Yule Baba aliongea kwa hasira sana.
Yule Daktari alitabasamu tena na kumjibu: “Daktari hawezi kurefusha maisha ya Binadamu. Nenda katulie na umuombee mwanao, sisi tutajitahidi kadri kwa uwezo tulionao kwa Baraka za Mwenyezi Mungu”
“Kutoa Ushauri kwa vitu visivyo wahusu ni rahisi sana” Alinong’ona yule Baba mwenye mtoto.
Upasuaji ulifanyika kwa masaa kadhaa mara tu baada ya kumalizika Daktari alitoka akiwa anafuraha, “Asante Mungu! Mtoto wako amepona!” Kama una swali lolote utamuuliza Nurse!!” Bila ya kumsubiri Baba Mwenye mtoto kujibu chochote aliondoka kwa haraka kwenye eneo la upasuaji.
“ Kwa nini ni mkorofi sana huyu Daktari? Yaani hawezi hata kusubiri kidogo nimuulize maendeleo ya mwanangu” Baba wa mtoto alimjadili akiwa na nurse baada ya Daktar kuondoka.
Nurse akamjibu, huku akitokwa na machozi:
“Mtoto wake alifariki jana kwenye ajali ya gari, alikuwa katika mazishi ya mtoto wake wakati tunampigia simu aje Hospitali kwa ajili ya upasuaji wa mtoto wako. Amefanikiwa kuyaokoa maisha ya mtoto wako, kwahiyo ameondoka kuwahi mazishi ya mtoto wake.”

HEKIMA:

1. “USIMHUKUMU MTU YEYOTE…. SABABU HUYAJUI MAISHA YAKE NA KIPI
KILICHOMKUTA KWENYE MAISHA YAKE.


2. “TENDA WEMA KADRI UWEZAVYO BILAYA KUJALI HALI ULIYONAYO.

Saturday, April 28, 2012

Mtaalam wa Upasuaji wa Moyo MBongo

 Tanzania inahitaji wataalam wa kila aina katika sekta ya afya, hasa wapasuaji.  Dr. Godwin Godfrey (32) anasomea upasuaji wa moyo wa watoto (Peadiatric Cardiac Surgeon) nchini Israel. Akirudi Tanzania, atakuwa mtaalam peke yake.  Inadaiwa watoto zaidi ya nusu milioni wana subiri huduma yake.

Nauliza, hivi mtaalam kama huyo atalipwa mshahara anaostahili?  Je, ataishia kuwa 'frustrated' na kukimilia nchi nyingine ambayo watamheshimu?

Mungu ambariki, na tuombe aweze kurudi Tanzania kuhudumia watoto wetu.

Asante Da Subi kwa kunistua kuhusu habari hii:

****************************************************
 
Picture
Dr. Godwin Godfrey

Article cross-posted from NationalPost.com, written by Peter Goodspeed
Friday, Apr. 27, 2012

It’s the numbers that fascinate Dr. Godwin Godfrey, a 32-year-old Tanzanian who is finishing a five-year training course in Israel to become a pediatric cardiac surgeon.

When he graduates next summer, he will become the first and only pediatric heart surgeon in all of Tanzania – a country of 43 million people.

Tanzania’s Ministry of Health already has a waiting list of nearly 500,000 patients who desperately need his services.

The government, which sends most of its patients who need heart surgery overseas to countries like India, can only afford to care for about 100 people a year.

“You can see the chances of making it are slim,” says the surgeon. “A child on the waiting list with a serious heart condition may wait maybe three or four years and die of complications like heart failure.

“Sometimes it can be very depressing being a doctor in a poor country like Tanzania,” he says. “Too many times you see children dying in front of your eyes. You know that you are supposed to do something, like give them medicine, but you don’t have it.”

When he first started his training as a pediatric surgeon in Israel’s Wolfson Medical Centre under a program sponsored by the Save A Child’s Heart charity, Dr. Godfrey said he experienced something akin to “culture shock.”

“I always used to see a lot of death,” he says. “In our department in Tanzania [in the Bugando Medical Center in the city of Mwanza — an 850-bed hospital that serves 15 million people] you could have five or seven children die every day. When I got to Israel to train I realized we weren’t seeing any children die — even in a month.

“This was really an eye-opener. Whatever we were doing; it was wrong,” he says. “It opened my eyes. There is so much that we don’t know. There is so much equipment that we don’t have. There is so much medication that we don’t have.”

‘I always used to see a lot of death’

The son of a surgeon, Dr. Godfrey, who was born in a small town on the slopes of Mount Kilimanjaro, has been familiar most of his life with the difficulties of practicing medicine in a developing country.

After graduating at the top of his class in high school in Tanzania, he won a scholarship to study medicine at Makerere University in neighbouring Uganda. When he returned home to serve his internship, he deliberately selected the Bugando Medical Centre in Mwanza, Tanzania.

“Most of our doctors are actually located in Dar es Salaam, the capital,” he says. “That’s the biggest city and all the government offices are there. But with me being interested in surgery, I thought if I went to work in one of the big hospitals I wouldn’t get the hands-on experience that I wanted.”

In Mwanza, he was overwhelmed with work and because of a shortage of surgeons and specialists found himself doing everything from pediatric cases to orthopedic, ophthalmology and neuro-surgery.

When he started a residency in the Mwanza hospital, he shifted to cardiac surgery, but found himself stymied by a lack of equipment and expertise.

‘Being in Africa, in this hospital, we didn’t have the equipment to conduct open-heart surgery’

“Being in Africa, in this hospital, we didn’t have the equipment to conduct open-heart surgery,” he says. “So we have had to start building our unit from scratch.”

When Dr. Godfrey investigated the possibility of getting some expert training in cardiac surgery, he discovered the only place he could do so in Africa was in South Africa, Egypt, Morocco or Tunisia. But when he tried to apply, he was told those countries weren’t interested in training foreign doctors.

Then in 2006 a visiting German doctor, working for a Christian charity, suggested Dr. Godfrey should apply to study in Israel under a humanitarian project sponsored by the Save A Child’s Heart organization.

Over the last 15 years, cardiac surgeons operating out of the Wolfson Medical Centre in Holon, Israel, have treated more than 2,800 children with congenital heart diseases and adolescents with heart valve diseases.

Patients are now flown into Israel from all over the world for about 225 emergency operations each year, with 43% of the cases coming from Africa and 47% from neighbouring Arab states.

Save a Child’s Heart offered Dr. Godfrey a full five-year scholarship to study pediatric cardiac surgery and has methodically begun to help him train a complete surgery team to work with him in Tanzania.

“Heart surgery is teamwork,” says Dr. Godfrey, who was in Toronto this week to tour Sick Children’s Hospital. “It’s not just the work of a surgeon. You need a cardiologist, an anesthesiologist, an intensive care unit internist, people to operate the heart pumps and ventilators.”

‘We had to stop her heart, go in and close this hole and then start the heart functioning again’

Last summer, a team of 13 doctors from Save a Child’s Heart travelled to Tanzania to stage a cardiac clinic in Dr. Godfrey’s hospital and operated on 13 seriously ill children, including the first ever open-heart operation on a child in Tanzania.

Four year-old Laurencia Simon, the daughter of farmers who live in a mud hut without electricity or running water three hours drive from Mwanza, underwent the historic surgery.

“She had a hole in her heart,” Dr. Godfrey explains. “We had to stop her heart, go in and close this hole and then start the heart functioning again.”

“In places like Canada, you can do this operation any day,” he says “You don’t let patients with the condition become six months old or even a year, without the operation. But in Tanzania, this little girl was four years old and she could have died while being on a waiting list.”

Now, she is healthy and back in school.

In a very small way, things are about to change in Tanzania.

• Email: pgoodspeed@nationalpost.com

Source: http://www.wavuti.com/4/post/2012/04/nearly-500000-children-waiting-for-tanzanias-only-surgeon-dr-g-godfrey.html?utm_source=feedburner&utm_medium=twitter&utm_campaign=Feed%3A+wavuti+%28Wavuti+%29#ixzz1tKF774au

Monday, April 09, 2012

Kanumba Alikufa Kwa Brain Concussion!

Duh! Kama kweli alipata concussion ina maana Steven Kanumba, alipigwa na kitu kizito kichwani au alianguka kweli.  Polisi wanasemaje?  Madakatari wanasema ubongo wake ulikuwa umevimba.

KUTOKA WEB MD

What is a concussion?
A concussion is a type of traumatic brain injury that is caused by a blow to the head or body, a fall, or another injury that jars or shakes the brain inside the skull. Although there may be cuts or bruises on the head or face, there may be no other visible signs of a brain injury.4


 
******************************************************************************
KUTOKA  GAZETI LA MWANANCHI:

NI BAADA YA JOPO LA MADAKTARI MUHIMBILI KUMFANYIA UCHUNGUZI, BABA YAKE AZUNGUMZA, WABUNGE WAANGUA KILIO

Florence Majani na Suzzy Butondo

MSANII nyota wa filamu nchini, Steven Kanumba amefariki dunia kutokana na tatizo la mtikisiko wa ubongo linalojulikana kitalaamu kama Brain Concussion, taarifa za kitabibu zimeeleza.


Taarifa hizo za ndani, zilizopatikana jana baada ya jopo la madaktari bingwa watano wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu huyo, zimeeleza kuwa tatizo hilo linaweza kumfanya mtu apoteze maisha mara moja au baada ya siku kadhaa. Mmoja wa madaktari hao ambaye aliomba jina lake lisitajwe gazetini alisema waligundua tatizo hilo baada ya kumfanyia uchunguzi huo kwa zaidi ya saa mbili.

“Tulianza kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 6:45 mchana na tukagundua kuwa marehemu alifariki kutokana na mtikisiko wa ubongo kwa kitaalamu, Brain Concussion,” alisema daktari huyo. Alisema Kanumba alipata mtikisiko wa ubongo ambao husababisha kufeli kwa mfumo wa upumuaji (cardio-respiratory failure) “Kilichomuua hasa ni mtikisiko wa ubongo, ambao endapo unatokea katika sehemu ya nyuma ya ubongo (cerebrum), huua kwa haraka” alisema daktari huyo na kuongeza kuwa mtikisiko wa ubongo wa nyuma, husababisha matatizo ya mfumo wa upumuaji na hilo limeonekana katika mwili wake.

“Baada ya ubongo wake kutikiswa kwa nguvu, mfumo wa upumuaji ulifeli na ndiyo maana tumekuta kucha za Kanumba zikiwa na rangi ya bluu, huku mapafu yake yakiwa yamevilia damu na kubadilika kuwa kama maini, hizo ndizo dalili za kufeli kwa mfumo wa upumuaji.”

“Mtu aliyepata mtikisiko wa ubongo huweza kutokwa na mapovu mdomoni na hukoroma kabla ya kukata roho na ndivyo ilivyokuwa kwa Kanumba kabla hajafariki.”

Daktari mwingine aliyeshiriki katika uchunguzi huo ambaye pia aliomba jina lake lisitajwe alisema ubongo wa mwigizaji huyo ulikuwa umevimba na kushuka karibu na uti wa mgongo na hivyo kuathiri mfumo wa upumuaji.
Alisema sehemu ya maini na majimaji ya machoni ya marehemu, vimepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili kubaini endapo kuna sumu au kitu kingine katika mwili huo.

Baba mzazi azungumza Baba mzazi wa mwigizaji huyo, Charles Musekwa Kanumba alisema kwamba alipata taarifa za kifo cha mwanawe Jumamosi saa 10:00 alfajiri baada ya kupigiwa simu na dada wa marehemu, Sara Kanumba. “Sara aliniuliza: ‘Una taarifa yoyote kuhusu mwanao Kanumba?’ Nikamjibu kuwa sina taarifa yoyote, ndipo aliponieleza habari za kifo hicho. Aliniambia Kanumba hatupo naye tena amefariki kwa kuanguka, amekorofishana na mpenzi wake.” alisema taarifa hizo zilimsababisha aishiwe nguvu kwa kuwa kilikuwa kifo cha ghafla… “Basi kuanzia hapo, nilianza kupigiwa simu za kupewa pole, ndipo nilipoamini kumbe mwanangu amefariki.”

Akizungumzia kuchelewa kufika msibani, alisema kumetokana na tatizo la mawasiliano. Awali, alikuwa amepanga mtoto wake Kanumba akazikiwe Mwanza kwa babu yake ndiyo maana hakufika mapema msibani. “Nilikuwa nimepanga apitishwe hapa kwangu Shinyanga aagwe, halafu tumpeleke Mwanza kwa babu yake kumzika huko lakini alipokuja mama yake alinishauri kuwa huko kutakuwa na nafasi ndogo kwa sababu watu ni wengi pia alikuwa na marafiki wengi, wengine wa kutoka nje ya nchi kwa hiyo alinishawishi na tukakubaliana kumzika Dar es Salaam,” alisema.

Pia alikanusha uvumi kuwa hajafika msibani kwa kuwa walikuwa na ugomvi na marehemu akisema walishamaliza tofauti zao. Alisema anatarajia kufika leo usiku tayari kushiriki mazishi hayo.

Wabunge kilio Jana, baadhi ya wabunge waliofika nyumbani kwa marehemu Kanumba waliangua vilio wakati walipotoa salamu zao za rambirambi.

Mbunge wa Viti Maalumu, Martha Mlata hakuzungumza na badala yake aliimba kipande cha wimbo uliozungumzia kifo na maneno ya wimbo huo yalionekana kuwagusa wafiwa na kusababisha vilio kuanza upya huku baadhi wakipoteza fahamu.
Mbunge mwingine, Neema Mwinyimgaya aliongeza majonzi masibani hapo alipounganisha msiba huo na wa mama yake… “Mama yangu amefariki miezi mitatu iliyopita, huko uliko mama, nakuomba umpokee kijana mwenzetu,” alisema mbunge huyo na kushindwa kuendelea.

Wabunge wengine waliohudhuria msiba huo ni Ismail Aden Rage (Tabora Mjini), Aboud Juma (Kibaha Vijijini), Mussa Azan Zungu (Ilala), Abbas Mtemvu (Temeke), Peter Serukamba (Kigoma Mjini) na Ritha Kabati (Viti Maalumu).
Kova na mchango wa Kanumba Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema anakumbuka mchango wa Kanumba katika kuzuia uhalifu jijini.

“Tulishirikiana naye pamoja na wasanii wengine kuandaa bonanza maalumu ambalo lilidhamiria kukabiliana na uhalifu hapa jijini na kwa kweli mchakato ule ulifanikiwa kwani uhalifu ulipungua kwa kiasi kikubwa” alisema Kova.
“Kifo chake kimekuwa cha ghafla mno na nafikiri kujiweka tayari (kiimani) ni jambo ambalo kila mmoja anatakiwa kuwa makini nalo katika maisha yake,” alisema Kova.

Ratiba ya mazishi
2:30 - Msafara kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili kupitia Barabara ya Umoja wa Mataifa na Ali Hassan Mwinyi hadi Viwanja vya Leaders Club.
3:30 - Misa ya kumuombea na salamu mbalimbali.
6:00 – Kuaga
9:00 - Kuelekea Makaburi ya Kinondoni kupitia Barabara ya Tunisia

SAHIHISHO
Rais Jakaya Kikwete jana alilazimika kubadili ratiba yake ya safari za ndani ya nchi ili kwenda kujumuika na waombolezaji wengine katika msiba wa msanii nguli, Steven Kanumba na hakuwa na safari nje ya nchi kama ilivyoripotiwa na gazeti hili jana. Mhariri.

SOMA HABARI ZAIDI HAPA:

Tuesday, May 10, 2011

Wazaliwa Vichwa Viwili Mwili Moja

Duh! Leo huko China maajabu. Mapacha wamezaliwa viajabu. Ingawa kuna vichwa viwili wana mwili mmoja! Sijui itakuaje wakiwa wakubwa! Mapacha hao ni wa kike. Madakatari wanasema kuwa hawataweza kuwatengenisha. Wangezaliwa Afrika watu wangesema uchawi. Mungu awabariki.

Kwa habari BOFYA HAPA:

Friday, June 26, 2009

Daktari wa Michael Jackson Anatafutwa na Polisi!

Jana, walisema wapelelezi wa mauaji (Homicide) wamekwenda kwenye nyumba aliyokodi Michael Jackson kufanya uchunguzi. Sasa kuna habari kuwa daktari aliyekuwa anamtibu nyumbani kwake haonekani!

********************************************************************
June 26th, 2009

Cops look for Jackson’s doctor

Posted: 12:29 PM ET

LOS ANGELES, California (CNN) — Police are looking for Michael Jackon’s personal physician but have been unable to contact him, they said Friday.

The doctor’s car was towed from Jackson’s home Thursday and impounded, authorities said.
The car may contain “medications pertinent to the investigation” into Jackson’s death, said Detective Agustin Villanueva of Los Angeles Police Department said.
Police did not release the doctors name.

Kwa habari zaidi soma:

http://www.google.com/hostednews/ap/article/ALeqM5iJN6FHrmT75HzSZChIb2PDzFEDXgD992F6Q00

Monday, April 06, 2009

The No. 1 Ladies Detective Agency

(kutoka kushoto - Anika Noni Rose, Jill Scott, Lucian Msamati)

Wadau, mkipata nafasi hebu tazama TV show, The No. 1 Ladies Detective Agency. Kama mnakumbuka niliwadokeza mwaka jana kuwa walikuwa wanapiga sinema huko Bostwana. Hiyo sinema imekuwa 'pilot' (Show ya kwanza) na sasa HBO wameagiza iwe series. Hivyo kila wiki tutafaidi show kutoka Botswana. Kwa sasa inaonyeshwa kwenye stesheni za HBO na BBC.
Stelingi wa The No. 1 Ladies Detective Agency ni mwimbaji Jill Scott ambaye ni MMarekani. Anayoigiza utadhani ni MBotswana. Stelingi mwingine ni Anika Noni Rose ambaye utamkumbuka alikuwa kwenye sinema Dreamgirls.

Stelingi mwingine ni Lucian Msamati, ambaye ana asili ya Tanzania ingawa ni MZimbabwe. Wazazi wake ni waTanzania. Alizaliwa Uingereza na alipelekwa Zimbabwe akiwa mdogo.
Nimefurahi kuona jinsi watu wanavyofurahi The No. Ladies Dectective Agency. Wazungu wanaipenda kweli na sasa tayari wameanza kusema kuwa huenda Jill Scott atapata Emmy Award! Hayo ni makubwa!
Botswana wanasema kuwa utalii kwenda Botswana unaongezeka na wanaishukuru hiyo show maana inaonyesha Botswana ilivyo ukweli. Serikali ya Botswana iliwaunga mkono hao watengeneza show na imekuwa na mafanikio makubwa. Kuna aerial shots (scenes zilizopigwa kutoka kwenye ndege) safi sana. Watu wanapata ajira kama wafanyakazi wa filamu, na pesa zinaingia kwenye kukodi mahoteli, chakula, usafiri na megineo.

Je, Tanzania tuko tayari kuwa na show ambayo inapigwa huko? Je, serikali itawaunga mkono watengeneza TV show wakiomba kupiga nchini Tanzania?
Na kwa wasiojua miaka ya 60, kulikuwa na TV show, 'Daktari' ambayo ilikuwa inapigwa Kenya.
Ilihusu daktari wa wanyama ambaye alikuwa mzungu. Stelingi wake alikuwa marehemu Marshall Thompson.