Showing posts with label Mama Bishanga. Show all posts
Showing posts with label Mama Bishanga. Show all posts

Wednesday, May 31, 2017

Mama Bishanga Amlilia Ivan X - Mume wa Zari

Pichani ni Mama Bishanga  aka Mrs. Marolen
MAMA BISHANGA AMLILIA IVAN X HUSBAND WA ZARI
Nimesikitishwa sana na kifo cha Ivan, ni mapema sana kwa yeye kuondoka duniani kuacha watoto wadogo sana, wanahitaji sana uwepo wa baba na mama, lakini Mungu ni Mwema amependezwa nae kuwa karibu yake mbinguni.
Zari binti yetu pole sana kwa pigo hili kubwa lisilozibika kwa wepesi, Mungu akutie nguvu. Wewe ni mmoja kati ya mabinti wachache walio na msimamo imara kimaisha, wasioyumba, wanaojitegemea zaidi kimaisha kwa kufanya biashara na shughuli mbalimbali kujipatia kipato, usieyumbishwa na mapito ya maisha ya dunia kirahisi. Naweza kusema nimekufahamu baada ya kuwa na mpenzi wako Diamond, umeonyesha msimamo na uimara wako ambao ni ushahidi mzuri kuwa utawatunza wanao watatu ambao sasa wako mikononi mwako forever. Usikate tamaa wengi tumepitia uliyopitia, kuvunjika kwa ndoa na kufiwa na wenzetu na kubakia na watoto, yalinikuta mimi binafsi hayo sikujua ada, nauli, kusomesha watoto  hadi mwenzangu alipofariki mwaka 1994 nikiwa Idara ya elimu ya juu na mshahara wa ualimu, na watoto kurudi kwangu, hapo ndio niliona jinsi Mungu huongeza baraka zake, na jinsi ukoo wa Kamota ulivyosimama nami kulea watoto. Nawewe daima muweke Mungu mbele mambo yatakuwa mazuri, hasa ukizingatia ulishajiimarisha na baba watoto wako amewaacha vizuri, Mungu atakuongezea na kukutia furaha ya maisha ya familia yako, na bila kusahau kuwa Diamond yuko pemebeni yako, tabasamu lake linatosha kukuongezea amani na nguvu ya maisha na kilo za uzito wa mwili confidence! Diamond amelelewa vizuri sana na mama yake na yuko wazi katika penzi lenu, sasa ni wakati wa kushikamana kikamilfu kupeana raha na amani na kuijenga familia yenu .
Kila la heri Zari, huenda tukaonana JHB maana sehemu ya maisha yangu ni JHB kwa mume wangu Orange Grove na Alexander township!
GOD BLESS YOU AND YOUR FAMILY ZARI
MAMA BISHANGA / MRS MAROLEN
CLEVELAND. OHIO

Wednesday, September 07, 2016

Mama Bishanga na Wadogo Zake Wafiwa na Mama Yao

MAMA BISHANGA NA WADOGO ZAKE WAFIWA NA MAMA YAO

         MWALIMU AGNES NDEMBO HATIA
Watoto wa marehemu mzee Isaya Innocent Hatia tumempoteza mpendwa mama
yetu mpendwa Mwalimu Agnes Ndembo Hatia kilichotokea hospitali ya Regency
 jana jumamamosi mchana. Mama yetu alikuwa nguzo pekee iliobakia nasi baada
ya kufariki baba yetu Mzee Isaya Innocent Hatia mwaka 2011. Tunamshukuru
Mungu sana kwa upendo wake kwa mama yetu aliempa nguvu ya kuishi miaka
tisini na sasa amempenda zaid mama yetu, bibi yetu na amempumzisha usingizi
wa milele na milele Ameni
Mwalimu Agnes Ndembo Hatia amefundisha watu wengi sana darasa la kwanza
tangia miaka ya hamsini hadi alipostaafu Tabora, Uhuru shule yamsingi.
Mama, ametuacha watoto wake Christina wa USA, Geofrey wa Namibia, Mwl
Mark Hatia wa Tambaza shule ya secondary, Bernadetta wa Dar, Isaya wa Finland,
Costancia wa Kibaha, na Oscar mdogo wetu wa mwisho. Ameacha wajukuu, na
vitukuu wengi ambao ni watoto na wajukuu zetu sisi watoto wake pamoja na dada
zetu marehemu Joyce Hatia na Mwalimu Cecilia Hatia. Picha zinaonyesha
mama Hatia mwaka 1966 akiwa na Constacia ambae picha yake pembeni ni Costancia
alivyo sasa, na zingine ni mama na wanae wajukuu na vitukuu
Kwa taarifa za maandalizi na ratiba piga simu zifuatazo. 0653 763 201 Kilian Kamota,
0755 333 948 Dick Hatia, 0788 627 430 Ibra Yunus, na 0763 833 893 Solmon.
 BWANA ALITOA, BWANA AMETWAA. TUMSIFU YESU KRISTO: AMEN
 

Saturday, August 20, 2016

Mama Bishanga Ndani ya White Party ya Birthday ya Rukia Hussein

Kwa Hisani ya Christina Marolen aka Mama Bishanga


            MAMA BISHANGA NDANI YA WHITE PARTY YA BIRTHDAY YA RUKIA HUSSEIN

Rukia mtoto wa marehemu Sheihk Yahya Hussein aliangusha bonge ya white party kusherehekea miaka 50 ya birthday yake kwenye hoteli babu kubwa ya Marrioti, jijini Cleveland Ohio. Mambo yalikuwa mambo haswaaa!

Rumba lilinoga kwa nyimbo za nchi mbali mbali za Africa na hasa za maarufu home TZ za Bado, number one, bora uende, colors of African, na nasema nae taarabu ambao mume wa Rukia ilibidi awekwe kitini na kukatiwa mauno kisawasawa na mkewe na waalikwa akina Mama Bishanga, Prisca Zenda, Michelle Mujuni nk walipotupia mduara wa nguvu! Wapendwa angalieni picha mpate picha ya mambo yalivyokuwa bam bam! 
        
          HAPPY BIRTHDAY RUKIA MUNGU AKUONGEZEE UMRI, MAFANIKIO, NA
                              FURAHA YA MAISHA YAKO NA NDOA NA FAMILIA YAKO!
Birthday Girl Dada Rukia Hussein Awasili

Mama Bishanga (Kulia) na Birthday Girl



Sunday, May 24, 2015

Mama Bishanga Afiwa na Kaka Yake - Casim Jaffer Manji

MAMA BISHANGA AMLILIA KAKA YAKE CASIM JAFFER MANJI

Leo hii tarehe 23/05/2015 asubuhi ya Tanzania nimefiwa na kaka yangu mkubwa Bw Casim Jaffer Manji (Jalejale) Kongowe kwa binti yetu Anna Kepha mtoto wa marehemu dada Mwl Cecilia Hatia.
Napenda kutumia nafasi hii kumjulisha Abasi Manji na akina Manji wa DSM. Familia ya Jaffer Manji wa Bombey, wadogo zangu Dr Geofrey Hatia Nambira wa Namibia, Isaya Hatia wa Finland, na aunt Eva Mack Hatia wa Finland. Familia ya marehemu mzee Abdruhaman Bellim, familia ya mzee Abdala, mzee Jalabi, na shangazi Anna Mchauru wa Masasi ya zamani na Mkuti, ukoo wa che Mbungo wa Lukuledi Masasi, na ukoo wa Hatia wa Ndanda. Na Deo mwalujua na familia yake wa Columbus Ohio.

Kwa taarifa za mipango na ratiba ya mazishi wasiliana na

Mwl Mack Hatia wa Azania sekondari 225 0754 290 013
Kilian kamota 225 653 0763 200
Constancia Hatia (Mrs Solmon) 225 0712 555 966
Musa Kamota 225 075 609 370 
Fidelis Mrope 225 0713 410 321 
Hendrich Nambira (Kenny) 225 0715 965 321
Joseph Hatia (Ndugu) 225 0713 987 173

Mungu amempenda Zaidi kaka yetu. Tushukuru kwa yote.

Mama Bishanga / Mrs Marolen

Ohio / USA

Sunday, December 07, 2014

Mama Bishanga Ampongeza Diamond Platinum

MAMA BISHANGA AMPONGEZA DIAMOND
Nimeona nisikae na duku duku la pongezi zangu kwa kijana wetu Diamond kwa kutwaa tunzo tatu kwa mpigo wiki iliopitai huko South Africa, huo ni ushindi mkubwa sana kwa Diamond, mama yake na sisi sote kama taifa la Tanzania. Mimi kwa niaba ya wazazi wenzangu bwana mdogo nakupongeza sana na ninampongeza sana mama yako Sandra kwa kukuandaa katika fani ya muziki, nguvu yake ndio mafanikio yako. Hii inanikumbusha hata mimi nilivyokuwa ninaandaa kazi zangu za sanaa wakati nafundisha Chuo cha Uhazili Tabora nilimtumia mwanangu Kenny (Hery) kuigiza nae na kucheza nae ili kumuelekeza mkondo uigizaji. Na hata Natasha alifanya hivyo kwa mwanae Monalisa, nz wengineo wengi, kumbe ni jambo zuri kwa wazazi kufanya hivyo kwa watoto wao kwa fani, elimu na ujuzi mbalimbali ili kuwapa msingi bora.
 Mimi niakukubali sana kimuziki na kimaadili na upendo na heshima unayompa mama yako na jamii nzima, na hii ngololo, ngololo, ngoololooo hii kibko hata sisi wazazi wako hii tunaisakata kama kazi!

Keep it up young boy from Tanzania! Home , sweet home Tanzania!

Mama Bishanga/ Mrs Marolen
Ohio/ USA

Mama Bishanga aka. Mrs. Christina Marolen

Sunday, October 12, 2014

Mama BIshanga na Rafiki Yake Julie Kutoka Liberia


MAMA BISHANGA WA TZ NA JULIE WA LIBERIA

Mama Bishanga na mfanya kazi mwenzake kutoka Liberia wanonekana wakiwa kazini, Adern Court Alzheimer Home Care wakifurahia uamuzi wa madaktari watano wa Tanzania wanokwenda kuongeza nguvu ya kusaidia kuwatibu raia wa Liberia, baada ya kusoma taarifa hizo kwenye magazeti ya Tanzania. Julie Blanton ambae alikuja Amerika miaka mingi mara baada ya vita iliotokea Liberia miaka ya themanini na tisini, huwa anenda kwao kila mwaka kusalimia ndugu zake. Julie ameshukru sana Rais Kikwete na watanzania kwa ujumla kwa moyo wao wa upendo na kusaidia nchi nyingine tangia miaka sana iliopita katika Nyanja mbali mbali. kasema GOD BLESS ALL TANZANIANS.

Pili: mimi Mama Bishanga na shost yangu Julie tuwapa heri ya kuzaliwa/ Happy Birthday kwa mwanetu Kenny @ Henrich na Raisi Kikwete, Bishop Desmund Tutu na wote waliozaliwa tarehe saba mwezi huu wa octoba, Mungu awaongezee upendo na nguvu ya kufanya kazi na kulitumikia taifa.

Christina I Marolen 

 Mama Bishanga

Ohio / USA

Sunday, September 14, 2014

Kenny, Mtoto wa Mama Bishanga Aoa!

KENNY MTOTO WA MAMA BISHANGA AOA MZANZIBAR

Hendrich Nambira au Kenny kama anavyojulika kwenye mchezo wa Mambo hayo katika runinga ITV,  alifunga pingu za maisha na mke wake Florence kutoka Visiwani Zanzibar. Harusi ilifanyika kanisa la Anglican UMCA, Upanga DSM tarehe 23/08/2014. Mama Bishanga na mumewe hawakuwahi siku ya harusi hiyo iliopendeza sana na kuhudhuriwa na wazazi wakimwemo wadogo wa mama Bishanga Mack Innocent Hatia na Constancia Innocent Hatia, baba mkubwa mzee John Kamota na shangazi Rehema Kamota, bibi wa Kenny mwalimu Agnes Innocent Hatia na ndugu zetu wengine, pia marafiki na wawakilishi wa wasanii toka Bongo movie. Sherehe ya kukata na shoka ilifanyika Lion Hotel.


Kenny akiwa na mkewe Florence. Auaga ukapera.
Bwana harusi Kenny na mkewe Florence wakiwa pwani Oster Bay mara baada ya kufunga ndoa

Florence na Herry waikikata Keki

Wanaharusi wakikabidhiwa Top Tier ya Keki yao

Wanaharusi wakigonga Champagne Toast na Wageni wao

Dada wa bwana harusi Sizelina ambae ni mtoto wa kwanza wa mama Bishanga akilisakata rumba kwa raha na furaha tele ya harusi ya mdogo wake.

Wayao na Wamakua wakicheza wimbo wao maarufu wa Tilamaundee huku wakiongozwa na aliyekuwa mbunge wao Mzee Ray Mrope

Sunday, May 25, 2014

Mama Bishanga Amlilia Kuambiana

OHIO: USA, MAMA BISHANGA AMLILIA KUAMBIANA

Nimepokea kwa huzuni taarifa ya kifo cha msanii mwenzagu wa fani ya filamu marehemu Adamu Philip Kuambiana, ni pigo kubwa kwa tasnina yetu na kwa taifa pia kwa kuondokewa na mtaalamu mahiri kama yeye, namuombea usingizi wa milele wa amani.

Adamu alikuwa mtoto wa mwalimu Philip Kuambiana mwalimu wangu wa major yangu chuoni Theater Arts, alikuwa director na producer mkali sana. Na kama itakumbukwa nilihojiwa mwaka 2001 baada ya kupokea  Award ya The Best Actress wa mwaka wa 2001, nilieleza mengi pamoja na production tuliocheza  mbele ya wabunge na  Rais wa kwanza Mwl Julius Nyerere, Marehemu Mwalimu Philip kuambiana ndie aliidirect, na alisimamia Nyanja zote, mandhari, costumes, sound, na hata lebasi za ulibwende (wale tuliokuwa darasa moja mnaikumbuka hiyo?), na alikuwa very serious kazi inapoanza, alikuwa akitutania kila tunapoanza mazoezi kuwa kila mtu aende chooni kabisa kwani kazi ikianza ni moto moja kwa moja, kazi moja tu, na hakika matokeo ya production zake yalikuwa mazuri sana. Na ndio hapo nilimjua Adamu akiwa mdogo sana mwaka 1982-83.

Mwaka 2011 niliporudi tz kufunga ndoa ndipo nilipoonana tena na Adamu akiwa mkubwa kabisa, na tulipanga kuicheza tena jukwaani ile production ya mtihani wetu wa mwisho, alisema pamoja  kuwa alikuwa mdogo sana lakini anakumbuka ile production ya mfalme Odepasi (The King Odepus) kutoka kwenye kitabu cha Shake Spear, ambayo kwa kifupi mfalme Odepas alifungwa miguu na mikono kwenye mti na kupewa wafugaji wakamtupe mtoni akafe maji, Odepus alikuja kuwa mfalme baada ya miaka mingi, alimuua baba yake bila kujua kuwa ni baba yake na alimuoa mama yake na kuzaa nae watoto wawili bila kujua! ni production nzuri sana na ninasikitika kuwa Adamu amefarika na ndoto ya kuicheza hii production tena jukwaani sijui ndio vipi! Pamoja na yote namuombea Amani ya kudumu,

Mwisho nawapa pole kwa familia yake, na kwa taifa Zima.

 Bwana alitoa, Bwana ametwaa; Pumzika kwa Amani Adamu Philip Kuambiana.

Christina Innocent Marolen
Mama Bishanga
OHIO  

The Late Adam Kuambana

Friday, March 21, 2014

Mama Bishanga Asherekea Miaka Minne ya Ndoa

MAMA BISHANGA AMEREMETA/ 4th WEDDING ANNIVERSARY
 
Nawasalimu na kuwashukuru wote mlionitumia kadi, txt, na kunipigia simu kunipongeza na kunitakia heri ya kutimiza miaka minne ya ndoa yangu. Nimeona nitumie njia hii nzuri na rahisi kuwafikishia shukurani zangu na za mume wangu Mzee Marolen. Mungu ni mwema ametupa faraja amani na furaha ya kuungana kwetu sote tukiwa ni mara yetu ya pili kufunga ndoa. Kwa upande wangu sikuweza kufunga ndoa na mchumba wangu wa kwanza kwa tofauti ya dini alikuwa muislamu toka Tanga. Nilifunga ndoa mwaka 1978 na marehemu Isaya Namajojo alikuwa anafanya kazi mamlaka ya bandari Mtwara na alikuwa mcheza mpira wa timu ya Bandari Mtwara na timu ya taifa. Na mume wangu huko Johannesburg alifiwa na mke wake mwaka 2009 kwa matatizo kisukari, na tunamshukuru Mungu kwa kutuunganisha na kujenga ndoa yetu. 
 
Tunawashukuru wote watoto wetu Sizelina, Kilian na Hendrick (Kenny), Floronce, Lucy, Nuru, Ibrahim, Amri, Thato na Zinzi na wajukuu zetu, ndugu zetu, marafiki zetu na wasanii wenzengu toka Tanzania JB, Natasha, Monalisa, George/Tyson, Bishanga, Lulu, Wema na wengine wote tunawapenda sana. AND GOD BLESS YOU!
 
MAMA BISHANGA/ MRS MAROLEN
OHIO
USA

Friday, January 03, 2014

Salamu Za Mwaka Mpya Kutoka Kwa Mama Bishanga

HAPPY NEW YEAR FROM MAMA BISHANGA
 
Wapendwa nyumbani TZ natumia nafasi hii kuwatakia heri ya mwaka mpya 2014 uwe wa Baraka na mafanikio kwetu na taifa letu kwa jumla. Nilipenda kuja Tz lakini ndoa imenishika ilibidi mimi na mume wangu tupite juu kwa juu hadi JHB na kurudi Ohio kuchapa kazi, na hali  ya Ohio ndio kama mnavyoiona ni winter kali sana, lakini ndani tulijirusha kama kawaida na mwanangu Kilian na wajukuu Mariam na Lalai Kamota kama mnavyoona,
 
Mwaka uliopita umeisha salama salimini ila tumepoteza watu maarufu akiwemo Tata Mandela baba na babu wa Africa na Tabu ley gwiji katika fani muziki naupenda kule Masasi  mzee Bellim kulikuwa na ile kitu ya kuzungusha mkono na kupiga santuri mama zangu wakicheza na baba yangu aliupenda sana ukawa unaimbwa kila kona na kubakia kichwani kwangu hadi sasa,kwa heshima tuwaombee walale mahali pema peponi, na mwaka uliisha vizuri kwa amani kwa aslimia kubwa ni fahari yetu na haki yetu kudumisha amani na upendo kifamilia na kitaifa. NAWATAKIA KILA LA HERI 2014
 
CHRISTINA I MAROLEN
MAMA BISHANGA
OHIO


Mama Bishanga na Mwanae Kiliana na Wajukuu

Monday, July 22, 2013

Mama Bishanga Ampongeza Natasha!



Mimi mama Bishanga na mwanangu Kilian Kamota tunakupa hongera kwa kazi nzuri uliotimiza
ya kufunga ndoa nasi huku tulikuwa tunasherekea ndoa pia ya wa tz wenzetu siku hiyo.

Uliniahidi mwaka 2011nilipokuja TZ kufunga ndoa kuwa nawe utafanya hivyo. Umetimiza ahadi
ya Mungu ya kuungana mume na mke kuwa kitu kimoja halali. Mmependeza sana mdogo wangu
tunza mzee wako, mapenzi ya uzeeni matamu sana. Mpe raha mumeo.

Christina Innocent / Mama Bishanga

OHIO

USA

Wednesday, March 27, 2013

Mam Bishanga Asherekea Birthday Ohio

WAJUKUU WAMTAKIA MAMA BISHANGA HAPPY BIRTHDAY!




Wajukuu wa mama Bishanga toka Ohio ni Mariam na Lalaih ambao ni watoto wa Kilian Muya Kamota wanamkabidhi bibi yao zawadi ya keki ya birthday bibi yao na kumtakia maisha marefu ya furaha, amani, na maendeleo.



Wajukuu wa mama Bishanga tokaTanzania, Kilian au Mzungu na Mariam ambao ni watoto wa Hery au Kenny wa Mambo hayo, wana sema happy birthday bibi, sisi tumekununulia keki na pipi na biskuti lakini tumekula wenyewe kwakuwa uko mbali, tunakusubiri utuletee zawadi ya ice cream, na daftari na kalamu, tunakupenda sana our grandmom.

***************************************************************
Ujue Mama Bishanga ni Nani. - Nyota katika Usanii Tanzania


Kutoka DAILY NEWS - TANZANIA

Mama Bishanga: The actress who filled the ‘Bongowood’ vacuum
By Women Reporter, 19th January 2011

Most knew her as Mama Bishanga, the legendary film actress whose portrayal of an irksome Haya mum left many believing she was from Kagera region. Some hardly believed that in reality she was just playing a part and her real name is Christina Innocent.

But the charming lady is actually a Makua from Masasi, in Mtwara region. Her role as Mama Bishanga in the TV drama not only confirmed her as one of the country’s greatest actresses, but also a pioneer of sorts of the local film industry thay is also referred to as ‘Bongowood’ But the charming Christina Innocent Hatia is actually a Makua from Masasi, in Mtwara region. Her role as Mama Bishanga in the TV drama not only confirmed her as one of the country’s greatest actresses, but also a pioneer of sorts. 

With her screen ‘son’ Bishanga (Raymond Allen) and ‘hubby’ Mzee Kambaulaya (Barnabas Maro) and others in the cast capping it with excellent acting, the weekly ‘ Mambo Hayo’ TV drama series became ITV’s hottest program.

“When I started acting in the Mambo Hayo TV series in 1998 I was the first elderly woman actress then”, says Mama Bishanga, who is in her mid 50s now. “I am happy and proud to be the pioneering figure of older women actresses”.

She is sitting in front of me at the office, where she breezed in to pay a courtesy call, about a week since she got back from the United States of America where she now resides, pursuing a degree at the Howard University in Washington DC. She also teaches Kiswahili part time there.
With her is Kenny, her actor son who has just completed University and contemplating going back into acting, after a seven year hiatus. He started acting almost a year earlier, and when his mother joined him in the Mambo Hayo series, the drama became an all time hit at the ITV station.

It was not by accident that Mama Bishanga became an actress. In point of fact, she is one of the few professional actresses who made their names on the silver screen. Thanks to the Butimba Teachers College where she attained an advanced diploma in theatre and fine art, majoring in theatre. That was between 1981 to 83.

Mama Bishanga is nostalgic as she recalls a play called ‘Odupus the King’ that she and her colleagues performed at the Bagamoyo college of art in front of then President Mwalimu Julius Nyerere and Members of Parliament who had met at the historical town and requested for a treat.

“That was the first ever stage play and the longest because it lasted for about 240 minutes and Mwalimu and the MPs were excited about it”, Mama Bishanga, who played queen, remembers. One Lwilomba played King.

“Mwalimu was exceptionally happy that he made on-the-spot recommendation that the whole class should be positively considered in the final exams because he regarded our performance as a sitting by itself”.

After completing her studies at Butimba, she went to work as a language and arts teacher at the Tabora Secretarial College in Tabora in 1983, six years later she left and went on to become an administrative officer at the National Arts Council (BASATA). In 1992 she went to Swaziland where she studied administration, remembering Kassim Mtawa and Blandina Mhina as some of her fellow students in the tiny South African Kingdom.

Upon her return to Tanzania in 1993 she went back to work at the Ministry of Science, technology and Higher learning. Five years later she went into acting as one of the ‘Mambo Hayo’ series cast. The rest, as they say, is history.

Mama Bishanga maintains that she went into acting due to a number of reasons, apart from feeling the need to utilizing her knowledge as an actress to the hilt.

“During the early days of TV drama series in the country, most actresses were just out-of-school youngsters. There were no older women. I went in with the objective of filling the vacuum. I guess I succeeded “, says Mama Bishanga with a radiant smile on her pretty face.

Indeed, she did succeed in engaging elderly actresses on TV and later on film, because soon after a host of other older women came into the picture, with Mama Mjatta becoming the second elderly actress to become a screen star alongside the youth crop of Waridi, Mona Lisa, Aisha and others.

In 2001 Mama Bishanga was awarded as the best Tanzania actress of the year by M-Net Africa, and she went on to win many a fan with sterling performances before ITV stopped showing ‘Mambo Hayo’ for reasons that have yet to be given.

Coincidently, Tanzania had on that year submitted MAANGAMIZI – THE ANCIENT ONE as its film entry in the Foreign Language Film category for the 74th Academy Awards.

The film, Produced by the Chairman of ZIFF Dr Martin Mhando, competed with foreign language films from 50 other countries around the world, the largest group ever in this category for the Academy. The only other African country in the running was Algeria and Tanzania remained the only sub-Saharan African country in the 2001 competition.

Maangamizi – The Ancient One represented the first ever entry by Tanzania. The film was selected by a group of film, television and theater professionals and was released in Tanzania the last week of October 2001, and was received by excited local audiences.

Yearning for further education despite her age, Mama Bishanga flew to the US in 2007 where she is now studying at the Howard University, where she also moonlights as a Kiswahili teacher. In her spare time she also studies film. She says she is too busy with college to continue acting.

“But I am closely following the film industry not only in Tanzania but also the whole of Africa, especially Western Africa, where they enjoy notable successes.

“The Tanzania film industry is vibrant but still at its embryonic stage. Producers are really doing a good job down here but they lack a lot of important elements that can go a long way into improving the quality and standards of local films.

“Tanzania need professionalism in all spheres of film production; from excellent lighting and sound and fitting location environments to serious casting, make-up and wardrobe”, says Mama Bishanga, who plans to meet with film stakeholders and try to encourage them to be more professional.

Of course, she plans to come back to Tanzania in the near future and show how things are done. For now she has great regard to the entrepreneurship spirit she has seen in Tanzanian women, calling them to try the film industry as well.

“Many women in other parts of the world engage themselves in the film industry which is one of the most lucrative businesses alongside music.

“One does not have to end up being an actress. There are plenty of avenues in this industry that is lacking real professional and passionate players.

“I guess women stand a better chance of turning the tables around if they choose to. Also remember, age ain’t nothing but a number. You know what-am-saying....?

"Therefore I call upon all women, irrespective of age, to enter into the film industry and become silver screen entrepreneurs.

“They wont regret that decision and I know what I am talking about”, concludes Mama Bishanga, as she gathers her things to rush to MAELEZO where she plans to book the auditorium for her press conference next Monday.

Monday, April 09, 2012

Mama Bishanga na Ohio Wamlilia Kanumba

MAMA BISHANGA NA OHIO WAMLILIA KANUMBA

Nimeguswa na kuumizwa sana na msiba  wa ghafla wa msanii wenzangu wa tasnia ya filamu,  Steve Kanumba, ndugu yetu, kijana wetu, rafiki yetu na mtanzania mwenzetu alietuachia pengo lisilozibika. Itatuchukua muda mrefu sana kusahau msiba huu wa taifa zima kutoka na umahiri wake, juhudi zake na kazi nzuri alizozifanya kwa kipindi kifupi cha uhai wake. 

Nachukua nafasi hii pia kuwapa pole wazazi wake, mimi kama mzazi niko nanyi katika kipindi hiki kigumu sana, nimekuwa nawakumbuka sana katika sala tangu jana nilipopata habari hizi. Poleni sana.

STEVE TULIKUPENDA, TUNAKUPENDA NA TUTAENDELEA KUKUPENDA, MUNGU AKUPOEE KWA AMANI NA MWANGA WA MILELE AKUANGAZIE KATIKA JINA LA YESU KRISTO BWANA NA MWOKOZI WETU, AMEN

MRS CHRISTINA INNOECENT MAROLEN
MAMA BISHANGA
OHIO/ USA

Wednesday, June 08, 2011

Mama Bishanga Afiwa na Baba Yake Mzazi

MAMA BISHANGA AFIWA NA BABA YAKE

Leo tunasikitika kuwaarifu kuwa baba mzazi wa msanii maarufu katika fani ya filamu Mrs Christina Innocent Marolen, Mama Bishanga, Mzee Isaya Innocent Hatia (mtoto wa Mwenye Hatia Chifu wa Wamakua, Ashinnahatia) amefariki dunia huko Ndanda hospital masasi jana.

Mzee Hatia alikuwa na miaka themanini na mbili, ameacha mke Mwalimu Agnes Hatia, watoto saba ambao ni Mama Bishanga, na wadogo zake Geofrey anayeishi Namibia, Mwalimu Marck wa Azania Sekondari, Bernadeta, Isaya anayeishi Finland, Constancia na Oscar. Pia ameacha wajukuu na vitukuu.

Mzee Hatia atakumbukwa kwa kuwa mmoja wa wafanyakazi bora na wa muda mrefu wa kampuni ya Posta na simu tangu enzi za East Community huko Nairobi na Mombasa, na hapa nchini Dae-E.s-salaam, Dodoma, Tabora nk

Mazishi yatafanyika Ndanda Masasi ijumaa.

Thursday, April 28, 2011

Mama Bishanga Ameremeta!!!

Bwana na Bibi Marolen baada ya kufunga ndoaKwa mila ya waMakua kwa wanawake hulala chini na bibi arusi kupita juu yao mpaka kwenye kiti atapokaa.
Familia ya Hatia, familia ya Mrope, na familia ya Kamota wakipiga picha ya pamoja na wanaarusi



Wadau, Mama Bishanga jina halisi Christina Innocent Hatia amefunga ndoa hivi karibuni huko Dar es Salaam, Tanzania. Bwana harusi ni Mr. Marolen kutoka Afrika Kusini.

Arusi ilifanyika siku ya tarahe 5 Machi, 2011 katika knaisa la St. Peters Oyster Bay. Reception ilifanyika Peacock Hotel.

Nawatakia maisha mema ya ndoa.