Thursday, September 06, 2007

Mawaidha kuhusu Ndoa - Sehemu ya Kwanza

Mwezi Julai nilitoa blogu kuhusu maswali ya kuuliza kabla ya kufunga ndoa. Sasa kwa bahati nimeona hii somo iliyoandikwa kwa kiswahili kuhusu maisha ya ndoa. Kwa kweli hii ni mambo ya wakubwa na kuna mambo nyeti. Lakini ni somo nzuri kwa wanajiandaa kufunga ndoa.

Somo hii imetayarishwa na Lazarus na Gloria Mbilinyi wa Kimara Dar es Salaam.

Kama unataka kuwaandikia e-mail yao ni:
lazarusmbilinyi@gmail.com au mbilinyilazaro@hotmail.com au tuma barua TAG- KIMARA Box 7725, Dar es Salaam Tanzania .
*********************************************************************************

NDOA NA NYUMBA

(Sehemu ya Kwanza)

UTANGULIZI

Somo la ndoa na nyumba ni somo ambalo ni gumu kufundisha kwa sababu halijapata mtu ambaye amewahi kufuzu mambo ya ndoa kwani mtu atafauru katika nyanja moja na kuwa hafifu katika nyanja nyingine.

Kwa hiyo wanandoa wanavyoendelea basi huongeza ujuzi mbalimbali na kufika mahali ambapo wanataka kwa kuzidi kujifunza zaidi. Mambo ya kuzinngatia katika somo la ndoa ni:-Kila mshiriki kuondoa aibu na woga usio na msingiKukubali kuwa hajui kwa lile usilolijua na kuwa tayari kupokea na kulifanyia mazoezi bila aibu.

KWANINI KUJIFUNZA NDOA NA NYUMBA

(i) Nyumba iwe mahali pa zuri pa kuishi
(ii) Tujue kwamba Mungu ndiye mwanzilishi na mtawala wa ndoa na nyumba

(iii) Kuondoa hofu na miiko ya kikabila ambayo imekuwa moja wapo ya vikwazo vya ndoa

(iv) Kurekebisha hitilafu katika ndoa

(v) Tuweze kuwafundisha wengine (walioana au wanaotarajia) kuhusu wajibu ulio mbele yao. Vijana wawe na uhakika siyo kubahatisha

NDOA NA NYUMBA

NDOA - Ndoa na iheshimiwe na watu wote na malazi yawe safi. (Ebr. 13:4 Kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu) Ni mtu mume na mtu mke walioamua kuishi pamoja kama mtu na mkewe wakiwa na kibali cha wazazi na Kanisa - hivyo ndoa ni fungamano.

NYUMBA - Nyumba si jengo la kuishi Joshua 24:15, Mith 14:1

NYUMBA NI:-

(a) Ni mahali ambapo mke na mume wataishi kwa kupendana, kuheshimiana na kuaminiana

(b) Ni mahali ambapo fedha siyo muhimu, kutoa pasipo kupokea. Ebr 13:5

(c) Ni mahali pa pumziko na kimbilio la amani unapokuwa umekata tamaa

(d) Ni mahali ambapo joto La moto wa upendo, mwangaza wa macho ya furaha, huruma na utii vinatawala

(e) Ni kanisa na shule za kwanza kwa watoto kujifunza

(f) Ni mahali ambapo ulimwengu huangalia uhusiano wa kanisa na Kristo
MSINGI (KANUNI) WA NDOA NA NYUMBA.

Mungu ndiye mwanzilishi wa ndoa na nyumba (Zab 127:1) na ndiye aliyeweka utashi (tamaa) wa kuoana ndani yetu

(a) Wazo la mke na mume ni wazo la Mungu - Mwanz 1: 27 uumbaji haukukamilika mpaka mwanamke alipoumbwa. Na aliwaumba kwa tofauti ambazo ndiyo kivutio kati yao.

(b) Mungu alitengeneza ndoa ili atatue tatizo la kwanza la mtu UPWEKE.

Mwanamke hakuumbwa awe mtumwa bali msaidizi Mwanz 2:18

(c) Ndoa ilipangwa na Mungu kuleta furaha sio huzuni. Aliweka raha zote ndani ya watu ili pawepo na upendo msisimuko na utoshelevu. Adamu alishangilia mwanamke Mwanz 2:23, Mith 18:22 Mwanmke - Laini/soft (kiebrania)

Ndoa lazima ianze na kuacha.

- Kuacha haina maana kutokujali bali ni kujitoa zaidi kwa mkeo au mumeo ( pamoja na huduma za Mungu ratiba ya kupendezesha mkeo/mumeo 1Kor 7:32 35) baadhi ya wainjilisti hujisahau\

- Kuacha kunawahusu wote mke/mume Zab 45:10,11 Mwanz 2:24 (Mwanamke kwenda kwao kila leo ni dalili kuwa huko aliko kuna shida)

- Mnatakiwa kuacha mambo yenu ya zamani mliyoyazoea kama vile, kutegemea tena wazazi, wazazi wa upande wowote wasiruhusiwe kuingilia maisha ya mmoja wenuBaba/mama mkwe huchonganisha na baadae hujifanya waamuziHumunyanyasa sana mkwe wao wakimwona kama mtu aliyekuja kufilisi mtoto wao na kuwa ameolewa kutokana na shida za za nyumbani kwao

-Kuendekeza ndugu (shemeji/wifi) kuachwe. Mara nyingi nao hufanya pia wamemwoa, hivyo hutoa amri za kipuuzi na hata kutumia vitu bila kibali cha mke wa kaka yao na akifa wao hufurahia mali. Mlinde mke wako kwa kila baya linalojitokeza.

- Shughulki za kazi (ofisini, kanisani, rafiki nk) visiwe muhimu kuliko ndoa.

- Hapa yatupasa kuwa na kiasi, asiye wajali wa kwao ni mbaya kuliko asiyeamini.

NDOA INAHITAJI KUAMBATANA KATI YA MUME NA MKE (Mwanz 2:24)

Ni kuungana (kushikamana) kiasi kwamba kutenganisha kutaleta madhara

- Mnaunganishwa katika nyanja zoteza kiakili, kimwili na kufikiria

- Katika kufanya mapenzi msiwe na mipaka mmoja akimtaka mwenzake basi pasiwepo na kikwazo. (1Kor 7: 3-5) kushirikiana katika vitu vya dunia mfano kucheka pamoja na kulia pamoja na kula pamoja kutembea pamoja.

- Mila za makabila mengine haziruhusu wanawake kula na wanaume

- lakini kwa mwanamke uliyeokoka kula na mumeo na oga na mumeo

- Iwapo mnalala pamoja mkiwa uchiiweje mpeane zamu kwenda kuoga?

- Mwendapo mahali usimtangulize au kumwacha mwenzako tembea bega kwa bega na mshikane mikono mkiongea

- Kiroho manaomba pamoja mkiombeana na kutiana moyo

- Kimapato msihirikiane na mawasiliano yawe mazuri, mpatapo mshahara kaeni pamoja mtoe fungu la kumi kasha mworodheshe mahitaji yenu na kupangia matumizi.

- Epuka kununu a vitu vya nje ya bajeti

- Mara nyingi anguko la kwenye uzinzi hutokana na kutokuambatana Mungu hapendi kuachana Malaki 2: 1 5

KUMBUKA KUWA MKEO:

Ametokana na ubavu - ili awe karibu nawe

Ametoka karibu na moyo - ili apendwe na wewe

Ametoka chini ya mkono - ili apate ulinzi wako.

SABABU YA KUOA NA KUOLEWA

1. Kuondoa upweke , umimi

2. Kupata raha (Ruth 1:9, 3:1, kumb 24:5) hapa biblia huzungumzia raha ya mke lakini pia mume hupata raha (kufurahishana)

a. Ubinafsi wa wanaume katika tendo la ndoa unasababisha raha inayotarajiwa sipatikane. Hawajali utoshelevu wa wake zao, kwa hali hiyo wake wanajiona kama vile wanatumiwa kama vyombo vya kutimizia tamaa za wanaume, kwa hali ya kawaida mume aweza kuridhika kwa muda usiozidi dakika moja lakini mwanamke anahitaji saa moja na zaidi ili atosheke.

b. Ubinafsi wa mke kumgomea mumewe akidhani kwamba ametosheka au hata kabla ya tendo la ndoa huondoa raha iliyotarajiwa

c. Hasira ya mchana iishie mlangoni muingiapo chumbani ili msiikose rahad. Mume na mke mtofautishe baina ya kupenda, kutii na kuheshimu

- Heshima muuache sebuleni, chumbani muingie na upendo, utii na uhuru

- Wengi kwa kuendekeza heshima wamejikuta wanang'ang'ania staili moja ya mke kulala chali (kifo cha mende) aikiogopa kuonekana ni muhuni akidai mtindo mwingine. Kwa kawaida kila mtindo una raha yake. Uoga huo ndiyo chanzo cha kuwa na wapenzi nje ya ndoa ili kuziba mapungufu ya ndani.

- Hakuna awezaye kumfurahisha/kumfundisha ila mumewe/mkewe tu

- Mke ni vibaya sana kuogopa kumuomba mumeo tendo la ndoa.

Ona Malaya anavyochangamkia mali isiyo yake (Mith 7: 4- 23)

JINSI GANI MUME AFANIKISHE RAHA YA MKEWE

Mambo yafuatayo ni muhimu

(d) Mawasiliano mazuri kati ya mume na mke tangu asubuhi hadi jioni.

(e) Mume na mke wajiandae

- Kwa kula chakula cha kutosha na cha kutia nguvu

- Kazi za mchana zisiwe nzito kiasi cha kuwaacha hoi na kuishia kulala.

-Fanya usafi, kuoga vizuri, kusukutua kwa dawa ili kuondoa harufu kinywani

-Kama hakuna umuhimu msichelewe kulala ili mpate muda mwingi wa kuongea na kucheza faragha (ukubwa wenu muuvue wakati huo)

- Mke awe amejipamba mapema ili amvutie mumewe (mume huvutiwa sana na kuona)

MUME AMWANDAE MKEWE IFUATAVYO

Kwa masimulizi mazuri na ucheshi (mwanamke yupo makini sana na yanayotamkwa na mumewe) matamshi makali humkatisha na kumshusha hamu yake

-Kupapasapapasa juu ya mwili wake bila ya kubagua

- kama hufanyi atakavyo ni vyema akuongoze yeye mwenyewe anapotaka mshike. Iwapo hawezi kusema atatumia vitendo. Kila utakachoutendewe basi mtendee mwenzako. Mume usione kinyaa kumshika mkeo zile sehemu nyeti na kuingiza vidole vyako pole pole na kuvitembeza humo, na kushika kinena na kuchezea kisimi huku ukimbusu.

Mume usiwe na haraka kumuingilia mkeo, subiri hadi amesisimuka kiasi cha kutosha kama ifuatavyo:

-(a) Joto la mwili wa mke hupanda na kutelemka mwili mzima na kujitupa tupa mwilini mwako kwa mahangaiko ya nyege.

(b) Kuta za ndani za kuma na zile kuta za pembeni huumuka kama andazi lililokolea hamila na kwa wengine kisimi hudinda kama mboo

(c) Uke utatoa majimaji kulainisha maingiliano na uume uingie kwa urahisi

(d) Mke atashika uume na kujiweka sawa kujiingiza ukeni kwake mwenyewe

(e) Wakati huu sasa mkeo atapumua kwa haraka, mapigo ya moyo yataongezeka, kama mlikuwa mnaongea atanyamaza kimya na kuanza kutoa sauti ya kuhema na mwisho akikaribia utoshelevu hutoa sauti ya kulia. Mume usisahau kunyonya matiti hata yakiwa malapa, hussisimua sana pamoja na kumbusu fanya kama unamg'ata shingoni.

(f) Wakati tendo la ndoa linaendelea msizime taa hadi limekamilika na mtazame usoni bila kuoneana aibu (Wimb 7: 1-6)

(g) Endapo mume utamtangulia mkeo, usichomoe mboo kumani endelea kunyonya matiti na kumshikashika mkeo(h) Ili kuendeleza msisimuko wa mkeo, uume ukiwa bado imara endelea mpaka mkeo atosheke ni vyema mkeo akiwa tayari mumalize pamoja

(i) Mume aacha uume ndani ya kuma mpaka akuambie mkeo kutoa kwani, utamu wake hauishi haraka kama wa kwako mwanaume. Kwa hiyo haraka ya kuchomoa ni chukizo na huharibu raha iliyokuwa imefikiwa.Mapenzi hayana muda (mchana, jioni, usiku wa manane nk) pia hayana kikomo, mpaka mtosheke - ni vizuri kutumia kioo kujiangalia mnavyofanya tendo la ndoa. Hii ni kumharakisha mwanamke kufikia kileleni.
3. Kupata moto (joto) kuinuana na kusaaidiana 1Falm 1: 1- 4 Muh 4: 9-11

4. Kupata uzao - watoto ni baraka, na zawadi kwa wazazi Mwanz 4: 1, 9: 1, 1: 28

10 comments:

Anonymous said...

Inatisha sana niliyonukuu sentensi niliyonukuu hapa inaonyesha huyo mke ni wa mtu maskini.

Eti inasema "Amwage mumewe akimtakia kazi njema baada ya kumuandalia
Maji ya kuoga"

Bafu siku hizi ni Self Contained zinatoa maji baridi na moto na huhitaji mtu wa kumwandalia maji mtu mwingine.

Wake wa watu maskini wana shida sana.

Mimi ndiyo maana Chemi nilikataa kuolewa na mtu maskini kukataa mambo kama hayo.

Anonymous said...

Biblia????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????

Anonymous said...

Da Chemi, nimefurahi sana kukuta somo la namna hii kwenye blogu yako. Kwani vitu kama hivi ni vya muhimu sana katika maisha ya familia hivyo ni vizuri vikawekwa wazi na kila mtu akajifunza jinsi ya kuishi na familia yake kwa maisha ya raha. Ningefurahi sana kama wangejitokeza watu na kuhakikisha kwamba taarifa kama hizi zinawafikia walio wengi hasa wale wasio na access ya network ili angalau wajue nini la kufanya pindi waanzapo maisha ya kujitegemea katika hatua ya mwanzo ya familia changa. Vitabu vidogo vingekuwa suluhisho, maana vingewafikia wengi hasa waishi vijijini na wale wasiojua kutumia kompyuta. Imani.

Anonymous said...

Dada chemi sasa mbona umesahau swala zima la mwanaume pia awe na ujuzi mzurii wa kumfikisha mkewe wakati wa mechi yao ya bedball.au unaonaje hiyo?

Anonymous said...

jamani nyie semeni yote ,jambo moja tu kwenye ndoa ni UVUMILIVU.BWANA WAWEZA TIMIZA YOTE LAKINI BADO MWANAUME AKAKUCHOKA TU,KUVUMILIANA TU ...........

Jacqueline Ngowi said...

Hongera sana Kaka Mbilinyi na Mkeo Dada Gloryia. I known this Couple.......Honestly ni mfano wa kuigwa
Bwana Awabariki Sana

Jacqueline Ngowi said...

Hongereni sana Mr. & Mrs. Mbilinyi
BWANA Awabariki

Anonymous said...

Jamani mi naogopa kumwambia mume wangu kama nikiwa nahitaji tendo la ndoa mpaka anianze yeye,nifanyeje?

Anonymous said...

Muonyeshe matendo ya kutaka mwanzo kabla ya yeye kukuanza....

Anonymous said...

Bwana asifiwe. Sikiliza maneno yangu. Usiangalie matendo. Mwakalukwa.