Showing posts with label Kisutu Court. Show all posts
Showing posts with label Kisutu Court. Show all posts

Thursday, January 01, 2015

Mhabusu Auwawa Mahakama ya Kisutu

MAHABUSU AUWAWA KWA  RISASI MAHAKAMA YA KISUTU AKIJARIBU KUTOROKA

Na Happiness Katabazi

JESHI la Magereza limefanikiwa kumdhibiti Mahabusu  wa Kesi ya dawa za kulevya ambaye ni Raia wa Sieralioni,  Abdul Koroma (33) asitoroke chini ya Ulinzi wa Askari Magereza ndani  Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkazi Kisutu Dar es Salaam, asitoroke chini ya Ulinzi  baada ya kumtwanga risasi na kumuua papo hapo.

Wakizungumza na mwandishi wa Habari hizi baadhi ya wanausalama waliopangwa kulinda Usalama Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa Masharti ya kutotajwa Majina Yao kwa Madai wao siyo wasemaji wa majeshi Yao wakisema mtuhumiwa ambaye anashitakiwa kwa makosa ya kuingiza nchini dawa za kulevya aina ya Heroin Zenye uzito wa Gramu 1229 na zenye thamani ya Zaidi ya Sh.Milioni 61 iliyopo mbele ya Hakimu Mkazi Waliarwande Lema alistahili kufanyiwa hicho alichofanyiwa.

Walisema Asubuhi marehemu Huyo ambaye ni mahabusu aliletwa na mahabusu wenzake na Askari Magereza na Kisha kufikishwa Katika mahabusu ya Mahakama hiyo mtuhumiwa aliomba apelekwe chooni kujisadia lakini ghafla mtuhumiwa akaanza jaribio la kuparamia ukuta akimbie ndiyo Askari waliokuwa akimsikindikiza chooni wakafyatua risasi hewani ili kumtaka aache ili jaribio lake lakini Inadaiwa Koroma aliendelea na jaribio lake.

" Ndipo itabidi mmoja wa Askari Magereza 'ameshone risasi' yaani amefyatulie risasi Koroma ambayo ilimpata na kumsababishia mauti papo hapo ....na baada ya Koroma kupekuliwa wanausalama Hao walipokuwa soski walikuta ndani ya soksi alilovaa kuna kikaratasi kilichochorwa ramani na namba za simu za watu wa kumpokea haoa Dar es Salaam" kilisema chanzo changu.

Tayari mwili wa Koroma ambaye alikuwa akikabiliwa na Kesi yake P121/2013 umeishaondolewa Katika eneo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu umepelekwa kuinadi wa Katika Hospitali ya Taifa ya Mhimbili.

Chanzo: Facebook: Happy Katabazi
Disemba 31 Mwaka 2014.


Kisutu Court Dar es Salaam


Tuesday, January 29, 2013

Hatimaye Lulu Apata Dhamana

Mcheza sinema, Elizabeth Michael, aka. Lulu amepata dhamana leo. Lulu alikaa rumande siku 274 kwa tuhumu za kumwua mpenzi wake, mcheza sinema maarufu, Steven Kanumba.



 Picha hizi zimetoka Millardayo.com

Lulu akilia machozi ya furaha baada ya kuaachiwa huru kwa dhamana

Lulu na mama yake mzazi wakilia baada ya kukutana nje ya Mahakama, Lulu amechiwa huru na Mahakama leo january 29 2013 mchana, pembeni ni mwigizaji Dr. Cheni ambae amekua karibu na familia ya Lulu kwa muda mrefu sana.


Taarifa ya habari ya saa saba machana ( Jumatatu 28/1/13)  kupitia TBC imesema:


Msanii wa filamu Elizabeth Michel, maaruf kama Lulu, anayekabiliwa na shitaka la tuhuma za mauaji ya aliyekuwa msanii mwenzake, Steven Kanumba, leo amepewa dhamana na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Dar es Salaam.

Masharti ya dhamana hiyo ni pamoja na:

- Kuwa na wadhamini wawili kwa dhamana ya Shilingi milioni 20 kila mmoja

- Kukabidhi pasi yake ya kusafiria kwa Msajili wa Mahakama

- Kuripoti Mahakamani kila tarehe Mosi ya kila mwezi.

- Marufuku kusafiri nje ya nchi.

Taarifa kwa kina kama ilivyowandikwa na Happiness Katabazi Happiness Katabazi

HATIMAYE Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imempatia masharti matano ya kupata dhamana kwa msanii wa filamu nchini Elizabeth Michael ‘Lulu’, anayekabiliwa na kesi ya kuua bila kukusudia aliyekuwa msanii mwenzake marehemu Steven Kanumba.

Masharti hayo yaliyolewa jana na Jaji Zainabu Mruke muda mfupi baada ya mawakili wa Lulu, Peter Kibatara, Kennedy Fungamtama na Fulgence Massawe kuiomba mahakama hiyo impatie dhamana mshtakiwa huyo ambaye anasota rumande tangu April mwaka jana ambapo walieleza kuwa ombi la dhamana wameliwasilisha chini ya kifungu cha 148(1) ,(2) Cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002 .

Jaji Mruke alisema ili mahakama impatie dhamana ni lazima asalimishe kwa Msajili wa mahakama hiyo hati ya kusafiria, kutotoka nje ya Dar es Salaam bila ruhusa ya mahakama, kuripoti kwa msajili kila mwezi, kuwa na wadhamini wawili ambao ni watumishi wa serikali ambao watasaini bondi ya Sh. milioni 20 kila mmoja.

Baada ya jaji huyo kutangaza masharti hayo Lulu na wakili wake walitoka nje ya ukumbi uliokuwa ukiendeshwa kwa shauri hilo kwa ajili ya kwenda kwa msajili kutimiza masharti hayo lakini kwa bahati mbaya Msajili hakuwepo ofisini na hivyo kufanya Lulu kurudishwa rumande hadi leo atakapoletwa kwa ajili ya kujatimiza masharti hayo mbele ya Msajili wa mahakama hiyo.

Kufuatia mahakama hiyo kumpatia masharti ya dhamana Lulu kutoka na ombi lake Na.125/2012 la kuomba mahakama hiyo impatie dhamana, bado kesi ya msingi inayomkabili Lulu ambayo ni ya kuua bila kukusudia haijapangiwa jaji wala tarehe ya kuanza kusikilizwa.

Desemba 21 mwaka jana, Hakimu Mkazi Christine Mbando wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu aliifunga kesi ya kuua bila kukusudia Lulu na kuiamishia rasmi kesi hiyo katika Mahakama Kuu, na uamuzi huo wa mahakama ulitokana na upande wa Jamhuri kumsomea maelezo ya kesi yake kwa kina mshtakiwa huyo na kuieleza mahakama kuwa wanakusudia kuleta jumla ya mashahidi tisa.

Wednesday, June 13, 2012

Mahakama Waendelea Kujadili Umri wa Lulu!

Wadau, Cheti cha Kuzaliwa Kinatosha kuthibiti umri wa mtu. Ila katika kesi hii, Lulu alikwishafanya party ya kutimiza 18, na pia alikuwa anawaambia wanahabari katika mahojiano kuwa yeye ni 18. Ndo matokeo ya kutaka kuwa mkubwa kabla ya siku zako!  Ukubwa amepata!

******************************************************


Elizabeth Michael Kimemeta aka. Lulu ana miaka mingapi? 17 au 18?
 Kutoka The Citizen

Court orders Lulu’s lawyers to Provide proof on her Age


Monday, 11 June 2012
By Rosina John

The Citizen Correspondent

Dar es Salaam. The High Court in Dar es Salaam yesterday ordered defence lawyers of movie actress Elizabeth Michael alias Lulu to present documents supporting their claim she is under the age of 18.Judge Fauz Twaibu ordered the defence lawyers to present the evidence and supporting documents by way of affidavit on June 13.

Lulu is charged at the Kisutu Resident Magistrate’s Court with murdering local movie star Steven Kanumba on April 7, this year, at Sinza Vatican.

Defence counsel led by advocate Peter Kibatala filed the application at the High Court seeking the determination of the accused’s age. The lawyers stated that Lulu has not attained the age of 18 years to merit prosecution in an adult court.

The application by Mr Kibatara followed a decision by the lower court to turn down their request to transfer the murder case to a juvenile court on the ground that the lower court lacked jurisdiction to entertain the matter. However, in his ruling yesterday, Judge Twaib quashed and set aside the decision by the resident magistrate’s court to refuse to entertain the application, saying it was an error in law and an abdication of duty.

“Consequently, I hold that the lower court was wrong to refuse to entertain the application, thinking that such an enquiry could only be done by this court.

I quash and set aside the decision of the Kisutu Court,” the judge ruled.

The judge said that, considering the seriousness of the charge facing the applicant and the urgency of determining whether or not the applicant is entitled to the benefits of the Child Act and in the interest of justice, the court is invoking its supervisory powers under Section 44 of the Magistrate’s Court Act and shall proceed to determine the correct age of the applicant in terms of Section 113 of the Child Act.

The judge said that the nature and seriousness of the charge facing the applicant, the lack of any possibility for securing bail, during the pendency of the charge and undisputed urgency of the matter require that the controversy about her age be determined the soonest.

He further ruled that, in the meantime, the proceedings of the murder case at the lower court should stay, pending determination of the applicant’s age in the High Court. The judge ordered the applicant’s counsel to produce evidence on their client’s age on June 13 while prosecution required submitting their reply on June 20 while the hearing would be on June 25.

Tuesday, June 05, 2012

Lulu Mahakamani Jana!

Lulu mahakamani Kisutu jana:


Lulu akisindikizwa na Askari magereza

Kutoka The Citizen:


Lulu Case Adjourned to June 18
Monday, 04 June 2012 22:17
By Rosina John
The Citizen Correspondent
Dar es Salaam. The Kisutu Resident Magistrate’s Court adjourned a murder case facing local film actress Elizabeth Michael alias Lulu to June 18, this year.Lulu is charged with murdering local movie star Steven Kanumba on April 7, this year, at Sinza Vatican.

The case was yesterday brought before Resident Magistrate Augustina Mmbando for mention, with the prosecution informing the court that investigations were still going on.“The case is before the court today for mention because the investigations are not complete,” said State Attorney Peter Sekwao.

Sekwao asked the court to set another date for mentioning the case and magistrate Mmbado adjourned it to June 18, this year.While the case continues at the Kisutu Court, the High Court will on June 11 this year rule on an application by the accused seeking the court’s order to determine her age.Advocate Peter Kibatala filed the application after a lower court turned down their request to transfer the case to a juvenile court.

According to the lawyers for the accused, she has not attained the age of 18 years to merit prosecution in an adults’ court. However, the lower court said that it lacked jurisdiction to entertain any application because the charge before it involved murder.

But in his application Mr Kibatala stated that the lower court has power to investigate the age of the accused according to section 113 of the Child Act.The advocate wants the court to take consideration of her age to maintain Lulu’s basic rights as a child, according to section 4(2) of the Child Act.

***********************************************************

Global Publishers wanasema Mimba ya Lulu Imetoka!
 

Kutoka Global Publishers:
 
Na Shakoor Jongo
ULE ujauzito wa miezi mitatu wa mwigizaji nyota wa sinema Bongo ambaye kwa sasa yuko nyuma ya nondo za Gereza la Segerea, Dar es Salaam kwa kesi ya kifo cha Steven Kanumba, Elizabeth Michael 'Lulu' umedaiwa kuchoropoka, Ijumaa Wikienda lina cha kushika mkononi.
CHANZO CHAFUNGUKA
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika ambacho ni makini, sababu kubwa ya mimba hiyo kutoka ni kutunga nje ya mfuko wa uzazi hali ambayo ingemletea matatizo Lulu.
“Nikwambie kitu, unajua wengi wanaamini Lulu ana mimba na hivi karibuini iliandikwa imefikisha miezi mitatu, ilikuwa sahihi, lakini ukweli ni kwamba kwa sasa imetoka.
“Sababu kubwa ni kwamba afya yake ilidorora, ukiachia ule ugonjwa wa U.T.I alioripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kwamba anao, lakini kingine ni kuwa iligundulika ujazuito wake ulitunga nje ya mfuko wa uzazi ikawa haina jinsi, ikabidi kutolewa na kusafishwa,” kilisema chanzo hicho bila kuainisha tukio hilo lilitokea lini.
ETI NI MIMBA YA TATU
Kikiendelea kuzungumza kwa umakini mkubwa, chanzo chetu kilidai kuwa eti ujauzito huo ni wa tatu kuchoropoka kwa msanii huyo.
“Unajua huu unakuwa ujauzito wa tatu kwa Lulu kutoka. Kwa kweli kama si hivyo angekuwa na mtoto,” kilisema chanzo bila kuweka wazi nyingine mbili zilitoka kwa matatizo gani.
“Kuna wakati Lulu alikwenda China, aliporudi alikuwa na ujauzito, lakini nao ulitoka, inaonekana ana matatizo kidogo kwenye upande wa kizazi,” kilidai chanzo hicho.
Kikaendelea: “Baada ya hapo, haukupita muda mrefu, akanasa nyingine ya mwanamuziki mmoja wa Bongo Fleva, pia hiyo nayo ikaja kutoka ya tatu ni hii ya Kanumba.”
MAMA LULU
Katika kupata mzani wa habari hiyo, Ijumaa Wikienda lilimsaka mama Lulu, Lucresia Karugila ili kusikia kutoka kwake lakini hakupatikana hewani kutokana na kuzima simu.
USHUSHUSHU GEREZANI
Ijumaa Wikienda lilituma ‘mpelelezi’ wake kwenye Gereza la Segerea ili kukutana na Lulu na kuzungumza naye kuhusu madai ya mimba yake kuchoropoka.
Ilikuwa kazi kubwa kumpata ‘laivu’ nyota huyo kutokana na ukweli kwamba kuna watu maalum watatu ambao ndiyo wenye ruhusa ya kumwona mtuhumiwa huyo, mbali na hao marufuku kwa wengine.
Hata hivyo, ‘shushushu’ huyo alifanikiwa kupata fursa ya kumjulia hali mahabusu mwingine aliyepo kwenye gereza hilo na ndipo akapata bahati ya kuonana na Lulu ambaye alionekana kuwa mnyonge.
Baada ya salamu, shushushu wetu alimuuliza Lulu kuhusu afya yake na ya ujauzito alionao ambapo alijibu kwa mkato.
“Nani amekwambia mimi nina mimba?”
MASTAA WA BONGO WANENA
Baadhi ya mastaa wa sinema Bongo ambao hawakuwa tayari majina yao kuchorwa gazetini, walipozungumza na gazeti hili kuhusu kuwepo au kutokuwepo kwa ujauzito wa Lulu walipishana ‘kiswahili’.
Wapo waliodai ujauzito huo ulitoka akiwa gerezani, wengine walidai ulitoka wiki moja kabla ya kifo cha Kanumba lakini wapo waliodai bado anao.
Staa wa kiume: “Lulu hana ujauzito, ulitoka. Ninavyojua mimi, wiki moja kabla ya kifo cha marehemu (Kanumba) ndiyo ulitoka, kwa hiyo hana.”
Staa wa kike: “Lulu bado ana mimba ila ni siri sana. Lakini hata nyiye wenyewe si mmeona tumbo lile, anao.”
Staa wa kike: Lulu mpaka anaingia kwenye matatizo kwa kifo cha Kanumba alikuwa na kibendi, hawezi kukitoa kwa sasa, maana yuko gerezani.”
Lulu anatarajiwa kufikishwa Mahakama Kuu ya Tanzania Mei 28, mwaka huu ili kujibu tuhuma zinazomkabili juu ya kifo cha Kanumba.
Lulu ana Mimba? Is Lulu Pregnant

Former Tanzanian film star Steven Kanumba's girlfriend Lulu Michaels is rumoured to be pregnant. Lulu who was charged with his murder is now three months pregnant. According to Tanzanian tabloids, Lulu, 17, is reportedly carrying the late actor's baby. She has however not commented on the pregnancy. Lulu is rumoured to have  previously dated Tanzanian Ali Kiba. They remained friends after they broke up. Kanumba’s  sudden death devastated his fans from both within and outside the country.
According to the police, Kanumba and Lulu were fighting over calls that were coming on her phone while she was at his home. He demanded to see the calls and the girl wasn't ready to surrender it. While he was taking it by force, she pushed him and he fell, hitting his head hard. She is still in police custody as the investigations are still underway.

Monday, April 23, 2012

Lulu Mahakamani Kisutu Leo

 Mcheza sinema Elizabeth 'Lulu' Michael alifikishwa katika mahakama leo kuhusiana na kesi yake kuhusiana na mauji ya Bongo Star Steven Kanumba.  Kesi leo ilikuwa ni kutajwa tu yaani Mention.
Mcheza Sinema, Elizbeth 'Lulu' Michael, katika Mahakama ya Kisutu leo hii 23/4/12 (Picha kwa hisani ya Michuzi Blog)  Kuona picha zaidi Mtembelee Kaka Michuzi


Katika hii picha ya Global Publishers Lulu anaonekana kuwa na kakitambi!   (picha kwa hisani ya Global Publishers)

MAELEZO KUTOKA GLOBAL PUBLISHERS

Mwigizaji Maarufu wa filamu za Kibongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ leo majira ya saa nne asubuhi amepandishwa kizimbani kwa mara ya pili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na kusomewa shitaka la kumuua Steven Kanumba. Baada ya kusomewa shitaka hilo na Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Mahakama hiyo Elizabeth Kaganda mbele ya Hakimu Rita Tarimo hakutakiwa kujibu lolote. Mwendesha Mashitaka huyo alisema upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamailika hivyo kesi hiyo iliahirishwa mpaka Mei 7 mwaka huu.


Wednesday, April 11, 2012

Lulu Mahakamani Kisutu Leo!

Lulu Akijiandaa kuacti Sinema
Hayati Steve Kanumba ni miongoni mwa wasanii maarufu wa Tanzania wenye nyota za umaarufu (Tanzania Walk of Fame) ndani ya ukumbi wa Dar Live jijini Dar Es salaam ambapo mara baada ya kifo chake wafanyakazi wa ukumbi huo na mashabiki wake wameweka mashada ya maua,kadi na kuwasha mishumaa kama ishara ya kuomboleza kifo chake.
 (Picha kw Hisani ya Abdallah Mrisho Blog)
MAELEZO KUTOKA MICHUZI BLOG:

Muigizaji wa Filamu nchini anaehusishwa na kifo cha Muigizaji Mwenzie, Marehemu Steven Kanumba,Elizabeth Michael a.k.a Lulu amepandishwa kizimbani mapema leo asubuhi kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam kwa kusomewa mashtaka yake kuhusiana na kuhusika kwa kifo cha Muigizaji huyo nguli hapa nchini.


Elizabeth Michael amesomewa mashtaka hayo mbele ya hakimu Agustino Mmbando na wakili Elizabeth Kaganda ya mauaji ya Muigizaji wa Filamu nchini,Marehemu Steven Kanumba yaliyotokea huko sinza vatcan jijini Dar es Salaam april 7 mwaka huu.

Elizabeth Hakutakiwa kujibu chochote Mahakamani hapo kwani mahakama hii haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji.

Kesi hiyo imeahirishwa na kupangwa kusikilizwa tena april 23 mwaka huu.

Muigizaji huyo aliletwa mahakamani hapo kwa mwendo wa kasi kama mshale na kwa ulinzi mkali na pia ndivyo alivyoondolewa Mahakamani hapo kiasi kwamba hakuna hata mwandishi alieweza kupata picha ya Muigizaji huyo mwenye tuhuma za mauaji Na kupandishwa katika gari ndogo nyeupe aina ya suzuki grand vitara yenye nambari za usajiri T 848 BNV huku kwenye kioo nambari zake zikisomeka PT 2565.

********************************************************************

Lulu kortini kwa kumuua Kanumba

Polisi wamficha, wakwepa waandishi
Ajifunika ushungi, avaa kandambili

Msanii wa uigizaji wa filamu nchini, Elizabeth Michael Kimemeta (18), maarufu kama Lulu, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, akikabiliwa na mashtaka ya mauaji ya msanii mwenzake, Steven Kanumba (28).

Tukio la msanii huyo kufikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashtaka lilikuwa kama mchezo wa filamu baada ya polisi kufanya siri na hata kugombana na baadhi ya waandishi wa habari waliotaka kuingia katika chumba cha mahakama kufuatilia kesi hiyo.

Kesi hiyo ilisomwa mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Augustina Mmbando.

Kabla ya kusomewa mashtaka hayo, hakimu alimtaka Lulu kutojibu chochote kuhusu tuhuma zinazomkabili.

Wakili wa Serikali, Elizabeth Kaganda, alidai kuwa Aprili 7, mwaka huu katika eneo la Sinza Vatican, jijini Dar es Salaam, mshtakiwa alimuua Kanumba.

Kwa mujibu wa Mwenendo wa Sheria ya Makosa ya Jinai (CPA), Lulu hakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji.

Hata hivyo, mara upelelezi utakapokamilika, kesi hiyo itahamishiwa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam kwa ajili ya kusikilizwa.

Kaganda alidai upelelezi bado haujakamilika, hivyo akaiomba mahakama kupanga tarehe ya kuitajwa kwa kesi hiyo.

Hakimu Mmbando alisema mshtakiwa atakaa mahabusu hadi Aprili 23, mwaka huu, kesi hiyo itakapotajwa.

Wakati mshtakiwa huyo akisomewa hati ya mashtaka alidai mahakamani hapo kwamba, umri wake sio miaka (18) kama ilivyoandikwa kwenye hati ya mashtaka bali ana miaka (17).

Pia wakati mashtaka yanasomwa hali mahakamani hapo ilikuwa shwari, huku watu wengine wakinong’ona bila kuwa na uhakika kuhusu msanii huyo kufikishwa mahakamani kutokana na kutoonekana kwa wanafamilia wake na watu wa karibu.

Mazingira ya Lulu kufikishwa mahakamani hapo yalikuwa kama mchezo wa kuigiza kutokana na jeshi la polisi kufanya kuwa siri kubwa.

Gari aina ya Suzuki Vitara liliingia katika viunga vya mahakama hiyo muda ambao haukufahamika likiwa na makachero wa Jeshi la Polisi wanne, wanawake wawili na wanaume wawili na mshtakiwa.

Lilifuatiwa na gari lingine aina ya Toyota Land Cruiser lililokuwa na askari polisi saba waliovaa sare za jeshi hilo wakiwa na silaha.

Hata hivyo, baada ya muda NIPASHE kupitia chanzo chake ilipata taarifa ya msanii huyo kufikishwa katika viunga vya mahakama hiyo na kwamba jalada la kesi yake lilikuwa limeshapangiwa hakimu.

Hatua hiyo ilisababisha waandishi wa habari za mahakama kujipanga na kuweka lindo katika kila kona ya jengo la mahakama hiyo huku wengine wakiwa kwenye mlango wa kutokea mahabusu, kwenye korido za milango ya kuingia katika ofisi za mahakimu.

Hata hivyo, kundi la waandishi waliokaa katika korido ya ghorofa ya kwanza kuelekea kwenye ofisi za mahakimu, ghafla saa 5:20 asubuhi walifanikiwa kumuona mshtakiwa huyo akiwa katikati ya makachero wanawake wawili na nyuma wanaume wawili akiwa amejifunika ushungi wa rangi ya udhurungi, gauni kubwa maarufu kama ‘dira’ la rangi ya njano na kandambili za rangi nyekundu.

Waandishi hao walikimbilia msafara huo uliokuwa na askari wanne pamoja na mshtakiwa, lakini kabla ya kuingia chumba cha hakimu, askari aliyekuwa ameshika simu ya upepo mkononi aliwazuia waandishi kuingia.

Hali hiyo ilisababisha majibishano ya muda na mwishowe alibadili nia ya kuzuia wanahabari hao kufanya kazi yao.

Mshtakiwa alisomewa mashtaka yake na baadaye alipitishwa njia ya mlango wa nyuma hadi kwenye gari aina ya Suzuki Vitara yenye namba za usajili T848 BNV yenye vioo visivyoonyesha ndani (tinted).

Ingawa gari hilo lilikuwa na namba za kirais, kwenye vioo liliandikwa namba PT 2565, na iliondoka mahakamani hapo kwa kasi kumpeleka mshtakiwa mahabusu ya Segerea kusubiri upelelezi wa kesi hiyo kukamilika.

Mapema jana saa 3:35 asubuhi, NIPASHE ilizungumza kwa njia ya simu na Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, ACP Charles Kenyela kuhusu hatima ya kufikishwa mahakamani kwa msanii huyo, mazungumzo yalikuwa kama ifuatavyo:

NIPASHE: Shikamoo afande.

Kamanda Kenyela: Marahaba. Nipigie baadaye niko kwenye kikao.

NIPASHE: Sawa afande. Lakini nilitaka kujua kama Lulu atapelekwa mahakamani leo (jana) na itakuwa mahakama gani Kinondoni au Kisutu?

Kamanda Kenyela: Mmmh! Kwa kweli bado uchunguzi unaendelea. Hivyo, jalada liko kwa Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP).

NIPASHE: Ahsante afande. Shida yangu ilikuwa hiyo tu endelea na ujenzi wa Taifa.

Kamanda Kenyela: Nashukuru sana mwandishi.

Kanumba alifariki dunia usiku wa kuamkia Jumamosi Aprili 7, mwaka huu, baada ya kudaiwa kutokea ugomvi kati yake na Lulu.

Maelfu ya watu, wakiwamo mawaziri, wabunge, viongozi wa siasa, vyama vya kiraia, wasanii wenzake na wananchi wa kawaida, walijitokeza katika msiba huo nyumbani kwake, Sinza Vatican, jijini Dar es Salaam na kwenye shughuli za kumuaga viwanja wa Leaders Club na kuuzika mwili wake katika makaburi ya Kinondoni.

Mazishi hayo yaliongozwa na Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal.


CHANZO: NIPASHE

Monday, September 22, 2008

Skandali nyingine Bank of Tanzania (BoT)






Kutoka kwa Mzee wa Sumo (Mpoki Bukuku) Blog:

" Hii ni kutoana nishaji jamani na ukiukwaji haki za wanawake yaani wengine wameamua kutoa wigi la urembo kujikinga na fedheha! Sijui wengine walikuwa na swaum? " - Mpoki Bukuku akizungumzia picha alizopiga.

TUHUMA za kuwepo kwa upendeleo wa watoto wa vigogo kwenye ajira za Benki Kuu ya Tanzania (BoT), zimesimamisha kizimbani wafanyakazi wanane ambao wameshtakiwa kwa kosa la kughushi vyeti.

Tuhuma dhidi ya watoto 16 wa vigogo ziliibuka wakati kashfa ya wizi wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), ikiwa imeshamiri kiasi cha kusababisha aliyekuwa gavana, Daud Ballali kusitishwa mkataba wake na kufanyika kwa mabadiliko kadhaa kwenye uongozi wa chombo hicho nyeti cha fedha.

Na Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, aliahidi kuzishughulikia tuhuma hizo wakati huo baada ya tuhuma hizo kushikiwa bango.

Jana, wafanyakazi wanane wa BoT, baadhi yao wakiwa wamejifunika nyuso kwa nguo na nywele za bandia, walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakishtakiwa kwa tuhuma za kughushi vyeti na kutoa hati za uongo.

Wafanyakazi hao, wengi wao wakiwa wanawake, ni Justina J Mungai, ambaye imeelezwa kuwa ni mtoto wa Joseph Mungai, ambaye amewahi kushika wizara tofauti ikiwemo ya elimu, Christina G Ntemi, Siamini Eddie Kombakono, Janeth John Mahenge, Beatha Constantine Massawe, Jacquiline David Juma, Philimina Philibert Mutagurwa na Amina Mohamed Mwinchumu.

Wafanyakazi hao walifikishwa katika mahakama hiyo saa 4.00 asubuhi na kusomewa shtaka mbele ya Hakimu Neema Chusi. Wakili wa serikali, Edgar Luoga, akisaidiana na Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Abubakar Msangi, ndio walioongoza mashtaka hayo.

Washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa hati za uongo kwa mwajiri wao, ambaye ni BoT.

Washtakiwa Mungai, Massawe na Mwinchumu, wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2001, wakati Ntemi, Kombakono, Mahenge na Mutagurwa wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2002. Wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa BoT hati za uongo, wakionyesha kuwa vimetolewa na Baraza la Mitihani la Taifa, wakati si kweli.

Ilidaiwa kuwa, Mutagurwa alighushi cheti hicho mwaka 2000.