Iinasemekana ni mtu na mpenzi wake. Ila baada ya mtoto kutiliwa mashaka akajaribu kuficha ficha leo ametegwa na kunaswa kwenye mtego ulioshuhudiwa na mama yake mzazi (mtoto akikutwa kitandani na baba wa kambo) hayo yalifanyika katika hotel ya Excutive iliopo pembeni ya makao makuu ya uhamiaji.
Showing posts with label Pemba. Show all posts
Showing posts with label Pemba. Show all posts
Saturday, May 28, 2016
Waziri wa Serikali ya Zanzibar Afumaniwa Gesti Akiwa na Binti yake wa Kambo!
Iinasemekana ni mtu na mpenzi wake. Ila baada ya mtoto kutiliwa mashaka akajaribu kuficha ficha leo ametegwa na kunaswa kwenye mtego ulioshuhudiwa na mama yake mzazi (mtoto akikutwa kitandani na baba wa kambo) hayo yalifanyika katika hotel ya Excutive iliopo pembeni ya makao makuu ya uhamiaji.
Labels:
Guest House,
Mh. Faki Dadi Faki,
Ngono. Kufumaniwa,
Pemba,
Sex,
Zanzibar
Thursday, March 28, 2013
Mazishi ya Mh. Khamis Yatakuwa Kesho Mjini Pemba
![]() |
| The Late Honourable Salim Hemed Khamis (MP Chambani Pemba -CUF) |
MAZISHI ya aliyekuwa Mbunge wa CUF, Jimbo la Chambani Pemba kisiwani Zanzibar, Marehemu, Salim Hemed Khamis, (62), yanataraji kufanyika kesho (Ijumaa Machi 29, 2013) mchana mjini Pemba.
Tarifa za awali kutoka Chama cha Wananchi CUF, zinasema kuwa Mwili wa Marehemu, Khamis utaagwa kesho asubuhi kuanzia majira ya saa 2:30-4:00 katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam ambapo Viongozi mbalimbali wa kitaifa na Kimataifa pamoja na wananchi na Wanachama wa CUF watapata fursa ya kutoa heshima za mwisho kwa Marehemu.
Taarifa hiyo ya Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julis Mtatiro inasema kuwa Msafara utaondoka Karimjee saa 4:00 kuelekea uwaja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambapo Msafara wa Ndege 2 utaondoka kwenda Pemba.
Saa saba mchana mazishi yatafanyika huko Pemba na maazishi hayo yataongozwa na Viongozi wa serikali, Wabunge na CUF.
Mtatiro amewaomba wanachama nba wafuasi wa CUF jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kuuga mwili wa Mbunge huyo aliyefikwa na umauti akiwa kazini katika vikao vya Kamati za Bunge, ambapo Marehemu alikuwa Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
***************************************************************************
Pichani ni Baadhi ya Maofisa wa Ofisi Ndogo ya Bunge,wakimsaidia kwa kumbeba Mbunge wa Chambani,Bwa.SalimHemed Khamis,mara baada ya kuanguka ghafla hapo jana jijini Dar akiwa katika vikao vya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kukimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu ya haraka.
======= ====== ======
Habari zilizoifikia Globu ya Jamii hivi punde inaelezwa kuwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Chambani-Pemba, Salim Hemed Khamis,ambaye hapo jana alianguka ghafla jijini Dar Es Salaam alipokuwa akihudhuria vikao vya kamati ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kukimbizwa hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu, amefariki dunia muda mfupi uliopita katika Hospitali hiyo ya Taifa ya Muhimbili,aidha chanzo cha habari hizi kimeongeza kuwa taratibu za kuusafirisha mwili wa Marehemu kuelekea Pemba kwa mazishi zinafanyika.Tutazidi kuwafahamisha zaidi kadiri ya habari zitakavyokuwa zikiingia.
Mungu ailaze Roho ya Marehemu mahali pema Peponi-Amin
***************************************
WADAU NINA SWALI. Hivi huko Bungeni, hakuna Stretcher ya kubeba wagonjwa? Je, hakuna watu wa First Aid? Hii ni mwaka 2013, wanatakiwa wawe na wahudumu wa afya, ambulance, wahudumu onsite. Watu wawepo wanaoelewa jinsi ya kubeba wagonjwa. Na hasa huko Bungeni waBunge wengi wana umri mkubwa na matatatizo ya kiafya. - Chemi
Wednesday, March 06, 2013
Sifa Za Mikoa ya Tanzania
Nimepokea kwa email:
HIZI NDIO SIFA ZA KILA MKOA TANZANIA:
1. DAR - Utapeli
2. ARUSHA - Ustaarabu
3. MBEYA - Matukio
4. MWANZA - Fujo
5. TANGA - Mapenzi
6. MOROGORO - Starehe
7. DODOMA - Bahati
8. IRINGA - Elimu bora
9. RUVUMA - Pombe
10. RUKWA - Uchawi
11. TABORA - Mikosi
12. SHINYANGA - Njaa
13. SINGIDA - Upole
14. KAGERA - Misifa
15. LINDI - Waoga
16. KIGOMA - Ubishi
17. PWANI - Uvivu
18. MTWARA - Hasara
19. KILIMANJARO - Ubahili
20. MARA - Hasira
21. MANYARA - Utajiri
22. GEITA - Presha
23. SIMIYU - Maradhi
24. NJOMBE - Haraka
24. KATAVI - Aibu
25. Visiwani kote- uchezaji wa karata na bao
Haya mwenzangu watokea mkoa gani?
HIZI NDIO SIFA ZA KILA MKOA TANZANIA:
1. DAR - Utapeli
2. ARUSHA - Ustaarabu
3. MBEYA - Matukio
4. MWANZA - Fujo
5. TANGA - Mapenzi
6. MOROGORO - Starehe
7. DODOMA - Bahati
8. IRINGA - Elimu bora
9. RUVUMA - Pombe
10. RUKWA - Uchawi
11. TABORA - Mikosi
12. SHINYANGA - Njaa
13. SINGIDA - Upole
14. KAGERA - Misifa
15. LINDI - Waoga
16. KIGOMA - Ubishi
17. PWANI - Uvivu
18. MTWARA - Hasara
19. KILIMANJARO - Ubahili
20. MARA - Hasira
21. MANYARA - Utajiri
22. GEITA - Presha
23. SIMIYU - Maradhi
24. NJOMBE - Haraka
24. KATAVI - Aibu
25. Visiwani kote- uchezaji wa karata na bao
Haya mwenzangu watokea mkoa gani?
![]() |
| WaHadzabe wakicheza Ngoma |
Friday, February 24, 2012
Sikummaliza Jumbe – " Maalim Seif"
![]() |
| Maalim Seif Sharif Hamad |
![]() |
| Mh. Aboud Jumbe Mwinyi |
Sikummaliza Jumbe – "Maalim Seif"
22 Februari 2012
Na Seif Sharif Hamad
Mwaka 1984, Rais wa Zanzibar, Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, na Makamo wa Pili wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Aboud Jumbe Mwinyi, alilazimishwa kujiuzulu katika Mkutano Mkuu wa CCM Dodoma akishutumiwa kutaka kuvunja Muungano. Kitendo hiki kimekuwa kikichukuliwa na Wazanzibari kama udhalilishaji mkubwa kwa nchi na heshima yao, na msimamo wa serikali tatu, ambao Jumbe anasemekana kuutetea umekuwa ndio msimamo wa Wazanzibari. Kujiuzulu kwa Jumbe kunaunganishwa na tafauti za kimtazamo baina yake na Katibu Mkuu wa sasa wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ambaye hata hivyo anasisitiza katika makala hii kwamba hajawahi kutafautiana na Jumbe kuhusu mtazamo wa Muungano.
Kwanza niweke kumbukumbu sawa. Mwaka 1984 wakati Mzee Aboud Jumbe anajiuzulu nyadhifa zake zote, mimi ni kweli nilikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Mkuu wa Idara ya Uchumi na Mipango ya Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa [NEC] ya CCM, na hivyo kuwa miongoni mwa viongozi wa juu wa Chama cha Mapinduzi. Hata hivyo wakati huo sikuwa miongoni mwa viongozi wa Serikali ya Mapinduzi. Kwani nilikuwa Waziri wa Elimu wa Zanzibar kuanzia mwaka 1977 hadi mwaka 1980. Nikateuliwa kuwa Waziri Kiongozi wa Zanzibar na Mzee Ali Hassan Mwinyi aliyeteuliwa kuwa Rais wa Muda wa Zanzibar mara baada ya Mzee Aboud Jumbe kujiuzulu mwaka 1984. Hivyo kuanzia mwishoni mwa 1980 hadi mwanzoni mwa 1984 sikuwa kiongozi katika Serikali ya Mapinduzi.
Pili, tangu Chama cha Wananchi CUF kiasisiwe hapo 1992, sera yake rasmi ni kuwepo kwa Muungano wa serikali tatu: yaani Serikali ya Muungano, Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Tanganyika.
Pengine itakumbukwa kuwa hata Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliwahi kusema kuwa Chama cha Siasa chochote kile kina haki ya kuwa na sera yake juu ya Muungano. Akasema kuwa kama vile ni haki ya CCM kuwa na sera ya serikali mbili kuelekea serikali moja, CUF wanayo haki hiyo hiyo ya kuwa na sera ya serikali tatu katika Muungano. Mwalimu Nyerere akamalizia kwa kusema kuwa na sera juu Muungano inayotafautiana na sera ya CCM si uhaini. Waachiwe wananchi waamue!
Hivyo basi msimamo wangu tangu kuasisiwa kwa Chama cha Wananchi, CUF haujapata kubadilika. Ni msimamo na sera ya Chama changu cha CUF. Sera ya kuwepo kwa serikali tatu katika Muungano wetu.
Hivyo niseme, kama nilivyokuwa nikisema kila nilipopata nafasi, kuwa bila ya kuubadili muundo wa Muungano wetu kutoka muundo wa sasa wa serikali mbili kwenda kwenye muundo wa serikali tatu, matatizo ya Muungano yataendelea kuutafuna Muungano wetu. Badala ya kuuimarisha tutakuwa tunaendelea kuudhoofisha. Kuimarisha Muungano sio kuongeza orodha ya Mambo ya Muungano katika Katiba. Hili linadhoofisha Muungano. Kwani nguvu za Muungano zitatokana na wananchi wa pande mbili kuukubali kwa dhati Muungano wenyewe. Kuhakikisha kuwa wananchi wa pande zote mbili wanaridhika na muundo wake, mamlaka na madaraka ya kila upande na serikali yake. Na zaidi kuliko yote, wananchi wa pande zote mbili kuridhika kuwa wanatendewa haki katika Muungano.
Vyenginevyo tutakuwa tukibadili misamiati tu: mara tutayaita matatizo ya Muungano; mara tuziite kero za Muungano, pengine tutakuja kuyaita mapungufu ya Muungano, au hata bughdha za Muungano, na kadhalika.
Suala la kutoka serikali mbili kwenda serikali moja hilo halitakubalika. Mimi silikubali. CUF hailikubali, na Mzanzibari mzalendo yeyote halikubali. Siamini kuwa Serikali ya Muungano itakuwa tayari kutumia vifaru, mizinga na madege ya kivita kulazimisha muundo wa serikali moja.
Baada ya kuweka msimamo huo, sasa nigeukie mambo mengine uliyoniuliza.
Kwamba Mzee Aboud Jumbe alituhumiwa kutaka kuwepo kwa muundo wa Muungano wa serikali tatu na akalazimishwa kujiuzulu. Wakati huo mimi nilitetea muundo wa sasa wa serikali mbili.
Ili hili lifahamike vyema na wananchi ni vyema kwanza kuelezea mazingira yaliyomfikisha Mzee Aboud Jumbe kujiuzulu.
Nitangulie kueleza kuwa mimi binafsi na kwa dhati ya nafsi yangu namuheshimu na namthamini sana Mzee Aboud Jumbe. Kwanza ni mwalimu wangu nilipokuwa nasoma katika skuli ambayo wakati huo ikiitwa The King George VI Secondary School (sasa Lumumba College).
Pili, ni Mzee Aboud Jumbe ambaye alisababisha mimi kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mara baada ya yeye kuwa Rais wa Zanzibar mwaka 1972, baada ya kukaa kwa miaka minane (8) tangu nilipomaliza masomo ya Kidatu cha Sita (Form VI) hapo 1963 na kuzuiwa na Serikali ya Mapinduzi kujiunga na masomo ya Chuo Kikuu, pamoja na kuwa kila mwaka nilikuwa napata nafasi katika vyuo mbali mbali duniani.
Tatu ni Mzee Aboud Jumbe huyo huyo aliyesababisha mimi kuwa kiongozi katika Serikali ya Mapinduzi na kuwa miongoni mwa viongozi wa juu wa CCM. Hivyo namshukuru na katu siwezi kumsahau kwa mchango wake mkubwa ulionifanya nilivyo.
Sasa nirejee kuelezea mazingira ya wakati huo ambayo yalikuwa kama ifuatavyo:
Nianzie mwaka 1982 ambapo kulikuwa na uchaguzi wa viongozi wa CCM. Katika kipindi kilichotangulia Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM wa 1982 wa kuchagua viongozi wa kitaifa, kulijitokeza makundi mawili miongoni mwa viongozi wa CCM kutoka Zanzibar yaliyokuwa yakikinzana. Kundi la kwanza likijulikana kama Liberators, na la pili likijulikana kama Frontliners. Kundi la Liberators kimsingi lilikuwa na viongozi ambao walikuwa wanapinga mabadiliko ya aina yoyote yale katika uendeshaji wa mambo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii katika Zanzibar.
Kwa lugha ya sasa unaweza ukaliita kundi la Wahafidhina. Kundi la Frontliners lilikuwa na vijana, damu mpya iliyoingia katika uongozi wa Chama na SMZ. Kundi hili lilitaka mabadiliko katika uendeshaji wa mambo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Unaweza ukaliita kundi la Reformers.
Uchaguzi wa viongozi wa kitaifa (Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa) wa 1982 ulishuhudia msuguano mkali kati ya makundi hayo mawili. Nia ya Liberators ilikuwa ni kuhakikisha kuwa Frontliners hawaingii katika Halmashauri Kuu ya Taifa. Nia ya Frontliners ilikuwa ni kuhakikisha damu mpya inaingia katika kikao hicho kikuu cha maamuzi cha Chama ambacho wakati huo kilikuwa ndio kimeshika hatamu zote za uongozi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Bahati njema Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM, kwa busara zake, uliwaingiza watu kutoka makundi yote mawili katika NEC na, baadaye, NEC ikawaingiza watu kutoka makundi yote mawili katika Kamati Kuu.. Frontliners walishukuru kuona kuwa miongoni mwao walifanikiwa kuchaguliwa kuingia katika vikao vyote viwili vikuu vya maamuzi vya Chama.
Kwa upande mwengine, Liberators hawakufurahi. Liberators hao walishaweka shinikizo kwa Mzee Aboud Jumbe (ambaye ndiye chanzo cha kuingiza damu mpya katika CCM ya wakati huo) kuwa vijana aliowaingiza watakujamgeukia na kuwaondoa wao, Liberators, na yeye mwenyewe katika uongozi. Inaelekea Mzee Aboud Jumbe alishawishika na shinikizo hilo, na hivyo naye, kwa njia zake (nyuma ya pazia), alitaka kuona kuwa Frontliners hawaingii katika NEC na Kamati Kuu ya Chama ambako pengine wangekuwa na ushawishi katika maamuzi ya sera za Chama. Frontliners walipoingia, ikawalazimu Liberators na Mzee Aboud Jumbe kutafuta njia nyengine ya kuweza kuwazingira ili, ikiwezekana, waweze kuondolewa katika ramani ya uongozi wa Chama na Serikali.
Hivyo basi, mara baada ya kikao cha Mkutano Mkuu wa Taifa kumalizika mwezi Novemba, 1982, Mzee Aboud Jumbe aliwataka Wajumbe wote wa NEC kutoka Unguja akutane nao Unguja, na Wajumbe wote wa NEC kutoka Pemba akutane nao Pemba. Katika mikutano hiyo, hotuba ya mwalimu wangu, Mzee Aboud Jumbe, ilitushtua wengi. Mzee Aboud Jumbe alishtumu kuwa kuna watu wanaoleta uchochezi kutaka kuvigawa visiwa vya Unguja na Pemba; kutaka kuigawa mikoa, yaani mkoa mmoja dhidi ya mwengine katika kila kisiwa; kutaka kuzigawa wilaya, yaani wilaya moja dhidi ya nyengine katika kila mkoa; na kutaka kuvigawa vijiji, yaani kijiji kimoja dhidi ya chengine katika kila wilaya. Akamalizia kwa kusema kuwa watu hao watahukumiwa na kuonja kile alichokiita “Revolutionary Justice”
Hili lilitushtua wengi, hasa sisi vijana wa wakati huo. Tukakumbuka historia ya Zanzibar tangu Mapinduzi ambapo watu walioshukiwa kuwa wapinzani wa serikali, na hasa wasomi, walivyoshughulikiwa kwa kuhakikisha kuwa wanatoweka kabisa. Khofu yetu ikawa jee, hawa wazee si wamekusudia kuturudisha huko huko tulikotoka? Tukasema kama hatukuchukua hatua za kichama kulizuia hili, basi kuna uwezekano wa historia kujirudia na watu wasiokuwa na hatia kupotea kwa kile kinachodaiwa kusimamisha “Revolutionary Justice”
Hivyo baadhi yetu tuliokuwa Wajumbe wa Sekretariati ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama, hasa sisi kutoka Zanzibar, tukamfuata Mzee Rashid Kawawa aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM na Mwenyekiti wa Sekretarieti na kumueleza khofu yetu hiyo. Mzee Kawawa akatuelewa na akaamua iletwe agenda juu ya suala hilo katika kikao kilichofuata katika Sekretarieti. Agenda ikaletwa. Ikajadiliwa kwa mapana yake, kisha ikawasilishwa katika kikao cha Kamati Kuu. Kamati Kuu ikaamua kuunda timu mbili kwenda kuchunguza madai yaliyotolewa na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mzee Aboud Jumbe. Timu moja ikaagizwa kufanya uchunguzi katika kisiwa cha Unguja, na timu ya pili ikaagizwa kufanya uchunguzi katika kisiwa cha Pemba. Timu moja iliongozwa na Marehemu Moses Nnauye na ya pili iliongozwa na Mheshimiwa Alfred Tandau.
Baada ya uchunguzi, timu zote mbili zikawasilisha taarifa zao katika kikao cha Kamati Kuu. Timu zote mbili ziliona kuwa madai ya Mzee Aboud Jumbe hayakuwa na msingi. Hivyo Kamati Kuu ikamsihi Makamu wa Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar na Makamu wa Mwenyekiti wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mzee Aboud Jumbe, kuzuia kuchukua hatua zozote zile ambazo zingeweza kusababisha ukiukwaji na uvunjaji wa haki za binadamu dhidi ya raia.
Inavyoonekana, hili halikumpendeza mwalimu wangu, Mzee Aboud Jumbe. Alihisi kuwa Chama, na Muungano unamuingilia katika kutekeleza azma yake na ile ya Liberators ya kuisafisha safu ya uongozi wa Chama Zanzibar kwa kuwaondoa kwa njia yo yote ile Frontliners na vijana wenye mawazo mapya .
Kipindi hicho kulikuwa na mjadala ulioanzishwa na Halmashauri Kuu ya Taifa juu ya mapendekezo ya marekebisho ya Katiba. Mzee Aboud Jumbe na timu yake wakaona kuwa waitumie nafasi hiyo kufanya kampeni kabambe kutaka muundo wa Muungano ubadilishwe. Sisi wa Frontliners tulitafsiri kuwa kampeni hiyo madhumuni yake ni kutaka kubadili muundo wa Muungano ili kundi la Liberators lipate uhuru zaidi, nguvu zaidi, na madaraka zaidi, ambayo, kwa mawazo yetu, yangetumika dhidi ya watu wenye mawazo mapya na ambao walionekana kama ni tishio kwa Liberators. Tulitafsiri kampeni hiyo kuwa na agenda iliyojificha ya kutaka kujiimarisha na kujichimbia katika madaraka kundi la Liberators ili kulinda “status quo.”
Ni kwa msingi huo ndipo mimi na wenzangu wa Frontliners tulimpinga Mzee Aboud Jumbe. Ifahamike kuwa hatukupinga dhana ya serikali tatu! Tulipinga nia iliyojificha ya Mzee Aboud Jumbe na wenzake ya kuibua agenda hiyo. Tulipinga njia zilizotumika katika kuisimamia na kuiendesha agenda hiyo. Ndio maana mara baada ya Chama cha Wananchi, CUF, kuundwa, tukabuni sera ya muundo wa Muungano wa serikali tatu. Ikumbukwe kuwa wengi wa waasisi wa CUF walitokana na kundi la Frontliners.
Ingalikuwa kulikuwa na nia njema, Mzee Aboud Jumbe angetuita, walau baadhi yetu na kutaka mawazo yetu. Nina hakika wengi tungekubaliana naye na tungezungumzia mkakati wa kulikabili suala hilo. Mimi nina hakika tungekwenda Kamati Kuu na baadaye Halmashauri Kuu kama uongozi wa Zanzibar ulioungana, wenzetu wa Bara wasingeweza kutupuuza. Na hapa niseme, tena kwa masikitiko makubwa, kwamba hili ndio limekuwa tatizo letu Wazanzibari. Wazanzibari tuna madai ya msingi katika Muungano. Lakini tunashindwa kuyasimamia madai yetu hayo hadi kupatikana mafanikio kwa kuwa tumekubali kugawiwa na tumegawika. Kugawika huko hakuyanufaishi maslahi ya Zanzibar.
Nitoe wito, kupitia gazeti lenu, kwamba wakati umefika kwa Wazanzibari bila kujali tafauti zetu za kiitikadi, kuungana ili kusimamia, kutetea na kuendeleza masilahi ya Zanzibar na watu wake katika Muungano.
Kwa kumalizia basi, kwa maoni yangu, Zanzibar ni nchi. Zanzibar ni taifa. Zanzibar ni dola.
Zanzibar ni nchi kwa sababu ni eneo lenye mipaka inayotambulikana na Katiba ya Zanzibar na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pia ina watu wanaotambulika.
Zanzibar ni taifa kwa vile Wazanzibari kwa ujumla wao wanatambulikana kuwa na mila na utamaduni wao. Wazanzibari wanaweza kutafautishwa na watu wa sehemu yoyote nyengine duniani. Taifa la Wazanzibari lina uhai na ni taifa endelevu.
Zanzibar ni dola kwa vile kuna mamlaka iliyowekwa na Katiba zote mbili, yaani Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar [SMZ] yenye madaraka yasiyoweza kuingiliwa na chombo chochote chengine katika mambo yasiyo kuwa ya Muungano katika nchi ya Zanzibar. Ni kweli kuwa Zanzibar haina jeshi lake wala polisi yake. Lakini ni kweli pia kuwa Zanzibar ina vyombo vyake vyengine vya maguvu vilivyoanzishwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar, Katiba inayotambuliwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano na sheria za Zanzibar. Hivyo ni vyombo vya maguvu vilivyo halali kwa mujibu wa sheria za nchi.
Ni kweli kuwa suala la Mambo ya Nje ni jambo lililomo katika orodha ya Mambo ya Muungano. Lakini ni kweli pia kuwa suala la mahusiano ya kimataifa halijawahi kuingizwa katika orodha ya Mambo ya Muungano. Hivyo Zanzibar ina uwezo kamili wa kushirikiana na mataifa na mashirika ya kimataifa katika kuwaletea maendeleo Wazanzibari. Ni bahati mbaya kuwa Serikali ya Muungano imejaribu na inaendelea kuiminya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kusimamia ushirikiano wa kimataifa. Mambo kama haya ndio yanaoudhoofisha Muungano wetu.
Kama kuna watu wanasema kuwa Zanzibar sio nchi, basi wasiishie hapo. Waeleze jee Zanzibar ni Mkoa, au ni Wilaya, au ni kijiji au ni kitongoji?
--
Labels:
Mh. Aboud Jumbe,
Muungano,
Pemba,
Seif Sharif Hamad,
Siasa,
Tanganyika,
Zanzibar
Thursday, September 15, 2011
MV Spice Islander Ilikuwa na Abiria 3,000 Ilipozama!
Wadau, kuna madai kuwa hiyo meli MV Spice Islander ilikuwa na abiria 3,000 wakati ilipozama! Maiti za waliokufa maji zinaanza kuonekana Mombasa.
Kutoka Gazeti la Mwananchi:
Elias Msuya na Jackson Odoyo, Zanzibar
MELI ya MV Spice Islanders iliyopata ajali mwishoni mwa wiki iliyopita na kusababisha vifo vya takriban watu 200 na majeruhi 619 ambao waliokopolewa, ilibeba abiria 3,000 wakati uwezo wake ni kubeba abiria 600 tu.Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa idadi hiyo kubwa ya abiria, haijumuishi mizigo ambayo kiasi chake bado hakijajulikana.
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Dadi Fakhi Dadi alisema jana kuwa mkoa huo umepoteza watu 1,600 katika ajali hiyo, huku Wilaya ya Wete pekee ikiwa imepoteza watu 1,141.Dadi alisema hayo alipokuwa akizungumza mbele ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.
“Wilaya ya Micheweni imepoteza watu 367, huku Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba ikipoteza watu 27 na Wilaya ya Chakechake imepoteza watu 148,” alisema Dadi na kuongeza:
“Kwa idadi hiyo ikijumlishwa na idadi ya watu 619 waliosalimika katika ajali hiyo na wengine 204 waliotambuliwa na kuzikwa na wengine watano waliookotwa Mombasa, huenda meli ile ilikuwa na watu 3, 000,” alisema Dadi.
Kutokana na takwimu zinazoendelea kukusanywa, hadi sasa zaidi ya watu 2,000 hawajulikani walipo, mbali ya wale 198 walioopolewa na kuzikwa na wengine 619 walionusurika.
Wabunge wa CUF wajiandaa kuishtaki Serikali
Wakati Serikali ikiendelea kukusanya takwimu za waliokufa au kupotea kwenye ajali hiyo, baadhi ya wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF), wamekuwa wakizunguka majimboni mwao kufanya tathmini kwa lengo la kuishtaki Serikali.
Mbunge wa Jimbo la Ziwani, Ahmed Juma Ngwali alisema anatafuta idadi kamili ya wananchi wake walioathirika kwa ajali hiyo ili afanye utaratibu wa kuishtaki Serikali kutokana na uzembe uliosababisha ajali hiyo.
“Tukishapata orodha kamili ya wananchi, nakwenda kutafuta orodha ya abiria waliokuwa kwenye meli, nalinganisha. Kwa wale waliokuwa na tiketi, nitasimamia walipwe bima zao na mmiliki wa meli. Wale waliozidi nitaishtaki Serikali kwa kuzembea,” alisema Ngwali.
Ngwali aliyekuwa akizunguka nyumba hadi nyumba kuorodhesha watu hao, alisema kwa kiasi kikubwa, Serikali ndiyo iliyofanya uzembe katika tukio hilo.
“Huu ni uzembe na ni lazima twende mahakamani. Ikiwa samaki wa Magufuli (Waziri wa Ujenzi), hadi leo wanasotesha watu mahakamani, itakuja kuwa watu?” alisema.
Mbunge wa Ole, Rajab Mbarouk alisema anakusudia kupeleka hoja binafsi bungeni ili kumwajibisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwa tukio hilo.
"Inaonyesha Serikali haina takwimu sahihi, ndiyo maana sisi tumeamua kufanya tathmini ya kina,” alisema na kuongeza kuwa tathmini hiyo itamsaidia kuratibu misaada anayopata kutoka kwa mashirika mbalimbali kwa ajili ya watu walioathirika katika tukio hilo.
“Kwa mfano sasa Benki ya Watu wa Kenya (KCB) imetoa ahadi ya kusomesha watoto yatima waliofiwa na wazazi katika ajali hiyo. Lazima niwe na takwimu sahihi za kuwapa benki hiyo,” alisema Mbarouk.
Akizungumzia suala la Waziri Mkuu mbunge huyo alisema: “Sisi ni wasemaji wa wananchi siyo Serikali. Nina mpango wa kupeleka hoja binafsi Bungeni ili Waziri Mkuu awajibike.”
Alieleza sababu za kutaka Waziri Mkuu awajibike kuwa ni pamoja na Serikali kupuuza swali lake alilouliza bungeni kuhusu usalama wa vyombo vya majini hadi sasa.
Kazi ya kuwaokoa walizama bado nguvu
Kazi ya uokoaji wa miili ya watu wanaosadikiwa kunasa ndani ya meli hiyo inaonekana kuwa ngumu baada ya wataalamu wa uokoaji kutoka Afrika Kusini kushindwa kuendelea na kazi kutokana na kina kirefu cha maji katika eneo hilo.
Tetesi za kushindikana kwa kazi hiyo zilianza kusikika jana kutoka kwa wavuvi ambao wamekuwa wakifanya kazi zao katika eneo hilo kwa kipindi kirefu huku. Wavuvi hao wanasema eneo hilo lina urefu wa zaidi ya mita 300 kutoka usawa wa bahari.
Mzamiaji kutoka eneo la Nungwi, Karim Abdallah alisema: “Hili eneo tunalifahamu lina kina kirefu sana unaweza kubeba kamba zinazojaza boti na ukifika eneo hilo na kutupa nanga haifiki chini, tulifahamu kwamba wataalamu hao hawawezi kufanya lolote katika eneo hilo.”
Kauli ya wavuvi hao ilionekana kuthibitishwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) ambayo iliamua kuondoa mahema yaliyokuwa yamewekwa katika fukwe za Nungwi kwa ajili ya kuhifadhi miili ilinayopatikana.
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Pembe Juma alisema wameamua kuanua mahema hayo kwa sababu uwezekano wa kupata miili iliyobaki ni mdogo.
“Tumelazimika kuondoa mahema hayo kwa sababu hali inavyoonekana ni wazi kuwa wataalamu hao wanaweza wakashindwa kupata miili ya watu wanaokisiwa kubaki katika eneo hilo” alisema Juma.
Hata hivyo, alipoulizwa juu ya hali ya waokoaji hao ambao bado wako katika eneo la tukio wakiongozwa na Kikosi cha Maji cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) alisema: “Sina mamlaka ya kuzungumzia mazingira ya wataalamu hao isipokuwa taarifa nilizonazo kwa sasa ndizo hizo nilizowapa.”
Wataalamu hao walitakiwa kuanza kazi hiyo juzi lakini wakashindwa kuendelea na kazi hiyo kwa sababu ya hali ya bahari kuwa mbaya. Hata hivyo, walianza tena kazi hiyo leo ingawa si kwa kuingia baharini kutafuta waliokwama chini ya maji, bali kutafuta maiti zinazoelea katika maeneo mbalimbali ya Tanga, Mombasa, Unguja na Pemba.
Katika hatua nyingine mtu mmoja alinusurika jana baada ya kuwadhihaki hadharani watu waliokumbwa na mkasa huo wa ajali ya meli kwa kudai kwamba walistahili.
Mashuhuda waliokuwapo katika eneo hilo walidai kuwa sekunde chache baada ya kutamka maneno hayo, alivamiwa na watu waliokuwa eneo hilo lakini akafanikiwa kukimbilia katika duka la vitabu la Masomo na hatimaye kuokolewa na Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiongozwa na Mkuu wa Polisi Kituo cha Malindi, Haji Mgoro.
Mkurugenzi wa duka hilo, Farouk Karim Karim alisema hatua ya mtu huyo kukimbilia dukani kwake ilihatarisha maisha yake baada ya umati watu kufunga mitaa yote inayozunguka Soko Kuu la Darajani ukimlazimisha kumtoa mtu huyo vinginevyo waingie kumtoa wenyewe.
“Kwa kweli mimi sikufahamu hata walipoanzia. Nilikuwa hapa dukani ghafla nikashtuka mtu anaingia ndani huku akisema nakufa, kabla hata sijamuuliza kilichomsibu umati watu ukawa umeshajazana dukani kwangu ndipo nilipolazimika kufunga mlango na kuwaita polisi,” alisema Karim.
Seif atoa mkono wa pole
Maalim Seif, jana aliongoza ujumbe wa viongozi wa Serikali kutoa pole kwa wafiwa waliopoteza ndugu na jamaa zao. Katika ziara hiyo, alifuatana Mawaziri wasiokuwa na Wizara Maalumu; Haji Faki Shaali na Machano Othman Said, Waziri wa Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Vijana, Wanawake na Watoto, Zainab Omar na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Said Ali Mbarouk.
Akizungumza na ndugu na jamaa wa marehemu hao katika Ukumbi wa Umoja ni Nguvu, Mkoani na baadaye Uwanja wa Gombani katika Mkoa wa Kusini Pemba, Maalim Seif aliwataka wakazi wa Zanzibar, kuvuta subira kwa kuwa msiba huo ni wa taifa zima na ni mipango ya Mungu.
Alisema Serikali inaamini kuwa kulikuwa na uzembe katika tukio hilo ndiyo maana imeamua kuunda tume huru ambayo itafanya uchunguzi wa kina kuhusu suala hilo.Alisema Serikali haitasita kumchukulia hatua mtendaji yeyote atakayebainika kuhusika katika uzembe uliosababisha ajali hiyo.Akiwa Mkoa wa kusini Pemba, Maalim Seif ametoa mkono wa pole na ubani kwa familia zaidi ya 112.
![]() |
| MV Spice Islander Ikipakia Mizigo Zanzibar |
Elias Msuya na Jackson Odoyo, Zanzibar
MELI ya MV Spice Islanders iliyopata ajali mwishoni mwa wiki iliyopita na kusababisha vifo vya takriban watu 200 na majeruhi 619 ambao waliokopolewa, ilibeba abiria 3,000 wakati uwezo wake ni kubeba abiria 600 tu.Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa idadi hiyo kubwa ya abiria, haijumuishi mizigo ambayo kiasi chake bado hakijajulikana.
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Dadi Fakhi Dadi alisema jana kuwa mkoa huo umepoteza watu 1,600 katika ajali hiyo, huku Wilaya ya Wete pekee ikiwa imepoteza watu 1,141.Dadi alisema hayo alipokuwa akizungumza mbele ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.
“Wilaya ya Micheweni imepoteza watu 367, huku Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba ikipoteza watu 27 na Wilaya ya Chakechake imepoteza watu 148,” alisema Dadi na kuongeza:
“Kwa idadi hiyo ikijumlishwa na idadi ya watu 619 waliosalimika katika ajali hiyo na wengine 204 waliotambuliwa na kuzikwa na wengine watano waliookotwa Mombasa, huenda meli ile ilikuwa na watu 3, 000,” alisema Dadi.
Kutokana na takwimu zinazoendelea kukusanywa, hadi sasa zaidi ya watu 2,000 hawajulikani walipo, mbali ya wale 198 walioopolewa na kuzikwa na wengine 619 walionusurika.
Wabunge wa CUF wajiandaa kuishtaki Serikali
Wakati Serikali ikiendelea kukusanya takwimu za waliokufa au kupotea kwenye ajali hiyo, baadhi ya wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF), wamekuwa wakizunguka majimboni mwao kufanya tathmini kwa lengo la kuishtaki Serikali.
Mbunge wa Jimbo la Ziwani, Ahmed Juma Ngwali alisema anatafuta idadi kamili ya wananchi wake walioathirika kwa ajali hiyo ili afanye utaratibu wa kuishtaki Serikali kutokana na uzembe uliosababisha ajali hiyo.
“Tukishapata orodha kamili ya wananchi, nakwenda kutafuta orodha ya abiria waliokuwa kwenye meli, nalinganisha. Kwa wale waliokuwa na tiketi, nitasimamia walipwe bima zao na mmiliki wa meli. Wale waliozidi nitaishtaki Serikali kwa kuzembea,” alisema Ngwali.
Ngwali aliyekuwa akizunguka nyumba hadi nyumba kuorodhesha watu hao, alisema kwa kiasi kikubwa, Serikali ndiyo iliyofanya uzembe katika tukio hilo.
“Huu ni uzembe na ni lazima twende mahakamani. Ikiwa samaki wa Magufuli (Waziri wa Ujenzi), hadi leo wanasotesha watu mahakamani, itakuja kuwa watu?” alisema.
Mbunge wa Ole, Rajab Mbarouk alisema anakusudia kupeleka hoja binafsi bungeni ili kumwajibisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwa tukio hilo.
"Inaonyesha Serikali haina takwimu sahihi, ndiyo maana sisi tumeamua kufanya tathmini ya kina,” alisema na kuongeza kuwa tathmini hiyo itamsaidia kuratibu misaada anayopata kutoka kwa mashirika mbalimbali kwa ajili ya watu walioathirika katika tukio hilo.
“Kwa mfano sasa Benki ya Watu wa Kenya (KCB) imetoa ahadi ya kusomesha watoto yatima waliofiwa na wazazi katika ajali hiyo. Lazima niwe na takwimu sahihi za kuwapa benki hiyo,” alisema Mbarouk.
Akizungumzia suala la Waziri Mkuu mbunge huyo alisema: “Sisi ni wasemaji wa wananchi siyo Serikali. Nina mpango wa kupeleka hoja binafsi Bungeni ili Waziri Mkuu awajibike.”
Alieleza sababu za kutaka Waziri Mkuu awajibike kuwa ni pamoja na Serikali kupuuza swali lake alilouliza bungeni kuhusu usalama wa vyombo vya majini hadi sasa.
Kazi ya kuwaokoa walizama bado nguvu
Kazi ya uokoaji wa miili ya watu wanaosadikiwa kunasa ndani ya meli hiyo inaonekana kuwa ngumu baada ya wataalamu wa uokoaji kutoka Afrika Kusini kushindwa kuendelea na kazi kutokana na kina kirefu cha maji katika eneo hilo.
Tetesi za kushindikana kwa kazi hiyo zilianza kusikika jana kutoka kwa wavuvi ambao wamekuwa wakifanya kazi zao katika eneo hilo kwa kipindi kirefu huku. Wavuvi hao wanasema eneo hilo lina urefu wa zaidi ya mita 300 kutoka usawa wa bahari.
Mzamiaji kutoka eneo la Nungwi, Karim Abdallah alisema: “Hili eneo tunalifahamu lina kina kirefu sana unaweza kubeba kamba zinazojaza boti na ukifika eneo hilo na kutupa nanga haifiki chini, tulifahamu kwamba wataalamu hao hawawezi kufanya lolote katika eneo hilo.”
Kauli ya wavuvi hao ilionekana kuthibitishwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) ambayo iliamua kuondoa mahema yaliyokuwa yamewekwa katika fukwe za Nungwi kwa ajili ya kuhifadhi miili ilinayopatikana.
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Pembe Juma alisema wameamua kuanua mahema hayo kwa sababu uwezekano wa kupata miili iliyobaki ni mdogo.
“Tumelazimika kuondoa mahema hayo kwa sababu hali inavyoonekana ni wazi kuwa wataalamu hao wanaweza wakashindwa kupata miili ya watu wanaokisiwa kubaki katika eneo hilo” alisema Juma.
Hata hivyo, alipoulizwa juu ya hali ya waokoaji hao ambao bado wako katika eneo la tukio wakiongozwa na Kikosi cha Maji cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) alisema: “Sina mamlaka ya kuzungumzia mazingira ya wataalamu hao isipokuwa taarifa nilizonazo kwa sasa ndizo hizo nilizowapa.”
Wataalamu hao walitakiwa kuanza kazi hiyo juzi lakini wakashindwa kuendelea na kazi hiyo kwa sababu ya hali ya bahari kuwa mbaya. Hata hivyo, walianza tena kazi hiyo leo ingawa si kwa kuingia baharini kutafuta waliokwama chini ya maji, bali kutafuta maiti zinazoelea katika maeneo mbalimbali ya Tanga, Mombasa, Unguja na Pemba.
Katika hatua nyingine mtu mmoja alinusurika jana baada ya kuwadhihaki hadharani watu waliokumbwa na mkasa huo wa ajali ya meli kwa kudai kwamba walistahili.
Mashuhuda waliokuwapo katika eneo hilo walidai kuwa sekunde chache baada ya kutamka maneno hayo, alivamiwa na watu waliokuwa eneo hilo lakini akafanikiwa kukimbilia katika duka la vitabu la Masomo na hatimaye kuokolewa na Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiongozwa na Mkuu wa Polisi Kituo cha Malindi, Haji Mgoro.
Mkurugenzi wa duka hilo, Farouk Karim Karim alisema hatua ya mtu huyo kukimbilia dukani kwake ilihatarisha maisha yake baada ya umati watu kufunga mitaa yote inayozunguka Soko Kuu la Darajani ukimlazimisha kumtoa mtu huyo vinginevyo waingie kumtoa wenyewe.
“Kwa kweli mimi sikufahamu hata walipoanzia. Nilikuwa hapa dukani ghafla nikashtuka mtu anaingia ndani huku akisema nakufa, kabla hata sijamuuliza kilichomsibu umati watu ukawa umeshajazana dukani kwangu ndipo nilipolazimika kufunga mlango na kuwaita polisi,” alisema Karim.
Seif atoa mkono wa pole
Maalim Seif, jana aliongoza ujumbe wa viongozi wa Serikali kutoa pole kwa wafiwa waliopoteza ndugu na jamaa zao. Katika ziara hiyo, alifuatana Mawaziri wasiokuwa na Wizara Maalumu; Haji Faki Shaali na Machano Othman Said, Waziri wa Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Vijana, Wanawake na Watoto, Zainab Omar na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Said Ali Mbarouk.
Akizungumza na ndugu na jamaa wa marehemu hao katika Ukumbi wa Umoja ni Nguvu, Mkoani na baadaye Uwanja wa Gombani katika Mkoa wa Kusini Pemba, Maalim Seif aliwataka wakazi wa Zanzibar, kuvuta subira kwa kuwa msiba huo ni wa taifa zima na ni mipango ya Mungu.
Alisema Serikali inaamini kuwa kulikuwa na uzembe katika tukio hilo ndiyo maana imeamua kuunda tume huru ambayo itafanya uchunguzi wa kina kuhusu suala hilo.Alisema Serikali haitasita kumchukulia hatua mtendaji yeyote atakayebainika kuhusika katika uzembe uliosababisha ajali hiyo.Akiwa Mkoa wa kusini Pemba, Maalim Seif ametoa mkono wa pole na ubani kwa familia zaidi ya 112.
Saturday, September 10, 2011
Ajali ya meli Zanzibar - Update
| (Picha -kutoka Michuzi Blog Watu wengi wamemiminika Nungwi kusubiri kutambua maiti na kujulia hali ya ndugu zao.) |
Zaidi ya watu 100 bado hawajulikani walipo, lakini watu 325 walionusurika wameokolewa, kwa mujibu wa waziri wa masuala ya dharura wa Zanzibar.
Meli hiyo, MV Spice Islander ilikuwa ikisafiri kati ya Kisiwa kikuu cha Unguja kuelekea Pemba.
Meli hiyo ilikuwa ikirejesha watu baada ya kumalizika kwa mfungo wa Ramadhani.
Msaada
Mamlaka za huko zimezidiwa na tukio hilo na zimeomba msaada kutoka nje.Serikali ya Zanzibar imeunda kituo cha uokoaji na kutoa wito kwa taasisi zote kusaidia katika shughuli za uokozi. Serikali hiyo pia imeomba msaada kutoka nchi nyingine za nje, kama vile Kenya na Afrika Kusini.
Walionusurika walichukuliwa na boti za kibinafsi na kupelekwa katika bandari ya Zanzibar, amekaririwa kamishna wa polisi wa Zanzibar Mussa Hamis.
Watu walionusurika wakipelekwa hospitali Miili ya watu imekuwa ikisukumwa katika pwani ya Zanzibar na mawimbi. Mpaka sasa miili ya watu 100 wamepatikana, amesema mwandishi wa BBC Ali Saleh akiwa Zanzibar.
Maelfu ya ndugu na jamaa wanasubiri kusikia taarifa za ndugu zao ambao walikuwa ndani ya meli hiyo, anasema mwandishi wetu.
Mohhamed Aboud, waziri wa masuala ya dharura wa Zanzibar anasema watu 259 walionusurika wameokolewa lakini 40 kati yao wamejeruhiwa sana.
Boti yetu imechelewa kwa sababu wanatumia vyombo vyote vya baharini kuokoa watuCatherine Purvis
Catherine Purvis, mtalii kutoka Uingereza aliyepo Zanzibar, akisubiri boti ya kwenda Dar es Salaam amesema ameshuhudia miili ya watu wengi ikitolewa ndani ya maji.
“Nimesimama katika bandari ya Zanzibar nikiwa na watalii wengine kama 10 wa Marekani na Uingereza.
“Boti yetu imechelewa kwa sababu wanatumia vyombo vyote vya baharini kuokoa watu”.
Rubani mmoja wa helikopta Kapteni Neels van Eijk alipita juu ya eneo la tukio.
“Tuliona walionusurika wakiwa wameshikilia magodoro na majokofu au chochote kile kinachoweza kuelea. Ni vigumu kusema idadi kamili, lakini naweza kusema walikuwepo zaidi ya watu 200 walionusurika ndani ya maji na miili ya watu pia,” ameiambia BBC.
Shughuli za uokoaji pwani ya Zanzibar “Wakati huo, kulikuwa na boti chache zilizofika katika eneo hilo. Walikuwa wakitafuta walionusurika, ingawa bahari haikuwa imechafuka sana, mawimbi walikuwa makubwa, kwa hiyo ilikuwa vugumu kuona walionusurika.
“Tulirusha ndege yetu na kuziongoza boti hadi kwa watu walionusurika ili waweze kuwachukua. Kulikuwa na miili kadhaa ndaniya maji.”
Meli hiyo iliondoka Unguja takriban saa tatu usiku saa za Afrika Mashariki na inadhaniwa kuwa ilizama majira ya saa saba usiku.
Ilikuwa imebeba abiria wengi kiasi kwamba baadhi ya abiria waligoma kupanda, amekaririwa abiria mmoja aliyenusurika Abdullah daid, akizungumza na shirika la habari la AP.
BBC
![]() |
| ( Body of Zanzibar Ferry Disaster Victim is Recovered -Picha kutoka The Guardian UK) |
Meli Imezama Zanzibar - Mamia Wamekufa!
Wadau, kumradhi muda huu nimegundua hii ya meli iliyozama ni feki. Siyo MV Spice Islandder. Picha ya Juu ndo MV Spice Islander. Picha hii ilipigwa 2007.
![]() | |
| (Pichani - Meli M.V. Spice Islanders ikiwa imezama Pwani ya Nungwi Picha kwa hisani ya mdau Ahmed Muhamed Ahmed wa Zanzinet) |
Meli M.V. Spice Islanders imezama baharini ikitoka Zanzibar kwenda Pemba. Habari zinasema kuwa meli iilikuwa imejaza kupita kiasi abiria na mizigo! Imezama eneo la Nungwi, pwani ya Zanzibar.
*********************************************************
STONE TOWN, Tanzania (AP) - An overcrowded ship sank in deep sea off mainland Tanzania on Saturday with about 600 people onboard, and about 370 people are believed missing or dead.
The ferry, M.V. Spice Islanders, was heavily overloaded and some potential passengers had refused to board when it was leaving the mainland port of Dar es Salaam, said
About 230 people had been rescued and 40 bodies had been recovered, said Mohamed Abud, the minister for the vice president's office.
Thousands of residents mobbed the docks of Stone Town on Zanzibar, an island near Pemba, waiting for news. One man was screaming that he had lost 25 members of his family, including his sisters, his wife and grandsons. He was too upset to give his name. Many of the crowd were crying or screaming.
Seven bodies have washed up so far, said witness Abdirizak Juma.
Many of those present expressed anger that the ship had been allowed to leave port so overloaded and called on government officials to resign.
The green and hilly island of Pemba is often described as one of the best scuba diving destinations in the world.
Subscribe to:
Comments (Atom)














