Thursday, January 03, 2013

Ujumbe Muhimu Kwa Tanzania Diaspora Kutoka Serikali ya TZ


KUWATUMIA WATAALAMU WA KITANZANIA WALIOKO UGHAIBUNI        (DIASPORA) NA NDANI YA NCHI KUJENGA UWEZO NA UFANISI WA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI MUHIMU ZA SERIKALI

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inakusudia kuwatumia wataalamu wa Kitanzania walioko ndani ya nchi na wale walioko ughaibuni (Diaspora) katika kutekeleza mipango yake kadhaa yenye umuhimu kwa Taifa.

Hapo awali, Serikali iliwatumia zaidi wataalamu kutoka nchi nyingine, ambapo kwa sasa lengo ni kuona kwamba wataalamu wa nchi nyingine wanatumika pale tu ambapo wataalamu wa Kitanzania walio ndani na nje ya nchi hawajapatikana kufanya kazi husika.

Katika kutekeleza azma hiyo, Serikali itapenda kupata wataalamu wa Kitanzania kwenye maeneo yafuatayo:-
(i) Mfumo mzima wa utafutaji, uchimbaji, uongezaji thamani na usambazaji wa gesi asilia na mafuta.

(ii) Kuimarisha matumizi salama ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika kuboresha utendaji wa Serikali na utoaji wa huduma kwa wananchi.

(iii) Kuboresha utekelezaji wa malengo ya Serikali na kupima matokeo kupitia mfumo unaokusudiwa kuhakikisha tunapata matokeo makubwa na ya haraka katika maeneo ya kipaumbele na kimkakati katika maendeleo ya Taifa.

Wataalamu watakaojitokeza na kukubaliwa kufanya kazi Serikalini katika maeneo haya, watafanya kazi kwa mikataba ya muda mfupi, lakini inayoweza kuongezwa iwapo utendaji utaridhisha.

Mwito unatolewa kwa Wataalamu wa Kitanzania popote walipo, ughaibuni au ndani ya nchi, kujitokeza na kuleta wasifu wao (CV’s) pamoja na maelezo ya kwa nini wanafikiri wao ni aina ya watu tunaowatafuta. Tumia anuani ifuatayo:-


Katibu Mkuu Kiongozi
Ofisi ya Rais, Ikulu
S.L.P. 9120
DAR ES SALAAM

Habari Njema kwa wanaotaka kuleta familia zao Marekani - Heko Rais Obama!

Kutoka New York Times

Immigration Change to Ease Family Separations

By JULIA PRESTON


Published: January 2, 2013

Obama administration officials unveiled rules on Wednesday that will allow many American citizens — perhaps hundreds of thousands — to avoid long separations from immediate family members who are illegal immigrants as they apply to become legal residents.

The rules, announced by Homeland Security Secretary Janet Napolitano, create a waiver that bypasses an arcane Catch-22 in immigration law. It had presented Americans with the prospect of being separated for up to a decade from immigrant spouses, children or parents who were applying for the legal documents known as green cards.

Until now, the risks for those immigrants of leaving the United States to return to their native countries to pick up their visas, even ones that were already approved, had been so great that countless families decided not to apply, adding to the numbers of immigrants living illegally in this country.

The immigration authorities will begin accepting applications for the waivers on March 3. Administration officials first announced the policy change a year ago, but they have been receiving public comments and making revisions before publishing the final rules.

It is generally straightforward for American citizens to obtain green cards for foreign-born spouses or minor children, and in some cases for parents. But if the immigrants entered the United States illegally, they must return to their native countries to receive their visas from American consulates there. However, under a 1996 statute, once illegal immigrants leave this country, they are barred automatically from returning for at least three and as many as 10 years.

Even immigrants who did not incur any bars to re-entry were often stranded overseas for many months while consulates completed their applications.

With the new rules, Americans’ family members can apply in the United States for a waiver from the bars to re-entry, before they leave to pick up their visas. Officials estimated the time immigrants would have to spend out of the country would be reduced to “a matter of weeks.”

“One of the critical benefits is that the individual will not be separated from the United States citizen family member during the application process,” said Alejandro Mayorkas, the director of United States Citizenship and Immigration Services, the agency that issues green cards.

For immigrants, officials said, having an approved waiver in hand before leaving the country would also eliminate many doubts about whether they would ultimately receive their visas.

“This rule is leaps and bounds better than what we have now,” said Laura Lichter, president of the American Immigration Lawyers Association. “For families that were sitting on the fence, unwilling to subject their loved ones to the uncertainty, now they don’t have to wait.”

Ms. Lichter said many families would still face a hurdle in coming up with the $585 application fee for the waiver.

One American who was heartened by the new rule is Erika Torres, 30. She has been married for six years to a Mexican man who was brought illegally to the United States 24 years ago, when he was 8. Ms. Torres, speaking by telephone on Wednesday, said she and her husband, who have known each other since they were children, now own a home and a winemaking business in Cambria, Calif.

Like many Americans, Ms. Torres said she expected no difficulty gaining legal documents for her husband once they were married. But after learning about the convoluted visa process, she said, “We have waited because we were just terrified of the separation.”

Ms. Torres said her husband would probably have to collect his visa from the American Consulate in Ciudad Juárez, Mexico, a city racked by drug trafficking violence. “He would be a prime target for kidnappers,” she said.

“We are a team,” Ms. Torres said, adding that she feared she would not be able to sustain their business without her husband’s help. She said they would apply for a waiver as soon as they became available.

The rules do not give any legal status to illegal immigrants or shortcut the underlying application. In order to receive green cards, immigrants must still show that it would cause “extreme hardship” to an American citizen if they were deported.

“It is a limited change, but a definitely a good step forward in the right direction,” said Randall Emery, president of American Families United, an organization of thousands of Americans with family members who are illegal immigrants.

Ms. Lichter called on Congress to change the law to eliminate the snag created by the automatic bars. “This is a great solution to a problem that should never have existed in the first place,” she said.

Msaidie Binti Nancy Peter Kwa Kuomba na Kufunga - Anaumwa Kansa

Ratiba ya kufunga na kuomba, mafungo ya Danieli January 2, 2013 mpaka January 23, 2013


Line ya maombi ni 213-417-9250 Access code 309038#

Namba ya Mama Nancy pamoja na Nancy 484-320-0044

Muda wa maombi tutaanza leo 01/01/ 13 mpaka 01/23/13 9pm to 10pm

Maombi ya mkesha Ijumaa 01/04/13 11pm to 5am- International Gospel Church

-Tunaomba kwa ajili ya nguvu za Mungu za uponyaji kwa ajili ya mdogo wetu, mtoto wetu na dada yetu Nancy Koku Rwechungura

-Pia kila mtu atafakari na kuorothesha vitu ambavyo anataka Mungu amfanyie mwaka huu 2013. Tumia muda huu wa pamoja kumtafuta Mungu kwa binafsi pia.

Mistari ya kusimamia- Kwa uponyaji wa Nancy

Psalms 107:19-20

Then they cried to the LORD in their trouble, and he saved them from their distress. 20 He sent out his word and healed them; he rescued them from the grave.

James 5:14-15 "Is any sick among you? Let him call for the elders of the church; and let them pray over him, anointing him with oil in the name of the Lord: And the prayer of faith shall save the sick, and the Lord shall raise him up; and if he have committed sins, they shall be forgiven him."

Deutoronomy 7:15 – Kumbukumbu la torati 7:15

15 The LORD will keep you free from every disease. He will not inflict on you the horrible diseases you knew in Egypt, but he will inflict them on all who hate you.

Jeremiah 30:17 For I will restore health unto thee, and I will heal thee of thy wounds, saith the LORD; because they called thee an Outcast, saying, This is Zion, whom no man seeketh after

Psalms 43:1 The LORD sustains them on their sickbed and restores them from their bed of illness.

Kwa maombi ya binafsi:

Isaiah 58:6-11

6 “Is not this the kind of fasting I have chosen: to loose the chains of injustice

and untie the cords of the yoke, to set the oppressed free

and break every yoke? 7 Is it not to share your food with the hungry

and to provide the poor wanderer with shelter— when you see the naked, to clothe them, and not to turn away from your own flesh and blood?

8 Then your light will break forth like the dawn, and your healing will quickly appear; then your righteousness[a] will go before you, and the glory of the LORD will be your rear guard. 9 Then you will call, and the LORD will answer;

you will cry for help, and he will say: Here am I. “If you do away with the yoke of oppression, with the pointing finger and malicious talk,

10 and if you spend yourselves in behalf of the hungry and satisfy the needs of the oppressed, then your light will rise in the darkness, and your night will become like the noonday. 11 The LORD will guide you always; he will satisfy your needs in a sun-scorched land and will strengthen your frame.

You will be like a well-watered garden, like a spring whose waters never fail.

Jeremia 33:3 Call to me and I will answer you and tell you great and unsearchable things you do not know.

2 Chronicles 7:14

14 if my people, who are called by my name, will humble themselves and pray and seek my face and turn from their wicked ways, then I will hear from heaven, and I will forgive their sin and will heal their land.

Psalms 145: 18-19

18 The LORD is near to all who call on him, to all who call on him in truth.

19 He fulfills the desires of those who fear him; he hears their cry and saves them.

Kila mtu yuko huru kupanga ratiba ya kula. Hakuna restriction ya kukaa bila kula siku nzima ila restriction ni kufuatilia vyakula vinavyoruhusiwa kuliwa. Angalia list hiyo ya vyakula. Pia tujitahidi na kukutana kwa maombi ya pamoja angalau mara moja kwa siku, kama huwezi kuingia kwenye maombi ya usiku niambie ili nipange muda wa kuomba nawewe au wewe na Nancy na mama au baba yake.

Daniel 10:2, 3

“In those days I, Daniel, was mourning three full weeks. I ate no pleasant food, no meat or wine came into my mouth, nor did I anoint myself at all, till three whole weeks were fulfilled.”

Please make sure to READ THE LABEL when purchasing packaged, canned or bottled foods. They should be sugar-free and chemical-free. Keep this in mind as you review this list of acceptable foods. They should also not contain cane sugar.

Foods to include in your diet during the Daniel Fast

All fruits. These can be fresh, frozen, dried, juiced or canned. Fruits include but are not limited to apples, apricots, bananas, blackberries, blueberries, boysenberries, cantaloupe, cherries, cranberries, figs, grapefruit, grapes, guava, honeydew melon, kiwi, lemons, limes, mangoes, nectarines, oranges, papayas, peaches, pears, pineapples, plums, prunes, raisins, raspberries, strawberries, tangelos, tangerines, watermelon

All vegetables. These can be fresh, frozen, dried, juiced or canned. Vegetables include but are not limited to artichokes, asparagus, beets, broccoli, Brussels sprouts, cabbage, carrots, cauliflower, celery, chili peppers, collard greens, corn, cucumbers, eggplant, garlic, ginger root, kale, leeks, lettuce, mushrooms, mustard greens, okra, onions, parsley, potatoes, radishes, rutabagas, scallions, spinach, sprouts, squashes, sweet potatoes, tomatoes, turnips, watercress, yams, zucchini, veggie burgers are an option if you are not allergic to soy.

All whole grains, including but not limited to whole wheat, brown rice, millet, quinoa, oats, barley, grits, whole wheat pasta, whole wheat tortillas, rice cakes and popcorn.

All nuts and seeds, including but not limited to sunflower seeds, cashews, peanuts, sesame. Also nut butters including peanut butter.

All legumes. These can be canned or dried. Legumes include but are not limited to dried beans, pinto beans, split peas, lentils, black eyed peas, kidney beans, black beans, cannellini beans, white beans.

All quality oils including but not limited to olive, canola, grape seed, peanut, and sesame.

Beverages: spring water, distilled water or other pure waters.

Other: tofu, soy products, vinegar, seasonings, salt, herbs and spices.

Foods to avoid on the Daniel Fast

All meat and animal products including but not limited to beef, lamb, pork, poultry, and fish.

All dairy products including but not limited to milk, cheese, cream, butter, and eggs.

All sweetenersincluding but not limited to sugar, raw sugar, honey, syrups, molasses, and cane juice.

All leavened bread including Ezekiel Bread (it contains yeast and honey) and baked goods.

All refined and processed food products including but not limited to artificial flavorings, food additives, chemicals, white rice, white flour, and foods that contain artificial preservatives.

All deep fried foods including but not limited to potato chips, French fries, corn chips.

All solid fats including shortening, margarine, lard and foods high in fat.

Beverages including but not limited to coffee, tea, herbal teas, carbonated beverages, energy drinks, and alcohol.

Remember, READ THE LABELS!

************************************************************



Hii fundraiser ilifanyika mwezi Novemba lakini juhudi za kumsaidia zinaendelea.

Maandamano dhidi ya Bomba la Gesi: Kilio cha Uwajibikaji

Maandamano dhidi ya Bomba la Gesi

Picha Hisani ya: Mtwara Kumekucha Blog by Baraka Mfunguo

'Dar inachangia asilimia 80 ya mapato. Kitovu cha Uchumi. Dar inachangia 90% ya ufisadi. Uti wa mgongo wa ufisadi nchini'


Na Mh. Zitto Kabwe
Malumbano kati ya wananchi wa Mtwara na Serikali kuhusu matumizi bora ya utajiri wa nchi yameendelea kwa takribani wiki moja sasa. Baada ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara na Waziri wa Nishati na Madini kuwaita Watanzania wa Mtwara Wahaini, wapuuzi na watu hatari, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania naye aliingia kwenye mjadala huo kwa kuonya watu wanaowaunga mkono watu wa Mtwara na kuwaita watu wanaotafuta umaarufu wa kisiasa na wanaotaka kugawa nchi. Siku moja baada ya hotuba ya Rais, Waziri wa Nishati na Madini alifanya mkutano na waandishi wa habari kueleza suala lile lile ambalo bosi wake alilielezea usiku wa kuamkia mwaka mpya 2013. Hii ni dalili ya Serikali kuweweseka.

Katika kauli ya Serikali, ambayo haikuwa na jipya zaidi ya wimbo ule ule wa ‘kugawa nchi’ ‘umaarufu wa kisiasa’ nk, Serikali ilitaka kuonyesha umma kuwa watu wa Mtwara hawana shukurani. Kwamba miaka yote toka Uhuru watu wa Mtwara wamekuwa wakilishwa na Pamba, Kahawa, Chai, Tumbaku, Sukari, Kidatu nk. Kwamba watu wa Mtwara na Lindi hawakuchangia hata kidogo kwenye hazina ya Taifa. Hivyo wao kupigia kelele gesi yao ni uchoyo na roho mbaya na kukosa shukurani. Kauli ya Serikali ni kauli ya chombo kinachoendelea kukosa ‘legitimacy’ ya kuongoza taifa. Ni kauli ya kukata tamaa. Ni kauli hatari sana dhidi ya Watanzania waliojitolea damu kulinda uhuru wa nchi yetu.

Moja, Serikali katika kauli yake haitaji kabisa kwamba toka Uhuru watu wa Mtwara na Lindi wamekuwa wachangiaji wakubwa sana katika uchumi wa Taifa kupitia zao la Korosho. Takwimu za Uzalishaji wa Korosho zinaonyesha kwamba kuanzia mwaka 1965 mpaka 2011 Korosho imeliingizia Taifa fedha kigeni jumla ya dola za Kimarekani 4.58 bilioni ( Cashewnuts Sub-sector study 2003, Hali ya Uchumi 2012, Cashewnuts Tanzania Report 2010). Katika Mwaka wa Uchumi unaoishia Novemba 2012, Korosho imeliingizia Taifa jumla ya dola za Kimarekani 151 milioni. Katika mwaka 2011 zao hili liliingiza dola 130 milioni wakati Pamba iliingiza dola 53 milioni tu. Licha ya Zao la Korosho kuingiza fedha hizi za kigeni (sawa ni shilingi trilioni 7.2) kwa nchi mikoa ya Lindi na Mtwara ipo miaka 50 nyuma kimaendeleo kulinganisha na mikoa mingine ya Tanzania. Serikali inataka kufuta historia ya mchango wa zao la Korosho kwenye uchumi wa nchi yetu kwa sababu ya uroho wa gesi asilia. Kwa nini kauli rasmi ya Serikali haijataja Korosho kabisa? Kauli hii ilipitishwa na ngazi zote za Serikali? Mawaziri wa Serikali wanaotoka mikoa ya Lindi na Mtwara walikubali kauli kama hii itoke dhidi ya wananchi wao wanaoteseka na zao la Korosho miaka nenda miaka rudi?

Pili, Serikali imesahau kabisa mchango wa watu wa Lindi na Mtwara katika ulinzi wa Taifa letu. Moja ya sababu ya mikoa ya Lindi na Mtwara kuwa nyuma kimaendeleo ni juhudi za ukombozi wa kusini mwa Afrika. Kambi ya wapigania uhuru wa Msumbiji ilikuwa Nachingwea. Kambi ya Frelimo iliwekwa kwenye Shamba la Mkonge kilometa 17 tu kutoka mjini Nachingwea ambapo ilikuwa makao makuu ya ukombozi wa Msumbiji. Rais Samora Machel, Rais Joaqim Chissano na Rais Guebuza waliendesha mapambano kutoka kusini mwa Tanzania. Makaburu wa Afrika Kusini na Wareno walikuwa wanashambulia nchi yetu na mikoa hii miwili ya Lindi na Mtwara ikawa ‘buffer zone’. Wakati Dar es Salaam inaendelea kwa kila aina ya maendeleo, mikoa ya Lindi na Mtwara ilikuwa inalinda ili wanaoishi Dar es Salaam na mikoa mingine waishi wa amani na starehe. Serikali inapimaje mchango huu wa mikoa hii? Tunaipima kwa fedha? Uroho wa gesi asilia kuzalisha umeme wa kufurahisha walalaheri asilimia 14 nchini ndio inaifanya Serikali kusahau kabisa ‘sacrifice’ ya watu wa Mtwara katika kulinda uhuru wa Taifa letu?

Tatu, Serikali inasema lazima bomba lije Dar es Salaam kwa sababu Dar ndio inazalisha asilimia 80 ya Mapato ya Serikali. Kwanza huu ni uwongo. Ni aibu Serikali kujitetea kwa uwongo. Dar es Salaam ni kituo tu cha kukusanyia mapato ya Serikali. Uzalishaji mkubwa wa nchi yetu wenye kuzalisha kodi unafanyika nje ya Dar es Salaam. Walipa kodi wakubwa wengi Ofisi zao Kuu zipo Dar es Salaam lakini uzalishaji wao unafanyika nje ya Dar es Salaam. Serikali itoe orodha ya walipa kodi wakubwa 100 tuone uzalishaji halisi wa mapato hayo unafanyika wapi. Hata hivyo inawezekana kuwa ikawa kweli Dar es Salaam inakusanya asilimia 80 ya mapato ya nchi. Basi na tuseme Dar es Salaam inachangia asilimia 90 ya ufisadi wote nchini. Kashfa zote kubwa za Ufisadi zinafanyika Dar es Salaam na fedha nyingi za ufisadi zinatumika Dar es Salaam.

Mwisho, maandamano ya watu wa Mtwara ni kielelezo tosha kwamba watu wa mikoa ya Lindi na Mtwara wamechoshwa na longolongo za Serikali. Wananchi wa Mtwara na Lindi wanataka Uwajibikaji wa Serikali kuhusu utajiri wa nchi. Mtanzania yeyote mwenye tahadhari ya nchi yetu kutokuwa na laana ya rasilimali ataungana mkono na watu wa Lindi na Mtwara kudai maendeleo. Nilitoa mfano wa Mgodi wa Golden Pride ambao umemaliza dhahabu yote tani 76 katika eneo la Lusu wilayani Nzega. Kampuni ya Resolute ya Australia iliwekeza dola 370 milioni kuanzia mwaka 1998 (mkataba wao ulisainiwa 25th June 1997). Katika kipindi cha uhai wa mgodi, miaka 14, Kampuni hii imeuza dhahabu ya thamani ya dola za kimarekani 3.3 bilioni. Kabla Serikali haijawaita watu Mtwara wahaini, wapuuzi na watu hatari, iwaambie watu Watanzania kodi kiasi gani imekusanywa kutoka mgodi huu katika kipindi cha miaka 14. Mpaka mwaka 2008, kwa mujibu wa Taarifa ya Kamati ya Bomani, kampuni hii ilikuwa imelipa mrahaba wa dola 11 milioni na kodi nyingine dola 16 milioni. Serikali itwambie ilipofika Disemba 2012 kodi kiasi imekusanywa kutoka kampuni hii?

Pia watu wa Mtwara na Lindi wameona historia ya bomba la Songosongo. Hata kodi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa (0.3%) ilikuwa inalipwa Halmashauri ya Manispaa Ilala na kampuni ya Pan Africa Energy. Ilichukua juhudi za mbunge wa Kilwa Kaskazini Murtaza Mangungu kuingilia kati ndio kodi ikaanza kulipwa Kilwa ambapo uzalishaji unafanyika. Watu wa Mtwara ni werevu, wanajua wafanyalo. Wanataka utajiri wa nchi unufaishe nchi kwa kuanzia kule utajiri ulipo. Kuna dhambi gani?

Uwajibikaji katika uvunaji wa Rasilimali ya Gesi ndio chanzo cha maandamano ya watu wa Mtwara. Serikali isikimbilie kulaumu wanasiasa kwamba ndio wamechochea maandamano haya. Haya ni maandamno ya wananchi wakitaka Serikali yao iwajibike kwao. Serikali ithubutu kufanya ubabe wa kujenga bomba la gesi bila ridhaa ya Wananchi wa Lindi na Mtwara. Wananchi wanapohitaji uwajibikaji ni wajibu wa Serikali kuwajibika kwao ni sio kuwaita wahaini, wachochezi, watu hatari, wapuuzi. Watu wa Mtwara wamechangia maendeleo ya Taifa letu kwa jasho na damu. Serikali ina wajibu wa kuwasikiliza, kuwaelimisha na kupata mwafaka. Kauli ya Serikali imewatukana watu wa Mtwara na Lindi. Hawatakubali kudhalilishwa. Hawatakubali historia yao kufutwa. Hawatakubali waendelee kubaki nyuma kimaendeleo. Serikali ifikirie tena.

Monday, December 31, 2012

Heri ya Mwaka Mpya 2013!

Nawatakia wadau wote Heri ya Mwaka Mpya 2013!

Happy New Year Everyone!

Saturday, December 29, 2012

Rais Kikwete Amjulia Hali Father Mkenda Aliyepigwa Risasi Zanzibar




Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali  Padri Ambros Mkenda wa Kanisa Katoliki la Mpendae mjini Zanzibar anayeuguza majeraha katika taasisi ya mifupa ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (Moi) jijijini Dar es salaam leo Jumamosi Dsemba 29, 2012 kufuatia kupigwa risasi sehemu za mdomoni na watu wasiojulikana mapema wiki hii  wakati akisubiri kufunguliwa geti  la nyumbani kwake maeneo Kitomondo Mjini Zanzibar akiwa ndani ya gari aliyokuwa akiendesha akiwa pekee yake. Rais Kikwete amempa Padri Mkenda pole nyingi na kumuombea apate nafuu haraka.

PICHA NA IKULU

Friday, December 28, 2012

Merry Christmas & a Happy New Year!


Natumaini mmesherekea vizuri Krimasi. Nawatakia pia Heri ya Mwaka Mpya!


Friday, December 21, 2012

Rais Kikwete Apongezwa na Wasanii Wakongwe Kwa Kuwajali





Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo Desemba 21, 2012 amepokea ujumbe wa wasanii wakongwe wa muziki wa dansi pamoja na filamu uliomtembelea Ikulu jijini Dar es salaaam kwa kuwajali wasanii wa aina zote na hata kuamua kutoa tuzo kwa wasanii ambapo mwaka huu amewatunuku Muhidin Maalim Gurumo na Hayati Marijani Rajabu.

PICHA NA IKULU

Thursday, December 20, 2012

Miss Tanzania Vazi la Taifa Katika Mashindano ya Miss Universe 2012


Wadau, hebu cheki hii Vazi la Taifa aliyovaa Miss Tanzania 2012, Winifrida Dominic, katika Mashindano ya Miss Universe. Samahani lakini sioni UTanzania! 
Miss Tanzania Winfrida Dominic performs onstage at the 2012 Miss Universe National Costume Show at PH Live in Las Vegas, Nevada December 14, 2012. The 89 Miss Universe Contestants will compete for the Diamond Nexus Crown on December 19, 2012. REUTERS/Darren Decker/Miss Universe Organization/Handout



Miss Bostwana 2012
Miss Ethiopia 2012


Tuesday, December 18, 2012

Tanzia - Angela Hiza Bavu


The Late Mrs. Angela Hiza Bavu


UPDATE 12/19/12 - Mwili wa marehemu Mrs. Angela Hiza Bavu, utawasili Dar es Salaam kutoka India na Qatar Airways kesho 12/12/12.  Mazishi yatakuwa Jumamosi 12/22/12, shambani kwa Prof. Bavu huko Kimara Stopover.

*****************************************

Wadau, nimepokea kwa majonzi habari ya kifo cha Mrs. Angela Bavu (nee Angela Hiza), mtoto wa Prof. Hiza. Tulikaa na familia ya Hiza Simba Road, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Mlimani) miaka mingi tangua 1970's hadi 1990's. Wao walikuwa 3 Simba Road, sisi namba 13 Simba Road. Watoto wa Chuo!

Sina details zaidi ya kuwa alikuwa amekwenda India kwenye matibabu.

Natoa pole kwa familia ya Prof. Hiza na Mrs. Hiza, Carolyne, Mary, Msaka, Mpindu, Mhaiyo,  Robert na wengine.

Mungu ailaze roho ya Angela mahala pema mbinguni. Amen.

Nitabandika updates nikizipata.

Athari za Sindano kama Njia ya Uzazi wa Majira

Hii ilichapishwa kwenye Gazeti la Mwananchi, mwezi uliopita (Novemba 2012).  Kwa wanawake wanaotumia sindano kama njia ya uzazi wa majira naona hii ni habari ya kutisha.!


****************************************


UTAFITI WABAINI ZINACHANGIA MAAMBUKIZI YA UKIMWI, ZACHOCHEA HAMU YA MAPENZI, UMATI WAUPONDA, WASEMA HAUJAJITOSHELEZA


UTAFITI umebaini kuwa sindano za uzazi wa mpango zinachangia kasi ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi kwa kuwa zina vichocheo vingi ambavyo vinahuisha virusi vya Ukimwi katika nyumba ya uzazi na kuvipa nguvu ya kusambaa.

Inaelezwa kuwa walio katika hatari zaidi ya maambukizi hayo ni wanawake walioko katika ndoa kwa kuwa ndiyo wanaotumia zaidi sindano hizo.

Utafiti huo uliofanywa na wanasayansi wa Marekani na kuripotiwa na gazeti la The Guardian la Uingereza, umebaini kuwa wanawake wanaotumia sindano za uzazi wa mpango wapo katika hatari mara mbili ya kupata maambukizi ya Ukimwi au kuwaambukiza wenzi wao, kuliko wengine.

Katika utafiti huo uliofanywa katika nchi saba zinazoendelea barani Afrika ikiwamo Tanzania, wanasayansi hao kutoka Chuo Kikuu cha Washington, walipendekeza ushauri zaidi utolewe kwa wanandoa kabla mtu hajajiingiza kwenye matumizi ya sindano kama njia ya kupanga uzazi.

Utafiti huo ulifanyika kwa wanandoa 3,790 kutoka nchi za Tanzania, Afrika Kusini, Zimbabwe, Uganda, Kenya, Rwanda na Botswana, ulichapishwa kwa mara ya kwanza katika Jarida la Afya la Lancet kabla ya kunukuliwa na gazeti la The Guardian.

Utafiti umebaini pia kuwa zaidi ya wanawake 140 milioni duniani wanatumia njia mbalimbali za uzazi wa mpango, huku wanandoa wengi katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, wanaoishi na VVU wakichagua kutumia sindano kama njia ya kuzuia mimba zisizotarajiwa.

Wanasayansi hao walikusanya taarifa kati ya wanandoa 3,790 ambao mmoja wao anaishi na VVU na mwenza wake akiwa hana maambukizo.

Aidha, wanawake ambao wanaishi na VVU na wanatumia sindano hizo pia walikuwa katika hatari zaidi ya kuwaambukiza wenzi wao.

Vipimo vilionyesha kuwa sindano hizo ambazo zina vichocheo ambavyo vinavipa nguvu virusi ndani ya nyumba ya uzazi (cervix).

Imeelezwa kuwa njia za uzazi wa mpango zinazohamasishwa zaidi na kupendwa zaidi na wanawake ni sindano, ambazo wanawake wanasema kuwa zinadumu kwa muda mrefu na zinaweza kutumika bila ya ruhusa au mume kufahamu.

Kiongozi mkuu wa utafiti huo, Renee Heffron wa Chuo Kikuu cha Washington alisema sindano za uzazi wa mpango zina vichocheo vingi ambavyo huvihuisha vijidudu vya Ukimwi katika nyumba ya uzazi na kuvipa nguvu ya kusambaa.

“Ni vyema sasa kama tutasisitiza njia za uzazi wa mpango ambazo ni salama zaidi kama vile mipira ya kiume au njia nyingine ambazo hazina vichocheo (hormones) au zina kiasi kidogo cha vichocheo,” alisema Dk Heffron.

Mwanasayansi mwingine, Charles Morrison wa Kituo cha Afya cha Durham, nchini Marekani alisema uhamasishaji wa matumizi ya sindano za uzazi wa mpango unachochea maambukizi zaidi katika nchi za Jangwa la Sahara.

“Ushauri wangu kwa nchi zinazoendelea ni kuacha matumizi ya njia za uzazi wa mpango zenye vichocheo, ili tupunguze maambukizi, jibu la tatizo hili linatakiwa litafutwe sasa, nchi zinazohusika zinatakiwa zishiriki katika hili,” alisema.

Alivitaka vituo vya afya vitoe ushauri kwa wanawake kutumia kondomu badala ya sindano au vidonge.

Mara nyingi watu wanaotumia vidonge, wengi si wanandoa, mtu anayemeza vidonge vya kuzuia mimba anaogopa zaidi mimba, si Ukimwi.

Huchochea Hamu ya Mapenzi

Mfamasia katika Kitengo cha Dawa kwa watu wanaoishina VVU katika Hospitali ya Amana, Christopher Masika alisema anaafiki kuwa sindano na hata vidonge vinaweza kuwa ni sababu inayochochea maambukizi kwa sababu ya uhuru.

“Ninachokiona mimi katika hilo ni uhuru. Mtu anapotumia sindano huwa huru kufanya ngono kwa kuwa hana hofu ya mimba, hicho kinaweza kumfanya apate maambukizi kwa urahisi, tofauti na anapotumia kondomu,” alisema.

Alisema wapo baadhi ambao wakitumia sindano hizo vichocheo vinawafanya wapate hamu zaidi ya kufanya mapenzi, hivyo huanza kutembea na wanaume wengine.

Aliongeza kuwa mtu anayeishi na VVU akizuia mimba kwa njia ya sindano, ni rahisi kupata maambukizi mapya kutoka kwa mwenza wake.

Masika alisema wanawake wapewe elimu zaidi kwani wapo ambao wanadanganywa kuwa njia za uzazi wa mpango kama sindano, povu zinaweza kuzuia maambukizi, jambo ambalo si la kweli.

Wakati huohuo baadhi ya wanandoa wanaoishi na VVU wanaopata matibabu katika Hospitali ya Amana wamesema kuwa tangu waanze kutumia dawa za kupunguza makali ya Ukimwi (ARVs) hamu ya kufanya mapenzi imeongezeka kwa kasi kubwa.

Mkuu wa Kitengo cha Utafiti cha Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (Tacaids), Dk Arodia Mulokozi, alisema taasisi yake haiwezi kuzungumza lolote kuhusu utafiti huo, badala yake alilitaka Mwananchi kuzungumza na Kitengo cha Afya ya Uzazi wa Mpango cha Muhimbili.

“Hatuhusiki na masuala ya uzazi wa mpango, nafikiri unaweza kuzungumza na Kitengo cha ‘Reproductive Health’ cha Muhimbili,” alisema Dk Mulokozi.

Waziri wa Afya hakupatika, lakini msemaji wa wizara hiyo, Nsachris Mwamwaja alisema ni mapema mno kuchangia kuhusu utafiti huo, atafanya hivyo pindi atakapopata taarifa zaidi.

Mratibu wa Mpango wa Uzazi wa Mpango Tanzania (Umati), Dk Morris Hiza amekiri kuufahamu utafiti huo, lakini akaeleza kuwa haujajitosheleza na bado una maswali mengi.

“Nilikuwapo wakati Heffron anawasilisha utafiti wake mjini Geneva, lakini nakumbuka mkutano ule wa WHO (Shirika la Afya Duniani) uliukataa,” alisema.

Alieleza kuwa Heffton alifanya utafiti huo kwa nyani na wanawake makahaba pekee.

CHANZO: GAZETI LA MWANANCHI

Saturday, December 15, 2012

Msiba - Springfield, MA - Mzee Edson Mwandemani

The late Mzee Edson Mwandemani
arifa za msiba wa mzee wetu, baba yetu Edson Mwandemani (72) alifariki jana Ijumaa akiwa amelazwa katika hospitali ya Bay State Medical Center.

Juhudi kubwa zinaendelea kukusanya michango kwa ajili ya kuurejesha mwili wa marehemu nyumbani Tanzania. Tafadhali tunaomba michango itumwe kwa kupitia Richard Mwandemani Bank Of America Routing number 011000138 Account #004643403251

Msiba uko nyumbani kwa Richard 113 Enfield Street, Indian Orchard, Mass 01151
Kwa taarifa zaidi za msiba unaweza kuwasiliana na:

Richard Mwandemani (413) 262-0400
Isaac Kibodya (413) 219-1153
Kawala Mgawe (413) 330-1609

Tutaendelea kuwaletea taarifa kadri tutakavyozipata.

Tanzania Madagascar Talks


 ARUSHA, Tanzania (AP) - Madagascar President Andry Rajoelina is wrapping up two-days of talks in Tanzania that are aimed at breaking a three-year political stalemate in the Indian Ocean island country.

 The visit comes days after deposed Madagascar leader Marc Ravalomanana said in Tanzania he won't try to stand in next year's elections. Ravalomanana was ousted in a coup in March 2009.

 Tanzania's Foreign Minister Bernard Membe said he is optimistic the Friday and Saturday talks between Tanzania President Jakaya Kikwete and Rajoelina will lead to a "positive settlement." Kikwete heads a southern block of African nations known as the SADC and has been tasked with finding a solution to Madagascar's political troubles.

   Membe said any political agreements should include a general amnesty for domestic and external opponents of Rajoelina.



President Jakaya Kikwete and Transitional President of Madagascar Andry Rajoelina

COMMUNIQUE OF THE MEETING BETWEEN H.E. DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AND H.E. ANDRY RAJOELINA, TRANSITIONAL PRESIDENT OF THE REPUBLIC OF MADAGASCAR
14TH DECEMBER 2012
1.     At the invitation of H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania and the current Chairperson of the SADC Organ on Politics, Defense and Security Cooperation, H.E. Andry Rajoelina, President of the Transitional Government of the Republic of Madagascar paid a two-day working visit to Tanzania from 14th to 15th December 2012.

2.     The invitation was in response to the conclusions of the SADC Extra-Ordinary Summit held on 8th December 2012 in Dar es Salaam, which mandated the Organ Chairperson to brief and hold consultations with H.E. Andry Rajoelina, President of the Transitional Government and H.E. Marc Ravalomanana, former President of Madagascar with regards to the political situation in Madagascar.

3.     It should be recalled that on 10th December 2012, President Kikwete in his capacity as the Chairperson of the SADC Organ met in Dar es Salaam with former President Marc Ravalomanana to discuss decisions of the SADC Summit.

4.     On 11th December 2012, H,E. Ravalomanana and his host, President Kikwete held a joint Press Conference where he officially announced his decision not to contest in the forthcoming Presidential Elections.

5.      On 14th December 2012, President Kikwete and H.E. Rajoelina held in-depth discussions on the conclusions of the Dar es Salaam SADC Summit. The talks were held in a cordial and friendly atmosphere and significant progress has been made. The two leaders agreed to have further consultations with relevant stakeholders prior to meeting again before the end of the month to conclude on the matter.

6.     President Rajoelina thanked his host President Kikwete for the warm hospitality accorded to him and his delegation. He further congratulated the SADC Summit for re-affirming the dates for the elections and for calling the respective parties to respect the same. He also expressed appreciation for SADC’s commitment to mobilize financial resources and logistical support from the International Community.


………………………………………..     …………………………………
Amb. Liberata Mulamula                                      Ms. Annick Rajoana
Senior Personal Assistant to the President          Spokesperson the Transitional
United Republic of Tanzania                                 President of the Republic of Madagascar


Done at Dar es Salaam, United Republic of Tanzania
14th December 2012.

Does Kenya Need a Handsome President?


Thursday, December 13, 2012

Rais Kikwete Akabidhi Nyumba Mpya 35 za Walioathirika na Mlipuko ya Mabomu Gongo la Mboto



Bila kujali mvua kubwa inayonyesha, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiakata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012


Bila kujali mvua kubwa inayonyesha, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mmoja wa walionufaika na hatua ya serikali ya kujenga nyumba mpya 35 kwa ajili ya waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012. Mama huyu ambaye alipoteza mume, amejengewa nyumba ya vyumba vitano pamoja na fremu ya duka.





 Baadhi ya nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala kama zinavyoonekqana leo Desemba 13, 2012 baada ya kuzinduliwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete


PICHA NA IKULU

Saturday, December 08, 2012

Kahawa ya Mavi ya Tembo!

Jamani waBongo! Changamkeni! Kuna kahawa inauzwa bei mbaya mno inayotokana na mavi ya tembo.  Yaani tembo analishwa mbegu za kahawa. Halafu kesho yake hiyo kahawa inachambuliwa kutoka kwenye mavi ya tembo na kusagwa. Wanasema kuwa hiyo kahawa ni tamu mno kwa vile mbegu zinapikwa taratibu ndani ya tumbo ya tembo. Kikombe kimoja kinauzwa kwa dola $50 yaani shs. 60,000/-! 

Tuna tembo kibao na kahawa tele Tanzania. Changamkeni! 



**********************************************
http://news.yahoo.com/coffee-elephants-gut-fills-50-cup-145400810.html
GOLDEN TRIANGLE, Thailand (AP) — In the lush hills of northern Thailand, a herd of 20 elephants is excreting some of the world's most expensive coffee.
Trumpeted as earthy in flavor and smooth on the palate, the exotic new brew is made from beans eaten by Thai elephants and plucked a day later from their dung. A gut reaction inside the elephant creates what its founder calls the coffee's unique taste.
Stomach turning or oddly alluring, this is not just one of the world's most unusual specialty coffees. At $1,100 per kilogram ($500 per pound), it's also among the world's priciest.
For now, only the wealthy or well-traveled have access to the cuppa, which is called Black Ivory Coffee. It was launched last month at a few luxury hotels in remote corners of the world — first in northern Thailand, then the Maldives and now Abu Dhabi — with the price tag of about $50 a serving.
The Associated Press traveled to the coffee's production site in the Golden Triangle, an area historically known for producing drugs more potent than coffee, to see the jumbo baristas at work. And to sip the finished product from a dainty demitasse.
In the misty mountains where Thailand meets Laos and Myanmar, the coffee's creator cites biology and scientific research to answer the basic question: Why elephants?
"When an elephant eats coffee, its stomach acid breaks down the protein found in coffee, which is a key factor in bitterness," said Blake Dinkin, who has spent $300,000 developing the coffee. "You end up with a cup that's very smooth without the bitterness of regular coffee."
The result is similar in civet coffee, or kopi luwak, another exorbitantly expensive variety extracted from the excrement of the weasel-like civet. But the elephants' massive stomach provides a bonus.
Think of the elephant as the animal kingdom's equivalent of a slow cooker. It takes between 15-30 hours to digest the beans, which stew together with bananas, sugar cane and other ingredients in the elephant's vegetarian diet to infuse unique earthy and fruity flavors, said the 42-year-old Canadian, who has a background in civet coffee.
"My theory is that a natural fermentation process takes place in the elephant's gut," said Dinkin. "That fermentation imparts flavors you wouldn't get from other coffees."
At the jungle retreat that is home to the herd, conservationists were initially skeptical about the idea.
"My initial thought was about caffeine — won't the elephants get wired on it or addicted to coffee?" said John Roberts, director of elephants at the Golden Triangle Asian Elephant Foundation, a refuge for rescued elephants. It now earns 8 percent of the coffee's total sales, which go toward the herd's health care. "As far as we can tell there is definitely no harm to the elephants."
Before presenting his proposal to the foundation, Dinkin said he worked with a Canadian-based veterinarian that ran blood tests on zoo elephants showing they don't absorb any caffeine from eating raw coffee cherries.
"I thought it was well worth a try because we're looking for anything that can help elephants to make a living," said Roberts, who estimates the cost of keeping each elephant is about $1,000 a month.
As for the coffee's inflated price, Dinkin half-joked that elephants are highly inefficient workers. It takes 33 kilograms (72 pounds) of raw coffee cherries to produce 1 kilogram of (2 pounds) Black Ivory coffee. The majority of beans get chewed up, broken or lost in tall grass after being excreted.
And, his artisanal process is labor-intensive. He uses pure Arabica beans hand-picked by hill-tribe women from a small mountain estate. Once the elephants do their business, the wives of elephant mahouts collect the dung, break it open and pick out the coffee. After a thorough washing, the coffee cherries are processed to extract the beans, which are then brought to a gourmet roaster in Bangkok.
Inevitably, the elephant coffee has become the butt of jokes. Dinkin shared his favorites: Crap-accino. Good to the last dropping. Elephant poop coffee.
As far away as Hollywood, even Jay Leno has taken cracks.
"Here's my question," Leno quipped recently. "Who is the first person that saw a bunch of coffee beans and a pile of elephant dung and said, 'You know, if I ground those up and drank it, I'll bet that would be delicious.'"
Jokes aside, people are drinking it. Black Ivory's maiden batch of 70 kilograms (150 pounds) has sold out. Dinkin hopes to crank out six times that amount in 2013, catering to customers he sees as relatively affluent, open-minded and adventurous with a desire to tell a good story.
For now, the only places to get it are a few Anantara luxury resorts, including one at the Golden Triangle beside the elephant foundation.
At sunset one recent evening in the hotel's hilltop bar, an American couple sampled the brew. They said it surpassed their expectations.
"I thought it would be repulsive," said Ryan Nelson, 31, of Tampa, Florida. "But I loved it. It was something different. There's definitely something wild about it that I can't put a name on."
His wife Asleigh, a biologist and coffee lover, called it a "fantastic product for an eco-conscious consumer," since the coffee helps fund elephant conservation.
But how does it taste?
"Very interesting," she said, choosing her words carefully. "Very novel."
"I don't think I could afford it every day on my zookeeper's salary," she said. "But I'm certainly enjoying it sitting here overlooking the elephants, on vacation."

Mavi ya Tembo yachumbuliwa huko Thailand

Bomu Imelipuka Nairobi!

 Duh! Kwa mara nyingine bomu imelipuka mjini Nairobi, Kenya. Habari zinasema kuwa watu wawili wamekufa na wanane wamejuruhiwa leo asubuhi.  Bomu ililipuka eneo ambao wanakaa waKenya wengi wenye asili ya Somalia.

**********************************************

NAIROBI, Kenya (AP) - The Kenyan Red Cross says two people have been killed and eight wounded after a blast in downtown Nairobi.

   Friday evening's blast was the second in three days. A blast Wednesday near a military base wounded eight people.

   Both explosions went off in a Somali neighborhood of Nairobi known as Little Mogadishu. Kenya has seen a series of small-scale explosions over the last year, many from grenades.  Kenyan media reported that a member of parliament was wounded in Friday's attack.

   Kenyan troops moved into Somalia in late 2011, prompting al-Shabab militants in Somalia to vow revenge attacks inside Kenya. Al-Shabab sympathizers are suspected in many of the blast attacks, though authorities have not clearly linked all the attacks to al-Shabab or its sympathizers.

Mh. Zitto Kabwe Ziarani Ulaya

PRESS RELEASE

Ndugu Zitto ziarani Ulaya
Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi, Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mbunge wa Kigoma Kaskazini ndugu Zitto Zuberi Kabwe ameanza ziara ya kikazi nchini Ujerumani ambapo atahudhuria na kuhutubia Mkutano mkubwa wa masuala ya ushirikiano wa kiuchumi kati ya Ujerumani na Africa. Mkutano huo “Economic Conference: Commitment to Africa Initiative” utafanyika Jijini Berlin kuanzia tarehe 9 – 11 Desemba 2012 na umeandaliwa na Wizara ya Ushirikiano wa Kimaendeleo ya Serikali ya Ujerumani.

Katika ufunguzi wa Mkutano huo ndugu Zitto atatoa mada kuhusu mgongano wa maslahi kati ya Kampuni binafsi na Jamii ambapo ataongelea suala zima la makampuni makubwa ya kimataifa yanavyonyonya rasilimali za Afrika bila kuwajibika kulipa kodi na kuendeleza jamii zinazozunguka shughuli zao. Atazungumzia pia mitaji kiduchu inayokuja Afrika na fedha nyingi inayotoroshwa Afrika kupitia rushwa, ukwepaji kodi na wizi wa rasilimali. Afrika inapoteza zaidi ya dola za kimarekani 583 bilioni kila mwaka kutokana na utoroshaji wa fedha unaofanywa na makampuni ya kimataifa kwa kushirikiana na baadhi ya viongozi wa Afrika. Hata hivyo Afrika inapokea takribani dola za Kimarekani 80 bilioni tu kwa mwaka kutokana na Uwekezaji (FDI) na Misaada (foreign Aid). Tanzania ni moja ya nchi inayopokea misaada mingi kutoka nje na moja ya nchi ambayo rasilimali zake zinatoroshwa na baadhi ya viongozi wake kutorosha fedha na kuzihifadhi kwenye mabenki ya Ulaya kama Uswiss.

Mnamo tarehe 11 Desemba ndugu Zitto atakuwa kwenye jukwaa moja na Waziri wa Maendeleo wa Ujerumani kuzungumzia namna bora ya kushirikiana kati ya Ujerumani na nchi za Kiafrika. Miongoni mwa mapendekezo ya Zitto ni kuondokana na mfumo wa sasa wa ushirikiano wa misaada na badala yake kuwe na ushirikiano wa kujengeana uwezo ili kila nchi iweze kuhimili maendeleo yake yenyewe.

Katika ziara hii Zitto atakutana na Mawaziri Wakuu wa majimbo ya Nord Rhein Westphalen jimbo ambalo limefanikiwa sana katika vita dhidi ya ukwepaji kodi unaotokana na raia wa Ujerumani kuficha fedha kwenye mabenki ya Uswiss na wa jimbo la Lower Saxony kwa ajili ya mazungumzo kuhusu ukarabati wa Meli ya Liemba na kujenga mahusiano kati ya Mkoa huu na Mkoa wa Kigoma pia kati ya mji wa PapenBurg na Manispaa ya Kigoma.

Zitto anatarajiwa kutembelea baadhi ya nchi nyingine za Ulaya na kukutana na watu mbalimbali katika kuimarisha mtandao wa kimataifa dhidi ya utoroshaji wa fedha kutoka Afrika (illicit money transfer). Pia atakutana na watu binafsi wenye ujuzi na weledi katika masuala haya ya kupambana na watoroshaji wa fedha. Zitto anataraji kurudi nchini mnamo tarehe 16 Desemba 2012. Kwa namna itaakavyowezekana umma utapewa taarifa kuhusu ziara hii kupitia akaunti ya twitter na facebook ya ndugu Zitto. Pia mada zote atakazowasilisha zitawekwa kwenye blogu ya zittokabwe.com kila itakapowezekana.

Waziri Kivuli wa Fedha na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni anawatakia Watanzania wote kila la kheri katika Sikukuu ya Uhuru wa Tanzania Bara. Utu, Uzalendo, Uadilifu na Uwajibikaji ni silaha muhimu sana za kujenga Taifa lenye heshima na jamii ya watu wenye fursa za kuendeleza maisha yao kwa haki na amani. Tutimize wajibu wetu katika kuijenga Tanzania tuitakayo kwa ajili yetu na kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Imetolewa na Ofisi ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini
8 Desemba 2012, Dar es Salaam