Tuesday, April 16, 2013

Msiba Dallas, Texas - Mtoto Zoelle Reeves (Alikuwa na Siku Nne Tu)

Wadau na wana Mlimani,

Nasikitika kutangaza kifo cha mtoto mchanga, Zoelle Imani Nalumansi Reeves.  Alizaliwa 9/4/13 na kufariki dunia 12/4/13. alikuwa duniani siku nne tu.  Wazazi wa Zoelle, ni Catherine Sembajwe-Reeves na Adrian Reeves wa Dallas, Texas. Alizaliwa mzima wa afya, alienda kupimwa kama kawaida ya watoto wachanga hapa USA.  Alifariki usingizini.  Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.

Familia ya Prof Sembajwe waliwahi kukaa Chuo Kikuu ch Dar es Salaam, Simba Road No. 12 (Mlimani).

No comments: