Saturday, March 20, 2021

Mh. Samia Suluhu Hassan Aapishwa kuwa Rais wa Sita wa Tanzania

Kutoka BBC SWAHILI

Samia Suluhu Hassan aapishwa kuwa Rais wa Tanzania na Jaji Ibrahim Juma katika Ikulu ya Jijini Dar es Salaam.

Mama Samia ameapishwa katika hafla ndogo iliyofanyika katika Ikulu ya Magogoni na kuhudhuriwa na marais wastaafu wa Tanzania na Zanzibar.

Mara baada ya kuapishwa alipigiwa mizinga 21 na kukagua gwaride maalumu kwa mara ya kwanza akiwa kama amiri jeshi mkuu wa majeshi ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.

Mama Samia mwenye miaka 61, ndio mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huu nchini Tanzania na wa pili Afrika Mashariki.




No comments: