Saturday, December 31, 2022

Papa Mstaafu Benedict wa XVI (16) Afariki Dunia



                                                      Hayati Papa Benedict XVI

 Papa Mstaafu Benedict XVI amefariki dunia leo asubuhi huko Vatican, Italia.  Ilitanganzwa mapema wiki hii kuwa afya ya Papa Benedict XVI ilikuwa imezorota.  Amefariki kwenye Monestari ya Vatican.  Alikuwa na miaka 95. Jina aliyozaliwa nayo ilikuwa Joseph Ratzinger. Alizaliwa Ujerumani mwaka 1927.

Atazikwa Alhamisi Ijayo huko Vatican baada ya Misa itakayosimamiwa na Papa Francis.  Papa Benedict XVI hakutaka mazishi enye makuu. 

Papa Benedict XVI  alistaafu ghafla mwaka 2013.   Alikuwa Papa wa kwanza kustaafu katika miaka 600 iliyopita ya Vatican. Kwa kawaida mtu anaachia upapa akifa.  Papa (Pope) ni mkuu wa kanisa Katoliki duniani.

Mungu Ailaze Roho ya Papa Benedict XVI mahala pema peponi.  Amen



No comments: