Monday, May 15, 2023

Tanzia - William Malecela aka. LeMutuz

 

Hayati William Malecela aka Le Mutuz
1961-2023

Yaani, kweli hujui siku utaaga dunia hii. Nimeshutuka sana kusikia habari ya kifo cha kaka yangu wa ubatizo, William Malecela 'aka' LeMutuz.  Baba yake  Mh. John Malecela, na marehemu mke wake walisimamia ubatizo wangu.

Nilikuwa namwona William Dar wakati nasoma Zanaki Girls Secondary School. William kipindi kile alikuwa na afro, kijana fit. Nilisikia alienda kuwa baharia, halafu nilikutana naye tena New York City.  Baada ya muda aliamua kurudi kimoja Tanzania. Tulikuwa tunawasiliana kwa muda lakini...ndo hivyo alivyokuwa King wa Social Media Tanzania, alikata mawasialiano maana skikubaliana naye kuhusu mambo kadhaa.  Nikawa namwona  kwenye mtandao tu...mara kanda za majungu..mara fashion show. 


Mara la mwisho kumwona William ilikuwa hivi na shati hiyo hiyo...tuliongea kidogo..Aliniaga na mikono hivyo hivyo  kama pichanai..kumbe ananiaga. Siku hiyo nilimwona Mlimani City, Dar es Salaam. Sikujua itakuwa mara la mwisho kumwona ana kwa ana.

Kaka William ametangulia.  Mungu ailaze roho yake mahal pema mbinguni. Amen

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

No comments: