Showing posts with label Daudi Mwangosi. Show all posts
Showing posts with label Daudi Mwangosi. Show all posts

Thursday, September 13, 2012

Polisi Anayedaiwa Kumwua Daudi Mwangosi Afikishwa Kizimbani

Huyo polisi mwenye miaka 23 inawezekana ni ' trigger happy'.  Yaani alikuwa na hamu sana ya kuonyesha upolisi wake na kutumia silaha yake.  Ndo tatizo la kuwapa watu wasiokomaa kiakili silaha. Rest in Peace Daudi Mwangosi.

*****************************************************
Kutoka Ippmedia.com

Mwangosi Killing: Policeman Charged


By The Guardian Reporter

13th September 2012
Police Constable Pacificus Cleophace Simoni (23) appeared before Iringa District Court yesterday charged with the murder of Channel Ten journalist Daudi Mwangosi.


The accused with a white hood draped over a good part of his face, and in a black jacket was escorted into the court by more than seven police officers.

The Public Prosecutor Michael Luena told Senior Magistrate Dyness Lyimo that Constable Simoni with number G2573 residing at FFU quarters in Iringa municipality killed Daudi Mwangosi on September 2 this year at Nyololo village in Mufindi District in Iringa region.

The accused was not allowed to enter any plea because the court has no jurisdiction over murder cases.

The case was adjourned to September 26 this year and he was remanded in custody since the charges facing him are not bailable.

Meanwhile, Home Affairs Minister Dr Emmanuel Nchimbi has said that the probe committee he formed to investigate the murder will continue with its work.

In a statement released in Dar es Salaam yesterday Minister Nchimbi said that the probe committee will continue with its work with a view to get a lasting solution to the misunderstandings between police and journalists and police with political parties.

He said the move also will help to improve the relations between police and civilians, calling on all stakeholders to allow the law to take its course.

Mwangosi who was a Channel Ten Representative in Iringa was killed on September 2 this year at Nyololo village in the region following skirmishes between police and Chadema supporters.

On Tuesday journalists countrywide staged a demonstration to condemn the brutal killing of their colleague vowing to continue pressing the government to take action against all people involved in the killing.

The journalists called on police to respect their work just as journalists recognise and respect members of the force.

Mwangosi who was born in 1972 was buried at Msoka village in Mbeya region on September 4 this year. He is survived by a wife and four children.

SOURCE: THE GUARDIAN

Tuesday, September 04, 2012

Mauaji Iringa Yamtesa IGP Mwema!

Kutola Gazeti la Mwananchi

Tanzania Inspector General of Poice Mr. Said Mwema

Mauaji Iringa Yamtesa

Tuesday, 04 September 2012
AJICHIMBIA KUTETA NA VIGOGO WA POLISI, VIONGOZI CHADEMA, DK NCHIMBI AKATISHA ZIARA AREJEA NCHINI

Waandishi Wetu

TUKIO la kuuawa kwa mwandishi wa habari wakati polisi wakipambana na wafuasi wa Chadema mkoani Iringa, limelitikisa jeshi hilo na jana Mkuu wake (IGP), Said Mwema alilazimika kujifungia na vigogo wa polisi Mkoa wa Iringa kujadili suala hilo.

Wakati IGP Mwema akifanya mkutano huo, uliodumu kwa zaidi ya saa mbili na nusu, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi amelazimika kukatisha ziara yake ya kikazi Afrika Kusini na kurejea nchini kushughulikia suala hilo.

Mwema alienda Iringa jana na kuitisha mkutano huo uliowahusisha pia viongozi wa Chadema, akiwamo Katibu Mkuu wake, Dk Willibrod Slaa katika mazingira yaliyoelezwa kuwa na ulinzi mkali.

Hii ni mara ya kwanza IGP Mwema kwenda mwenyewe kwenye mikoa kunakotokea vurugu kati na vyama vya siasa na baadaye mauaji ya raia.

Julai 15, mwaka huu vurugu za aina hiyo zilitokea mkoani Singida ambako Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Kata ya Ndago wilayani Iramba, Yohana Mpinga aliuawa kwa kupigwa na silaha za jadi.

Pia mkoani Morogoro, Ally Zona aliuawa katika vurugu zilizoibuka baina ya polisi na wafuasi wa Chadema katika haraka za jeshi hilo kuwasambaratisha wafuasi hao kwa kile ilichoeleza kuwa maandamano yao yalipigwa marufuku.

Katika vurugu zote hizo, IGP amekuwa akituma wawakilishi au kutumia polisi kwenye mkoa husika kushughulikia matatizo hayo.

Makubaliano ya Kikao

Taarifa kutoka ndani ya kikao hicho zimeeleza kuwa polisi imekubaliana na Chadema na Umoja wa Vyama vya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) kusitisha majadiliano yote yanayohusu kifo cha mwandishi huyo hadi mazishi yake yatakapokamilika.

Mwenyekiti wa UTPC, Kenneth Simbaya alisema baada ya mkutano huo kuwa wamekubaliana kuwa na mkutano mwingine baada ya shughuli za mazishi kukamilika.

“Tulichoomba kifanyike ni kwamba, tumzike mwenzetu halafu majadiliano mengine juu ya ilikuwaje kwa nini na nini kifanyike kwa siku za usoni yatakuja,” alisema Simbaya.

Alisema sasa wanasubiri mwili wa Mwangosi ufanyiwe uchunguzi na wataalamu kutoka Dar es Salaam kabla ya kukabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya maandalizi ya mazishi.

Katibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa (IPC), Francis Godwin alisema uchunguzi wa awali wa IPC unapingana kwa asilimia zote na taarifa ya jeshi hilo kwa kuzingatia taarifa zilizotolewa na baadhi ya waandishi waliokuwapo katika tukio hilo.

“Taarifa kutoka katika vyanzo vyetu zinaonyesha kwamba Mwangosi alipigwa kwa virungu kabla ya kulipuliwa na bomu hilo ambalo kwa vyovyote vile mhusika wake mkuu anaweza kuwa jeshi hilo na ili taarifa hiyo potofu isiendelee kuugubika umma, IPC imeamua kutoa tamko linalolenga kuviarifu vyombo huru viingilie kati uchunguzi,” alisema Godwin.

Nchimbi Katisha Ziara

Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi jana alilazimika kukatisha ziara yake ya kikazi, Afrika Kusini na kurudi nchini ambako pamoja na mambo mengine, atazungumza na waandishi wa habari leo kuhusu tukio hilo.

Nchimbi anarejea nchini wakati Naibu wake, Pereira Ame Silima akikataa kulizungumzia akisema uchunguzi umeshaanza.

Silima alisema tukio hilo linachunguzwa kwa pamoja kati ya Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba na IGP Mwema... “Mwema na Manumba wanaelekea Iringa ikiwa ni sehemu ya uchunguzi wa tukio hilo na baadaye ndipo jeshi la polisi litaweza kueleza ni kitu gani hasa kimetokea.”

Alisema kwa sasa lolote litakalozungumzwa juu ya tukio hilo litakuwa ni hisia tu na ukweli utajulikana baada ya uchunguzi huo kukamilika.

ongozi wa kampuni ya Africa Media Group ambao wanamiliki Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, umeitaka Serikali kuanzisha uchunguzi huru ili kubaini sababu na mazingira ya kuuawa kwa mwandishi huyo ambaye alijiunga na kampuni hiyo mwaka 2006.

Taarifa iliyotolewa na kampuni na kusainiwa na Mhariri Mkuu wa Channel Ten, Dina Chahali imetaka uchunguzi huru kufanyika na kuhakikisha wahusika wa tukio hilo wanachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

“Tunalaani vikali tukio hili ambalo halikubaliki kwa jinsi yoyote ile, tunataka kuanzishwa uchunguzi huru na hatimaye nguvu za kisheria zitumike,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.

CHADEMA Yamtaka Rais Kikwete Kuwawajibisha Polisi!

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi Chadema, John Mnyika akionesha picha ya polisi wakizingira Ofisi ya Tawi la chama hicho katika Kijiji cha Nyololo, Mufindi iliyochapishwa na gazeti la Tanzania Daima

DAR ES SALAAM, Tanzania


CHAMA cha Demokrasi na Maendelea (Chadema), kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kuwasimamisha kazi vigogo wote wa Jeshi la Polisi, ambao wamekuwa wakitoa taarifa mbalimbali za uongo kuhusu mauaji ya mwandishi Daudi Mwangosi, ama awatake wajiuzuru nyadhifa zao, kupisha uchunguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho, John Mnyika, aliwataja vigogo hao wa polisi kuwa ni Kamanda wa Operesheni wa Polisi, Paul Chagonja na RPC wa Iringa, Michael Kamuhanda

Wawili hao kwa mujibu wa Mnyika, kwa nyakati tofauti walidai kuwa marehemu alifikwa na mauti baada ya kuchoropoka kutoka kwa kundi la wafuasi wa Chadema na kukimbilia mikononi mwa Polisi na ghafla kulitokea mlipuko wa bomu la machozi uliosababisha kifo chake, jambo ambalo sio la kweli.

Mnyika alisema maneno hayo yanayotafuatiana na kuyaita kuwa ni ya uongo ukizingatia kwamba picha mbalimbali zimeonesha ikiwemo waandishi waliokuwemo eneo la tukio kutoa ushuhuda wao.

Kutokana na hali hiyo, Mkurugenzi huyo alisema ipo haja ya vigogo hao kung’oka kupisha uchunguzi, ili uweze kufanyika kwa haki na kuongeza kwamba Rais atumie madaraka yake kuhakikisha askari saba wanaoonekana katika picha 'wakimsghulikia' marehemu kukamatwa haraka na kuhojiwa ni nani alifyatua bunduki, kwa namna gani na vigogo gani walitoa amri hiyo.

Kwa mujibu wa Mnyika, Polisi imekuwa na tabia ya kukamata raia wanaokuwa eneo la tukio pindi kunapotokea mauaji kama hayo, hivyo ni wakati sasa wa Polisi wanaoonekana katika picha wakimshambulia marehemu Mwangosi nao kukamatwa.

Aidha alilitaka Jeshi la Polisi nchini lisitumie vibaya fedha za walipa kodi kwa kuchunguza nani alihusika na mauaji hayo wakati wauaji wanaonekana.

Mwandishi wa Habari Auwawa na Polisi Bongo!

The Late Daudi Mwangosi
Tanzanian Journalist Killed Reporting Police-Opposition Clash

               SEE HOW HE WA MURDERED AND HIS BODY MUTILATED HERE:
By Fumbuka Ng'wanakilala

DAR ES SALAAM
Tue Sep 4, 2012
DAR ES SALAAM (Reuters) - A leading Tanzanian editor accused police on Tuesday of beating up and killing television journalist Daudi Mwangosi, who died on Sunday during clashes between anti-riot police and supporters of the opposition CHADEMA party.

A police commissioner denied police responsibility but said he had ordered a joint military-police inquiry into the killing. Photos of the victim were uploaded onto the Internet and published by local newspapers.

Opposition leaders and activists linked the incident to a wider trend of rapidly growing violence against dissent in Tanzania and called for an independent inquiry.

Mwangosi was killed in a village in the Iringa region, about 500 km (315 miles) west of the capital Dar es Salaam, while reporting the clashes between police and CHADEMA supporters.

It was the first time in modern Tanzanian history that a journalist had been killed while doing his job, the Tanzania Editors' Forum (TEF) said.

"It was a deliberate move by the police, who clearly targeted this journalist. Eyewitnesses said the journalist was surrounded by police, beaten up and brutally killed," TEF secretary-general Neville Meena told Reuters.

Police fired a tear gas shell into Daudi's stomach at close range, Meena said. "Photos of fragments of Daudi's blown-up body hit the Internet less than one hour after the incident. We believe that the police are deliberately targeting journalists in a violent crackdown."

The police denied responsibility and said they had moved in to disperse an illegal gathering of opposition supporters.

"Police deny any deliberate involvement in the death of the journalist," police commissioner of operations Paul Chagonja said in a statement. "A commission of inquiry comprising officials from the police and military has been formed to investigate the death of the journalist."

Journalists at the scene uploaded images onto the Internet that they said showed Mwangosi's mutilated body lying on the ground, his abdomen ripped open and intestines spilling out.

Local newspapers published photos that showed a man lying on the ground, surrounded by anti-riot police officers who were beating him. The newspapers identified the man as Mwangosi, though the face was not recognizable.

"We condemn the killing ..." the Guardian newspaper of Tanzania said in an editorial. "It is unacceptable for the government and the public to rely on police investigations, knowing only too well that they are in this case one of the parties being blamed for the death of our colleague," it added.

Mwangosi's death came a week after one person was killed and several were wounded when police fired tear gas to break up an opposition protest in Morogoro town, a stronghold of the ruling CCM party.

(Editing by Yara Bayoumy and Tim Pearce)

MNAWEZA KUONA PICHA ZA MAUJI NA MAZISHI YA MAREHEMU DAUDI KWA KUBOFYA HAPA: