Showing posts with label Mrs. Rita Che-Mponda. Show all posts
Showing posts with label Mrs. Rita Che-Mponda. Show all posts

Saturday, September 08, 2012

Wazazi Wangu Washerekea Miaka Hamsini ya Ndoa

Wadau, napenda kuwafahamisha kuwa wazazi wangu, Dr. Aleck na Mrs. Rita Che-Mponda wamesherekea miaka hamsini ya ndoa wiki iliyopita mjini Dar es Salaam. Ndoa yao ilibarikiwa katka kanisa la Anglikana St. Albans, Dar es Salaam. Walifunga ndoa mwaka 1961, baba akiwa mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Howard. Mama alikuwa amemaliza masomo yake ya unesi.

Mungu azidi kuwabariki.

Dr. & Mrs. Aleck Che-Mponda 
Misa ya Kuwabarika St. Albsans




Wazee wakiwa na baadhi ya ndugu


Thursday, May 24, 2012

Mwanangu Apata Nondoz!

Wadau, nafurahi kuwatangazia kuwa mwanangu Elechi Henry Kadete amepata shahada, Degree of Bachelor of Arts' kutoka Chuo Kikuu cha Brandeis (Brandeis University), Waltham, Massachusetts.  Major yake ilikuwa ni Business.  Sherehe ilikuwa jumapili iliyopita. Kweli safari ilikuwa ndefu na kulikuwa na matuta mengi njiani, lakini kafika. Baba yake marehemu Prof. Henry Kadete, lazima anatabasamu kutoka mbinguni.

Brandeis ni Chuo Kikuu cha Wayehudi, lakini wanapokea wanafunzi kutoka nchi mbalimbali na dini mbalimbali.  Imam alisoma sala ya kufungua sherehe. Baadaye Rabbi wa kiyehudi, na Padre wa Kikristo walitoa sala za kufunga sherehe.


Hongera Elechi!


L-R Dr. Aleck Che-Mpomda (babu), Mimi, Elechi, Camara (kaka), Malaika (mama mdogo) na Mrs. Che-Mponda (bibi)  Watoto wadogo ni watoto wa Malaika
Mimi na Elechi
Elechi na Bibi na Babu yake

Mama na Mwana

Graduates wa  Bachelor of Arts wakitoka ukumbini
Elechi akiwa na siku tatu tangu azaliwe,, Hapa ni 21 Kileleni Road UDSM 1989
Imam akisuali kabla ya ceremony kuanza

Elechi na Babu yake, Dr. Aleck Che-Mponda