Mother Africa /Mama Afrika
Kushelia, Linda na Catrina walioigiza kama watumwa
Muongozaji (Director) Wetu Lee Smith na Oscar feki tuliyomkabidhi kama shukurani kwa kazi nzuri. Lee aliigiza kama Langston Hughes pia.
Mimi na Ruby Hill tukiwa tumevaa costumes kwa ajili ya Party Scene.
Mimi niligiza kama Mother Africa pia, safari hii. Father Africa alikuwa David Bowden. Kwa mara ya kwanza walikuwa na Mother Africa ambaye anaongea lugha ya Afrika. Khanga na vitenge nilinunua nilivyokuwa Dar mwezi Novemba. Ungo nilinunua Ubungo TANESCO. Nilikuwa na nyingine ambaye nilikuwa nafanya mazeozi nayo, ilibiwa pale tulipokuwa tunafanya mazoezi! LOL!
Costume yangu ya awali kama Ms. Thelma anayetafuta mapenzi na ana ndoto ya kushinda bahati nasibu.
Mimi na Charles Jackson aliyeigiza kama Joe the Bartender. Mwanzo Ms. Thelman anamkataa Joe, lakini baadaye anamkubali na wanafunga ndoa.
Wadau, jana jioni (Ijumaa) niliigiza katika mchezo wa kuigiza, The Harlem Renaissance Revisited with a Gospel Flavor. Mchezo wa Harlem Renaissance umetungwa na Haywood Fennell Sr.















