Showing posts with label Ziara. Show all posts
Showing posts with label Ziara. Show all posts

Saturday, January 27, 2018

Waziri Tillerson wa Marekani Atatembelea Nchi Kadhaa za Afrika mwezi Machi!

 
Rais Trump wa Marekani akimwangalia Mh. Waziri Rex Tillerson

ADDIS ABABA, Ethiopia (AP) - President Donald Trump in a new letter to African leaders says he "deeply respects" the people of Africa and that Secretary of State Rex Tillerson will make an "extended visit" to the continent in March, his first in that role.

   The letter dated Thursday is addressed to African leaders as they gather for an African Union summit this weekend in Ethiopia's capital.

   U.S. diplomats have scrambled for days to address shock and condemnation after Trump's reported comparison of African nations to a dirty toilet. Trump has said he didn't use such language, while others present say he did.

   Many in Africa were taken aback by the comments after nearly a year of little attention by the Trump administration to the world's second most populous continent. Concerns have been widespread over proposed deep cuts to U.S. foreign aid and a shift from humanitarian assistance to counterterrorism.

   Trump's letter, seen by The Associated Press and confirmed by two U.S. officials, says the U.S. "profoundly respects" the partnerships and values shared by the U.S. and Africans and that the president's commitment to strong relationships with African nations is "firm."

   The letter offers Trump's "deepest compliments" to the African leaders as they gather for Sunday's summit of their 55-nation continental body. It also notes that U.S. soldiers are "fighting side by side" against extremism on the continent and that the U.S. is working to increase "free, fair and reciprocal trade" with African countries and partnering to "safeguard legal immigration."

   The letter gives no details on Tillerson's upcoming visit. A State Department official said it was expected to include stops in four to six countries.

   On Friday, Trump had a rare meeting with an African leader at the World Economic Forum in Davos, Switzerland, calling Rwanda's president and new African Union chair Paul Kagame a "friend."

   For his part, Kagame tweeted: "Had very good bilateral meeting with (at)realDonaldTrump!" The Rwandan government said Kagame had "observed that many of the world's fastest-growing economies are in Africa."

   Neither side referred to Trump's vulgar comment.

   But African leaders are expected to respond to Trump during Sunday's summit. The U.S. will be represented at the gathering by Ambassador Mary Beth Leonard, the U.S. envoy to the AU, instead of the traditional high-level Washington delegation.

   An AU spokeswoman has said the organization was "frankly alarmed" by Trump's remark, and a number of African nations have spoken out or summoned U.S. diplomats for an explanation. Ugandan President Yoweri Museveni, however, countered by expressing his love for Trump and saying he should be praised for not mincing his words.

   Dozens of former U.S. ambassadors to African countries wrote a letter to Trump expressing "deep concern" over his comments and asking him to reconsider.

   The State Department's Bureau of African Affairs, in trying to calm things down, has tweeted that "the United States will continue to robustly, enthusiastically and forcefully engage" with African countries.

Saturday, March 11, 2017

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utallii Yatembela Eneo lenye Mgogoro la Por Tengefu la Loliondo

Msafara wa Magari ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi,Malisili na Utaalii,yakpita katika maeneo mbalimbali ya Pori Tengefu la Loliono kwa ajili ya kujionea hai halisi ya mgogoro ulioo katika eneo hilo.
Mwenyekii wa Kamati ya Kudumu ya Ardhi ,Maliasii na Utalii,Atashasta Ndetiye (katikati) akiongozana na wajumbe wengine wa kamati hiyo kutizama vyanzo vya maji vilivyoko katika Pori Tengefu la Loliondo.
Waziri wa Malisili na Utalii ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo,Prof Jumanne Maghembe akiongozana na wataalamu katika ziara ya kamati hiyo.
Mtafiti Mkuu wa Idara ya Ikolojia (TAWIRI) Dkt Edward Khoi akitoa maelezo ya kitaalamu kwa wajumbe wa kamati ya kudumu ya Ardhi,Malisili na Utalii wakati wakitembela Pori tengefu la Loliondo.
Baadhi ya wajumbe wa kamato hiyo wakifuatilia maelezo kutoka kwa wataalamu wa Ikolojia na Uhifadhi.
Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti,William Mwakilema akiwaeleza wajumbe w kamati hiyo madhara yatakayojitokea endapo eneo la Pori Tengefu la Loliondo halita hifadhiwa.
Wajumbe wa Kamati ya Maliasili na Utalii,wakitizama eneo linalotajwa kutengenezwa na wafugaji kwa ajili ya kunyweshea maji mifugo yao ndani ya Pori Tengefu la Loliondo.
Eneo linalouiwa na wafugaji unyweshea mifgo yao.
Sehemu ya Mabirik yanayotajwa kutengenezwa na jamii ya wafugaji kwa ajili ya kunywesha mifgo yao.
Mwenyekiti a Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Utalii,Atashsta Ndetiye (kulia) pamoja na Waziri wa Malisili na Utalii,Prof ,Jumanne Maghembe wakitizama eneo ambalo i mapiio ya maji katik Pori Tengefu la Loliondo.
Moja ya Makundi ya Ng'ombe yaliyokutwa na Kamati hiyo katika Pori Tengefu la Loliondo.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Utalii wakizungumza na mmoja wa wafugaji waliokutwa wakichunga Ngombe ndani ya Pori Tengefu la Loliondo. 
Kamati ilikutana pia na Changamoto ya uboovu wa Miundombinu ya barabara hali iliyolazimu magari kupita kwa tahadhari .
Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Utalii wakitizama moja kati ya vyanzo vy maji vinavyotiririsha maji yake katika mto Gurumeti uliopo katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Mbunge wa Jimbo la Sumve ambaye pia ni mjube wa kamati hiyo,Richard Ndasa akizungumza jambo mara baada ya kutizama moja ya vyanzo vya maji vilivyoko katika eneo la Pori Tengefu la Loliondo.
Sehemu ya Makundi ya Mifugo pamoja na Mashamba yaliyopo katika eneo la Pori Tengefu la Loliondo.


Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazinia

Friday, July 29, 2016

Pastor Daniel Moses Kulola Kutembelea Marekani

"Greetings my friend, Again God has given to me a chance to come to America, this time i wont stay in USA for long time it is just for 2 weeks then i come back home Tanzania.

My schedule will be in Boston from 9th to 14th August then 15th August to Dallas, Houston to 22nd, on 23rd to Arizona. my ticket back to Tanzania reads on 25th from Arizona to Boston and Boston to Tanzania.
I thought it is good to let you know so that you can pray for me and also call me for greetings". Pastor Kulola States.

Wednesday, July 24, 2013

Rais Kikwete Awasili Bukoba Kwa Ziara ya Kikazi ya Siku Sita

RAIS KIKWETE AWASILI BUKOBA KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU SITA
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mkuu wa mkoa wa Kagera Mhe. Fabia Massawe baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Bukoba leo tayari kuanza ziara ya kikazi ya siku sita mkoani humo
 Rais Kikwete akisalimiana na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman ambaye pia yuko mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi
 Rais Kikwete akisalimiana na Mstahiki Meya wa Bukoba Mhe Anatory Amani
 Vijana wa Skauti wa Bukoba wakimlaki Rais Kikwete uwanjani hapo
 Wanahabari toka vyombo mbalimbali vya habari wakiwa kazini
 Kijana wa Skauti akipiga saluti kuomba kumvisha skafu Rais Kikwete
 Rais Kikwete akivishwa skafu
 Rais Kikwete akisalimiana na Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli. Kushoto ni Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe
 Rais Kikwete akisalimiana na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo
 Rais Kikwete akisalimiana na viongozi na wananchi waliofika uwanjani kumlaki
 Rais Kikwete akisalimiana na Mkuu wa JKT
 Rais Kikwete akisalimiana na viongozi wa dini mbalimbali waliokuwepo uwanjani
 Rais Kikwete akiangalia ngoma za utamaduni
 Ngoma ya Kihaya ikimlaki Rais Kikwete Bukoba
 Karibu Bukoba mheshimiwa Rais....
 Sehemu ya viongozi waliohudhuria sherehe ya kuweka jiwe la msingi la ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba
 Viongozi wa dini wakiwa bega kwa bega kwenye sherehe hizo
 Waziri wa Uchukuzi Dkt Harrison Mwakyembe akimkaribisha Rais Kikwete kuongea na wananchi kabla ya kuweka jiwe la msingi la ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba
 Rais Kikwete akiongea na wananchi kabla ya kuweka jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
 Rais Kikwete akipata maelezo kabla ya kuweka jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
 Rais Kikwete akifunua kitambaa kama ishara ya kuweka  jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
 Waziri wa Uchukuzi Dkt Harrison Mwakyembe na Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Miundombinu Mhe Peter Serukamba wakishangilia wakati Rais Kikwete akiweka jiwe la msingi
 Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wadau baada ya kuweka jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
 Rais Kikwete akisalimiana na Mhashamu Methodius Kilaini, Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba
 Sehemu ya uwanja wa ndege wa Bukoba unaokarabatiwa na kupanuliwa
 Rais Kikwete akiwasili Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Rais Kikwete akisalimiana na wanachama wa KCU alipowasili Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Rais Kikwete akisalimiana na wananchi waliofurika kushuhudia ufunguzi wa  jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Rais Kikwete akiendelea kusalimia wananchi
Mwenyekiti wa Bodi ya KCU (1990)LTD John Binushu  akimkaribisha Rais Kikwete Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Sehemu ya umati wa wananchi kwenye ufunguzi wa jengo hilo
 Jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Rais Kikwete akipokea risala toka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya KCU (1990)LTD John Binushu 
 Rais Kikwete akipokea zawadi ya kahawa toka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya KCU (1990)LTD John Binushu 
 Rais Kikwete akifunua kitambaa kama ishara ya Kufungua rasmi jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Rais Kikwete akikata utepe Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Rais Kikwete akihutubia wananchi baada ya Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Wananchi wakimsikiliza Rais Kikwete
 Rais Kikwete akihutubia
Rais Kikwete katika picha ya pamoja na viongozi wa KCU baada ya kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
---------------------------------------------------------------
Ndugu Wananchi, kama ambavyo nimewahi kuwajulisha mara nyingi kupitia vyombo vyetu vya habari juu ya Mkoa wetu wa Kagera kupewa heshima kubwa ya kuandaa maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa kitaifa mwaka 2013, leo napenda kuwajulisha juu ya maandalizi ya maadhimisho hayo ambayo yataadhimishwa tarehe 25/07/2013 hapa mkoani kwetu katika Wilaya ya Muleba katika Kambi ya Jeshi la Wananchi Kaboya. Pia nawajulisha kuwa maadhimisho hayo yataambatana na ziara ya kikazi ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mkoa wa Kagera.

MAADHIMISHO YA MASHUJAA MWAKA 2013
Ndugu Wananchi, Maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Kumbumbu ya Mashujaa mkoani Kagera yanaendelea vizuri kamati mbalimbali za maandalizi zinatekeleza majukumu yake ya mwisho ili kufanikisha maadhimisho siku ya Alhamisi ya wiki hii tarehe 25 Julai, 2013. Kamati zinazoandaa maadhimisho hayo ni Kamati ya Mapokezi, Usafiri na Malazi; Kamati ya Ujenzi Uwanja na Mapambo; Kamati ya Chakula na Afya; Kamati ya Ulinzi na Usalama; na Kamati ya Burudani, Habari na Uhamasishaji.

Ndugu wananchi, Kwa kiwango kikubwa maandalizi yote yamekamilika na tunatarajia kuanzia leo kupokea wageni kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya mkoa, pia nje ya nchi watakaohudhuria maadhimisho hayo.
Mkoa wetu umejipanga vizuri kuwapokea wageni wote watakofika mkoani hapa kwa ukarimu na bashasha kubwa.

Wajibu wa Wananchi
Ndugu wananchi, Napenda kutumia fursa hii kuwaomba kuwa wakarimu kwa wageni wetu wote tunaowatarajia kuanzia leo kwa kutekeleza majukumu yenu kama Wanakagera kama ifuatavyo;
Ø Kila mwananchi kuhakikisha maeneo yake na mazingira yanayomzunguka yanaendelea kuwa katika hali ya usafi kama utamaduni wetu. Pia kumwajibisha mtu yeyote atakaeonekana anachafua mazingira yetu. Hili ni jukumu la kila mwananchi.
Ø Kila mwananchi kushiriki kikamilifu katika kuadhimisha Siku yenyewe ya Kumbukumbu ya Mashujaa tarehe 25 Julai, 2013 huko Kaboya Wilayani Muleba. Kwani hatuna budi kuwakumbuka Mashujaa wetu kwa sababu ya historia ya mkoa wetu kushiriki katika vita ya kumwondoa adui aliyekuwa amevamia nchi yetu kupitia ardhi ya mkoa huu mwaka 1978 hadi 1979.
Ø Kila mwananchi kuhakikisha anaitunza amani na utulivu kama destuli ya mkoa wetu kwa wakati wote wageni wetu watakapokuwepo hapa mkoani na baada ya maadhimisho ya Mashujaa. Aidha, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa imejipanga vizuri kuhakikisha amani na utulivu vinatawala wakati wote. Kwa mwananchi yeyote atakayeona viashiria vya uvunjifu wa amani atoe taarifa mara moja ili taarifa hizo zifanyiwe kazi mara moja.

Wajibu wa Vyombo vya Habari
Ndugu Wananchi, Vyombo vyetu vya habari vina wajibu wa kuhakikisha vinaendelea kutoa taarifa mbalimbali kwa wananchi kuhusu Maadhimisho ya Mashujaa kama ambavyo vimekuwa vikifanya kuanzia mwezi Mei, 2013.

Aidha, nawaombeni Waandishi, Wahariri na Wamiliki wa vyombo vya habari kutumia fursa hii kuutangaza mkoa wetu wa Kagera katika sekta mbalimbali za uwekezaji na fursa mbalimbali zinazopatikana katika mkoa wetu.
Vilevile nawaombeni Wamiliki wa vyombo vya habari hasa redio zetu za jamii kutoa muda wa kutosha katika vituo vyenu vya redio kurusha habari na matukio ya Kumbukumbu za Mashujaa papo kwa papo (live coverage) siku ya maadhimisho ili wananchi ambao hawatapata muda wa kufika Kaboya wazipate habari hizo kupitia redio zetu za Jamii.

ZIARA YA MHE. RAIS MKOANI KAGERA
Ndugu Wananchi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiye atakayekuwa mgeni Rasmi Katika Maadhimisho ya Kumbukumbu ya Mashujaa tarehe 25 Julai, 2013. Pia Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete anatarajia kufanya ziara ya kikazi katika mkoa wetu wa Kagera.
Ndugu Wananchi, Katika ziara hiyo Mheshimiwa Rais Kikwete anatarajia kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo katika mkoa wetu kama ifuatavyo:
§ Kuweka jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
§ Kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami ya Kagoma - Rusahunga
§ Kuweka jiwe la msingi barabara ya kiwango cha lami Kyaka hadi Bugene
§ Kufungua Jengo la Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba.
§ Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
§ Kuzindua mradi wa maji Muleba
§ Kuzindua kivuko kipya Rusumo (Ngara)
§ Kuzindua mradi wa usambazaji umeme vijijini Nyaishozi (Karagwe)
§ Kuzindua Wilaya Mpya ya Kyerwa
Ndugu Wananchi, Vilevile Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ataongea na wananchi kupitia mikutano mbalimbali ya hadhara katika Wilaya zetu ndani ya mkoa.
Ndugu Wananchi, nawaombeni kujitokeza kuanzia tarehe 24/07/2013 uwanja wa ndege wa Bukoba ili kumpokea Mheshimiwa Rais, pia atakapokuwa anafanya ziara katika Wilaya zetu tujitokeze kwa wingi kumsikiliza. 
Mwisho; Nawatakia ushiriki mzuri katika kuadhimisha Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa na mapokezi mazuri ya wageni wetu hasa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Kagera: Amani na Maendeleo. 
Amani na Maendeleo; Kagera.

Imetolewa na: Kanali Mstaafu Fabian I. Massawe
Mkuu wa Mkoa
KAGERA