Tuesday, February 20, 2007

Marudio - Wapenzi wa Matako Makubwa



Naona blog ya 'Matako Makubwa' ilikuwa na hits nyingi sana, nilibandika kwanza 12/2005. Hivyo nimeamua kuirudia.

Nimesikia wazungu wakisema hiyo kupenda matako makubwa eti ni 'cultural thing' kwa watu weusi, na hawajakosea. Ni mila na desturi ya mwafrika kupenda matako makubwa. Na kuyasifia. Hata wengi wa waMarekani weusi wanapenda mpaka kutunga nyimbo za 'bootylicious'. Huwa nacheka nikiona mzungu anasifia mwanamke ambaye huko nyuma kapigwa pasi. Yaani fleti. Lakini kuna wesui ambao wamekuwa 'zungunized' na wanapenda matako fleti. Shauri zao!

Matako Makubwa Oyee!



************************************************************************

From my 12/2005 Blog:


Wapenzi wasomaji, leo nimeamua kuzungumzia suala ya matako makubwa. Tafadhali msione kama ni matusi lakini hapa USA ni issue kubwa, maana watu wanayachukia!

Nimeona nizungumzie suala ya matako makubwa kwa vile jana kazini, mzungu aliyekondeana mno kasema ni mnene na akila keki eti yote itaenda matakoni. Nilishangaa na kusikitika sana.Uzuri kwa wazungu ni kuwa na matako fleti kama vile yamepigwa pasi. Sijui kwa nini. Mtu anashepu ya mbao, mwanamke hana hips kakaa kama dume vile eti ndo uzuri. Kumbe ni kwa sababu hao models na wacheza sinema wako hivyo!

Basi wasichana na akina mama wanajinyima chakula kusudi wakonde na eti wapendeze. Ndo maana magonjwa kama Bulimia na Anorexia zimeshamiri hapa. Lakini ukitazama sinema za miaka ya nyuma kama za 1930's na 1940's, wanawake walikuwa na shepu na walikuwa wamejaa na hata wanaume wa kizungu walikuwa wanasifia. Mpaka 1950's kulikuwa na mcheza sinema Marilyn Monroe, alikuwa na zinga la figure 8, na wanaume wote walikuwa wanampapatikia. Ama kweli mambo yanabadilika. Hivi sasa wanasema eti walikuwa ni obese yaani wanene!

Mbona mimi naona matako fleti kama chapati ni mabaya na hayapendezi? Au ni kwa sababu nimekulia Africa? Brothas (waMarekani Weusi) wanapenda mwanamke awe na matako ya maana! Akipita mwanamke mwenye mbarikio utasikia brothas wakisifia, "umm, umm umm!" Kuna siku nilisikia wanaume wa kizungu wakijadili sababu ya wanaume weusi kupenda matako makubwa, walisema ni "cultural thing". Kwa kweli ni culture yaani utamaduni! Kama umekulia katika mazingara ya kupenda kitu utakipenda. Na ndo maana kuna weusi USA wanataka kuwa na shepu iliyokondeana kama mzungu kumbe haiko katika 'genes' zake. Wajitahidi kupunguza mzigo lakini wapi, iko pale pale.

Sisi wanawake wenye asili ya Afrika tumebarikiwa huko nyuma. Yaani boxi, siha, wowowo, booty, na nasikia waGhana wanaita yokohama, matako makubwa yana majina mengi. Waafrika tunaona kama ni urembo, lakini wazungu na waliokulia uzunguni wanaona kinyaa. Wanasema eti ni dalili ya ulafi na uvivu! Lakini kama ni dalili ya ulafi mbona hata mwanamke mwembamba mwafrika anaweza kuwa na kamzigo huko nyuma?

Ubaya mwenye matako makubwa anaweza kubaguliwa kwa vile bosi anaweza kuona kuwa ni 'ugly' (mbay) na mwenye nacho anachafua mazingira ya ofisi. Kweli kabisa!Hayo matako makubwa ni 'genes' za sisi waafrika. Lakini ajabu kuna siku nilisikia wazungu wakisema eti waafrika tuna matako makubwa kwa sababu ya utumwa. Eti mabibi zetu walinyimwa chakula hivyo matako ndo ilikuwa 'godown' ya mafuta ya akiba. Nadhani ni uzushi kama ile ya ngamia kuweka maji kwenye nundu zake!

Mimi mara nyingi nimeambiwa nina matako makubwa, niyapunguze kwa kwenda gym kufanya mazoezi. Hayo mazoezi haisadii kitu ni makubwa vile vile! Lakini msione kama naona haya, wala! Mtu akiniambia nina matako makubwa namwambia mbona kama ni madogo, na ningependa yawe makubwa zaidi! Wanabakia kushangaa hasa nikiwaambia kuwa Afrika, matako makubwa ni uzuri.Na amini usiamini kuna opresheni ya kuyapunguza inaitwa Liposuction. Wanawake wengi weusi na wazungu wamefanya hiyo liposuction ya matako, akiwemo mwimbaji Janet Jackson. Ubaya, ni kuwa ukishafanya hiyo liposuction, mafuta yataenda kwingine mwilini, hivyo utakuwa na shepu ya ajabu!

Sisi waafrika tunapenda kuringia huo mbarikio wa matako makubwa. Nilipokuwa nacheza ngoma shuleni na jeshini, tulikuwa tunatia nguo ndani ya bukta kusudi tuonekana na matako makubwa kweli kweli! Lakini, mara nyingi mitaani hapa USA, nimesikia akina dada wakifokewa, "You got a big a-s!" Kuna siku nilikuwa kwenye kituo cha Subway hapa Boston, kapita mama fualni Mganda, aisei alikuwa amejaliwa kweli huko nyuma, mpaka nikaona wivu. Basi ungeona wazungu walivyokuwa wanamtazama kwa mshangao ungecheka. Ila nilishuhudia baba fulani Mmarekani Mweusi akimtazama kwa furaha na kawa kama vile anamezea mate.

Nampenda sana mecheza sinema, Whoopi Goldberg. Nilikuwa nasoma jinsi akienda kwenye audition au akiwa kwenye movie shoot, wazungu wanamwambia kuwa ana matako makubwa au avae nguo ya kuzificha. Yeye alichoka, na mwishowe kusema, " Mimi ni mwanamke mweusi, nina matako makubwa niache kama nilivyo!" Wanawake wote tungedai heshima kama Whoopi nadhani wazungu wangeheshimu matako yetu makubwa.

Tatizo linigine la kuwa na matako makubwa USA ni kupata nguo. Ukienda kununua sketi au gauni uanweza kukuta mbele refu nyuma umepanda. Au unavaa hiyo nguo lakini kwenye hips na matako haipiti! Hii ni kwa sababu nguo imeshonwa kwa ajili ya wazungu wenye matako fleti. Na kupata Jeans inayofiti ni vigumu. Mtu ambaye atatengeneza nguo 'molded for the black woman' atapata wateja kweli kweli, maana tunalilia nguo kama hizo.

Pamoja na yote haya sasa wazungu wameibuka na staili ya kuwa ka ka-butt. Yaani jeans inakuwa na pedi ndani kusudi mtu aonekana ana matako. Loh! Watu hawaridhiki! Sijui tuseme asante J-Lo (mwimbaji Jennfier Lopez) au nini. Kwanza walikuwa wanamcheka J-Lo na matako yake makubwa lakini naona watu wanaanza kuyapenda. Mpaka kuna opresheni sasa ya kuongeza matako. Wacha wafanye haitapendeza kama matako natural tulyiozaliwa nayo waafrika.

Matako Makubwa Oyee!

19 comments:

Anonymous said...

jungu ni kitu watu wengi wanafagilia,,singida-dodoma..

Anonymous said...

Kweli kabisa..nimejaribu mara kadhaa kujizuia kupenda matako makubwa lakini imeshindikana kabisa kabsaaa!.Sasa sijui huu ni ugonjwa ama.....
Nisaidieni jamani mwenzenu.

Tabora boy.

Anonymous said...

nafikiri weusi tunapenda kama ukimshika mdada uwe na sehemu ya kushika, sio mifupa tu. Kwa hiyo matako oyeeee!!

Anonymous said...

chemi tupe picha'ko uliovaa gauni na kanga tukuone

Anonymous said...

Chemi,

Du, huo ugonjwa wa kupenda tukunyema!tukunyema nadhani ninao, ila sijui sababu yake. Utamaduni? Labda. Lakini kama alivyosema anon hapo juu, sisi Watu wa Africa tunapenda kushika kinachoshikika, kufeel ule mbonyeobonyeo wa mwili wa yule uliyenaye wakati huo.
Ugonjwa huu uko mpaka katika harakati za usafiri wa daladala, utakuta mtu anang'angania nyuma ya mdada fulani kajibania kwake kwa nguvu. Huwa natamani kucheka.
Basi, we acha tu. Endelea kutupa michapo. Waambie wazungu waendelee kupenda vimbaumbau vyao. Hayo ni yao.

Anonymous said...

Inaelekea Chemi una matako makubwa. Hebu tuoneshe basi yalivyo!!

Anonymous said...

JAMANI DA CHEM IVI NI KWAMBA UKO BUSY SANA AU NI NINI/ MI NAIPENDA BLONG YAKO LAKINI TATIZO UNACHELEWA SANA KUWEKA HABARI MPYA, HUI UP DATE MARA KWA MARA BLONG YAKO KWA NINI? NDO MANA NAULIZA NI MAJUKUMU MENGI AU HII BLONG SIO PRIORITY KABISA KATKA KAZI ZAKO?

Anonymous said...

mambo, mi niko tz lakini napenda kujua mtu akiwa nje ya tz ana iview vipi tanzania, mfano,mtu akiona mlima kilimanjaro anagundua kweli kama hii ni tz kama ambavyo ukiona piramids moja kwa moja you think of egypt?? or is there any thing that symbolize tanzania by itself without a name tz being rwritten on it apart from national flag. hope you got what i mean and will appreciate if i hear back from you....te te te.

Chemi Che-Mponda said...

Ananonymous wa 1:46, asante kwa maoni yako. Kwa sasa nina matatizo ya computer access. Najaribu kutatua. Site zangu nashindwa ku-update kwa sasa.

Anonymous said...

Hiyo picha ya huyo manzii anayeplay tennise tayari nina hamu naye ile mbaya kisa haya matako yalivyojipanga vizuri.Jamani mama Africa.Wazungu nanii zao fupi na ni wavivu,sisi tunatafuta vitu vya kutukata kiu ile mbaya.Mademu wembamba hawakati kiu kabisa.

Anonymous said...

kitu gani hasa kinachpatikana kwenye matako makubwa? kama ni shughuli basi hata wanawake wembamba wanaweza fanya!!! i'm told big women get tired fast!!! sasa lipi la kweli hapo

Anonymous said...

Ukweli ni kwamba watu hawaridhiki na walivyonavyo, iwe ni matako, maziwa, vifua, mapaja, matumbo nk.

Labda kusahihi hapo Chuk Palumbo, matako makubwa siyo unene. Kuna wanawake wembamba wenye matako makubwa vile vile. Kama asemavyo Chemi ni maumbile ambayo inabidi tuyapende na kuyatunza.

Kugusia huo mfanyo wa J-Lo, wazungu walipoona J-Lo ana matako makubwa na anajivunia (amekatia bima ya kila tako lake - maana ni rasili mali nadhani kila tako analilipia $10000 kwa mwaka). Walipoona hivyo basi wakaanza kusifia "behind" kama ya J-Lo. Wanashindwa kutambua waafrika wamekuwa na "behind" kubwa kabla hata ya J-Lo. Kwa nini wasitusifie sisi waafrika. Je kitu chema hakiwezi afrika?

Chemi Che-Mponda said...

Na hao watu waSpanish wengi wamechanganya damu na weusi. Matako ya J-Lo yanatokana na weusi katika damu yake.

Anonymous said...

sister chemi hiyo picha inanitia nyege kinoma yaani hapa kitu kimekwenda mnara kishenzi,hebu tafuta nyingine zaidi ya hiyo tuwekee tujidai nayo hapa

Anonymous said...

mimi nipo flati nyuma yaani nimepigwa pasi,nimekuja ulaya,nipo ktk shule moja hivi,eti wanashangaa nina matako makubwa.
nikawaambia i wish ningekuwa nayo hayo matako,wakaniambia am stupid,eti urembo ni kuwa flat kama wao,its means wao ni wazuri kuliko mimi mwenye matako,ambayo nikikaa na waafrica wenzangu waliojaaliwa mimi ni flat,sasa sielewi which is which.
MANYUNYU

Anonymous said...

walisema uzuri uko kwa muonaji kama ni tafsiri sahihi ya "beauty lies in the eyes of the beholder". ila uongo si kazi, vikalio vikubwa vina dili. hata katika burudiko tu la macho tu na nafsi achilia mbali hizo wishes kubwakubwa kama za kupata pa kushika [ ref. anonymous 10.39pm] na ku feel.. tehe tehe. inaleta ladha kusema za ukweli ukiona uumbaji maridhawa wa mtu katoka zake huku juu akiwa wa kawaida then akarutubishwa na nyama sehemu husika hizo za matako.

MM oyeee!

Mikundu Matako Makalio Manundu said...

Dada Chemi, asiependa matako hayajuwi raha zake. Mimi kwa kupenda hayo matako namik...u imebidi nianzishe blogu mpya ya kuhusiana na hayo tuu.

Natamani ningepate picha za wabongo au wwafrika in general nizipambie kwenye blogu yangu.. Kama ni mpenzi wa Matako tafadhali tembelea:

http://mikundu.blogspot.com/

Anonymous said...

Chemi, we si mbongo? Basi fanya hivi, badala ya ile picha ya mcheza trennis pale mwanzo tuwekee picha yako ikionesha jinsi ulivyo, hususan ile uliyopiga na swimming suit au..., hata ile uliyokuwa 90% naked. Tunaka kuona ati, si unajuwa midume ya bongo tunavyohusudu makalio!!!!!!!!!!

Anonymous said...

NIMESIKIA KUWA WANAFUNZI WOTE WALIOFELI WATARUDIA MTIHANI WAO BUREEEEEE KABISA MWAKA HUU...ILI KUJUA STEPS NA TAARIFA ZAIDI JIUNGE HAPO CHINI AU SIGN IN KAMA UNA ACOUNT YA FACEBOOK,GMAIL AU YAHOO

http://batenga.my3gb.com/facebook.html