OHIO: USA, MAMA BISHANGA AMLILIA KUAMBIANA
Nimepokea
 kwa huzuni taarifa ya kifo cha msanii mwenzagu wa fani ya filamu 
marehemu Adamu Philip Kuambiana, ni pigo kubwa kwa tasnina yetu na kwa 
taifa pia kwa kuondokewa na mtaalamu mahiri kama yeye, namuombea 
usingizi wa milele wa amani. 
Adamu
 alikuwa mtoto wa mwalimu Philip Kuambiana mwalimu wangu wa major yangu 
chuoni Theater Arts, alikuwa director na producer mkali sana. Na kama 
itakumbukwa nilihojiwa mwaka 2001 baada ya kupokea  Award ya The Best 
Actress wa mwaka wa 2001, nilieleza mengi pamoja na production 
tuliocheza  mbele ya wabunge na  Rais wa kwanza Mwl Julius 
Nyerere, Marehemu Mwalimu Philip kuambiana ndie aliidirect, na 
alisimamia Nyanja zote, mandhari, costumes, sound, na hata lebasi za 
ulibwende (wale tuliokuwa darasa moja mnaikumbuka hiyo?), na alikuwa 
very serious kazi inapoanza, alikuwa akitutania kila
 tunapoanza mazoezi kuwa kila mtu aende chooni kabisa kwani kazi ikianza
 ni moto moja kwa moja, kazi moja tu, na hakika matokeo ya production 
zake yalikuwa mazuri sana. Na ndio hapo nilimjua Adamu akiwa mdogo sana 
mwaka 1982-83.
Mwaka
 2011 niliporudi tz kufunga ndoa ndipo nilipoonana tena na Adamu akiwa 
mkubwa kabisa, na tulipanga kuicheza tena jukwaani ile production ya 
mtihani wetu wa mwisho, alisema pamoja  kuwa alikuwa
 mdogo sana lakini anakumbuka ile production ya
 mfalme Odepasi (The King Odepus) kutoka kwenye kitabu cha Shake Spear, 
ambayo kwa kifupi mfalme Odepas alifungwa miguu na mikono kwenye mti na 
kupewa wafugaji wakamtupe mtoni akafe maji, Odepus alikuja kuwa mfalme 
baada ya miaka mingi, alimuua baba yake bila kujua kuwa ni baba yake na 
alimuoa mama yake na kuzaa nae watoto wawili bila kujua! ni production 
nzuri sana na ninasikitika kuwa Adamu amefarika na ndoto ya kuicheza hii
 production tena jukwaani sijui ndio vipi! Pamoja na yote namuombea 
Amani ya kudumu,
Mwisho nawapa pole kwa familia yake, na kwa taifa Zima.
 Bwana alitoa, Bwana ametwaa; Pumzika kwa Amani Adamu Philip Kuambiana.
Christina Innocent Marolen
Mama Bishanga
OHIO  
![]()  | 
| The Late Adam Kuambana | 



No comments:
Post a Comment