Kutoka Hapa Kwetu Blog
Kuhusu Kunyanyaswa kwa Jaji Warioba
Kati ya mambo
yaliyonishtua sana mwaka huu ni kunyanyaswa kwa Jaji Warioba. Kadhia hii
imetokana na kazi murua aliyofanya Jaji Warioba na tume yake ya
kukusanya mawazo ya wananchi kuhusu Katiba Mpya.
Kumekuwa na mlolongo wa matukio kadhaa ya unyanyasaji huo, ambao, kwa
kadiri ninavyofahamu, mwanzilishi wake ni Ikulu. Tukio la kupigwa Jaji
Warioba mkutanoni, ambalo limeripotiwa sana, ni kilele cha utovu huu.
Wengi tunaamini kuwa Jaji Warioba ananyanyaswa kwa sababu ya uwazi na
uwakilishi wa mawazo ya wananchi, jambo ambalo ni mwiba kwa mafisadi.
Nimeshtushwa vile vile na kauli ya Rais Kikwete kuhusu tukio hili la
vurugu na kupigwa Jaji Warioba. Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya
habari, Rais Kikwete aliishia tu kusema kuwa anaomba yasimkute
yaliyomkuta Jaji Warioba. Sikuona popote kama aliongelea suala hili kwa
undani na mapana kama linavyostahili.
Yeye kama Rais, nilitegemea kwanza atambue kuwa vurugu zile ni aibu kwa
nchi anayoiongoza. Nilitegemea awakemee walioleta vurugu zile
zilizohusisha pia kunyanyaswa kwa Jaji Warioba.
Nilitegemea Rais Kikwete atumie fursa ile kuwakumbusha wa-Tanzania,
wajibu wao wa kuheshimiana na kulumbana kwa hoja, sio kwa mabavu.
Angefanya hivyo, nigesema Rais ameonyesha busara za kiuongozi.
Nilitegemea angekemea utovu wa ustaarabu uliojitokeza. Angewakumbusha
wa-Tanzania njia ya usataarabu. badala ya yeye kujiwazia yeye binafsi,
kwamba anaomba yasimpate. Je, kauli yake hii si sawa na kumezea uovu?
Kauli yake haikuonyesha busara za kiuongozi.
Halafu, kuna pia kauli ya Samuel Sitta, ambayo nayo imenikera. Sitta
aliripotiwa akisema kuwa Jaji Warioba alijitakia yaliyomkuta. Niliposoma
taarifa hii, sikuamini kama mzee Sitta, anayetegemewa ana busara,
angeweza kuwa na msimamo kama huo.
Nasikia Sitta ni msomi. Nami najiuliza: ni msomi gani ambaye hatambui
wala kutetea mijadala au malumbano ya hoja. Kusema kuwa Jaji Warioba
alijitakia yaliyompata ni sawa na kumezea suala la mjadala kuingiliwa na
vurugu ambazo hazikubaliki katika mijadala. Kauli ya Sitta ni kama
inahalalisha ukosefu wa ustaarabu unaotegemewa hasa kwa wasomi.
Sijui Sitta alikulia wapi na katika maadili gani. Sisi wengine
tulilelewa katika maadili ya kuwaheshimu wazee. Kitendo cha kumpiga
mzee, kwa mujibu wa maadili yale, ni mwiko kabisa. Kama hukubaliani na
mzee, unapaswa kutafuta namna ya kujieleza, ambayo ni ya heshima kabisa.
Nilitegemea Sitta atambue na kuzingatia hilo. Atoe mfano kwa watoto na
vijana.
Tena na tena, katika jamii yetu, tumezoea kukemea tabia tunazoziiita
haziendani na maadili au utamaduni wetu. Nimeshangaa kuona kuwa Sitta,
ambaye ni mzee, anayetegemewa kuwa mlinzi na mtetezi wa maadili bora,
haonekani kutambua kuwa Jaji Warioba kama mzee, hawezi kuletewa vurugu
kama alizoletewa. Nimekerwa kabisa na kauli ya Sitta na kauli ya Rais..
Showing posts with label Katiba. Show all posts
Showing posts with label Katiba. Show all posts
Friday, November 14, 2014
Sunday, November 02, 2014
Jaji Warioba Anusurika Kupigwa Kwenye Mkutano!
Nchini
Tanzania vurugu zimekatisha mdahalo ulioitishwa kujadili yatokanayo na
rasimu ya katiba iliyopendekezwa. Waziri Mkuu mstaafu na aliyekuwa
mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya
Katiba, Joseph Warioba, alikuwa jukwaani wakati vurugu zilipozuka.
Wanaounga mkono rasimu wamedaiwa kusababisha vurugu ukumbini.Wapo watu
waliojeruhiwa. Nini maoni yako na umelipokea vipi tukio hilo? Habari
zaidi katika Amka na BBC.
Labels:
Fujo,
Jaji Joseph Warioba,
Katiba,
Paul Makonda
Saturday, May 24, 2014
Saturday, March 01, 2014
Rasimu ya Katiba imewashau Vijana! - Makonda
Mimi ni Kijana, ninayoyazungumza,ninayoyafanya yana reflect
uhalisia huo. Hivyo kwa wito wa Ujana najikuta nashawishika sana kuongeza
umakini katika masuala yahusuyo vijana hasa kwenye Katiba.
Ni ajabu lakini kweli kuwa sehemu inayotaja juu ya Haki na Wajibu wa Vijana katika Rasimu yote ni Ibara ya 44 tu, tena inataja kwa ujumla wake bila hata kuweka ibara ndogo ama vipengele vya ufafanuzi.
Ibara hiyo inasema;
Ni ajabu lakini kweli kuwa sehemu inayotaja juu ya Haki na Wajibu wa Vijana katika Rasimu yote ni Ibara ya 44 tu, tena inataja kwa ujumla wake bila hata kuweka ibara ndogo ama vipengele vya ufafanuzi.
Ibara hiyo inasema;
"..kila kijana ana haki na wajibu wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya Jamhuri ya Muungano pamoja na jamii kwa ujumla, na kwa mantiki hiyo, Serikali ya Jamhuri ya Muungano, serikali za nchi washirika na jamii zitahakikisha kuwa vijana wanawekewa mazingira mazuri ya kuwa "Raia Wema" na kupatiwa fursa za kushiriki kikamilifu katika nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni..."
Sikuwa nategemea huu unaweza ukawa ndio mwisho wa maelezo ya Rasimu kuhusu Vijana. Nilitegemea nitakuta vipengele vinavyobainisha namna vijana watakavyonufaika na rasilimali, namna ambavyo sheria ndogo na taratibu baguzi ktk upatikanaji wa ajira na fursa zitakavyobainishwa kikatiba ili kumaliza kabisa matatizo ya Vijana.
Nilidhani Rasimu itaweka bayana Uanzishwaji wa Baraza La Vijana la Taifa ili kiwe chombo cha kikatiba cha Vijana.
Nikitumia fursa na nafasi yangu kama mbunge wa bunge maalum la Katiba zipo hoja hizo kuu (3) tatu ambazo nitazisimamia ziingie kwenye Katiba kwa manufaa na mustakabal mwema wa Vijana bila kujali tofauti ya itikadi, dini ama kabila.
Na nakaribisha mawazo na michango ya fikra ktk hoja zihusuzo Vijana.
IMETOLEWA NA:
PAUL MAKONDA.
MBUNGE WA BUNGE MAALUM LA KATIBA.
Saturday, April 07, 2012
TAARIFA YA RAIS KIKWETE KUZINDUA TUME YA KATIBA IJUMAA APRIL 13, 2012
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 Fax: 255-22-2113425 | | PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete atazindua rasmi Tume ya Kukusanya na Kuratibu Maoni ya Mabadiliko ya Katiba na kuapisha wajumbe wa Tume hiyo Ijumaa ijayo, Aprili 13, mwaka huu, 2012.
Tume hiyo itazinduliwa na wajumbe wake kuapishwa kulingana na matakwa ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011 iliyounda Tume hiyo. Aidha, Tume hiyo itazinduliwa rasmi wiki moja baada ya kuwa imetangazwa rasmi. Rais Kikwete alitangaza Tume hiyo jana, Ijumaa, Aprili 6, 2012, kwenye mkutano wa wahariri uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam.
Tume hiyo itakayoongozwa na Mwenyekiti Jaji Joseph Sinde Warioba akisaidiwa na Makamu Mwenyekiti Jaji Mkuu Mstaafu, Jaji Augustino Ramadhan ina wajumbe 30, ikiwa ni wajumbe 15 kutoka kila moja ya pande mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wajumbe wa Tume hiyo kutoka Tanzania Bara ni Profesa Mwesiga L Baregu, Ndugu Riziki Shahari Mngwali, Dkt. Edmund Adrian Sengodo Mvungi, Ndugu Richard Shadrack Lyimo, Ndugu John J Nkolo, Alhaji Saidi El Maamry na Ndugu Jesca Sydney Mkuchu.
Wajumbe wengine wa Tume hiyo kutoka Bara ni Profesa Palamagamba Kabudi, Ndugu Humphrey Polepole, Ndugu Yahya Msulwa, Ndugu Esther Mkwizu, Ndugu Maria Malingumu Kashonda, Mheshimiwa Al-Shaymaa J Kwegyir, Ndugu Mwantumu Jasmine Malale na Ndugu Joseph Butiku.
Wajumbe wa Tume hiyo kutoka Tanzania Visiwani ni Dkt. Salim Ahmed Salim, Ndugu Fatma Saidi Ali, Ndugu Omar Sheha Mussa, Ndugu Raya Suleiman Hamad, Ndugu Awadh Ali Saidi, Ndugu Ussi Khamis Haji na Ndugu Salma Maoulidi.
Wengine kutoka Visiwani ni Ndugu Nassor Khamis Mohammed, Ndugu Simai Mohammed Said, Ndugu Muhammed Yussuf Mshamba, Ndugu Kibibi Mwinyi Hassan, Ndugu Suleiman Omar Ali, Ndugu Salama Kombo Ahmed, Ndugu Abubakar Mohammed Ali na Ndugu Ally Abdullah Ally Saleh.
Shughuli za Tume hiyo zitaratibiwa na Sekretarieti ambayo Katibu wake atakuwa Ndugu Assaa Ahmad Rashid na Naibu Katibu atakuwa Ndugu Casmir Sumba Kyuki.
Mwisho.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
07 Aprili, 2012
Subscribe to:
Posts (Atom)