Showing posts with label Martha Shani. Show all posts
Showing posts with label Martha Shani. Show all posts

Saturday, November 16, 2013

Mazishi ya Martha Shani Tanzania

Na Swahili TV
Kwa niaba ya Familia, Kamati ya Mazishi Marekani na Tanzania na ndugu na jamaa wote kwa ujumla tumeona ni vyema nanyi mkaona matukio yote kwani mlishiriki katika msiba huu. Kwa mara nyingine tena tunatoa shukrani zetu za dhati kwa wote mliofanikisha Shughuli zote Usafiri, Maandalizi mbalimnbali na hatimaye kuuhifadhi mwili wa mpendwa wetu, dada yetu, rafiki na kipenzi chetu Bi. Martha Shani.Mazishi yalifanyika Puma Sindiga siku ya Alhamisi ya Octoba 31, 2013. Video ya matukio yote tutaiweka soon hapa hapa Swahili TV Blog.

PICHA ZA MATUKIO YOTE
Alex akipewa pole na Shangazi wa Martha

Kushoto; Vincent Mughwai, Joseph, Alex akimshikia mtoto Chris beleshi akiweka udongo katika kaburi la Mama yake, huku Mchungaji Peter Ihema wa Kanisa la Pentekoste Puma akitazama . Mazishi yalifanyika Alhamis Oktoba 31, 2013 Puma-Singida.
Alex, Joseph, DMK, Muddy wakiwafuatilia shughuli za Mazishi Alhamis Oktoba 31, 2013 Puma-Singida.
AU INGIA

Saturday, October 26, 2013

Msiba wa Marsha Shani - Washington D.C., USA

DAKIKA 90 ZA DUNIA: Msiba wa Martha Shani DC na mapambano dhidi ya uvutaji sigara nchini Marekani
Katika kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA wiki hii... Kutoka nchini Marekani, tuanze na habari za msiba ulioikumba jamii ya waTanzania waishio maeneo ya Washington DC.
Marehemu Martha Shani
NA KISHA......
Uvutaji sigara, ni sababu kubwa ya vifo vinavyozuilika nchini Marekani. Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Kituo cha Kudhibiti Maradhi nchini Marekani (CDC) kifo kimoja kati ya vitano nchini Marekani hutokana na athari za uvutaji sigara, na zaidi ya watu milioni 43.8 nchini humo ni wavutaji wa sigara.
Lakini vita dhidi ya uvutaji huo vimekuwa vikipamba moto, na teknolojia imekuwa ikishirikishwa katika vita hivyo. Na ni vita hivyohivyo dhidi ya uvutaji vinavyoanza kutiliwa mashaka nchini humo.

Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).

Hii ilikuwa ripoti ya Oktoba 26, 2013