Showing posts with label Mpira. Show all posts
Showing posts with label Mpira. Show all posts

Saturday, June 24, 2017

Shujaaz Wawafunda Waandaaji wa Mashindano ya East Africa Cup 2017

Mkuu wa utafiti wa Kampuni ya Well Told Story,Dkt Anastasia Mirzoyants akitoa maelezo kwa washiriki wa Warsha iliyoandaliwa na  Mradi wa Shujaaz  iliyofanyika Hotel ya Uhuru mjini Moshi.
Baadhi ya Washiriki wa Warsha iliyoandaliwa na watayarishaji wa Mradi wa Shujaaz kwa ajili ya kutoa eimu juu ya maswala mbalimbali ikiwemo Ujasiliamali pamoja na Kilimo,Warsha ambayo inafanyika sambamba na Mashindano ya Kimataifa ya Vijana kwa vijana wa nchi za Afrika Mashariki.
Mkuu wa utafiti wa Kampuni ya Well Told Story,Dkt Anastasia Mirzoyants akitoa maelezo kwa washiriki wa Warsha iliyoandaliwa na  Mradi wa Shujaaz  iliyofanyika Hotel ya Uhuru mjini Moshi
Washiriki katika Warsha hiyo.
Mkuu wa utafiti wa Kampuni ya Well Told Story,Dkt Anastasia Mirzoyants akizungumza na Wanahabari mara baada ya kumalizika kwa Warsha iliyoandaliwa na  Mradi wa Shujaaz  iliyofanyika Hotel ya Uhuru mjini Moshi
Baadhi ya Vijana waliofanikiwa kuingia katika Kijiji cha Shujaaz wakionesha umahiri wao katika uimbaji ambapo pia walipata zawadi kutoka Shujaaz.
Timu za watoto chini ya miaka 13 za Msimamo na Right to Play kutoka Dar es Salaam zikichuana katika mashindano ya East Africa Cup 2017 yanayofanyika katika viwanja vya shule ya sekondari ya Moshi Ufundi.
Vijana chini ya miaka 13 wakioneshana umahiri  katika kusakata soka katika mashindano ya East Africa Cup 2017 yanayofanyika katika viwanja vya Moshi Technical.
Baadhi ya vijana wakifuatilia mchezo huo.
Katika Kijiji cha Shujaaz wakishiriki michezo mbalimbali ikiwemo ya kukimbia huku wakiwa ndani ya magunia.
Kijiji cha Shujaaz kimekuwa kivutio kikubwa kwa vijana wanaoshiriki mashindano ya East Africa Cup 2017.

Na D ixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini.

Tuesday, July 08, 2014

Brazil Wapondwa Vibaya na Ujerumani Katika Mashindano ya World Cup!

Katika Mashindano ya Kombe la Dunia huko Brazil, Brazili ilipondwa vibaya sana na Ujerumani!  Brazil wameanguka  1-7.  Duh! Hata Pele ana aibu!

Kwa habari za Ushindi wa Ujerumani BOFYA HAPA:

Shabiki wa Brazil akilia machozi baada ya Brazil Kutolewa katika mashindao ya World Cup. Unaweza kuona picha zaidi kwa  KUBOFYA HAPA:

Saturday, August 25, 2012

Mpira London


MASHABIKI ARSENAL WAMTEMEA MOTO ROBIN VAN PERSIE

Urban Pulse na Freddy Macha waweletea habari moto moto siku moja baada ya kutangazwa kuhama kwa mshambuliaji na nahodha wa Arsenal, Robin Van Persie kwenda Manchester United  adui  wake mkubwa. Mahojiano yalifanywa kando kando ya uwanja maarufu wa Emirates ambapo washabiki walikuwa wakielekea kufurahia mechi ya kwanza ya ligi (2012-2013) baina ya Arsenal na Sunderland.