Showing posts with label Ocean Road Hospital. Show all posts
Showing posts with label Ocean Road Hospital. Show all posts

Thursday, March 26, 2009

Wagonjwa wazidi kuongezeka Ocean Road Hospital


Wagonjwa wa Saratani (Kansa) wanazidi kuongezeka Ocean Road Hospital. Ina maana kuwa ubora wa huduma huko itapungua. Wadau, nawauliza kwa nini ugonjwa wa saratani unaongezeka Tanzania? Je, watu walikuwa nayo zamani ila hatukujua ni nini, tunasema kalogwa? Je, ni kwa vile maisha yanabadilika na kuwa ya kizungu (vyakula nk.).?
*********************************************************

Kutoka ippmedia.com

Taasisi ya Saratani ya jijini Ocean Road imeanza kuzidiwa

2009-01-24 12:04:06

Na ITV Habari

Taasisi ya Saratani ya jijini Ocean Road imeanza kuzidiwa kutoa huduma za tiba hiyo kwa wagonjwa wapya kutokana na idadi ya wagonjwa hao kuongezeka kila mwaka na kufikia wagonjwa elfu arobaini wanaohitaji tiba hiyo kwa mwaka .

Wakizumgumza baada ya ufunguzi wa mkutano wa siku tatu kujadili mikakati ya kuthibiti ugonjwa wa saratani uliohudhuriwa na wataalam wa tiba na madkatari wa saratani nchini baadhi ya washiriki wamesema kuna haja ya kuongeza jitihada katika kuwahamasisha wanajamii wa maeneo ya vijijini umuhimu wa kuwahi tiba ya saratani ikiwa kwenye awamu za mwanzoni wakati bado kuna matumaini ya mgonjwa huyo kupona.
SOURCE: ITV

Tuesday, February 17, 2009

Wizi Ocean Road Hospital

Wadau, mnaweza kuamini kuwa vifaa hivi vya chemotherapy vimeibiwa kutoka Ocean Road Hospital. Ocean Road ni hospitali kuu Bongo ya kutibu ugonjwa wa saratani (cancer). Yaani wametoa huo mtambo mkubwa bila mtu yeyote kuona kweli? Walinzi walikuwa wapi? Wafanyakazi walikuwa wapi? Najua pale kuna manesi na madaktari 24/7!
Yaani huo wizi lazima ilikuwa ni inside job. Lazima kulikuwa na watu waliojua kuitoa huko bila kuiharibu. Hivi wanausalama wanafanya nini siku hizi huko Bongo?
***********************************************************************
Picha na Maelezo ya chini kutoka Michuzi Blog:
Hii ndo aina ya mashine zilizoibwa yapata wiki mbili zilizopita pale ORCI zaitwa Control Console, zimenunuliwa tena mpya kwa gharama ya Dola za US 22,000/- na hivyo wagonjwa wameanza tena leo kupata huduma baada ya kusimama kwa muda wote huo.

Mdau Bernard Rwebangira anashindwa kuelewa mashine kubwa na nyeti kama hii iliiniwaibiwaje? ungana naye kujadili hilo kwa kubofya hapa

Monday, August 25, 2008

Da Nuru Mkeremi akumbuka Wagonjwa wa Kansa Tanzania


Hivi karibuni, Dada Nuru Mkeremi alifiwa na Mama yake mzazi Mama Nellie Kidela, ambaye alikuwa mtangazaji miaka mingi Radio Tanzania. Dada Nelie aliugua kansa ya ziwa muda mrefu. Alifariki mwaka jana mjini Dar es Salaam. Rest in Peace.

Juzi Da Nuru alituma huo ujumbe kwa marafiki zake
.

********************************************************************

Hi yall, I was comforted when I heard that my mom was surrounded by people of God when she was on her dying days........It still hurts, don't get me wrong.

This morning I remembered all those cancer patients at Ocean Road Hospital who have been referred from other hospitals............who is there to comfort them? Who is there to cry with them? How many people really pray for them and their families? I just mentioned Ocean Road hospital to represent all other hospitals.

I guess I was called for this, I ask my friends for supports both spiritually and materially. I do this in honor of all those who were there for my mom. God bless you all mightly in Jesus name!!Amen