Showing posts with label Politics. Show all posts
Showing posts with label Politics. Show all posts

Sunday, December 06, 2015

Balozi Wilson Masilingi Aanza Ziara ya Kutembelea Vyama Vya Siasa DMV

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi leo Jumamosi Desemba 5, 2015 alihudhuria mkutano wa Halmashauri ya CCM tawi la DMV ikiwa ni moja ya ziara zake anazotarajiwa kuzifanya kutembelea matawi ya vyama vya siasa nchiMarekani yenye lengo la kudumisha mshikamano na ushirikiano wa Watanzania bila kujali itikadi za vyama vyao.

Akiongea kwenye mkutano wa Halmashauri ya CCM DMV Mhe. Wilson Masilingi amesema lengo kuu ni kuwa karibu na vyama vya siasa kwa lengo la kuleta umoja na mshikamano ndani ya Jumuiya za Watanzania nchini Marekani na pia kuvitambua kama sehemu na sura ya Diaspora na kutoa wito kwa Watanzania waishio Marekani kuelekeza nguvu katika kuwekeza nyumbani bila kujali ufuasi wa chama unachoamini au kushabikia, wote ni Watanzania.

Mhe. Balozi Wilson Masilingi aliiomba Halmashauri hiyo ya CCM DMV kusaidia katika maendeleo ya Tanzania kwa kupanua wigo wao pamoja na kwamba lengo lao ni siasa na siasa ni sehemu ya maisha ya jamii na maendeleo ya jamii yanategemea siasa, kwa hiyo basi mnaposikia kuna muwekezaji yupo tayari kuwekeza Tanzania msisite Ubalozi upo wazi na utafanya kila liwezekanalo kuhakikisha muwekezaji huyo hapati vikwazo vyovyote.

Mwisho Balozi Wilson Masilingi aliwashukuru Watanzania kwa kuwa mabalozi wazuri nchini Marekani na kuwaasa kuishi kwa kufuata misingi na sheria za nchi ya Marekani.

 Mhe. Balozi Wilson Masilingi akiongea jambo na mwenyekiti wa tawi CCM DMV Bwn. George Sebo kwenye mkutano wa Halmashauri ya CCM DMV siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 mkutano uliofanyika Hampton Inn, College Park, Maryland. Picha na Kwanza Production/Vijimambo Blog
Mkutano ulianza kwa sala na kuwakumbuka wote waliotangulia mbele ya haki.

Mwenyekiti tawi la CCM DMV Bwn. George Sebo akifungua kikao cha Halmashauri ya CCM DMV kilichofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 katika ukumbi wa Hampton Inn, College Park, Maryland.

Sunday, January 12, 2014

Mzee George Liundi Afariki Dunia

 Taarifa kutoka Tanzania, zinasema kuwa Mzee George Liundi, amefariki dunia leo.  Nakumbuka kazi aliyofanya wakati ule waliporuhusu vyama vingi Tanzania.  Yeye alikuwa Msajili.

Mungu ailaze roho yaka mahala pema mbinguni. Amen.

*****************************************
KWA HISANI YA KAKA MAGGID MJENGWA

TANZIA: NDUGU GEORGE LIUNDI AFARIKI DUNIA

Ndugu zangu,
Kama wengi wenu, nami nimepokea kwa masikitiko usiku huu, taarifa za kifo cha ghafla cha Ndugu George Liundi ambaye alikuwa Msajili wa kwanza kwa vyama vya siasa hapa nchini.

Kwa mujibu wa maelezo ya mwana wa marehemu, Taji Liundi, Ndugu Liundi amefariki leo mchana.

Mwezi Agosti mwaka jana, mara tu baadada ya Jaji Mutungi kuteuliwa kushika nafasi ya Ndugu John Tendwa kama msajili wa vyama, niliandika makala juu ya tukio hilo. Hii hapa chini ni sehemu ya makala hiyo iliyomhusu Ndugu George Liundi pia...

"Miaka 20 iliyopita nilipata bahati ya kukutana na Msajili wa kwanza wa Vyama Vya Siasa. Ni Bw. George Liundi. Ni mwaka 1993, ilikuwa ni katika mwaka wake wa kwanza kama Msajili. Nakumbuka vema, nikiwa kijana mdogo tu, George Liundi alinipokea kwenye ofisi zake pale Mtaa wa Shaaban Robert. Tulikunywa chai na kuongea kwa kirefu.

Sijui George Liundi yuko wapi siku hizi, hakika ningependa nikutane nae nimkumbushe juu ya mazungumzo yetu yale. Maana, baadhi ya changamoto za mfumo wa vyama vingi tulizoziongea na Bw. Liundi miaka 20 iliyopita ndio zinazoonekana sasa.

Nakumbuka Liundi alikuwa mtu muwazi sana. Alionyesha hata wakati huo, wasiwasi wake juu ya vyama kufichaficha mambo yao ya ndani na kuwa vingine vilikuwa ni kama NGO ya mtu au kikundi cha watu. Kwamba kulikuwa na tatizo la uwepo wa demokrasia ya ndani ya vyama- Intra party democracy.

Hata wakati ule, niliona kupitia mazungumzo yangu na Liundi, kuwa dhana ya kuwa Msajili wa Vyama ilionekana kwenye macho ya Chama Dola na jamii kwa ujumla kuwa ni kuwa mlezi wa vyama vinavyoanzishwa. Kwamba CCM ni chama kikongwe na hakikuhitaji ‘ kulelewa’ na Msajili.

Kwa wakati huo vyama vilivyosajiliwa havikuonekana kuwa na impact sana na hata kuwa tishio kwa CCM. Vingi vilikuwa kwenye ugomvi wa ndani kitu ambacho CCM kwa wakati huo haikuwa kabisa na tatizo hilo.

Nilichokipata kwenye mazungumzo yangu na Liundi miaka 20 iliyopita ni ukweli, kuwa hakukufanyika review ya kina juu ya katiba za vyama kabla ya kusajiliwa. Ndio maana, masuala kama haya ya vyama kuwa na vikosi au vikundi vyake vya ulinzi yalipaswa kupigwa marufuku na Msajili tangu wakati huo bila kujali kama CCM wana Green Guards." ( Raia Mwema)

Mungu Amlaze Mahali Pema Peponi Ndugu George Liundi.

Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam.


Saturday, August 10, 2013

Rwanda Sasa Yaruhusu Chama Mpinzani


Map of Rwanda
KIGALI, Rwanda (AP) - Rwandan President Paul Kagame's government has legalized an opposition political party that spent four years trying to get registered.

   The Democratic Green Party, led by Frank Habineza, said late Friday it received a certificate of registration after years of attempts, during which time one of its vice presidents was murdered in 2010. It is not clear if the party will be able to participate in Sept. 16 parliamentary elections. The deadline for submissions is Monday. The party asked the National Electoral Commission to extend the deadline.
Oppo
   "If not we will start preparing for the 2017 presidential polls," Habineza said. "But all in all, this is a very important step forward in the democratization process of Rwanda. The struggle to get the party registered has taken four years. The party was officially launched on 14th Aug. 2009, and the journey has been very tough."

   Rwanda has several political parties, but most are loyal to Kagame's Rwanda Patriotic Front. Habineza's party is seen as a true opposition party.

   Rwanda has received international praise for the economic progress it has made since its 1994 genocide. But it also receives international criticism for a lack of free political space. The country has yet to see a flourishing opposition party, and Human Rights Watch and Amnesty International warn that Kagame's government is increasingly becoming more intolerant of dissenting voices.

   The recognition of the Rwandan Greens came a few days after the country's parliament passed a new law that will make it difficult for political parties in Rwanda to operate without depending on government funds. The new law, which is one of the many bills expedited by the current house as it wound up work ahead of the September polls, bars political parties from receiving external support from donors or friends outside Rwanda.

   The Green Party and others like the unregistered Unified Democratic Forces, a party led by the jailed Victoire Ingabire, will no longer be allowed to take funds from outside the country.

   "It's a tough law. It will be difficult for other parties to exist alongside Rwanda Patriotic Front (RPF) which has abundant resources," said Habineza, referring to the party of Rwandan President Paul Kagame.

   Habineza said the new law will make it difficult for other parties to compete with RPF, which has held a firm grip on power for the last 19 years. Kagame's party also dominates the country's private sector and government tendering processes.