Showing posts with label Shaka Zulu. Show all posts
Showing posts with label Shaka Zulu. Show all posts

Monday, November 05, 2007

Aliyeigiza kama Shaka Zulu Amefariki!




Mwigizaji maarufu wa Afrika Kusini, Henry Cele, amefariki dunia kwao Durban. Wengi tunamfahamu kama SHAKA ZULU.
Habari zinasema kuwa alifariki jana baada ya kuuguua ugonjwa wa kifua. Alikuwa amelazwa wodi ya wagonjwa mahututi kwa zaidi ya wiki mbili. Habari za kusikitisha zinasema aliugua muda mrefu na hapo mwisho alikuwa anatukana na kupiga watu ovyo mpaka ilibidi afungwe na kamba kwenye kitanda chake cha hospitali.
Henry Cele aliigiza kwenye sinema kadhaa lakini hakupta umaarufu aliyotegemea. Agent wake anasema kuwa hapo mwisho offa za kazi zilianza kuingia lakini Cele alikuwa ni mgonjwa hivyo hakuweza kuzifanya.

Alifanya kazi nzuri mno kuigiza maisha ya mfalme maarufu ya huko Afrika Kusini, Shaka Zulu. Hiyo sinema inajulikana kama sinema bora na inayoonyesha maisha ya Shaka Zulu kutoka upande wa mwafrika. Na Shaka Zulu mwisho wa maisha yake alikuwa kama kichaa maana alikuwa anaua watu ovyo na kusababisha maelfu ya wafrika kusini kukimbia kwao.

Kabla ya kuingia kwenye dunia ya uigizaji, Henry Cele, alikuwa ni mcheza mpira maarufu wa Afrika Kusini. Alikuwa anaitwa, The Black Cat. (Paka Mweusi) kwa sababu alikuwa ni mweusi sana kulinganisha na wafrika kusini wengine.

Kwa habari zaidi someni: