Monday, November 05, 2007

Aliyeigiza kama Shaka Zulu Amefariki!




Mwigizaji maarufu wa Afrika Kusini, Henry Cele, amefariki dunia kwao Durban. Wengi tunamfahamu kama SHAKA ZULU.
Habari zinasema kuwa alifariki jana baada ya kuuguua ugonjwa wa kifua. Alikuwa amelazwa wodi ya wagonjwa mahututi kwa zaidi ya wiki mbili. Habari za kusikitisha zinasema aliugua muda mrefu na hapo mwisho alikuwa anatukana na kupiga watu ovyo mpaka ilibidi afungwe na kamba kwenye kitanda chake cha hospitali.
Henry Cele aliigiza kwenye sinema kadhaa lakini hakupta umaarufu aliyotegemea. Agent wake anasema kuwa hapo mwisho offa za kazi zilianza kuingia lakini Cele alikuwa ni mgonjwa hivyo hakuweza kuzifanya.

Alifanya kazi nzuri mno kuigiza maisha ya mfalme maarufu ya huko Afrika Kusini, Shaka Zulu. Hiyo sinema inajulikana kama sinema bora na inayoonyesha maisha ya Shaka Zulu kutoka upande wa mwafrika. Na Shaka Zulu mwisho wa maisha yake alikuwa kama kichaa maana alikuwa anaua watu ovyo na kusababisha maelfu ya wafrika kusini kukimbia kwao.

Kabla ya kuingia kwenye dunia ya uigizaji, Henry Cele, alikuwa ni mcheza mpira maarufu wa Afrika Kusini. Alikuwa anaitwa, The Black Cat. (Paka Mweusi) kwa sababu alikuwa ni mweusi sana kulinganisha na wafrika kusini wengine.

Kwa habari zaidi someni:


3 comments:

Anonymous said...

REST IN PEACE! Sounds like he died a horrible death. You know what happens is that people expect a certain level of stardom when it doesn't happen they become frustrated. This is very sad how he died. YOU ARE AT PEACE AT LAST.

Anonymous said...

Rest Peace. He was indeed a great actor who did not get the acclaim that he deserved. He gave and Oscar winning performance in Shaka Zulu.

Anonymous said...

Wena Wendlovu, Zulu .... to Henry Cele

Sithi Bayethe, wena owakhula silibele

Ndlovu ebusa kuzo zonke, wena owazalelwa thina abesizwe'

Zulu, bonke abakhothame kuye'

Impi ngeyakho Ndlovu, Shaka

Wonke amehlo akabheke kuye'

Uyinkosi yesizwe esiphakeme' Zulu

Esaziwa ngesandla sakho esiqinile'

Uyindlovu eyaziwayo phakathi kwamabutho' wonke

Umbuso uwuthatha uwubkekisa phezulu ndlovu, ka Ndaba

Nkosi' wena waziwa ngoshisisa impi' banda' sithi Bayede

Konke okwakho okwande Zulu

Henry Cele wawu nguye impela' Zulu Kasenzangakhona'

Bayede ..... Wena wendlovu