Showing posts with label Stroke. Show all posts
Showing posts with label Stroke. Show all posts

Tuesday, June 09, 2015

Muigizaji 'Mzee Kankaa' Afariki Dunia

Kutoka Tanga Yetu Blog:

MSANII mkongwe wa filamu nchini, Juma Ally Salim ‘Mzee Kankaa’ amefariki dunia leo alfajiri akiwa nyumbani kwake Tandale jijini Dar es Salaam baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi kwa muda mrefu.

Mwili wa Mzee Kankaa unatarajiwa kuzikwa leo saa 10 jioni katika makaburi ya Ali Maua jijini Dar es Salaam.

Marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi kwa zaidi ya miaka mitatu. Msiba upo nyumbani kwa marehemu eneo la Tandale-Chama jijini Dar.


The Late Mzee Kankaa
 Kwa habari zaidi Tembelea TANGA YETU BLOG

Thursday, April 24, 2014

Tanzia - Mrs. Greene Kapepela Chale (1933 - 2014) Shangazi Yangu

Wadau, ninasikitika kutangaza kifo cha shangazi yangu, Mrs. Greene Kapepela Chale, ni dada wa baba yangu mzazi tumbo moja. Amefariki saa 8 usiku wa kuamkia leo, huko Kitete Hospital, Tabora. Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen. 

Misiba imefululiza. alipoteza wajukuu watatu katika miezi chache na wiki iliyopita alifariki Shangazi Mrs. Rozina Che-Mponda Hauli, mke wa baba mdogo,  ghafla.  Dada yangu anasema  kuwa shangazi alilia sana huzuni zilimzidi na inaeleke alipata stroke (kiharusi).

***************************************
I would like to thank all of those who offered prayers for my Aunt, Mrs. Greene Kapepela Chale (maiden name Che-Mponda). I am deeply saddened to announce that she passed away this morning at 2:00am, Tanzanian time at Kitete Hospital in Tabora, Tanzania. May she rest in peace. We are grief stricken.

Aunt Greene you were such fun despite the tragedies that plagued your life. You now join Uncle Selwin, your children, James, John & Happiness, and your many grandchildren and great grandchildren who died before you, in Heaven. No one should endure the grief you endured, but you stayed strong until you could take it no more. We will always remember you my dear Shangazi Greene.

Rest in Peace. 



Shangazi (mwenye Kilemba), Dada Eliza (katikati), na wifi Mrs, Mburuma (kushoto)

Mimi na Shangazi Greene mwaka 2010 nilipoenda Tanzania

Mrs. Greene Kapepela Chale (1932 - 2014)

Thursday, March 28, 2013

Mazishi ya Mh. Khamis Yatakuwa Kesho Mjini Pemba


The Late Honourable Salim Hemed Khamis (MP Chambani Pemba -CUF)

MAZISHI ya aliyekuwa Mbunge wa CUF, Jimbo la Chambani Pemba kisiwani Zanzibar, Marehemu, Salim Hemed Khamis,  (62), yanataraji kufanyika kesho  (Ijumaa Machi 29, 2013) mchana mjini Pemba.

Tarifa za awali kutoka Chama cha Wananchi CUF, zinasema kuwa Mwili wa Marehemu, Khamis utaagwa kesho asubuhi kuanzia majira ya saa 2:30-4:00 katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam ambapo Viongozi mbalimbali wa kitaifa na Kimataifa pamoja na wananchi na Wanachama wa CUF watapata fursa ya kutoa heshima za mwisho kwa Marehemu.

Taarifa hiyo ya Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julis Mtatiro inasema kuwa Msafara utaondoka Karimjee saa 4:00 kuelekea uwaja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambapo Msafara wa Ndege 2 utaondoka kwenda Pemba.

Saa saba mchana mazishi yatafanyika huko Pemba na maazishi hayo yataongozwa na Viongozi wa serikali, Wabunge na CUF.

Mtatiro amewaomba wanachama nba wafuasi wa CUF jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kuuga mwili wa Mbunge huyo aliyefikwa na umauti akiwa kazini katika vikao vya Kamati za Bunge, ambapo Marehemu alikuwa Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

***************************************************************************

KUTOKA MICHUZI BLOG:

Pichani ni Baadhi ya Maofisa wa Ofisi Ndogo ya Bunge,wakimsaidia kwa kumbeba Mbunge wa Chambani,Bwa.SalimHemed Khamis,mara baada ya kuanguka ghafla hapo jana jijini Dar akiwa katika vikao vya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kukimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu ya haraka.



======= ====== ======

Habari zilizoifikia Globu ya Jamii hivi punde inaelezwa kuwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Chambani-Pemba, Salim Hemed Khamis,ambaye hapo jana alianguka ghafla jijini Dar Es Salaam alipokuwa akihudhuria vikao vya kamati ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kukimbizwa hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu, amefariki dunia muda mfupi uliopita katika Hospitali hiyo ya Taifa ya Muhimbili,aidha chanzo cha habari hizi kimeongeza kuwa taratibu za kuusafirisha mwili wa Marehemu kuelekea Pemba kwa mazishi zinafanyika.Tutazidi kuwafahamisha zaidi kadiri ya habari zitakavyokuwa zikiingia.
Mungu ailaze Roho ya Marehemu mahali pema Peponi-Amin

***************************************

WADAU NINA SWALI.  Hivi huko Bungeni, hakuna Stretcher ya kubeba wagonjwa?  Je, hakuna watu wa First Aid?   Hii ni mwaka 2013, wanatakiwa wawe na wahudumu wa afya, ambulance, wahudumu onsite. Watu wawepo wanaoelewa jinsi ya kubeba wagonjwa. Na hasa huko Bungeni waBunge wengi wana umri mkubwa na matatatizo ya kiafya.  - Chemi