Tuesday, June 09, 2015

Muigizaji 'Mzee Kankaa' Afariki Dunia

Kutoka Tanga Yetu Blog:

MSANII mkongwe wa filamu nchini, Juma Ally Salim ‘Mzee Kankaa’ amefariki dunia leo alfajiri akiwa nyumbani kwake Tandale jijini Dar es Salaam baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi kwa muda mrefu.

Mwili wa Mzee Kankaa unatarajiwa kuzikwa leo saa 10 jioni katika makaburi ya Ali Maua jijini Dar es Salaam.

Marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi kwa zaidi ya miaka mitatu. Msiba upo nyumbani kwa marehemu eneo la Tandale-Chama jijini Dar.


The Late Mzee Kankaa
 Kwa habari zaidi Tembelea TANGA YETU BLOG

No comments: