Showing posts with label nyanya. Show all posts
Showing posts with label nyanya. Show all posts

Thursday, May 28, 2009

Nyanya Zamponza Da Veronica

Wadau, samahani lakini roho imeniuma sana nilivyona hizi picha. Yaani mtu anatafuta riziki kwa kuuza nyanya, halafu anayang'anywa! Na ninajua hao mgambo wanaenda kugawana bidhaa walizoiba! Ndiyo nimesema hao mgambo wameiba! Nilivyokuwa Tanzania mara nyingi nilishuhudia hao wanaojiita mgambo wakiwaibia machinga, mama ntilie na wengine mali yao! NANI ANAVUNJA SHERIA HAPO? Tanzania bado iko vile vile! Hao mgambo wafanye kazi ya kukamata vibaka na wezi waliozagaa juko mitaani na waache watu wanatafuta riziki kwa njia za heshima! Angekuwa CD wala wasingemsumbua!

*******************************************************************



Picha na Maelezo kutoka JIACHIE BLOG:

Mfanyabiashara wa nyanya katika soko la Kariakoo aliye fahamika kwa jina moja la Veronica akipambana na Askari Mgambo wa Jiji wakati walipokuwa wakichukua bidhaa zake ,kitendo hicho kimempelekea mama huyo kumwacha uchi jambo ambalo ni kinyume cha haki na sheria za binadamu.

JIACHIE inalaani vikali vitendo vya udharirishaji kama hivi,ambavyo kimsingi vinavuka mipaka ya haki na sheria za binadamu,hakuna mwenye haki ya kumvua nguo mwenzake hadharani,mbele ya watu lundo kama hivi.!

Tuesday, June 10, 2008

Nyanya Adimu Marekani!


Sisi wapenzi wa kachumbari tulie tu! Kama unapenda kula nyanya na salad au kwenye hamburger ulie tu!

Kwa sasa haziuzwi supermarket na kwenye restarurant. Kisa eti zingine zina ugonjwa wa Salmonella! Na wataalamu wanasema hii siyo salmonella ya kawaida bali ni salmonella saintpaul!

Ukipata Salmonella unaumwa kwa masaa 12 hadi 72. Tumbo inauma sana na unaharisha na kutapika. Pia uinakuwa na homa. Watoto wadogo, wazee na pia watu wenya magonjwa yanayoathiri kinga ya mwili wanaweza wakafa.

Kwa sasa watu 150 katika majimbo 17 ya Marekani wameumwa. Hakuna aliyekufa.

Ila unaweza kununua zile grape tomatoes yaani zile nyanya ndogo ndogo ambazo zilaliwa nzima nizma.
Tunagojea all clear kwa hamu tuendelee kula nyanya. Zimejaa vitamin C na A!

Someni:



http://www.sfgate.com/cgi-bin/article.cgi?f=/c/a/2008/06/10/BAA51162BT.DTL