

Huyo mtoto mweusi ni mtoto wa miezi kumi na tatu, David Banda ambaye baada ya miezi kumi na nane atakuwa mtoto wa mwimbaji maarufu Madonna na mume wake, Guy Ritchie. David yuko Uingereza sasa na familia yake mpya.
Juu, ni picha ya Madonna na watoto wake wote, chini ni picha ya David na baba yake mpya Guy Ritchie. Yaani wiki mbili tu, mtoto kanawiri na kuonekana mwenye furaha!
Madonna alimpata David kutoka kwenye nyumba ya watoto yatima huko Malawi. Mama yake alikufa katika uzazi na pia wakubwa zake walifariki shauri ya malaria. Baba yake mzazi Yohane Banda, alishindwa kumtunza mwanae na kumpeleka huko kwa watoto yatima. Baba yake anasema ni bora amchukuea maana angebakia Malawi angekufa.
Huyo mtoto atalelewa katika nyumba ya fahari na atakuwa na mahitaji yake yote na atasoma digrii zote anazotaka kusoma. Pia mama yake Madonna lazima atamwachia mamilioni ya dola za kurithi. Si uwongo kulelewa katika familia ni tofauti na kulelewa kwenye nyumba ya yatima.
David Banda kazaliwa katika umaskini, lakini leo anaishi katika utajiri. Na lazima kuna watu wanamwonea wivu!
3 comments:
me nafikiri hawa wanasheria/watetezi wa haki za binadamu wanatafuta ulaji tu. Kama baba ya mtoto ametoa ruksa, wao ni nani kuanza kuzuia zuia??
Mie swali moja linalonila kichwa sana kwenye maswala ya adoption ni hili; je adoption ni kwa ajili ya wazazi wanao adopt au kwa ajili ya mtoto?
Kwa jinsi nionavyo mimi mara nyingi wazazi wanaoadopt huwa wao ndio wanataka wafaidi zaidi kulikko watoto kwani wanawatumia watoto kutimiza haja zao. kwa mfano, wazazi waneza kuwa hawajabahatika kupata mtoto kwa ivo wanajiona wako lonely kwa hiyo wanaamua kuadopt mtoto ili achangamshe nyumba. Ndio in the process mtoto anafaidika lakini hawa watu wanamtumia mtoto kama therapy ya wao kujisikia vizuri.
Haya hawa wangine matajiri wenye watoto saa zingine wanaamua kuadopt ili kuendeleza umarufu wao.
Kwa kweli mie naona ni wachache sana wanao adopt ili kumuendeleza mtoto kwa faida ya mtoto. Kwa mfano, huyo madona si ana pesa sana? kama anataka kusaidia kwanini asijenge kitua baaabu kuibwa cha watoto ili kisaidie watoto beyond David?
Kama kweli hao akina anjelina joliii na madona wanataka kusaidia na kuweka difference kwa watoto wasikini basi wangefanya kama oprah alivofanya. Pesa si wanazo bana na wanataka kuzishea kwa kusaidia?
natumaini madona anajua analofanya na kwa faida ya david kwa kuwa kuna watu wengi siku hizi wamegeuza matatizo ya watu kuwa maarufu wanapowasaidia,kujenga majina yao
siku hizi mtu anakusaidia kwa kuwa anataka kuwa maarufu ,kujenga jina lake....
Post a Comment