Tuesday, March 09, 2010

Mzungu Am 'Kanye West' Mweusi kwenye Oscars

Umesikia kituko kilichotokea kwenye Oscars juzi? Huyo Roger Ross Williams alikuwa anapokea tuzo kwa ajili ya sinema ya 'Music by Prudence'. Ghafla katokea bibi wa kizungu, Elinor Burkett, na kuanza kusema, "mwache mwanamke aongee" na maneno mengine ambao watu hawakuelewa.

Sisi watazamaji tulishangaa sana inatokea nini. Kumbe huyo mzungu aliwahi kuwa producer wa hiyo sinema lakini waligombana na Williams. Burkett alimpeleka mahakamni lakini walisuluhisha nje ya mahakama. Burkett aklisem hakupenda jinsi sinema ilivyokuwa inaenda. Ajabu, jinsi ilivyoenda ndo ikashinda Oscar!

Lakini wadau , hii kituko kisingetokea tusingekumbuka habari ya hiyo sinema, Music by Prudence. Pia hao Williams nad Burkett wasingejulikana. Sasa hivi Letterman, Leno na wengine wanamtania huyo Burkett. Bila shaka na Saturday Night Live watamtania!

Pia wanamwita Burkett, Lady Kanye! Kumuka mwaka jana Kanye West alivyoingia hotuba ya Taylor Swift kwenye tuzo za MTV.

2 comments:

Anonymous said...

Doh! Huyo mama kwelia anastahili kuitwa Lady Kanye!

Anonymous said...

Halafu anamwita Williams boy! Hiyo ni tusi kwa wamaerekani weusi. Huyo jamaa ni baba zima!