Wednesday, November 10, 2010

Mwanamke Atakuwa Spika?

Wadau, hii kweli ni mapinduzi. CCM wamewachagua wanawake watatu kugombea nafasi ya Spika kwenye tiketi ya CCM. Nao ni wanasiasa wakongwe, Anna Abdallah, Kate Kamba na Anna Makinda. May the Best Woman Win!

Habari zingine zinasema kuwa Chama cha Chadema wamemsimamisha Mh. Mabere Marando.

Akina Mama Oyeeee!

************************************************************
Kutoka Michuzi Blog:

KAMATI KUU LEO IMEPENDEKEZA MAJINA MATATU YA WANA CCM WATAKAOGOMBEA NAFASI YA USPIKA KATI YA WAGOMBEA 13 WA CHAMA HICHO WALIOJITOKEZA. MMOJA WAO NDIYE ATAYETEULIWA KUSIMAMA KUGOMBEA BAADA YA KUPITISHWA

NAO NI MH. ANNA ABDALLAH,
MH. KATE KAMBA NA MH. ANNA MAKINDA.

MAJINA YA WANAOWANIA UNAIBU SPIKA YANATAKIWA YAFIKE OFISI ZA BUNGE KESHOKUTWA NOVEMBA 15, 2010.

KATIBU MKUU WA CCM AMESEMA SASA HIVI KWAMBA KAMATI KUU YA CCM IMEAMUA KWA MAKUSUDI KUMPA NAFASI MWANAMKE KUONGOZA MOJA WA MIHIMILI MITATU YA NCHI KWA MARA YA KWANZA KATIKA HISTORIA YA JAMHURI YA MUUNGANO.

1 comment:

emu-three said...

Nafasi hii itakwenda kwa mwanamke, siunajua tena bunge asilimia kubwa ni SISIEMU!