Tuesday, March 01, 2011

LUKU Za TANESCO Zina Mambo!

Haya ni maoni ya mdau:

Nasikia "wajanja" wa Tanesco wana-program LUKU, wewe unalipa Shs 1,000 kwa mwezi lakini unapata umeme wa kuweza kuwasha tanuru (kama unalo).
Malipo tofauti mnalipana chembaz na programmer.

Habari hizi umeshazipata au wewe hawakukufundisha hii programming pale Chuo cha Tanesco.

Sasa kama Tanesco wananunua umeme Dowans na kukuuzia wewe, hasara na faida tunajua napata nani :-)

Maelezo zaidi kuhusu THAMANI na BEI utatupiga "tuisheni" baadaye :-)

Halafu mnataka kutulaumu sisi tulioko Florida ........ati makosa yetu hatukusomea Chuo cha Tanesco.

Hebu DM atufafanulie kama anaujua huu mpango wa ku-program LUKU za Tanesco ili kujipatia umeme wa chee.
Huu ndiyo mpango wa UMEME KWANZA kwani KILIMO KWANZA ni kwa ajili ya Ng'wakitolyo
Uchakachuaji hadi kwenye LUKU.
Tanesco pandisheni bei ya umeme, watumiaji tuna mbinu zetu .....mechi droo.
Sijui "kisowia" ni nani kati ya Tanesco na wateja?? :-)

Mdau O.S. M.

No comments: