![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEirji9dTM6jPNhlUooXr_hWxOCr0kdt0F-NoOaFRUGn-68lTkhztLPdshH-M2U65Y8MZiJQ884G9VPbuRo9dba4hay58edl3VOl1mfixP_fILg5hLmD9iRs8YgVoDlxZAnr0K4p/s400/Mwaigoga.jpg)
Marehemu bibi yangu, Gandula, kabla ya kufariki alisimulia hivi.... Walikuwa kijijini wanafanya shughuli zao. Ghafla wakaona zinga la wimbi la inakuja, walikimbia mlimani. Kijiji karibu chote kikamezwa. Maajabu hakuna aliyekufa wakati huo. Nyumba za wanavijiji, nyumba za mkoloni, miti, mibuyu, shule, makaburi, kila kitu kilimezwa na ziwa!
Wanasema kuna Mzee fulani, Mzee Kwiyanja, aliwaambia miaka mingi, hameni hapo Ilela, maana kijiji kitamezwa. Bibi alisema kuwa walikuwa wanamcheka yule Mzee na kumwona mwendawazimu. Yeye alihama na kujenga mlimani. Baada ya tukio wakamwona yule mzee kama mtume (prophet).
Kuna sehemu ya Ilela imebaki. Na nilipoenda kutembea nilikutana na wanavijiji wengi walionikumbuka hasa kwa ajili ya utundu wangu nikiwa mdogo. Picha zaidi za Ilela zinakuja.
2 comments:
Umenikumbusha mbali sana kutoka Manda kwenda Lundo sijui ni umbali gani maana huko ndo nilikozaliwa mimi. Ahsante kwa hadithi ya bibi na bahati mbaya kumbukumbu nyingine zimepotea. Taswira nzuri sana. Nasubiri picha nyingine.
mandhari nzuri ya ziwa hii. beautiful beach, this one.
Post a Comment