Sunday, November 09, 2014

Rais Kikwete Anaendelea Vizuri Baada ya Upasuaji John Hopkins Hospital (USA)




Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Balozi wa Tanzania nchini
Marekani Mhe Liberata Mulamula aliyekwenda kumjulia hali katika
hospitali ya John Hopkins iliyopo Baltimore, Maryland, nchini
Marekani, leo Jumapili, siku moja baada ya kufanyiwa upasuaji wa Tezi
Dume.

Habari kutoka hospitalini hapo zinasema Rais Kikwete anaendelea vyema
na leo asubuhi alianza mazoezi ya kutembea, kuashiria kwamba mambo
yote ni mswano. Tutaendelea kwuashirikisha taarifa ya maendeleo yake
mara kwa mara. Tuzidi kumuombea apate nafuu haraka ili arejee nyumbani
kulijenga Taifa.

PICHA NA IKULU

No comments: