Saturday, June 27, 2015

Onyo - Sindano Za Kuongeza Saizi ya Makalio!

Wadau, nimewaambia mpende Mwenyezi Mungu alivyowaumba. Acheni huo mtindo wa kujichubua na kutaka matako yako yawe makubwa sana!  Kuna mtindo Afrika sasa ya kutaka  kuongeza saizi ya matako kwa kuchoma sindano.  Sindano zingine na nyingi ni feki na zina sumu kama Fix a Flat ambayo inatumika kama tairi ya gari ikipata pancha. Sasa unalipa hela yako, wahuni wanakuchoma hiyo sindano, siku mbili tatu unatamba na matako yako waliyovimba kama puto halafu baada ya wiki unaona matakao yako yanaoza.  Hebu ona yaliyompata mwenzenu.


1 comment:

Anonymous said...

Huyo mwenye pinki yuko fiti sana!