Wednesday, September 07, 2016

Mama Bishanga na Wadogo Zake Wafiwa na Mama Yao

MAMA BISHANGA NA WADOGO ZAKE WAFIWA NA MAMA YAO

         MWALIMU AGNES NDEMBO HATIA
Watoto wa marehemu mzee Isaya Innocent Hatia tumempoteza mpendwa mama
yetu mpendwa Mwalimu Agnes Ndembo Hatia kilichotokea hospitali ya Regency
 jana jumamamosi mchana. Mama yetu alikuwa nguzo pekee iliobakia nasi baada
ya kufariki baba yetu Mzee Isaya Innocent Hatia mwaka 2011. Tunamshukuru
Mungu sana kwa upendo wake kwa mama yetu aliempa nguvu ya kuishi miaka
tisini na sasa amempenda zaid mama yetu, bibi yetu na amempumzisha usingizi
wa milele na milele Ameni
Mwalimu Agnes Ndembo Hatia amefundisha watu wengi sana darasa la kwanza
tangia miaka ya hamsini hadi alipostaafu Tabora, Uhuru shule yamsingi.
Mama, ametuacha watoto wake Christina wa USA, Geofrey wa Namibia, Mwl
Mark Hatia wa Tambaza shule ya secondary, Bernadetta wa Dar, Isaya wa Finland,
Costancia wa Kibaha, na Oscar mdogo wetu wa mwisho. Ameacha wajukuu, na
vitukuu wengi ambao ni watoto na wajukuu zetu sisi watoto wake pamoja na dada
zetu marehemu Joyce Hatia na Mwalimu Cecilia Hatia. Picha zinaonyesha
mama Hatia mwaka 1966 akiwa na Constacia ambae picha yake pembeni ni Costancia
alivyo sasa, na zingine ni mama na wanae wajukuu na vitukuu
Kwa taarifa za maandalizi na ratiba piga simu zifuatazo. 0653 763 201 Kilian Kamota,
0755 333 948 Dick Hatia, 0788 627 430 Ibra Yunus, na 0763 833 893 Solmon.
 BWANA ALITOA, BWANA AMETWAA. TUMSIFU YESU KRISTO: AMEN
 

No comments: