Saturday, September 17, 2016

Mwenge wa Uhuru Wawasili Mkoani Singida na Ishara ya Uhuru wa Tanganyika

MWENGE wa Uhuru baada ya kuwasili mkoani Singida Mwenge huu ni ni kitu mfano wa kikombe chenye mpini mrefu na utambi ambacho aghalabu huwasha na kukimbizwa katika kusheherekea au kutukuza tukio fulani
Askari wa Jeshi la Polisi wakiulinda Mwenge ishara ya kuwasili muda mfupi kabla ya kukabidhi kwa uongozi wa Mkoa wa Singida

Kushoto ni Katibu tawala wa Mkoa wa Singida Dkt Angelina M. Lutambi akimkabidhi Mwenge Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe Geofrey Mwambe tayari kwa ajili ya kumulika Miradi 18 katika Wilaya hiyo

Baadhi ya viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Dodoma walipowasili kukabidhi Mwenge katika Kijiji cha Lusilile Kata ya Kintinku Wilaya ya Manyoni
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akiwa ameushikia Mwenge ishara ya Makabidhiano mara baada ya kuwasili
Katibu tawala wa Mkoa wa Singida Dkt Angelina M. Lutambi akikabidhiwa Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bi Rehema S. Madenge
 Wananchi wakishuhudia kwa karibu zoezi la makabidhiano ya Mwenge
Wakuu wa Wilaya za mkoa wa Singida wakishuhudia zoezi la makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru
 Wengi wamefika kushuhudia Mwenge ukiwasili mkoani Singida
 Viongozi wa Mkoa wa Singida wakifanya mazoezi ya maandalizi ya kuupokea Mwenge
 Timiza wajibu wako kata Mnyoro wa Rushwa
Katibu tawala wa Mkoa wa Singida Dkt Angelina M. Lutambi akisoma salamu za shukrani mara baada ya kupokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma katika Kijiji cha Lusilile

No comments: